ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, September 6, 2024

Darassa & Harmonize - Mazoea (Visualiser)

 Music by Darassa & Harmonize performing "MAZOEA", Conveys a powerful message about the strength of love and the memories it leaves behind in a relationship. The chorus reminds us that while love may fade, the habits and memories shared by lovers remain, often becoming the source of true sorrow. The song is filled with a sense of regret and carries a message of seeking forgiveness in the hope of rekindling the relationship. Audio produced by Abbah process & Visual shot by Mbongo.

MAMA KOKA AUNGANA NA RAIS SAMIA KUBORESHA SEKTA YA ELIMU SHULE YA MSINGI BOKO TIMIZA

 


NA VICTOR MASANGU,KIBAHA


Mke wa Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini Mama Selina Koka aunga mkono juhudi za Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan katika kuboresha sekta  ya elimu  ameahidi kuchangia viti na meza kwa ajili ya walimu wa shule ya msingi Boko Timiza.

Mama Koka  ametoa kauli hiyo wakati wa sherehe ya mahafali kwa wanafunzi wa liohitimu darasa la saba katika shule ya msingi Boko Timiza iliyopo Kata ya Tumbi Wilaya ya Kibaha.

Mama Koka amesema kwamba licha ya kuahidi kuchangia viti na meza pia amechangia matofali  500 kwa ajili ya kuendeleza mradi wa ujenzi wa madarasa katika shule.

"Nimesikia risala yenu na mimi kama mke wa Mbunge  nipo pamoja na nyinyi na nitasaidia viti na meza pamoja na matofali 500 ambayo yatasaidia katika mradi unaondelea wa madarasa.
Aidha Mama Koka amesema Mbunge anatambua elimu ni ufunguo wa maisha hivyo ataendelea  kushirikiana bega kwa bega katika kuiboresha zaidi shule ya msingi Boko Timiza ili iwe katika mindombinu  mizuri.

Kadhalika aliwahimiza wazazi na walezi kuwalinda na kuwatunza watoto wao ikiwa pamoja na kuwapatia malezi bora,maadili pamoja na kuwapatia mahitaji mbali mbali ya msingi.

Kwa upande wake Mkuu wa shule hiyo  Ramadhani Mfinanga amempongeza kwa dhati Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini kwa kuweza kuchangia kiasi cha shilingi milioni 2 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa.

Pia amemebainisha kwamba  kwa sasa shule hiyo ambayo imeanzishwa mnamo mwaka 1978 ambapo kwa sasa  ina jumla ya ya wanafunzi wapatao 75 ambapo ina madarasa 7 kwa ajili ya kusomea wanafunzi.



Naye  mmoja wa wanafunzi katika shule hiyo  Nuru akisoma risala kwa niaba ya wanafunzi wenzake amebainisha kwamba bado shule hiyi inakabiliwa na changamoto ya madarasa ikiwa pamoja na uhaba wa matundu ya vyoo.

Shule ya msingi Boko Timiza ambayo ipo katika Halmashauri ya Wilaya Kibaha mjii  imeanzishwa tangu 1978 lakini  bado inakabiliwa na changamoto mbali mbali ambazo zinahitajika juhudi za makusudi katika kuzitafutia ufumbuzi.

Thursday, September 5, 2024

WAHAMASISHWA KUTUMIA NISHATI SAFI ZA KUPIKIA

 


Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inaendelea kuhamasisha wananchi kutumia Nishati Safi za Kupikia kwa lengo la kuwezesha utunzaji wa mazingira, kuboresha afya na ustawi wa jamii sambamba na kukuza uchumi wa mwananchi mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla.

 

Mhandisi wa Miradi kutoka REA, Mhandisi Kelvin Tarimo amesema hayo hivi leo Septemba 04, 2024 Jijini Dodoma alipokuwa akiwasilisha mada ya Nishati Safi ya Kupikia kwa wanawake zaidi ya 650 katika Mkutano Mkuu wa kwanza wa Mtandao wa Wanawake wa Jeshi la Magereza.

 


“Matumizi ya Nishati Safi za Kupikia ni ajenda inayolenga kukabiliana na ongezeko la uharibifu wa mazingira pamoja na athari za kimabadiliko ya tabianchi pamoja na athari za kiafya zinazotokana na matumizi ya nishati zisiyo safi za kupikia,” amesema Mhandisi Tarimo.

 

Alifafanua kuwa matumizi ya Nishati zisizo safi na salama za kupikia huchangia uharibifu wa mazingira ambapo alibainisha kuwa inakadiriwa zaidi hekari zipatazo Laki Nne za misitu hukatwa kila mwaka kwa ajili ya shughuli mbalimbali za kibinadamu ikiwemo matumizi ya kuni na mkaa jambo ambalo alisema limekua likisababisha madhara mbalimbali ya kimazingira ikiwemo uharibifu wa vyanzo vya maji na ikolojia kwa ujumla.

 


Mhandisi Tarimo alisema katika kukabiliana na hali hiyo, Wakala kama moja ya mdau mkuu wa masuala ya Nishati Vijijini itaendelea kuhakikisha inatimiza vyema lengo kuu la utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia 2024-2034 ambao umelenga hadi kufikia Mwaka 2034 asilimia 80 ya wananchi wawe wanatumia Nishati Safi za Kupikia. 

 

Amesema REA imejipanga kuhakikisha adhma hiyo inafikiwa kikamilifu kwa kuwezesha utekelezaji wa miradi mbalimbali ya Nishati Safi ya Kupikia na amewasisitiza wananchi hususan wanawake kuendelea kuchangamkia fursa mbalimbali zilizopo kwenye mnyororo mzima wa thamani wa masuala ya Nishati Safi ya Kupikia.

 


“Hatua tunazoendelea nazo sasa ni pamoja na kuongeza uelewa kwa wananchi kuhusu umuhimu wa matumizi ya Nishati Safi za Kupikia; kuhakikisha upatikanaji wa Nishati Safi, nafuu, endelevu na za uhakika za Kupikia kote nchini haswa maeneo ya vijijini na kuhamasisha Uwekezaji katika Sekta Ndogo ya Nishati Safi ya Kupikia,” amefafanua Mhandisi Tarimo.


KOKA KUIPIGA JEKI SHULE YA MSINGI TUMBI KATIKA KUBORESHA MIUNDOMBINU

 


NA VICTOR MASANGU,KIBAHA 


Shule ya msingi Tumbi iliyopo katika Halmashauri  Kibaha mji kwa sasa bado inakabiliwa na changamoto mbali mbali ikiwemo kutokuwa na bwalo la kulia chakula,uhaba wa kompyuta  pamoja na upungufu mkubwa wa matundu ya vyoo 21.

Hayo yamebainika wakati wa halfa ya mahafali ya 53 kwa wanafunzi wa darasa la saba waliohitimu  katika shule ya msingi Tumbi na kuhudhuliwa na viongozi mbali wa chama,serikali pamoja na wazazi na walezi wa wanafunzi.

Katika kuliona hilo Mbunge Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini Mhe.Silvestry Koka ameamua kulivalia njuga suala hilo la kuahidi kulitafutia ufumbuzi suala hilo ili kuwawekea wanafunzi mazingira mazuri ya kujisomea.

Koka amebainisha kwamba lengo lake kubwa ni kuboresha kiwango cha elimu na kwamba atatumia fedha za mfumo wa Jimbo kwa ajili ya kutatua changamoto hiyo ya matundu ya vyoo katika shule hiyo.

"Nimesikiliza  risala yenu kuhusiana na suala la changamoto ya uhaba wa matundu ya vyoo na mm kama Mbunge wenu nitatumia fedha za mfuko wa Jimbo kwa lengo la kuweza  kukabiliana na changamoto zilizopo katika shule hii,"alisema Mhe.Koka 

Alisema kwamba pamoja na kupambania suala la miundombinu ya vyoo pia ataisaidia shule hiyo kuwatafutia wadau mbali mbali wa maendeleo katika kuwasaidia kuwapatia kompyuta ili wanafunzi kupata fursa ya kujifunza zaidi.

Mbunge huyo pia alimshukuru Rais wa awamu ya sita Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuweza  kutenga fedha ambazo zimekwenda kutekeleza miradi mbali mbali ya maendeleo.

Aidha alisema kwa kipindi cha kipindi cha miaka mitatu katika Jimbo la Kibaha mjini limeweza kupata fedha ambazo zimeza kufanikisha ujenzi wa shule mpya saba zikiwemo za Sekondari na msingi.

Katika hatua nyingine Koka amewahimiza wazazi na walezi kuwalinda watoto wao katika suala zima la malezi ikiwa sambamba na  kuchangia suala la chakula cha mchana kwa wanafunzi.

Kwa upande wake mkuu wa shule ya Tumbi Jane Moses  ametoa pongezi kwa Mbunge kwa kuweza kuonyesha ushirikiano wa kutosha katika suala zima la kuboresha sekta ya elimu.

Naye Mkurugenzi wa Shirika la elimu Kibaha Robert Shiringi amempongeza Rais Samia pamoja na Mbunge kwa kuweza kutekeleza ilani  ya chama kwa vitendo katika nyanja mbali mbali.

Shiringi amebainisha kwamba katika kipindi cha miaka mitatu kuna hatua kubwa ya kimaendeleo ambayo imefanyika katika Halmashauri ya mji Kibaha ikiwemo sekta ya afya,maji,elimu pamoja na miundombinu ya barabara.

Monday, September 2, 2024

MBUNGE KOKA APANIA KUWAINUA KIUCHUMI UVCCM KUPITIA MRADI WA KAMPUNI

 


NA VICTOR MASANGU, KIBAHA

 
Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini Silvestry Koka katika kuleta mabadiliko chanya ya kimaendeleo amepania kuwainua vijana na kuwaondoa katika wimbi la umasikini kwa kuwachangia gharama mbali mbali kwa ajili ya kuanzisha kampuni ya  umoja wa vijana wa (UVCCM) Wilaya ya Kibaha mjni ambayo itawasaidia katika kujikwamua kiuchumi.

Koka ametoa kauli hiyo wakati wa kikao cha baraza la UVCCM Wilaya ya Kibaha mjini na kusema kwamba amekubali kwa moyo mmoja kuwaunga mkono juhudi ambazo zinafanywa na vijana hao ya kutaka kuanzisha kampuni ambayo itakuwa  ikijikita zaidi katika shughuli mbali mbali.

Alibainiwa kwamba lengo lake kubwa ni kuhakikisha anaweka mipango madhubuti kwa vijaana hao kuweza kuwa na miradi mbali mbali ya kimaendeleo hivyo atachangia gharama mbali mbali ambazo zitahitajika ikiwemo kufanya usajili wa kampuni hiyo ambayo itaweza kuwa ni mkombozi mkubwa kwa vijana hao.

"Vijana  mimi kama mbunge wenu nipo pamoja na nyinyi na Risala yenu nimeisikia ya kutaka kuwa na kampuni ambayo itakuwa ikifanya shughuli mbali mbali kwa hiyo mimi nitachangia  gharama mbali mbali ikiwemo kampuni hiyo kupata usajili na nina imani kwamba taratibu zote zikikamilika kampuni hiyo itaanza kufanya kazi kwa maslahi mapana ya vijana wa jimbo la  Kibaha mjini,"alisema Koka

Aidha Mbunge huyo aliwataka vijana hao kuhakikisha wanakuwa kitu kimoja na kuachana kabisa na kuwa na makundi hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa ambao unatarajiwa kufanyika Novemba 27 mwaka huu kwani lengo ni kuweza kushinda katika mitaa yote 73.


 Kadhalika  Mbunge Koka  amewasihi vijana kufanya kazi zao kwa ushirikiano ikiwa pamoja na  kuheshimu viongozi mbali mbali wa chama na serikali walioko madarakani kwa ngazi zote za kiutawala na kutengeneza misingi imara ya kuwa karibu na jamii kwa makundi yote bila ya kuwa na ubaguzi wowote.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa UVCCM  Wilaya ya Kibaha mjini Ramadhani Kazembe amesema kwamba malengo ambayo wamejiwekea ni kubuni miradi mbali mbali ya kimaendeleoambayo itaweza kuwasaidia vijana kuondokana na umasikini ikiwa pamoja na kujiongezea kipato.

Kazembe alisema kwamba ana imani kubwa kampuni hiyo pindi itakapokamilika itakuwa ni moja ya fursa ya kipekee kwa vijana wa UVCCM kuweza kupata fursa za ajili kutokana na  shughuli mbali mbali ambazo zitakuwa zikifanyika na kuwahimiza vijana waweze kuwa na umoja na mshikamano katika kukijenga chama pamoja na jumuiya zake zote.



Sunday, September 1, 2024

CRDB Bank Foundation yazindua Kampeni ya Kuwaunganisha Wajasiriamali Wadogowadogo nchini na programu ya IMBEJU

 

  
Dar es Salaam, 30 Agosti 2024 – Taasisi ya CRDB Bank Foundation imezindua rasmi kampeni maalum ya IMBEJU inayolenga kuwaunganisha vijana na wanawake wajasiriamali nchini na programu ya IMBEJU. Hafla hiyo ya uzinduzi ilifanyika katika Makao Makuu ya Benki ya CRDB, na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali pamoja na washirika wa programu hiyo.

Akizungumza Mkurugenzi wa Wateja Wadogo na Wakati wa Benki ya CRDB, Bonaventura Paul, ambaye aliipongeza CRDB Bank Foundation kwa kuja na kampeni hiyo iliyopewa jina la ‘IMBEJU Uwezeshaji’ ambayo inalenga kuwafikia wajasirimiali wadogo wadogo kote nchini hususani wale walio maeneo ya pembezoni na vijijini jambo ambalo litasaidia si tu kukuza ujumuishi wa kifedha bali pia kukuza sekta ya ujasiriamali na uchumi wa Taifa kwa ujumla.
"Huduma za kifedha zina mchango mkubwa katika maendeleo ya kiuchumi, na ndio maana Benki ya CRDB imekuwa mstari wa mbele kubuni bidhaa na huduma zinazolenga makundi mbalimbali ya jamii. 
 
Tunajivunia kuwa sehemu ya kampeni hii inayoendeshwa na wenzetu wa CRDB Bank Foundation ambayo tunaamini itakwenda kukuza ujumishi kwa wanawake na vijana wengi ambao ndio sehemu kubwa ya wajasiriamali nchini," alisema Bonaventura.
Aidha, Bonaventura amewataka wanawake na vijana wajasiriamali kote nchini kujiunga na programu ya IMBEJU ili kukuza na kuboresha biashara zao huku akieleza kuwa katika matawi yote ya Benki ya CRDB zaidi ya 260 kuna dirisha maalum kwa ajili ya programu hiyo.

"Malengo yetu ni kuwa baada ya kuhitimu programu hii, wataweza Kuunganishwa na uwezeshaji kupitia Benki yao ya CRDB ambapo kupitia Idara yetu ya Wateja Wadogo na Wakati wataweza kukopeshwa hadi shilingi bilioni 3 kulingana na uwezo wa ulipaji wa biashara zao," aliongeza.
Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Foundation, Fadhil Bushagama, ameeleza kuwa kampeni hiyo ya IMBEJU Uwezeshaji ni sehemu ya juhudi za taasisi hiyo katika kukuza ujumuishi wa kifedha na kiuchumi ili kuboresha maisha ya vijana na wanawake wajasiriamali.

"Programu ya IMBEJU imeleta mapinduzi makubwa katika kuchochea ujumuishi wa kifedha, ambapo zaidi ya wanawake na vijana wajasiriamali 600,000 wamefikiwa na mitaji wezeshi ya zaidi ya shilingi bilioni 11 imetolewa," alisema Bushagama.
Bushagama amesema awamu ya kwanza ya kampeni ya ‘IMBEJU Uwezeshaji’ inatarajiwa kuanzia Kanda ya Nyanda za Juu katika mikoa ya Mbeya, Songwe, Ruvuma, Njombe, Katavi, na Rukwa ambapo wajasiriamali zaidi ya 12,000 na vikundi vya wajasiriamali 1,000 vinatarajiwa kufikiwa.

“Timu yetu kutoka Makao Makuu kwa kushirikiana na matawi ya Benki yetu ya CRDB katika mikoa hiyo, pamoja na Maafisa Maendeleo ya Jamii tutashirikiana kwa pamoja kutoa elimu ya fedha, mafunzo ya biashara na ujasirimali. Baada ya kanda hiyo tutakwenda Kanda ya Kusini na Kanda ya Kati,” aliongezea Bushagama.
Akitoa shukrani kwa washirika wa programu ya IMBEJU, Bushagama ameishukuru Serikali chini ya uongozi wa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuweka sera na mazingira wezeshi ya uwezeshaji wa vijana na wanawake nchini. 
 
Amesema Serikali kupitia Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake, Watoto, na Makundi Maaulum pamoja na Wizara ya TAMISEMI imekuwa mshirika wa karibu katika utekelezaji wa programu ya IMBEJU.






MATI SUPER BRANDS LTD YAPEWA TUZO MAALUMU NA CHUO CHA UKAMANDA NA UNADHIMU (CSC) CHA JWTZ


Na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG.

Kampuni ya Mati Super Brands Limited inayozalisha vinywaji changamshi yenye makao yake Makuu Mjini Babati Mkoani Manyara imepewa tuzo ya maalumu kutoka Chuo cha Ukamanda na Unadhimu (CSC) cha Jeshi la Wananchi wa Tanzania kwa kutambua mchango wa kampuni hiyo katika kusaidia jamii inayowazunguka pamoja na kushirikiana na taasisi mbali mbali za kiserikali.

Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa tuzo hiyo na Mwakilishi wa Mkuu wa Chuo cha Ukamanda na Unadhimu (CSC) chenye makao yake Mkoani Arusha, Colonel Verus Chrysostom Mbuzi katika ziara maalumu ya kimafunzo iliyofanywa na Maafisa hao wa ngazi za juu wa Kijeshi kutoka mataifa mbali mbali katika kampuni ya Mati Super Brands Ltd.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mati Super Brands Limited, David Mulokozi ametoa shukrani zake kwa Chuo hicho cha kijeshi kwa kutambua mchango wa kampuni hiyo katika masuala mbali mbali ikiwemo kurudisha sehemu ya faida wanayoipata kwa jamii inayowazunguka.

Mulokozi amesema kuwa Tuzo hiyo inawapa chachu ya kuendelea kufanya vizuri kuendelea kushirikiana na taasisi za umma pamoja na kuzalisha bidhaa bora zinazozingatia ubora na usalama wa mtumiaji.

Mwakilishi wa Mkuu wa Chuo cha Ukamanda na Unadhimu (CSC) , Colonel Verus Chrysostom Mbuzi amepongeza Kiwanda kwa kuwa karibu na jamii na taasisi za serikali pamoja na kutoa fursa wa mafunzo kwa vitendo vya Maafisa wa Kijeshi juu ya masuala mbali mbali ikiwemo usalama wa chakula .