ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, August 20, 2021

MPIGA PICHA WA AYO TV MWANZA APUMZISHWA KWENYE NYUMBA YAKE YA MILELE.


Msafara ulioubeba mwili wa aliyekuwa mpigapicha wa Ayo Tv Mwanza, marehemu Nelson Brigeri ‘Nelly TZA ukitoka nyumbani kwao Kanyerere wilayani Nyamagana mkoani Mwanza kuelekea makaburi ya Kanyerere.
Gari lilobeba mwili wa aliyekuwa mpigapicha wa Ayo Tv Mwanza, marehemu Nelson Brigeri ‘Nelly TZA likiwa kwenye msafara kutoka nyumbani kwao Kanyerere wilayani Nyamagana mkoani Mwanza kuelekea makaburi ya Kanyerere.
Sehemu ya umati uliojitokeza makaburi ya Kanyerere.
Jeneza lililoubeba mwili wa aliyekuwa mpigapicha wa Ayo Tv Mwanza, marehemu Nelson Brigeri ‘Nelly TZA likiwasili katika makaburi ya Kanyerere.
Mkurugenzi wa Ayo Tv, Bwana Millard Ayo (aliyeshika picha) alikuwa mmoja wa washiriki kwenye mazishi hayo ya aliyekuwa mpigapicha wa Ayo Tv Mwanza, marehemu Nelson Brigeri ‘Nelly TZA.
Kwaheri Nelson Brigeri ‘Nelly TZA 
Marafiki mbalimbali wamejitokeza kwa wingi kuuaga na kukamilisha safari ya mwisho ya pumziko la milele yake marehemu Nelson Brigeri ‘Nelly TZA aliyefariki kupitia ajali mbaya ya gari iliyotokea eneo la Kibaha usiku wa kuamkia tarehe 18 Agasti 2021 baada ya kugongana uso kwa uso na gari la mizigo.
Jeneza lililobeba mwili wa marehemu Nelson Brigeri ‘Nelly TZA likishushwa kaburini.
Safiri salama Nelson Brigeri ‘Nelly TZA
"Binadamu ni mavumbi na mavumbini tutarejea, safiri salama Nelson Brigeri ‘Nelly TZA"
Mstahiki Meya wa jiji la Mwanza Mhe Sima Costantine alikuwa ni miongoni mwa walioshiriki mazishi ya mwanahabari wa Ayo Tv Mwanza, Nelson Brigeri ‘Nelly TZA

 Wanafunzi toka shule mbalimbali za jijini Mwanza nao walioshiriki mazishi ya mwanahabari wa Ayo Tv Mwanza, Nelson Brigeri ‘Nelly TZA

Pumzika kwa amani ewe rafiki.
Bwana alitoa na Bwana ametwaa jina lake lihimidiwe.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.