ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, June 22, 2011

OLIVER 'TUKU' MTUKUDZI KUACHIA ALBAMU YAKE YA 56, JULY, 2011

(Msanii kutoka nchini Zimbabwe, Oliver 'Tuku' Mtukudzi akiwa katika picha ya pamoja na mlogishaji, Cathbert Angelo).

Msanii nguli barani afrika anayetokea nchini Zimbabwe Oliver 'Tuku' Mtukudzi anatarajia kuachia albamu yake ya 56 ifikapo mwezi wa saba.

Akizungumza na blog hii alipokuwa ametembelea nchini kwa ajili ya ufunguzi wa tamasha la Zanzibar filamu lijulikanalo kama 'ZIFF' lililozinduliwa June 18, na kuendelea mpaka tarehe June 24, 2011, msanii huyo alisema kuwa mpaka sasa anaalbamu zipatazo 55.

'Nimeshatoa albamu zipatazo 55 na zote zipo sokoni na zinafanya vizuri japo sikumbuki nyimbo zake zote, albamu ambazo ninazo mpaka sasa ni 1978 Ndipeiwo Zano (re-released 2000), 1979 Chokwadi Chichabuda, 1979 Muroi Ndiani?, 1980 Africa (re-released 2000), 1981 Shanje, 1981 Pfambi, 1982 Maungira, 1982 Please Ndapota, 1983 Nzara, 1983 Oliver's Greatest Hits, 1984 Hwema Handirase, 1985 Mhaka, 1986 Gona. Nyingine ni 1986 Zvauya Sei?, 1987 Wawona, 1988 Nyanga Yenzou, 1988 Strange, Isn't It?, 1988 Sugar Pie, 1989 Grandpa Story, 1990 Chikonzi, 1990 Pss Pss Hallo!, 1990 Shoko, 1991 Mutorwa, 1992 , 1992 Rumbidzai Jehova, 1992 Neria Soundtrack, 1993 Son of Africa, 1994 Ziwere MuKobenhavn, 1995 Was My Child, 1996 Svovi yangu.

Aliongeza albamu nyingine ni 1995 The Other Side: Live in Switzerland, 1997 Ndega Zvangu (re-released 2001), 1998 Dzangu Dziye, 1999 Tuku Music, 2000 Paivepo, 2001 Neria, 2001 Bvuma (Tolerance), 2002 Shanda soundtrack, 2002 Vhunze Moto, 2003 Shanda (Alula Records), 2003 Tsivo (Revenge), 2004 Greatest Hits Tuku Years, 2004 Mtukudzi Collection 1991-1997, 2004 Mtukudzi Collection 1984-1991, 2005 Nhava, 2006 Wonai, 2007 Tsimba Itsoka, 2008 Dairai (Believe), 2010 Rudaviro, 2010 Kutsi Kwemoyo (compilation) na 2011 Rudaviro. Nilipomuuliza ni tuzo ngapi ambazo amezipata tokea ameanza muziki? msanii huyu alisema kuwa yeye huwa haesabu na wala hana takwimu yoyote, kwa vile ni nyingi na huwa hajali kwa vile yeye anachojali ni kuchaguliwa kwani hiyo ndiyo heshima kwake.

'Wasanii wengi huwa wanajali sana tuzo bila kujali suala la kuchaguliwa, ni heshima tosha maana inaonyesha ni jinsi gani watu waliweza kukuthamini,' alisema Oliver Mtukudzi.

Oliver "Tuku" Mtukudzi (amezaliwa mnamo 22 Septemba, 1952 mjini Highfield, Harare) ni mwanamuziki wa Kizimbabwe. Oliver ni miongoni mwa wanamuziki walio maarufu kwa muda mrefu sana katika nchi hiyo ya Zimbabwe. Na alianza shughuli za muziki kunako miaka ya 1977 pale alipojiunga na bendi ya Wagon Wheels, ambayo pia alikuwemo na mwanamuziki wa zamani Bw. Thomas Mapfumo.

Nyimbo ya kwanza ilikuwa "Dzandimomotera" iliyoheshimika sana, na hapo ndipo Tuku alipotoa albamu yake ya kwanza, nayo pia ilileta mafanikio makubwa kabisa. Mtukudzi nae pia ni mmoja wa wanakundi la Mahube, kundi la muziki la nchi za Afrika ya Kusini.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.