NA ALBERT G. SENGO/MWANZA
Hayawi hayawi sasa yamekuwa hatimaye zile mbio za riadha zijulikanazo kama Transec Lake Victoria Marathon inakwenda kushika kasi yake kesho Jumapili Julai 02, 2023 jijini Mwanza. Hilda Viggo ni mratibu wa Transec Lake Victoria Marathon anasema mpaka sasa watu 1380 wamekwisha jiandikisha kwenye ushiriki wa mbio hizo, mwamko umekuwa mkubwa tofauti na miaka miwili iliyopita huu ukiwa mwaka wa 3unaoshuhudia mapinduzi makubwa hasa ya maandalizi, ubora wa tuzo na uwekaji wa kumbukumbu. Kwa mwaka huu 2023 Transec Lake Victoria Marathon imekuja ikilenga kuhamasisha utalii wa ndani, uhifadhi wa Ziwa Victoria pamoja na kusaidia matibabu ya watoto wanaotibiwa saratani katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando.
WAZIRI KIKWETE: MFUMO MPYA KUWEZESHA WATANZANIA KUPATA FURSA ZA AJIRA NJE
YA NCHI
-
Na Mwandishi Wetu; Dodoma
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Watu Wenye
Ulemavu, Mhe. Ridhiwani Kikwete, amesema katika mwaka wa...
2 hours ago