NA ALBERT G. SENGO/MWANZA
Hayawi hayawi sasa yamekuwa hatimaye zile mbio za riadha zijulikanazo kama Transec Lake Victoria Marathon inakwenda kushika kasi yake kesho Jumapili Julai 02, 2023 jijini Mwanza. Hilda Viggo ni mratibu wa Transec Lake Victoria Marathon anasema mpaka sasa watu 1380 wamekwisha jiandikisha kwenye ushiriki wa mbio hizo, mwamko umekuwa mkubwa tofauti na miaka miwili iliyopita huu ukiwa mwaka wa 3unaoshuhudia mapinduzi makubwa hasa ya maandalizi, ubora wa tuzo na uwekaji wa kumbukumbu. Kwa mwaka huu 2023 Transec Lake Victoria Marathon imekuja ikilenga kuhamasisha utalii wa ndani, uhifadhi wa Ziwa Victoria pamoja na kusaidia matibabu ya watoto wanaotibiwa saratani katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando.
MONGELLA ATOA WITO WA AMANI KWA WANA~CCM UCHAGUZI MKUU 2025
-
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, Ndugu John Mongella,
amewataka wanachama wa chama hicho kudumisha amani na utulivu kuelekea
Uchaguzi M...
11 minutes ago