ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, August 20, 2021

MPIGA PICHA WA AYO TV MWANZA APUMZISHWA KWENYE NYUMBA YAKE YA MILELE.


Msafara ulioubeba mwili wa aliyekuwa mpigapicha wa Ayo Tv Mwanza, marehemu Nelson Brigeri ‘Nelly TZA ukitoka nyumbani kwao Kanyerere wilayani Nyamagana mkoani Mwanza kuelekea makaburi ya Kanyerere.
Gari lilobeba mwili wa aliyekuwa mpigapicha wa Ayo Tv Mwanza, marehemu Nelson Brigeri ‘Nelly TZA likiwa kwenye msafara kutoka nyumbani kwao Kanyerere wilayani Nyamagana mkoani Mwanza kuelekea makaburi ya Kanyerere.
Sehemu ya umati uliojitokeza makaburi ya Kanyerere.
Jeneza lililoubeba mwili wa aliyekuwa mpigapicha wa Ayo Tv Mwanza, marehemu Nelson Brigeri ‘Nelly TZA likiwasili katika makaburi ya Kanyerere.
Mkurugenzi wa Ayo Tv, Bwana Millard Ayo (aliyeshika picha) alikuwa mmoja wa washiriki kwenye mazishi hayo ya aliyekuwa mpigapicha wa Ayo Tv Mwanza, marehemu Nelson Brigeri ‘Nelly TZA.
Kwaheri Nelson Brigeri ‘Nelly TZA 
Marafiki mbalimbali wamejitokeza kwa wingi kuuaga na kukamilisha safari ya mwisho ya pumziko la milele yake marehemu Nelson Brigeri ‘Nelly TZA aliyefariki kupitia ajali mbaya ya gari iliyotokea eneo la Kibaha usiku wa kuamkia tarehe 18 Agasti 2021 baada ya kugongana uso kwa uso na gari la mizigo.
Jeneza lililobeba mwili wa marehemu Nelson Brigeri ‘Nelly TZA likishushwa kaburini.
Safiri salama Nelson Brigeri ‘Nelly TZA
"Binadamu ni mavumbi na mavumbini tutarejea, safiri salama Nelson Brigeri ‘Nelly TZA"
Mstahiki Meya wa jiji la Mwanza Mhe Sima Costantine alikuwa ni miongoni mwa walioshiriki mazishi ya mwanahabari wa Ayo Tv Mwanza, Nelson Brigeri ‘Nelly TZA

 Wanafunzi toka shule mbalimbali za jijini Mwanza nao walioshiriki mazishi ya mwanahabari wa Ayo Tv Mwanza, Nelson Brigeri ‘Nelly TZA

Pumzika kwa amani ewe rafiki.
Bwana alitoa na Bwana ametwaa jina lake lihimidiwe.

DK MWIGULU: TOZO YA MIAMALA SI MICHANGO YA KIRAFIKI NI SHERIA YA BUNGE.

 


Waziri wa Fedha na Mipango nchini Tanzania, Dk Mwigulu Nchemba amesema  tozo za miamala ya simu si michango ya kirafiki ni sheria iliyopitishwa na  Bunge baada ya kujadiliwa kwa kina  akibainisha kuwa wabunge ni wawakilishi wa wananchi.

Dk Nchemba amezungumza hayo leo Ijumaa Agosti 20, 2021 katika mkutano wake na waandishi wa habari akieleza kuwa fedha zilizopatikana baada ya ukusanyaji wa tozo tangu sheria ilipoanza kutumika mwezi mmoja uliopita,  zimetumika kuboresha sekta ya afya,  elimu na miundombinu.

 “Yaani inanyesha mvua moja tu mtoto inabidi alale shuleni hivi nani anaweza kumuamini jirani tu mtoto alale kila siku mto unapofungwa embu niambie mzazi unalala usingizi wa aina gani, kuna vitu ni serious kweli kweli ambavyo wabunge wanavisemea ambavyo vinatulazimisha tufunge mikanda, ”amesema Dk Mwigulu.

Amesema  nchi ndio zinavyojengwa hivyo amewapongeza watanzania wote ambao wanatoa mawazo mazuri ya kuboresha jambo hilo.

Leo Waziri huyo ameeleza kuwa katika kipindi cha wiki nne tangu kuanza kukata tozo ya miamala,   Serikali imekusanya Sh48.4 bilioni huku zaidi ya Sh22 bilioni zimepelekwa katika vituo vya afya.

Thursday, August 19, 2021

ANGELINA JIMBO CUP 2021 KUANZA KUTIMUA VUMBI KESHO.

MASHINDANO ya Angeline Jimbo Cup 2021, ambayo yatashirikisha timu 19, kutoka kata zote zilizopo jimboni Ilemela yanatarajia kuanza kutimua vumbi Agousti 20,mwaka huu,huku jumla ya milioni 24,zitatumika katka mashindano hayo.

Mashindano hayo ambayo yalianzishwa rasmi mwaka 2016, na Mbunge wa Jimbo la Ilemela, Naibu Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt.Angeline Mabula,kwa lengo la kuinua vipaji kupitia michezo jimboni humo.

Akizungumza katika hafla ya kukabidhi vifaa vya michezo kwa timu hizo zitakazo shiriki mashindano hayo, Mbunge wa Jimbo la Ilemela,Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Angeline Mabula alisema
kutokana na yeye kuwa mwanamichezo pamoja na kutekeleza Ilani ya Chama Cha Mapinduzi ndio maana alianzusha mashindano hayo.

Dkt.Angeline,amesema michuano ya msimu huu imeboreshwa zaidi kupita michuano iliyopita kuanzia kwenye zawadi wameboresha kutoka mshindi wa kwanza hadi wa nne msimu huu.

Amesema,mshindi wa mashindano hayo kwa msimu huu atajinyakulia zawadi ya milioni 2 mshindi wa pili milioni 1.5, mshindi wa tatu milioni 1 huku mshindi wa nne atapata 500,000.

Pamoja na zawadi hiyo mshindi wa kwanza hadi wa tatu watapewa kombe, jezi seti moja na mpira huku mshindi wa nne atapewa jezi na mpira tu ambapo zawadi za washiriki bora zikitolewa pia.

Mbunge wa Jimbo la Ilemela,Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Angeline Mabula( wa kwanza kulia),akimkabidhi vifaa vya michezo kiongozi wa timu moja wapo kati ya timu 19 kutoka kata zote zilizopo jimboni Ilemela,zitakazo shiriki mashindano ya Angeline Jimbo Cup yanayotarajia kuanza kutimua vumbi Agousti 20,mwaka huu.picha na Judith Ferdinand

Mratibu wa Mashindano hayo,Katibu wa Chama cha Mpira Wilaya ya Ilemela Almasi Moshi Almasi,amesema michuano hiyo itachezwa kwa mtindo wa makundi,manne ambayo yatatumia viwanja vya Buswelu, Kona ya Bwiru, Saba Saba na Bugogwa.

Amesema,jumla ya timu 19,kutoka kila kata jimboni Ilemela zinatarajia kushiriki mashindano hayo ambayo yamekuwa yakiongezeka hamasa kila mwaka huku ukiwa ni msimu wake wa tatu toka yaanze.

Kwa Upande Ofisa Michezo wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela Kizito Bahati, amesema suala la matibabu ya kwanza kwa wachezaji watakaoumia limezingatiwa,waamuzi(refals) wa kusimamia sheria 17,wapo hivyo timu shiriki zipambane uwanjani ili zipate ushindi.

Mbunge wa Jimbo la Ilemela Dk. Angeline Mabula ambaye pia ni Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi amesema kuwa jumla ya kiasi cha shilingi milioni Ishirini na nne zimetengwa kwa ajili ya mashindano ya Angeline Jimbo Cup 2021 yanayotarajia kuanza mnamo Tarehe 20 Agosti, 2021.







HAWA NI VIUMBE 10 WA AJABU WANAOPATIKANA GAHARINI.i

 

a

CHANZO CHA PICHA,ASHER FLATT/NESP MARINE BIODIVERSITY HUB/CSIRO)

Viumbe wa ajabu wanapatikana kila mahali, wapo wanaofahamika na wasiofahamika. Wapo wanaoishi angani, ardhini napo wanaoishi majini ambao ndio hasa tunawatazama katika Makala haya.

Kwa mujibu wa wanasayansi kuna mamilioni ya viumbe wa majini wanaoishi na kupatikana kwenye vyanzo mbali mbali vya maji kama mito, maziwa na bahari. Lakini wengi wanaofahamika ni samaki wanailiwa na wasioliwa lakini ukweli ni kwamba kuna viumbe wengi wa ajabu kuwahi kushuhudiwa duniani wanaoshi baharini kama walivyobainika mwaka 2017 na wanasayansi mbalimbali. Miongoni mwao ni hawa.

Ratfish

g

CHANZO CHA PICHA

Hii ni aina mpya ya Papa ambaye amegunduliwa mwaka huu Januari, huko Afrika Kusini na kuweka rekodi mpya. Ana urefu wa karibu futi 3 kama mita moja hivi, akiwa anashika nafasi ya pili kwa ukubwa kwa aina ya Papa walioogundulika . Hiyo ni kwa mujibu wa watafiti wa Pacific Shark Research Center huko California, Marekani.

Aina hii ya Papa wa ajabu ni ya 50 kugundulika duniani na ni wa tatu kwenye kundi la Hydrolagus, kwa maana ya "panya wa majini. Muonekano wake unatisha na ndio hasa sababu ya kupewa jina la Ratfish ama Ghost Shark.

Watafiti wanamuona papa huyu kama sio papa kwa sababu ya muonekano wake unaotisha na wa ajabu lakini akiwa na sifa za kufanana kiasi na mapezi makubwa zaidi yanayomtofautisha papa wa aina hii na papa wa kawaida wenye mkia wa kipekee.

Cannibal corpse

James Ormiston

CHANZO CHA PICHA,

Kiumbe kingine cha ajabu kilichogunduika mwezi Februari 2017 karibu na mji wa Moosonee kwenye uwanda wa Hudson Bay huko Ontario, Canada. Anafahamika pia kwa jina la Bobbit worm kwa maana ya Minyoo ya majini ya Bobbit.

Ni kiumbe kikongwe zaidi kilichowahi kuishi miaka 400 million iliyopita , na kufanya kuwa minyoo mikongwe zaidi kuwahi kuishi duniani. Kutokana na maumbile yake na taya zake, Bobit ana uwezo wa kujirefusha na kufikia urefu wa futi 3. Kwa sababu ya ukubwa wake, watafiti wametoa jina la Websteroprion armstrongi.

"Cosmic" jellyfish

NOAA

CHANZO CHA PICHA,

Samaki huyu anapatika kwenye maji yenye kina kirefu zaidi , anapenda kuishi kwenye kina cha kuanzia angalau futi 9,800 kama urefu wa kilometa 3 chini ya maji. Amegundulika kwenye kina cha bahari ya Pasific karibu na Samoa, akitajwa kama aina mpya ya jellyfish.

Ni ngumu kumuelezea alivyo, lakini umbuile lake lilionekana kwa mbali kupitia National Oceanic and Atmospheric Administration (NOAA), waliokuwa wanaendesha shughuli za kuzamia maji.

Walitumia kifaa cha kuonea vitu vilivyo mbali (microscope) na kusaidia kumgundua na kugundua wanapopatikana. "Tulivyokuwa tunaendelea kuangalia , tukaanza kupata picha ya namna maisha yalivyo huko chini ya maji -pengine ni makazi makubwa zaidi ya viumbe wa aina hii," alisema Michael Ford, mtaalam kutoka NOAA.

Shipworm

Marvin Altamia

CHANZO CHA PICHA,

Anafahamika kitaalamu kama Slimy mollusks au Shipworms, wanaotajwa kula mbao na wanaweza kuuchangamkia na kuumaliza mtumbwi ama boti ya mbao kwa muda mfupi..

Ni minyoo mikubwa yenye mkia wa ajabu ambao huwekwa kwenye kundi la Kuphus polythalamia, ingawa, kwa muda mrefu wa miaka na miaka haikuwahi kuonekana mpaka mwezi Aprili mwaka huu.

Watafiti walikusanya minyoo hii mitano kutoka kwenye mkondo mmoja huko Philippines kwa ajili ya kuifanyia utafiti. Tofauti na minyoo ya kawaida, minyoo hii inayokula mbao ina urefu wa kati ya futi 3 mpaka 5 ni kama mita moja mpaka mita 1 na nusu. Inaishi katika matope, na hujizungusha katika magamba magumu yanayoonekana kama mkonga wa tembo.

Lizard fish

NESP Marine Biodiversity Hub

CHANZO CHA PICHA,

Wanasayansi walikuwa wamepanda boti kutafuta samaki mashariki mwa pwani ya Australia, walipokutana kwa bahati mbaya tena bila kutegemea na kiumbe huyu anayejulikana kama Bathysaurus ferox, mweye muonekano wa sura kama mjusi na anayetajwa kama kiumbe hatari kinachoishi kwenye kina kirefu cha maji:

Anaishi kwenye kina cha bahari chenye urefu wa futi 3,300 mpaka 8,200 kama kilometa 1 mpaka kilometa 2.5 kutoka kwenye usawa wa bahari.

Akiwa anaogelea, matezi yake yanadaka vyakula. "Kama atafanikiwa kukudaka kwenye matezi yake, hauna la kufanya: Namna utakavyokuwa unapambana ujiondoe, ndo unavyozidi kutitita kwenye mdomo wake," Asher Flatt, aliandika mmoja wa wanasayansi hao waliokuwa kwenye boti.

Loch Ness

James Campbell

CHANZO CHA PICHA,

Ukifikiria kuhusu kiumbe huyu wa ajabu Loch Ness, pengine akilini mwako picha itakayokujia haraka ni ya plesiosaur — au madinosa yenye shingo ndefu na mabawa manne, au kiumbe mwenye ummbo la mamba.

Mapema Agosti 23 mwaka 2017, watafiti waliwasilisha utafiti wao kuhusu kiumbe mwenye umri wa miaka milioni 76 alioyeonekana huko Alberta, Canada.

Kiumbe huyu alikuwa na 'ukubwa wa kama gari'— akiwa na urefu wa futi kati ya 13 mpaka 16 sawa na mita kati ya 4 mpaka 5. Alikuwa hai kabisa kwa mujibu wa watafiti kutoka chuo kikuu cha Calgary.

Ingawa kwa kimo hicho ana onekana mkubwa, lakini watafiti wanasema ukumbwa wake unaweza kufikia mpaka futi 50 ama mita 15, ukubwa wa kama basi la kisasa la abiria.

Diamond Squid

Jay Wink

CHANZO CHA PICHA,

Kiumbe hiki kimeonekana katika bahari karibu na Australia, kiasi cha kushangaza dunia kilipoonekana mwezi September mwaka 2017.

Muonekano wake, ni kama mnyoo si mnyoo, au kiumbe ambacho ni kama kipya kabisa kuwahi kuonekana duiani. Rebecca Helm, mtafiti kutoka Woods Hole Oceanographic Institution huko Massachusetts, Marekani, alitegua kitendawili hicho:

"Kiumbe hiki kiko kundi la Thysanoteuthis rhombus sakifahamika kwa jina linguine kama 'diamond squid', lakini ni ngumu kusema ni nani hasa," Helm aliiambia Live Science.

Diamond squid anaweza kukua kwa urefu wa futi mpaka 3, uzito wa kilo mpaka 30. Kiumbe hiko kinaweza kutaga mayai mpaka 24,100 mpaka 43,800 kwa wakati mmoja katika mudo wa kama bomba unaoweza kukua mpaka urefu wa futi 6 kama mita 1.8, kwa mujibu wa Helm.

Kleptopredator

Gabriella Luongo

CHANZO CHA PICHA,

Kiumbe kingine cha ajabu kinachopatikana majini anayefahamika kama Cratena peregrina na wanaopenda kula viuvimbe vinavyojitokeza ama vilivyopo katika viumbe vingine, igawa wanasayansi wengine wanasema kiube hiki hupenda kula viuvimbe baada ya kumaliza kula mlo wake mkuu hasa wa nyakati za jioni.

Deep-ocean shark

d

CHANZO CHA PICHA,

Wavuvi wanaovua ahari ya kina kirefu huko Ureno kwa bahati mbaya walimvua kiumbe huyu mwezi Novemba 2017.

Wanasayansi hao walikutana na kiumbe hiki cha ajabu kinachojuikana kama Chlamydoselachus anguineus — mwenye meno makali. Kwa mujibu wa watafiti kiumbe hiki kimekuwa na mabadiliko katika kipindi cha miaka milioni 80 kiasi cha kuelezewa na watafiti kama "living fossil."

Anatajwa kuwa na meno 300, ambayo ni makali na yanatisha akiwa na urefu unaoweza kufikia futi 5. Kiumbe hiki ni ngumu sana kuonekana na watu kwa sababu kinapenda kuishi na kuogelea kwenye kina kirefu kama futi 4,600 kama mita 1,400 au kilometa 1.4 kutoka usawa wa bahari

Bone-filled fish

f

CHANZO CHA PICHA,

Bonny fish mzito zaidi kuwahi kuvuliwa duniani ni yule aliyepatikana kwenye fukwe za Japan mwaka 1996. Alikuwa na kilo 2,300. Kwa iongo kadhaa sasa, wanasayansi wakisema aina hiyo ya samaki ama kiumbe ni kutoka kundi la Mola mola.

Lakini kwa mujibu wa taarifa iliyochapishwa baadae mwaka huo huo wa 2017, mwezi Disemba, na jarida la Ichthyological Research, kiumbe hiko kilichovuliwa ama kupatikana Japan kinafahamika kama Mola alexandrini.

Miili yao ni mikubwa na ya umbo la duara kiasi na wanaweza kukua mpaka urefu wa futi 10. Kwa sababu ya urefu na uziito wao huo, imekuwa ngumu kiumbe hiki kusafirishwa

Wednesday, August 18, 2021

TFF YAKANUSHA KUACHANA NA POULSEN.

 

Shirikisho la mpira wa miguu nchini Tanzania (TFF) linasisitiza kuwa Kim Poulsen bado ni kocha mkuu wa timu ya Taifa (Taifa Stars).

Taarifa zinazosambaa kwenye mitandao ya kijamii kuwa TFF, inafanya mazungumzo na kocha Jamal Sellami kwaajili ya kuinoa Taifa Stars sio za kweli.

TFF inaendeshwa kiuweledi hivyo haiwezi kufanya maongezi na kocha mwingine wakati inamkataba na Kocha Poulsen.

Februari mwaka huu, TFF ilimteuwa Poulsen Kuwa Kocha wa timu ya Taifa Stars kwa mkataba wa Miaka Mitatu.

MWANDISHI WA MILLARDAYO.COM MWANZA AFARIKI DUNIA KWA AJALI.

Enzi za uhai wake marehemu Nelson Brigeri ‘Nelly TZA.
 ⚫▶Nimeumizwa na taarifa za msiba wako mdogo wangu Nelly umekuwa mpiga picha mahiri na fundi wa MillardAyo.Com Mwanza, ...............Amefariki dunia kupitia ajali mbaya eneo la Kibaha usiku wa kuamkia leo baada ya kugongana uso kwa uso na gari ya mizigo.

.

Walikuwa watatu kwenye gari private ambapo wengine waliokuwa naye ni pamoja na Dullah TZA (yuko hospitali akipatiwa matibabu) na mfanyabiashara wa magari wa jijini Mwanza Mujitaba Yusuf Abbas (PICHANI CHINI).

Enzi za uhai wake marehemu Mujitaba Yusufu Abbas

"Binafsi moyo wangu umekunjika, unauma, hofu imenitanda, huruma kwa rafiki ambaye alikuwa mpole na mtiifu, .......oh my....." 😭😭😭

Taarifa zinaeleza kuwa ndani ya gari hilo dogo binafsi kulikua na watu watatu ambapo mmoja wao, Nelly amepoteza maisha pamoja na Mujitaba naye amefariki dunia.
 Dullah (pichani) aliyepata majeraha anaendelea na matibabu.



Uongozi na Wafanyakazi wa Jembe Fm pamoja na Gsengo Blog tunatoa pole kwa Mkurugenzi wa Ayo TV, Millard Ayo, wafanyakazi wote wa Ayo TV, ndugu pamoja na marafiki kwa kuondokewa na mpendwa wao.

Mwenyezi Mungu azilaze mahali pema peponi za marehemu, AMEN!

#RiPElly

#RiPMujitaba 

CC:- #KaziNaNgoma

@bongewajue

@mustafakinkulah 

@kikotifredy 

@florenciapeter_tz


MWANAFUNZI WA KIDATO CHA SITA IFUNDA ABUNI KIFAA CHA KUZUIA MOTO MABWENINI.

 


Na Ezekiel Mtonyole, Iringa.

Wanafunzi wa kidato cha sita katika Shule ya Sekondari ya Ufundi Ifunda iliyopo mkoani Iringa Oscar Herman amebuni kifaa kitakachoweza kutoa taarifa pindi inapotokea hitilafu ya umeme inayoweza kusababisha  jengo uungua moto.

Akizungumza wakati wa ziara ya waandishi wa habari walipotembelea shule hiyo ikiwa ni ziara ya kutembelea miradi ya Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia amesema aliamua kubuni kifaa hicho kwa lengo la kuzuia majanga ya moto hasa kwenye mabweni.

"Hivi karibuni yametokea majanga mengi shule kuungua moto na mabweni ndio maana nikaamua kuja na ubunifu huu hii itakuwa suluhisho" amesema Mwanafunzi Oscar.

Amebainisha kuwa ufanisi wa kifaa hicho ni kwamba kumekuwa na tabia ya wanafunzi kukata nyaya juu ya dali za mabweni kwa lengo la kutumia umeme kwa kificho lakini kwa sasa akikata nyaya ya umeme kifaa hicho kitatoa taarifa kwa msimamizi wa bweni.

Ameongeza kuwa "ni miezi sita tangu nianze ubunifu huu hata nikiwa likizo naendelea na pindi nikirudi shule naendelea na sasa niko hatua nzuri tu kukamilisha kifaa hiki" amesema.

Aidha akishirikiana na  mwanafunzi wa kidato cha kwanza Isaya Faustine wanabuni  Roboti Maalum litakalokua linasaidia wakulima kupulizia dawa kwenye mazao yao mashambani.

Akizungumzia ubunifu huo, Isaya Faustine wa kidato cha kwanza amesema wamekuja na wazo hilo ili kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Serikali katika kuwainua wakulima na sekta ya kilimo kwa ujumla.

Amesema kwa sasa wako kwenye hatua za awali za utengenezaji wa roboti hiyo na wanatarajia kukamilisha ndani ya wiki moja kwani tayari washapata kibali cha kuanza mradi wao huo wa kutenegeneza roboti hilo.

" Wote tunafahamu kilimo ndio uti wa mgongo wa Nchi yetu hivyo sisi kama wabunifu tumeona tuje na kifaa hichi ambacho kitasaidia wakulima kuweza kupuliza dawa kwenye mashamba yao wakiwa majumbani mwao.

Roboti hili tutalitengeneza kwa mfumo wa Gari lakini halitokua na matairi bali minyororo kama vilivyo vifaru vile vya Jeshi, halafu Mkulima atapaswa kuwa na application kwenye simu yake ambapo akitaka kunyunyuzia dawa Mazao yake analipigia simu na lenyewe linafanya kazi hiyo," Amesema Isaya.

Amesema kukamilika kwa kifaa hicho siyo tu kitakua kinaokoa muda wa wakulima lakini pia kitawaepusha wakulima na maradhi ambayo wamekua wakiyapata kutokana na upulizaji wa dawa wanaoufanya kwenye mazao yao," Amesema Isaya.

Kwa upande wake Oscar Metwa ambaye amebuni pia kifaa cha kuzuia madhara yanayosababishwa na umeme ameiomba Serikali kuwatupia macho wabunifu vijana ili nao waweze kutoa mchango wao kwa Taifa lao.

" Mbali ya mpango wetu huu wa Roboti lakini pia nimebuni kifaa hiki cha kuzuia madhara yanayosababishwa na shoti za umeme ambapo tayari kifaa hiki kimefungwa kwenye mojawapo ya mabweni hapa shuleni na kinafanya kazi," Amesema Metwa.

Ametoa wito kwa wanafunzi wenzake nchini kutoogopa masomo ya Sayansi kwa kisingizio cha kwamba ni magumu bali waweke bidii katika kujisomea kwani hakuna somo gumu endapo utaliwekea bidii na kulipenda.

Nae Mkuu wa Shule hiyo, Yusuph Mwagala amesema katika kusapoti vipaji vya wanafunzi wao ambao wamekua wakifanya ubunifu mbalimbali wamekua wakiwaunganisha na Taasisi zinazokuza wabunifu pamoja na Vyuo mbalimbali ikiwemo Chuo Kikuu Cha Sayansi na Teknolojia Mbeya (MUST) pamoja na Chuo Cha DIT kwa ajili ya kujiendeleza zaidi.

" Kama Shule tumekua tukiunga mkono juhudi za vijana wetu wanaofanya tafiti na ubunifu kwa kuwaunganisha na taasisi zinazokuza ubunifu lakini pia kuwaunganisha na Vyuo kama MUST na DIT ambapo kote huko wanaenda kujiendeleza zaidi.

Kuna ubunifu mbalimbali ushafanywa na vijana wetu ikiwemo kutengeneza pampu ya kumwagilia bustani lakini pia ubunifu mwingine ni huu wa kifaa cha kuzuia madhara yanayosababishwa na umeme ambapo kupitia kifaa hiki sasa tunatumia mfumo wa DC na siyo AC ," Amesema Mwalimu Mwagala.'