ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, June 25, 2011

SHAGGY KESHA TUA MWANZA, KULA SATO NA SANGARA LEO KISHA KESHO JUMAPILI KUWASHA MOTO CCM KIRUMBA

Pichani pale kati Shaggy akiongozana na mwenyeji wake ambaye ni mmoja wakurugenzi wa Prime Times Promotion Godfrey Kusaga(kushoto) sambamba na wadau husika show ya kwanza Serengeti Fiesta 2011 itakayofanyika Jumapili hii (26juni2011)

Mwenyekiti wa Bodi ya Serengeti Breweries LTD Bwana Mark Bomani akisalimiana na Mwanamuziki wa kimataifa Shaggy mara baada ya kutua uwanja wa ndege Mwanza kwaajili ya kutoa burudani ndani ya msimu wa Dhahabu 2011.

Shaggy in Mwanza

Ncha Kali, Shaggy na Mchomvu on Air

Michuzi jr kwachaaa!!!..

Stage CCM Kirumba

WAZIRI WAZAMANI RWANDA AFUNGWA MAISHA

Mwanamke wa kwanza kushtakiwa kwenye mahakama ya kimataifa kufuatia mauaji ya kimbari nchini Rwanda amehukumiwa kifungo cha maisha jela.

Waziri huyo wa zamani wa masuala ya Familia, Pauline Nyiramasuhuko, amepatikana na hatia ya kupanga mauaji hayo na kuratibu ubakaji wa wanawake na wasichana wakati wa mauaji yaliotokea mwaka 1994.

Bi Nyiramasuhuko mwenye umri wa miaka 65, alifika katika mahakama ya uhalifu wa kivita nchini Rwanda (ICTR), ilioko mjini Arusha Tanzania leo.

Waziri huyo wa zamani na mtoto wake wa kiume Arsene Shalom Ntahobali, walikuwa wanakabiliwa na mashtaka kumi na moja, yakiwemo mauaji, ubakaji na kuwatesa watutsi na wahutu wenye msimamo wa wastani. Mashtaka ya dhidi yake kuhusu ubakaji yalikubalika kwa kuwa korti iliridhika kuwa alijua wasaidizi wake walikuwa wanafanya vitendo hivyo lakini hakuchukua hatua kuwazuia.

Mahakama hiyo imeambiwa kuwa waziri huyo wa zamani na familia yake alishiriki kuunda vikundi vya wanamgambo waliotekeleza mauaji hayo. Mahakama hiyo ilielezewa kuwa alihusika na mauaji yaliotokea maeneo ya kusini mwa jimbo la Butare.

Mahakama ya ICTR ilibuniwa mwaka wa 1994 kufuatia mauaji hayo ya kimbari ambapo inakadiriwa kuwa watu 800,000 waliuawa.

MISS MWANZA USIKU HUU NDANI YA GOLD CREST

LEO jiji la Mwanza linakwenda kupata mwakilishi katika barangeni la tasnia ya ulimbwende nchini, mshindi ambaye atajumuika na washiriki wengine kwenye kinyang'anyiro cha miss Lake zone na hatimaye lile kubwa Vodacom Miss Tanzania.

Mkurugenzi wa Clouds Ruge Mutahaba, Zamaradi Mketema, Msanii Mwasiti na Reuben Ndege nao ni moja kati ya mashuhuda usiku huu.

Vazi la ufukweni linaendelea kuchukua nafasi.

Katika pozi tofauti tofauti wakazi wa Mwanza waliobahatika kuingia ukumbini hapo kwani kuna wengine wengi waliamua kuishia mlangoni kutokana na kukosa nafasi juu ya nyomi lilokuwamo ndani.

Friday, June 24, 2011

MWANA FA, PROFESA J, CHIDDY BENZ, MWASITI WATUA MWANZA JIONI HII TAYARI KWA FIESTA

Shughuli ndiyo hivyoo imeiva na wageni mbalimbali sambamba na washereheshaji wanazidi kumiminika jijini Mwanza pichani mkali wa hip hop bongo Mwanafalsafa akitinga Mwanza tayari kwa Show ya Serengeti Fiesta itakayo fanyika jumapili hii kwenye uwanja wa CCM Kirumba Mwanza, Nasi tukitinga kwa kiingilio cha shilingi 5,000 tu.

Chiddy Benz nae huyoo akiwa na mtangazaji wa kipindi cha Ala za Roho Clouds Fm Lovenes love.

Mwana hip-hop Prof J nae ameonekana akiwa mwenye furaha mara baada ya kutua uwanja wa ndege Mwanza kutokea jijini Dar es salaam kwaajili ya shughuli za Fiesta.

Sakafu ya jukwaa.
Wasanii wengine wanaotarajiwa kuperform siku hiyo ni pamoja na Mataluma, Barnaba, Linah, Godzillah, Sajna, Diamond, Recho, Makomandoo, Chriss Wamalya, Fid Q na mkali wa muziki wa Dancehall, Ragga & Reggae - Shaggy.

NB: Kuanzia saa sita kamili mchana kila nusu saa droo itachezeshwa na mshindi kujinyakulia kitita cha shilingi laki tano taslimu, zoezi hilo la zawadi litadumu hadi itakapotimu saa nane mchana "CHANGAMKIA MZIGO HUO MWANAWANE"

Thursday, June 23, 2011

YANAYOENDELEA SASA KIRUMBA KUELEKEA SERENGETI FIESTA MWANZA

Jukwaa la show kali ya kwanza ya Fiesta 2011 ambalo litatumiwa na mwanamuziki wa kimataifa Shaggy, sanjari na wasanii wengine maarufu hapa nchini Tanzania limeanza kufungwa leo rasmi katika uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza ilikuwa ni majira ya saa 3 asubuhi nalo likifungwa hatua kwa hatua mpaka jioni hii. .

Wataalam wakiwa bize na ramani nzima vichwani mwao...

Mmm Eeeh baba!!

Umeme ni fulu hatukopeshi.

Live toka CCM Kirumba.

Ncha kali akihojiana na msanii chipukizi Ami Kiga aliyesafiri toka mkoani Morogoro hadi Mwanza kwa raslimali zake kwaajili tu! ya kuifuata Fiesta ya 10 na ya kwanza kwa mwaka huu 2011 tarehe 26juni.

Ncha kali, Zamaradi na Babra Hassan wakizijadili sms zilizotumwa na wasikilizaji kuhusu msanii huyo chipukizi ambapo... mwisho wa siku alifanikiwa kupata chansi kutinga fiesta, kutokana na sms za watu kumtaja kuwa anastahili.

NB:

Wednesday, June 22, 2011

MISS MWANZA KUPATIKANA IJUMAA HII

Hatimaye Zawadi za washindi wa Vodacom Miss Mwanza 2011, zimetangazwa leo katika ukumbi wa Hoteli mpya ya Gold Crest iliyopo katikati ya jiji la Mwanza. Akitangaza zawadi hizo Katibu wa Sisi Entertainment Mukhsin Mambo maarufu Mc Stopper ameeleza, kifuta jasho kwa washiriki nafasi ya sita hadi ya kumi na nne watapata Tsh. 100,000/=

Nafasi ya Tano- 200,000/= Nafasi ya Nne- 200,000/= nafasi ya Tatu- 300,000/= Nafasi ya Pili- 500,000/= na Vodacom Miss Mwanza 2011- 1,000,000/=

Matembezi na elimu ya Vodacom.

Wakipata maelezo Idara kwa idara..

Hii ni kwa mara ya kwanza kwa Miss Mwanza kuzawadiwa donge nono la Tshs. 1,000,000/=

Mara baada ya warembo hao kupata fursa ya kutembelea ofisi za Vodacom Mwanza kushuhudia shughuli zinazofanywa katika ofisi hizo walipiga picha ya pamoja nje ya ofisi za Vodacom Mwanza.

OLIVER 'TUKU' MTUKUDZI KUACHIA ALBAMU YAKE YA 56, JULY, 2011

(Msanii kutoka nchini Zimbabwe, Oliver 'Tuku' Mtukudzi akiwa katika picha ya pamoja na mlogishaji, Cathbert Angelo).

Msanii nguli barani afrika anayetokea nchini Zimbabwe Oliver 'Tuku' Mtukudzi anatarajia kuachia albamu yake ya 56 ifikapo mwezi wa saba.

Akizungumza na blog hii alipokuwa ametembelea nchini kwa ajili ya ufunguzi wa tamasha la Zanzibar filamu lijulikanalo kama 'ZIFF' lililozinduliwa June 18, na kuendelea mpaka tarehe June 24, 2011, msanii huyo alisema kuwa mpaka sasa anaalbamu zipatazo 55.

'Nimeshatoa albamu zipatazo 55 na zote zipo sokoni na zinafanya vizuri japo sikumbuki nyimbo zake zote, albamu ambazo ninazo mpaka sasa ni 1978 Ndipeiwo Zano (re-released 2000), 1979 Chokwadi Chichabuda, 1979 Muroi Ndiani?, 1980 Africa (re-released 2000), 1981 Shanje, 1981 Pfambi, 1982 Maungira, 1982 Please Ndapota, 1983 Nzara, 1983 Oliver's Greatest Hits, 1984 Hwema Handirase, 1985 Mhaka, 1986 Gona. Nyingine ni 1986 Zvauya Sei?, 1987 Wawona, 1988 Nyanga Yenzou, 1988 Strange, Isn't It?, 1988 Sugar Pie, 1989 Grandpa Story, 1990 Chikonzi, 1990 Pss Pss Hallo!, 1990 Shoko, 1991 Mutorwa, 1992 , 1992 Rumbidzai Jehova, 1992 Neria Soundtrack, 1993 Son of Africa, 1994 Ziwere MuKobenhavn, 1995 Was My Child, 1996 Svovi yangu.

Aliongeza albamu nyingine ni 1995 The Other Side: Live in Switzerland, 1997 Ndega Zvangu (re-released 2001), 1998 Dzangu Dziye, 1999 Tuku Music, 2000 Paivepo, 2001 Neria, 2001 Bvuma (Tolerance), 2002 Shanda soundtrack, 2002 Vhunze Moto, 2003 Shanda (Alula Records), 2003 Tsivo (Revenge), 2004 Greatest Hits Tuku Years, 2004 Mtukudzi Collection 1991-1997, 2004 Mtukudzi Collection 1984-1991, 2005 Nhava, 2006 Wonai, 2007 Tsimba Itsoka, 2008 Dairai (Believe), 2010 Rudaviro, 2010 Kutsi Kwemoyo (compilation) na 2011 Rudaviro. Nilipomuuliza ni tuzo ngapi ambazo amezipata tokea ameanza muziki? msanii huyu alisema kuwa yeye huwa haesabu na wala hana takwimu yoyote, kwa vile ni nyingi na huwa hajali kwa vile yeye anachojali ni kuchaguliwa kwani hiyo ndiyo heshima kwake.

'Wasanii wengi huwa wanajali sana tuzo bila kujali suala la kuchaguliwa, ni heshima tosha maana inaonyesha ni jinsi gani watu waliweza kukuthamini,' alisema Oliver Mtukudzi.

Oliver "Tuku" Mtukudzi (amezaliwa mnamo 22 Septemba, 1952 mjini Highfield, Harare) ni mwanamuziki wa Kizimbabwe. Oliver ni miongoni mwa wanamuziki walio maarufu kwa muda mrefu sana katika nchi hiyo ya Zimbabwe. Na alianza shughuli za muziki kunako miaka ya 1977 pale alipojiunga na bendi ya Wagon Wheels, ambayo pia alikuwemo na mwanamuziki wa zamani Bw. Thomas Mapfumo.

Nyimbo ya kwanza ilikuwa "Dzandimomotera" iliyoheshimika sana, na hapo ndipo Tuku alipotoa albamu yake ya kwanza, nayo pia ilileta mafanikio makubwa kabisa. Mtukudzi nae pia ni mmoja wa wanakundi la Mahube, kundi la muziki la nchi za Afrika ya Kusini.

Tuesday, June 21, 2011

ZIMEBAKI SIKU TANO TU! HAINA MAJOTROOOOO!!!!

'''Chuki zenu hatuzisikii, hatuongei, na wala hatuoni....EEeeeh'''

Paparazi.

Ni pilikapilika za show kubwa kuliko zote hapa nchini SERENGETI FIESTA 2011 inayoanzia jiji la Miamba Mwanza 'Mtu mzima Shaggy in tha house' siku ya jumapili ya tarehe 26 juni pichani toka shoto ni Zamaradi, G.Sengo na Baba Johnii aka Mchomvu ndani ya 88.1 leo mchana.

Street pande za Kirumba Mwanza.
Wakazi wa Rock City wameonekana katika pilika za huku na huko madukani kujinunulia mavazi kuhakikisha kuwa wanashaini ile kisawasawa kuilaki burudani ya kweli ile hali upande wa watoa huduma mbalimbali iwe za mahoteli, malazi, chakula, wadau wa usafiri maduka ya mavazi na kadhalika wao wameahidi kutoa huduma safi katika kipindi hiki cha matayarisho hata kwa siku husika.

BALIMI TRADITIONAL DANCE COMPETITION IN MWANZA.

Special Event Erick Mwayela congratulates Godifrey Majula after his group Utandanazi Cultural Group from Ukerewe emerged the winner receiving Tshs 500,000/=, the second winner were Mang’ombega Kijiji from Misungwi received Tshs 400,000/=, the third were Angano Cultural Group from Ilemela Mwanza received Tshs 300,000/=. The fourth were Chapakazi from Nyamagana Mwanza and fifth were Makumbusho from misungwi.

Balimi Traditional Dance committee from left Head of Culture lake zone Mufungo P. Mufungo, Cultural Officer Mwanza Makenke, TBL Sales Manager Andrew Mbwambo, Special Event Erick Mwayela and judges from butimba.

Utandanazi Group from Ukerewe showed why they deserved to be the winners.

Mwanalyaku Group from Magu performing during the Balimi Traditional Dance 2011 held at CCM Kirumba Stadium on 18/6/2011.

Utandanazi Group in action.

TIGO YACHEZESHA DROO YA KWANZA YA KUMPATA MSHINDI WA PROMOSHENI YA ENDESHA PIKIPIKI NA TIGO

Afisa Uhusiano wa Kampuni ya Tigo Jackson Mmbando (kulia) wakati wa kuchezesha droo ya kwanza ya kumpata mshindi wa promosheni ya Endesha Pikipiki na Tigo jana jijini Dar es Salaam. Wengine ni Catherine Kasimbazi wa Solid Ltd, Pamela Shelukindo kutoka Tigo na Humudi Abdulhussein kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha.

UTUMISHI WA UMMA

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na baadhi ya washiriki wa mkutano wa Utumishi wa Umma kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es salaam. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

20 JUNE'' SIKU YA KUZALIWA CEDRICK A. G. SENGO

Cedrick akiwa amembeba mtoto. .

Cedrick na darasa lake...

Kata keki tuleeee...kata keki tuleeee...

Cedrick akimlisha keki mdogo wake Obama ambaye alifika shuleni hapo kumpatia sapraiz hiyo...

Ikafuata zamu ya mwenye birthday.

Akimlisha moja ya marafiki zake.

Zamu ya mwalimu wake.

Mwalimu wa darasa.

Teachers...

Hatimaye keki hiyoooo ikafika ofisi za Mkuu wa Shule Alliance Schools.

Cedrick na Class mate wake.

"Mwanangu nakupenda, Zingatia elimu"
*from your Mom*
Oliver