ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, August 29, 2015

MAGUFULI AMJULIA HALI NA KUMPA POLE MEYA WA JIJI LA MBEYA MH ATHANAS KAPINGA BAADA YA KUPATA AJALI

 
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi (CCM),Ndugu John Pombe Magufuli akimjulia hali na kumpa pole aliyekuwa Meya wa jiji la Mbeya Mh.Athanas Kapunga aliyepata ajali wilayani Momba mkoani Mbeya wakati wa mbio za maandalizi ya Kampeni hivi karibuni,Mh Kapunga amelazwa kwenye chumba maalum cha wagonjwa  mahututi (ICU) katika hospitali ya Rufaa mjini humo.
 Mmoja wa Wauguzi walioko kwenye chumba maalum cha wagonjwa  mahututi (ICU),akimpa maelezo mafupi Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi (CCM),Ndugu John Pombe Magufuli alipokwenda kumjulia hali n kumpa pole aliyekuwa Meya wa jiji la Mbeya Mh.Athanas Kapunga aliyepata ajali wilayani Momba mkoani Mbeya wakati wa mbio za maandalizi ya Kampeni hivi karibuni.
 Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi (CCM),Ndugu John Pombe Magufuli akisalimiana na baadhi ya Wauguzi walioko katika chumba maalum cha wagonjwa mahututi (ICU) katika hospitali ya Rufaa Mbeya,mara baada ya kumjulia hali na kumpa pole aliyekuwa Meya wa jiji la Mbeya Mh.Athanas Kapunga aliyepata ajali wilayani Momba mkoani Mbeya wakati wa mbio za maandalizi ya Kampeni hivi karibuni.
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi (CCM),Ndugu John Pombe Magufuli akisalimiana na Mke wa Meya Mama Kapinga mara baada ya kutoka kumjulia hali na kumpa pole aliyekuwa Meya wa jiji la Mbeya Mh.Athanas Kapunga aliyepata ajali wilayani Momba mkoani Mbeya wakati wa mbio za maandalizi ya Kampeni hivi karibuni.

 PICHA NA MICHUZI JR-MBEYA

WHO YATOA DAWA ZA MILIONI 42.2 KUPAMBANA NA KIPINDUPINDU NCHINI

 Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk.Donan Mmbando (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo asubuhi wakati akipokea msaada huo kutoka WHO. Kulia ni Mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Nchini Dk. Rufaro Chatora.
 Taarifa ikitolewa kabla ya kupokea msaada huo.
 Hapa wakitiliana saini mkataba wa kupokea msaada huo.
Mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Nchini Dk. Rufaro Chatora (katikati), akimkabidhi Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk.Donan Mmbando (kushoto), dawa ya maji zenye thamani ya sh.milioni 42.2 zilizotolewa na WHO kwa ajili ya kusaidia kukabiliana na magonjwa ya mlipuko nchini,  Dar es Salaam leo asubuhi. Anayeshuhudia tukio hilo kulia ni Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Uhakiki na Ubora wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk.Mohamed Ali Mohamed.

Na Dotto Mwaibale

SERIKALI imepokea msaada wa dawa ya  kutakasa maji ya Waterguard kutoka Shirika la Afya Duniani (WHO),kwa lengo la kukabiliana na magonjwa ya mlipuko zenye thamani ya sh. milioni 42.

Akizungumza Dar es Salaam leo asubuhi mara baada ya kupokea dawa hiyo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Donan Mmbando, alisema dawa hizo ni waterguard cotton (1000) na Cresol Saponated Liquid (100) litres  ambayo itasaidia kutakasa maji ili kuepusha magonjwa ya mlipuko kama kipindupindu. 

Alisema dawa hiyo itasaidia kudhibiti ugonjwa huo kwani kila siku zinavyozidi kwenda wagonjwa wanazidi kuongezeka hivyo dawa hiyo itatumika kupunguza maambukizi mapya.

"Hali ya mazingira bado hairidhishi idadi ya wagonjwa inazidi kuongezeka hadi sasa, tangu ugonjwa uanze kuripotiwa wagonjwa walioripotiwa kwa Dar es salaam ni 385 na vifo vya watu 8," alisema.

Alitaja mgawanyiko wa wagonjwa katika kila manispaa Kinondoni  292 , Ilala  60 na Temeke 33, aliongeza idadi ya wagonjwa waliopo kwenye kambi za matibabu hadi Agosti 27, jumla ni 74 ambapo kituo cha Mburahati 53 , Buguruni ikiwa na wagonjwa 14 huku Temeke 7.

"Kwa Mkoa wa Morogoro idadi ya wagonjwa hadi Agosti 28, wagonjwa 60 na walioko kambini ni 9 na kifo 1...moja ya sababu ambazo zinachangia kuendelea kua na ugonjwa huu hapa nchini ni kunywa maji yasiyo safi na salama,"alisema.

Mmbando alitoa tahadhali kwa wananchi kujizuia kunywa maji yasiyo safi na salama,kuepuka kula chakula kilichopoa au kuandaliwa katika mazingira yasiyo safi hali hiyo itasaidia kutokomeza ugonjwa huo na kuwataka kuchemsha  maji ya kunywa na kuweka dawa. 

Akikabidhi msaada huo  Mwakilishi Shirika la afya duniani (WHO), Dr. Rufaro Chatora alisema anamini dawa hizo zitasaidia kukabiliana na mlipuko wa ugonjwa wa  kipindupindu.

"Msaada huu tuliyotoa utasaidia wananchi kwa kiasi kikubwa katika kupunguza maambukizo mapya ya ugonjwa huu ambao huwa unaua kwa kiasi kikubwa,"alisema.

MAGUFULI AHIDI KUANZISHA MAHAKAMA YA MAFISADI NA WALA RUSHWA IWAPO ATACHAGULIWA KUWA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA.

 Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi,Dkt John Pombe Magufuli akihutubia maelfu ya wananchi katika viwanja vya Nzovwe mjini Mbeya,kwenye mkutano wa kampeni ya kuwaomba ridhaa Watanzania ya kuwaongoza katika awamu ya tano.

Dkt Magufuli amesema kuwa serikali atakayoingoza atakapopata ridhaa ya kuingia Ikulu,itazifanya huduma za Afya kuwa bora na kuwabana wahudumu wa afya wenye tabia ya kuchukua dawa na kuziuza kwa watu binafsi.

Magufuli ambaye yupo katika mikoa ya Nyanda za juu kusini katika kampeni ya kusaka nafasi ya kuwa raisi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania,amesema suala la afya litakuwa moja ya ajenda zake muhimu atakapoingia madarakani.

Katika hatua nyingine Dkt Magufuli amewaleza wananchi kuwa iwapo watampa ridhaa ya kuiongoza Tanzania,atahakikisha anaanzisha mahakama maalumu ya Mafisadi na Wala rushwa.

PICHA NA MUCHUZI JR-MBEYA.
 Mbunge wa zamani wa jimbo la Kyela Mzee John Mwakipesile akimpigia debe Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Dkt  John Pombe Magufuli wakati mgombea huyo alipofika jimboni humo kuomba kura za wananchi ili wamchague kuwa rais.Mzee Mwakipesile amesema kuwa anamuunga mkono Dkt Magufuli na atahakikisha anashiriki kikamilifu kuhakikisha mgombea huyo anaibuka na ushindi kwa kishindo.
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kyela Dkt Harrison Mwakyembe akimpigia debe Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Dr. John Pombe Magufuli wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika katika viwanja vya Nzovwe mjini Mbeya jionu ya leo.
  Naibu Waziri wa Fedha Mh Mwigulu Nchemba akihutubia katika  mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika viwanja vya Nzovwe mjini Mbeya,ambapo Mwigulu aliwaomba wananchi hao waliojitokeza kwa wingi kumpigia kura za ndio Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli na hatimae aweze kuiongoza Tanzania katika awamu ya tano kwa sababu ana sifa zoto za kuongoza nchi.
 Maelfu ya Wananchi waliojitokeza kwa wingi katika viwanja vya Nzovwe Mbeya jioni ya leo,ambapo Mgombea Urais wa CCM Dkt Magufuli aliwahutubia wananchi hao.
 Naibu Waziri wa Fedha Mh Mwigulu Nchemba akihutubia katika  mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika viwanja vya Nzovwe mjini Mbeya,ambapo Mwigulu aliwaomba wananchi hao waliojitokeza kwa wingi kumpigia kura za ndio Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli na hatimae aweze kuiongoza Tanzania katika awamu ya tano kwa sababu ana sifa zoto za kuongoza nchi.
 Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi,Dkt John Pombe Magufuli akihutubia maelfu ya wananchi katika viwanja vya Nzovwe mjini Mbeya jioni ya leo,kwenye mkutano wa kampeni ya kuwaomba ridhaa Watanzania ya kuwaongoza katika awamu ya tano,Magufuli amewaambia wananchi hao kuwa atahakikisha  huduma za afya zinaimarishwa ipasavyo,katika suala la Elimu Magufu aliwaeleza Wananchi kuwa iwapo watamchagua katika nafasi hiyo ya Urais atahakikisha elimu kuanzia darasa la kwanza mpaka kidato cha nne itatolewa bure,aidha pia amewataka Watanzania kuwa wamoja katika kuhakikisha wanailinda na kuitunza amani iliyopo nchini. 
 Wananchi wakimsikiliza Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli alipokuwa akiwahutubia katika mkutano wa kampeni katika viwanja vya Nzovwe mjini Mbeya. 
 Wafuasi na wapenzi wa chma cha CCM wakishangilia 
Maelfu ya Wananchi waliokusanyika katika viwanja vya Nzovwe mjini Mbeya wakimsikiliza Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika jioni ya leo.
 Jicho la samaki katika ubora wake kwenye mkutano wa kampeni za CCM katika viwanja vya Nzonvwe mjini Mbeya.
 Mmoja wafuasi wa chama cha chadema ambaye aliikabidhi kadi yake kwa Mgombea Urais wa CCM,Dkt John Pombe Magufuli na kutanganza kuhamia chama cha CCM,katika mkutano wa kameni uliofanyika katika uwanja wa Tandale,Tukuyu mjini wilayani Rungwe
 Baadhi ya Wananchama kadhaa wa Chadema wakiwa katika picha ya pamoja na Dkt Magufuli mara baada ya kutangaza rasmi kukihama chama hicho na kujiunga na ccm
 Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli akiwapungia wananchi waliokuwa wamefika katika uwanja wa Tandale mjini Tukuyu kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni.
 Baadhi ya wananchi wa mji wa Kiwila wakiwa wamefunga barabara wakitaka kumsikiliza na kumuona mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli aliyekuwa akipita kuelekea wilayani Kyela kwenye mkutano wa kampeni.
 Heka heka za wafuasi wa CCM
 Wananchi wa Kyela wakiwa wamejitokeza kwa wingi katika uwanja wa John Mwakangale mjini Kyela,kwa ajili ya kumsikiliza Mgombea Urais wa CCM Dkt Magufuli kwenye mkutano wake wa kampeni mjini humo.
 Dkt Magufulia akiwahutubia wananchi wa Kyela mjini Ipinda
 Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Dr. John Pombe Magufuli akimnadi mgombea wa jimbo la Kyela kwa  wananchi wa mji wa Ipinda wilayani Kyela wakati alipofika katika mji huo kufanya mkutano wa kampeni, Dr. John Pombe Magufuli amewaomba wananchi wa Kyela kumpa kura za ndiyo Dr. Harrison Mwakyembe ili  aweze kumtumia mara atakapochaguliwa na kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

 Dkt Magufuli akiwapungia wananchi wa Tukuyu mjini alipowasili mjini humo kuwahutubia wananchi kwenye mkutano wa kampeni.
 Wananchi wakishangilia jambo kwenye mkutano wa kampeni 
 Mh.David Mwakyusa akimwombea kura mgombea Urais wa CCM Dkt Magufuli kwa wananchi ili apate ridhaa ya kuwatumikia wananchi akiwa Ikulu.
 Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli akiwahutubia wananchi wa Tukuyu mjini kwenye kutano wa kampeni uliofanyika katika uwanja wa Tandale mjini gumo.

Friday, August 28, 2015

JUMA AMIR AFUNGUKA JUU TUKIO LILILOMTESA KATIKA MAISHA YAKE YA SOKA

Sehemu ya pili ya mazungumzo yangu na mchezaji wa zamani wa timu za Cop United, Pamba zote za jijini Mwanza pamoja na Simba ya jijii Dare es salaam Juma Amir Maftah al-maarufu kama Pellewa Mwanza, hii hapa. 

Aeleza visa vitamu na vichungu katika soka. 

Jeh Ni tukio gani lililo muumiza na hato lisahau?

Soka la Mwanza limekwama wapi?

Jeh Nani amemuandaa kurithi kipaji chake?

BOFYA PLAY KUSIKILIZA.

MBUNGE WA LUDEWA DEO FILIKUNJOMBE APINGWA KUPITA BILA KUPINGWA MCHAKATO WA UCHAGUZI MKUU

 Mgombea Ubunge Jimbo la Ludewa kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Msambichaka Mkinga (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo asubuhi, wakati akipinga kupitishwa bila kupingwa mgombea mwenzake wa jimbo hilo kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Deo Filikunjombe na kudai kulikuwa na hujuma. Kulia ni Wakili wake, Paulo Kalomo.
  Mgombea Ubunge Jimbo la Ludewa kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Msambichaka Mkinga, akionesha fomu namba 10 ambazo alikabidhi kwa Msimamizi wa Uchaguzi. 
 Wakili wake, Paulo Kalomo, akizungumza katika mkutano huo kuhusu sheria inavyoelekeza.
Wanahabari wakichukua taarifa hiyo.

Na Dotto Mwaibale

MGOMBEA Ubunge wa Jimbo la Ludewa kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Msambichaka Mkinga amepinga vikali kupitishwa bila kupingwa mgombea mwenzake wa jimbo hilo kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Deo Filikunjombe na kudai kulikuwa na hujuma.

Mkinga alitoa malalamiko hayo mbele ya waandishi wa habari Dar es Salaam leo asubuhi na kueleleza kuwa sababu zilizotolewa na msimamizi wa uchaguzi wa jimbo hilo kuwa hakupeleka fomu namba 10 hazikuwa na ukweli wowote.

"Nilipofika ofisi ya msimamizi wa uchaguzi Jimbo la Ludewa nilisaini na kukabidhi tamko la kuheshimu na kutekeleza maadili ya uchaguzi ya mwaka 2015 (fomu namba 10) na baada ya kusaini nilimkabidhi msimamizi wa uchaguzi pamoja na fomu namba 8B,picha, stakabadhi ya malipo ya dhamana ambapo vilihakikiwa na Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi, Gervas Lupembe" alisema Mkinga.

Mkinga alisema katika jambo lisilo la kawaida msimamizi wa uchaguzi wa jimbo hilo hilo hakubandika kwenye ubao wa matangazo tamko hilo na alipomfuata msimamizi huyo kumuulizia msaidizi wake Lupembe alikiri kupokea na kuziwasilisha kwa kiongozi wake ili kutia saini ambaye naye alikiri kuzipokea lakini wakati ana bandika tamko hilo la Mgombea wa CCM fomu hiyo hakuiona.

Alisema katika pingamizi alilowekewa dai mojawapo ni kutokuwepo  tamko hilo kwenye fomu zake hali inayoonesha wazi kuwa kulikuwa na mchezo mchafu uliofanyika ili kumpitisha Filikunjombe bila kupingwa.

Mkinga alisema kuwa kuwaondoa wagombea kwa sababu zisizo za msingi ni kuiminya demokrasia na kuirudisha nchi nyuma kwani kunaweza kusababisha kukosa viongozi wazuri na kubakia na viongozi wasiofaa na wasiotaka kushindanishwa kwa kuwapa nafasi wananchi ya kumchagua kiongozi wanayemtaka.

Mgombea huyo alisema kutokana na sintofahamu hiyo alimuomba msimami wa uchaguzi wa jimbo hilo kutupiliambali pingamizi lililotolewa dhidi yake na mgombea mwenzake ambapo anasubiri majibu baada ya kuandika barua ya malalamiko.

ALLIANCE, MARSH MABINGWA AIRTEL RISING STARS MZA

Nahodha wa timu ya Alliance Academy Ally Hamisi (kushoto) akikabidhiwa kombe na Mwenyekiti wa Soka Mkoa wa Mwanza (MZFA)Bw. Jackson Songora baada ya kutwaa ubingwa wa U-17 Airtel Rising Stars mkoa wa Mwanza upande wa wavulana jana.
Nahodha wa timu ya wasichana ya Marsh Meriany Kimbuya (kushoto) akikabidhiwa na kombe na Meneja Masoko wa Airtel Kanda ya Ziwa Bw. Emmanuel Raphael baada ya kutwaa ubingwa wa U-17 Airtel Rising Stars mkoa wa Mwanza upande wa wasichana jana. 
 ALLIANCE, Marsh mabingwa Airtel Rising Stars Mza Timu ya wavulana ya Alliance Academy ya jijini Mwanza jana imetwaa uchampioni wa michuano ya soka kwa vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Aitel Rising Stars kwa kuwafunga Misungwi Academy 3-1 kwenye uwanja wa CCM Kirumba. 

Kwa upande wa wasichana timu ya Marsh ndio iliyotawazwa mabingwa kwa kushinda timu ya TSC kwa magoli 3-2 katika mchezo mkali uliovuta hisia za watamazaji waliojitokeza kushuhuduia mtanange huo. 

Akikabidhi vikombe kwa washindi, Mwenyekiti wa soka mkoa wa Mwanza Bw. Jackson Songora amewataka wachezaji waliochaguliwa kuiwakilisha Mwanza vyema kwenye fainali za Taifa za Airtel Rising Stars zinatarajiwa kufanyika jijini Dar es Salaam kuanzia Septemba 11 hadi 21. Songora alisema kwamba kikosi kilichochaguliwa kitaanza mazoezi Jumamosi. 

Naye Meneja masoka wa Airtel kanda ya Ziwa Emmanuel Raphel alizipongeza timu zote kwa kushiriki na kuwaasa wachezaji kulinda na kuviendeleza vipaji vyao ambavyo ni hazina kwa taifa. Aliseema lengo lilikuwa ni kuibua vipaji na kuwaasa vijana ambao hawakuchaguliwa kutokata tama na badala yake wajinge kufanya vizuri mwakani. 

Kukamilika kwa michuano hiyo jijini Mwanza ndio kunafunga pazia la Airtel Rising Stars ngazi ya mkoa iliyoanza kutimua vumbi mwezi uliopita. 

Hivi sasa kombaini za mikoa zilizochaguliwa kuwakilisha mikoa yao zinajiandaa kwa fainali za taifa na mwenyekiti wa soka la vijana wa shirikisho la mpira nchini Bw. Ayoub Nyenzi amesema kuwa maandalizi ya michuano hiyo yamekamilika. Mashindano ya Airtel Rising Stars ambayo mwaka huu yanashirikisha mikoa ya Ilala, Kinondoni, Temeke, Morogoro, Mbeya, Mwanza na Arusha inatarajiwa kuingia kwenye hatu nyeti ya fainali za Taifa iliyopangwa kufanyika kwenye Uwanja wa Karume, Dar es Salaam, kuanzia Septamba 11 hadi 21.

PICHA ZA LOWASSA AKIHUTUBIA BARAZA LA WANAWAKE WA CHADEMA JIJINI DAR

Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa na Mgombea mwenza wake, Dkt. Juma Haji Duni wakiwasalimia baadhi ya Wanawake wanaounda Baraza la Wanawake wa Chadema, waliokuwa wamefurika kwa wingi nje ya Jengo la LAPF, Kijitonyama jijini Dar es salaam, wakati walipowasili kwa kuhutubia Baraza hilo. PICHA ZOTE NA OTHMAN MICHUZI.
Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake wa Chadema (BAWICHA), Mh. Halima Mdee akizungumza na Umati wa Kinamama wa Chama hicho, uliokuwa umefurika kwa wingi nje ya Ukumbi wa Mikutano wa Jengo la LAPF, Millennium Tower,  Kijitonyama jijini Dar es salaam leo Agosti 27, 2015, kabla ya kufanyika kwa Mkutano wa Baraza hilo, uliohutubiwa na Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa.
Mke wa Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, Mama Regina Lowassa akiwasalimia Wanawake wa Chama hicho waliokuwa wamefurika kwa wingi nje ya Ukumbi wa Mikutano wa Jengo la LAPF, Millennium Tower,  Kijitonyama jijini Dar es salaam leo Agosti 27, 2015, kabla ya kufanyika kwa Mkutano wa Baraza la Wanawake wa CHADEMA (BAWICHA).

Wakinamama hao wakimshangilia Mh. Lowassa na Babu Duni wakati walipowasili Ukumbini hapo.
Mwenyekiti Mwenza wa UKAWA, Mh. James Mbatia akiwasalimia kina mama hao ambao walikosa nafasi ndani ya Ukumbi na kuamua kukaa nje.
Mgombea Mwenza wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dkt. Juma Haji Duni akiwasalimia kina mama hao.

Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa akizungumza machache wakati akiwasalimia maelfu ya Wanawake wanaounda Baraza la BAWICHA, waliokuwa wamekaa nje ya jengo la LAPF kutokana na kukosa nafasi ndani ya Ukumbi huo. Mh. Lowassa alilazimika kusimama na kuwasalimia kinamama hao kabla ya kuingia Ukumbini kulihutubia Baraza hilo.
Mh. Lowassa na Ujumbe wake wakiwasili Ukumbini.
Baadhi ya Wadau wa Sanaa ya Filamu nchini waliokuwepo kwenye Mkutano huo wa BAWICHA.
Shangwe Ukumbini.
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Freeman Mbowe, akiteta jambo na Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa pamoja na Mgombea Mwenza, Dkt. Juma Haji Duni, wakati wa Mkutano wa Baraza la Wanawake wa Chadema (BAWICHA), Uliofanyika jana Agosti 27, 2015.
Mmoja wa Kinamama wanaowakilisha Watu wenye ulemavu akizungumza kwenye Mkutano huo.
Mh. Kaihula na Kinamamam wenzake wakifatilia Mkutano huo.
Viongozi wa Kuu.
Keki ya Siku ya Kuzaliwa kwa Mh. Lowassa iliyotolewa na Baadhi ya Washanii wanaomuunga Mkono.
Mmoja wa Wasanii wa Filamu nchini, Jacqueline Wolper akizungumza kwa niaba ya wasanii wenzake.
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa akipokea Keki ya kusherehekea siku yake ya kuzaliwa kutoka kwa Msanii wa Filamu nchini, Aunt Ezekiel.
 Jacqueline Wolper akizungumza kwa niaba ya wenzake.
Mke wa Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, Mama Regina Lowassa akitoa hotuba yake mbele ya Wanawake wa Chama hicho waliokuwa wamefurika kwa wingi kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jengo la LAPF, Millennium Tower,  Kijitonyama jijini Dar es salaam leo Agosti 27, 2015, wakati wa Mkutano wa Baraza la Wanawake wa CHADEMA (BAWICHA).
Mh. Mbowe na Mh. Lowassa wakiteta jambo.
Taswira mbali mbali katika Mkutano huo.
Mh. Lowassa akimpongeza Mkewe kwa hotuba nzuri aliyoitoa.
Msanii na Muziki wa Injili, Florah Mbasha akitoa burudani.

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Freeman Mbowe, akitoa hotuba yake, kwenye Mkutano wa Baraza la Wanawake wa Chadema (BAWICHA), Uliofanyika leo Agosti 27, 2015, kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jengo la LAPF, Millennium Tower,  Kijitonyama jijini Dar es salaam.

Mh. Mbatia akizungumza.
Mgombea Mwenza wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dkt. Juma Haji Duni, akitoa hotuba yake, kwenye Mkutano wa Baraza la Wanawake wa Chadema (BAWICHA), Uliofanyika leo Agosti 27, 2015, kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jengo la LAPF, Millennium Tower,  Kijitonyama jijini Dar es salaam.
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa akimueleza jambo, Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake wa Chadema (BAWICHA), Mh. Halima Mdee wakati akilihutubia Baraza hilo.
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa ,akitoa hotuba yake, kwenye Mkutano wa Baraza la Wanawake wa Chadema (BAWICHA), Uliofanyika leo Agosti 27, 2015, kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jengo la LAPF, Millennium Tower,  Kijitonyama jijini Dar es salaam.