ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, July 1, 2023

MBIO KUBWA KULIKO ZOTE KANDA YA ZIWA KUKIWASHA JUMAPILI HII 02 july 2023 MWANZA

 NA ALBERT G. SENGO/MWANZA

Hayawi hayawi sasa yamekuwa hatimaye zile mbio za riadha zijulikanazo kama Transec Lake Victoria Marathon inakwenda kushika kasi yake kesho Jumapili Julai 02, 2023 jijini Mwanza. Hilda Viggo ni mratibu wa Transec Lake Victoria Marathon anasema mpaka sasa watu 1380 wamekwisha jiandikisha kwenye ushiriki wa mbio hizo, mwamko umekuwa mkubwa tofauti na miaka miwili iliyopita huu ukiwa mwaka wa 3unaoshuhudia mapinduzi makubwa hasa ya maandalizi, ubora wa tuzo na uwekaji wa kumbukumbu. Kwa mwaka huu 2023 Transec Lake Victoria Marathon imekuja ikilenga kuhamasisha utalii wa ndani, uhifadhi wa Ziwa Victoria pamoja na kusaidia matibabu ya watoto wanaotibiwa saratani katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.