ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, August 5, 2017

MUDA HUU NDANI YA CCM KIRUMBA MWANZA.









PICHA NA ZEPHANIA MANDIA WA GSENGO BLOG.

Friday, August 4, 2017

SAIDA KAROLI ALISIMAMISHA JIJI LA MWANZA KWA MUDA, KESHO KUFANYA YAKE CCM KIRUMBA.

 Mwanamuziki nguli wa muziki asili nchini Tanzania leo asubuhi amewasili jijini Mwanza na kupata mapokezi makubwa kutoka uwanja wa ndege jijini hapa. Mamia ya wananchi wa viunga mbalimbali wakifuatilia matangazo ya moja kwa moja kutoka eneo la tukio kuitia Jembe Fm waliitikia kujitokeza kwenye njia mbalimbali na kumlaki mkali huyo.
Saida Karoli katika ardhi ya jiji la Mwanza kwaajili ya show yake itakayofanyika jumamosi hii ya tarehe 5 August 2017 katika uwanja wa CCM Kirumba.
Saida Karoli nje ya uwanja wa ndege Mwanza.
Mkurugenzi wa Jembe Media Group Dr. Sebastian Ndege kushoto akihakiki wasanii na wanamuziki waliowasili viwanjani hapo. Katikati ni mwanahip hop kutoka kundi la WEUSI G.Nacko akishow love na mratibu Hellen Kazimoto.
Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Jembe Media Group Dr. Sebastian Ndege, G. Nacko na Hellen Kazimoto.
Mambo ni motto.
The Crew.
Msafara wa mapokezi wa wasanii waliotinga jijini Mwanza.
Mdau aka shabiki akikimbilia kushikana mkono na mwanamuziki Saida Karoli.
Hatua kwa hatua toka uwanja wa ndege wa Mwanza.
Viunga vya Ilemela na marafiki asubuhi na mapema leo hii.
Msafara.
Mbele marafiki wa usafiri wa bodaboda.
Jembe ni Jembe
Saida na mashabiki zake.
Mama mama ......hawa ni wachuuzi wa Samaki wanaofuatilia kazi za mwanamama Saida Karoli na ujio huu umekuwa kama faraja kwao.
Msafara wa Saida Karoli view toka juu ya daraja la Magufuli Mwanza.
Jembe Live.
Sisi.
Mapema asubuhi barabara ya Nyerere jijini Mwanza.
Katikati ya viunga vya jiji hapa ni Dampo.
Soko la Kirumba jijini Mwanza.
Mahaba ya wana wa nyumbani.
Nimerudi......
Aksanteni tukutane CCM Kirumba Mwanza kama ni viingilio tizama hapo chini.
Salaaam salaam katikati ya jiji la Mwanza.
Watoto nao wanamjua.
Hapa ilimlazimu kuzungumza japo kiduchu na wadau wake.

Na tuliamshEeee sasa ndani ya uwanja wa #CCMkirumba Jumamosi hii tarehe 5 August 2017 miaka 15 ya Salida Karoli. Kulia atasimama @chegechigunda kushoto @gnakowarawara juu @officialnandy na pale kati ni #WEWE shabiki usiyekosa show kali kama hizi.
Tsh 3,000/= WATOTO
Tsh 5,000/= KAWAIDA
Tsh 20,000/= VIP
 ▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬
Kama unamfahamu vyema na unaweza kumwelezea vyema #Saida_Karoli Muda wako sasa kuyaoga #MAKOMPLIMENTARI Mpango mzima powered by @jembenijembe sponsored by @Jembefm #Uhuru_Hospital #New_mwanza_Hotel #JambO #AirTanzania na @cloudsfm ▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬

MAJAMBAZI YAPORA MAMILIONI KIWANDANI, MATATU YADAKWA.

RPC Ahmed Msangi.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza, linawashikilia watu watatu wanaodaiwa kuwa majambazi kwa kosa la unyang’anyi wa kutumia silaha na kupora Sh464 milioni.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi alisema jana Alhamisi, Agosti 3 kuwa watu hao walikamatwa Julai 19 mwaka huu mkoani Singida walipokimbilia baada ya kufanya uhalifu.

Kamanda Msangi amesema watu hao walikamatwa na fedha halali za Kitanzania   Sh40 milioni na Dola za Marekani 190,000 na silaha aina ya Short gun vilivyoibiwa katika kiwanda kinachojihusisha na biashara ya mabondo ya samaki cha Weish AST Ltd jijini hapa.

Amewataja watu hao kuwa ni Seif Waziri (37), Daud Mwakalinga (35) wote wakazi wa Dodoma waliokamatwa wakiwa mkoani Singida wakiwa wamebaki na Sh2 milioni na Dola za Marekani 20,000.

Pia amesema watu hao walikutwa na silaha aina ya   shortgun yenye namba 011765714 na car namba 00107210 vitu vilivyoporwa jijini Mwanza. Mwingine ni Emmanuel Mwakilili aliyekamatwa jijini Mwanza baada ya kutajwa na wenzake.

Kwa mujibu wa Kamanda Msangi tukio hilo la uporaji lilitokea jijini Mwanza Julai 14, mwaka huu  ambapo majambazi watano walivamia kiwanda hicho wakiwa na silaha za jadi na kumpiga mlinzi na kitu kizito kichwani na kumpora silaha kisha kuingia ndani na kupora kiasi hicho cha fedha na kutokomea kusikojulikana.

Amesema polisi walipokea taarifa za kiintelijensia kuwa majambazi hao wamekimbilia mkoani Singida ndipo askari walikwenda wakishirikiana na wamkoa wa Singida na kufanikiwa kuwatia mbaroni wawili.

“Baada ya mahojiano ya awali walipoletwa Mwanza, majambazi hao walikiri kuhusika na tukio hilo kisha walionyesha walipokuwa wameficha silaha na kumtaja mwezao amabaye naye alikamatwa,” amesema Kamanda Msangi.

RC MAKONDA APOKEA MSAADA WA ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 300


Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mheshimiwa Paul Makonda leo amepokea Vitanda 150 na Magodoro 150 vyenye tamani ya zaidi ya shilingi Million 300 kutoka kampuni ya mafuta ya Camel chini ya Kampuni tanzu za Amsons Group iliyomua kuunga mkono juhudi za Mkuu wa Mkoa katika kuboresha sekta ya Afya.

Vitanda hivyo ambabyo pia vina Magodoro pamoja na Mashuka yake vitapelekwa kwenye Wodi mpya ya Mama na Mtoto iliyojengwa kwenye Hospital ya Amana chini ya ufadhili wa kampuni ya Amsons Group ambayo ujenzi wake umekamilika kwa Asilimia mia moja.
Akizungumza baada ya kupokea Vitanda hivyo, Makonda amesema amedhamiria kuhakikisha changamoto zote zinazoikabili sekta ya Afya katika Mkoa wa Dar es Salaam zinamalizika ili kuhakikisha Wananchi wanapata huduma bora za afya.

“Sitaacha kutafuta kwaajili ya Wananchi wa Dar es salaam, nitabisha hodi kila panapostahili ili mradi Wananchi wangu wawe wanapata huduma za Afya katika mazingira mazuri ili siku moja waone kazi kubwa inayofanywa na Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dr. John Magufuli” Alisema Makonda.

“Tumedhamiria kuhakikisha Mama,Mtoto na Wananchi wote wa Mkoa wa Dar es salaam wanapata huduma bora, na huduma bora zipo kwenye Afya,kama Wagonjwa wasipopata huduma bora inakuwa ni tatizo,tayari kama mnavyofahamu tuna Majengo ya kisasa tunayoendelea kujenga Chanika, Amana, Temeke na Mwananyamala ambapo kukamilika kwake yataongeza tija ya upatikanaji wa huduma za bora za Afya, sasa Vitanda hivi 150 ni tafsiri tosha kuwa vinakwenda kupunguza adha kwa kinamama wanaokwenda kujifungua kwenye Hospital ya Amana” Aliongeza Makonda.
Kwa upande wake Suleiman Amour meneja uendelezaji wa biashara kampuni ya Camel Oil amesema vitanda hivyo ni uendelezaji wa kutoa mchango wao kuunga mkono juhudi za mkuu wa mkoa za kuhakikisha wananchi wa Dar es salaam wanapata huduma bora za afya.

Ikumbukwe kuwa Kampuni tanzu ya Mafuta na Saruji za Amsons Group ndio wanaojenga wodi za mama na motto kwenye Hospital za Amana, Temeke na Mwananyamala baada ya mkuu wa Mkoa kuwashirikisha dhamira yake ya kumaliza kero kwenye sekta ya Afya.

MASAUNI ATEMBELEA KITENGO CHA POLISI CHA KUDHIBITI DAWA ZA KULEVYA,KILWA ROAD JIJINI DAR ES SALAAM.

 Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akizungumza na watumishi wa Kitengo cha Jeshi la Polisi cha Kuzuia Dawa za Kulevya pamoja na waandishi wahabari (hawapo pichani), wakati alipofanya ziara katika kitengo hicho kilichopo Barabara ya Kilwa, jijini Dar es Salaam, ambapo aliwaagiza kuhakikisha wanapambana na uingizwaji wa dawa hizo  kupitia bandari bubu na mianya yote ya uingizwaji na usambazaji. Pichana Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
 Naibu Kamishna wa Kitengo cha Jeshi la Polisi cha Kuzuia Dawa za Kulevya, DCP Mkonyi, akitoataarifafupiyahaliyauzuiajiwaDawazaKulevyambeleyaNaibu Waziri waWizaraya Mambo ya Ndani ya Nch. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
 Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akisomewa takwimu za matukio ya ukamataji wa Dawa za KulevyanammojawaafisawaKitengo cha Jeshi la Polisi cha Kuzuia Dawaza Kulevya wakati alipofanya ziara katika kitengo hicho kilichopo Barabara ya Kilwa, jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akiongozana na Naibu Kamishna wa Polisi, DCP Mkonyi, wakati alipotembelea Kitengo cha Jeshi la Polisi cha Kuzuia Dawa za Kulevya kilichopo Barabara ya Kilwa, jijini Dar es Salaam, ambapo aliwaagiza kuhakikisha wanapambana na uingizwaji wadawa hizo kupitia bandaribubu na mianya yote ya uingzwaji na usambazaji. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

MAGUFULI: NEEMA YAJA TANZANIA

RAIS John Magufuli amesema amedhamiria kwa dhati kuleta maendeleo nchini, kupitia uwekezaji na uzalishaji mali katika uchumi wa viwanda; na pia amedhamiria kuufungua kiuchumi Mkoa wa Tanga.

Amewataka wananchi kuhakikisha wanafanya kwa bidii shughuli za uzalishaji mali ikiwemo mboga, vyakula na matunda ili kukidhi mahitaji ya soko, litakalotokana na mradi wa bomba la mafuta kutoka Hoima Uganda mpaka Chongoleani jijini Tanga ambako kesho ataweka jiwe la msingi na Rais Yoweri Museveni wa Uganda.

Alitoa kauli hiyo kwa nyakati tofauti akiwa katika miji ya Mkata, Komkonga, Kabuku, Hale, Muheza na Mkanyageni katika wilaya za Handeni, Korogwe na Muheza, alipozungumza na wananchi wakati alipowasili mkoani Tanga kuanza ziara yake ya kikazi.

Dk Magufuli alisema pamoja na ziara hiyo, ataweka jiwe la uzinduzi wa mradi wa bomba la mafuta Chongoleani jijini Tanga. Alisema mradi huo utafungua fursa za kiuchumi mkoani huko na kuwataka wananchi kuchangamkia. Tanga inazaliwa upya “Mradi huu wa bomba la mafuta kutoka Hoima nchini Uganda hadi Chongoleani Tanga utatoa ajira zaidi ya 45,000 za kudumu pamoja na vibarua, lakini pia kundi jingine la wananchi wa Mkoa wa Tanga litapata ajira mbadala kupitia biashara mbalimbali za kuuza vyakula, kujenga nyumba za kupangisha,” alisema Dk Magufuli.

Aliongeza, “Nataka niifufue upya Tanga hii ya watani wangu ili tulete maendeleo. Tanga inazaliwa upya, Tanga sasa inafunguka. Inafunguka kupitia uwekezaji bomba la mafuta hivyo nawataka sasa tujifunze kufanya kazi kwa bidii kwa sababu hakuna vitu vya bure lazima tufanye kazi ili kuzalisha mahitaji ya chakula na vitu mbalimbali vitakavyotumiwa na wafanyakazi kwenye mradi huo.”

Alisema Tanga ilikuwa ikisifika kwa uchumi wa viwanda katika miaka ya nyuma, lakini katika miaka ya karibuni uchumi wake umedorora, lakini kuanzishwa kwa bomba la mafuta na miradi mingine ikiwamo ya kiwanda kikubwa cha saruji kinachoanzishwa, kitaufanya mkoa huo kuinuka tena kiuchumi. Aagiza uchunguzi Handeni Aidha, Rais Magufuli ametoa siku 15 kwa kamati itakayoundwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu kukamilisha uchunguzi wa matumizi ya Sh milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya katika Kata ya Mkata, Jimbo la Handeni Vijijini wilayani Handeni.

Utekelezaji wa hatua hiyo utawezesha serikali kupata thamani halisi ya fedha na kuwabaini waliohusika kuhujumu ujenzi huo, ulioshindwa kuendelezwa kwa zaidi ya miaka miwili sasa. Alikuwa akijibu kero nne za wananchi wa Mkata zilizotolewa na Mbunge wa Handeni Vijijini, Mboni Mhita pamoja na Diwani wa Kata ya Mkata, Mussa Mwanyumbu, baada ya kuwasili na kudai kusita kwa ujenzi huo kumetokana na serikali kuacha kupeleka fedha kwa miaka miwili sasa na kusababisha usumbufu wa upatikanaji wa huduma ya uhakika kwa wananchi katika kata za Sindeni, Mkalamo, Kang’ata na Mkata pamoja na wasafiri wanaotumia Barabara kuu ya Segera - Chalinze.

“Kero yetu nyingine ni kiwanda cha Mkata Saw Mills kilichotelekezwa baada ya kutaifishwa na serikali mwaka 1998 na kukabidhiwa mwekezaji ambaye mpaka sasa bado hajakiendeleza tunaombwa serikali ikirejeshe kwetu ili wananchi tuendeleze uzalishaji na nyumba nane zilizopo kiwandani wapewe watumishi wa halmashauri yetu ili watekeleze shughuli zao wakiwa hapa hapa Mkata,” alisema.

Awali kabla ya kutoa maagizo hayo, Rais Magufuli alimkaribisha waziri Ummy kujibu kero kuhusu ujenzi wa hospitali, ambao alikiri kuwepo kwa viashiria vya ubadhirifu na kusema kwamba serikali inatarajia kupeleka Sh milioni 800 kuendeleza ili ujenzi. “Ni kweli mheshimiwa Rais, Halmashauri ya Wilaya ya Handeni kwa sasa haina hospitali, lakini tayari wizara yangu kwa kushirikiana na Tamisemi katika bajeti ya mwaka huu 2017/2018 tumetenga shilingi milioni mia nane kuendeleza ujenzi, lakini tunahitaji kufanya tathmini kwa sababu kazi ya shilingi milioni mia tano zilizotolewa awali ina mashaka ... tumekubaliana kwamba fedha hizo shilingi milioni mia nane hazitakuja mpaka kamati itakapokamilisha kazi,” alisema Ummy.

JKT wapokonywa ardhi Dk Magufuli alisema, “natoa siku kumi na tano kwa hiyo kamati ya kuchunguza ujenzi wa hospitali kukamilisha kazi hiyo kwa sababu tayari yameonekana mashaka hivyo lazima tuyamalize na wale waliohusika kutafuna fedha mimi ndiyo mtumbua majipu na ninawaahidi hilo ili serikali iweze kuleta haraka zile shilingi milioni mia nane kuendeleza ujenzi.”

Aidha, kuhusu kero ya maji, Dk Magufuli alisema serikali imetoa Sh bilioni mbili kutekeleza mradi huo hivi sasa kati ya Sh bilioni nne zinazohitajika kukamilisha mradi wote. Pia alimwagiza Mkuu wa Kikosi cha JKT Kabuku, Luteni Kanal Erasmus Bwegoge kurejesha kwa uongozi wa kijiji cha Kabuku eneo la ekari 50 walizokabidhiwa miaka saba kwa ajili ya ujenzi wa kiwanda cha kuchakata matunda na kumtaka Mbunge wa Handeni Vijijini, Mboni Mhita kusimamia utekelezaji wa agizo hilo.

Muheza kutiririka maji Akiwa Muheza na Mkanyageni, Dk Magufuli alieleza kuwa serikali imetenga zaidi ya Sh bilioni 30 kwa ajili ya ujenzi wa miradi mbalimbali mikubwa ya majisafi ili kumaliza kero inayowakabili wananchi katika Halmashauri ya Wilaya ya Muheza. Fedha hizo zinajumuisha Sh bilioni mbili kupitia bajeti ya serikali ya mwaka huu pamoja na nyingine Sh bilioni 30 kutoka Serikali ya India ambao utahusisha mikoa 17 nchini, ikiwemo wa Tanga ambao utawakilishwa na Halmashauri ya Wilaya ya Muheza.

Aliposimamisha msafara wake mjini Muheza, Rais Magufuli alisema anatambua kero kubwa ya uhaba wa majisafi inayowakabili wananchi hapo na kuahidi kwamba hatawaangusha bali atahakikisha miradi mikubwa ya maji inaelekezea wilayani humo ili kuwezesha wananchi kufurahia maisha. “Ndugu zangu wa Muheza nimesimama hapa na msafara wangu ili niwashukuru sana kwa kunipa kura nyingi za urais na mbunge.

Napenda niwaeleze kwamba kero yenu ya maji naijua na nimeshaanza kuishughulikia kwa kutoka shilingi bilioni mbili katika bajeti ya mwaka huu, lakini fedha hiyo ni sawa na breakfast (kifungua kinywa) tu kwenu mradi mwingine mkubwa wa maji unakuja kutekelezwa hapa,” alisema Dk Magufuli na kuongeza: “Pia nimetenga shilingi bilioni thelathini nyingine kwa ajili ya kutekeleza mradi mkubwa wa maji hapa kupitia ufadhili wa Serikali ya India.

Fedha kutoka serikali hiyo za kutekeleza miradi ya maji zitapelekwa katika jumla ya mikoa kumi na saba hapa Tanzania na Muheza nimeishachagua kuwakilisha Tanga, wote mnaelewa kwamba ahadi ni deni kwa hiyo sitaki kuonekana kwamba nimesema uongo, bali niwahakikishia kwamba miradi hii ya maji itatekelezwa.”

Mashamba yarudishwa Kuhusu mashamba makubwa ya mkonge, alieleza, “Tayari nilikwishatoa uamuzi kuhusu hekta 14, 000 za mashamba matano kati ya 72 yaliyopo hapa Tanga ambayo hayaendelezwi nimeyafuta na tayari nimempa mkuu wa mkoa ili waweke utaratibu wa matumizi bora ya ardhi lakini asilimia fulani ya ardhi hiyo nimewaagiza igawanywe bure kwenu ninyi wananchi,” Aidha, alibainisha kwamba eneo litakalosalia katika ardhi hiyo litatumika kwa shughuli za uwekezaji wa viwanda ili kuwezesha kupanua wigo wa wananchi kumiliki uchumi wa viwanda kupitia fursa ya ardhi yenye rutuba iliyopo.

Kuhusu Barabara ya Muheza mpaka Amani yenye urefu wa kilometa 35, alisema serikali imetenga Sh bilioni tatu ili kuanza ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami. Akiwa katika mkutano wa hadhara Mkanyageni, alisema serikali imepeleka mradi mwingine wa majisafi wenye thamani ya Sh bilioni 2.9 kutoka Pongwe mpaka Mkanyageni ili kuwezesha wananchi hapo kupata huduma. Awali Mbunge wa Muheza, Balozi Adadi Rajabu alimpongeza rais kwa kusaidia kupunguza kero ya maji ikiwemo Sh bilioni tano zilizopelekwa katika bajeti ya mwaka huu ili kukarabati mabomba chakavu.

CHANZO:- HABARI LEO