ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, March 22, 2026

UWANJA MKUBWA NA MRADI WA MICHEZO WAPANGWA KUJENGWA JIJINI MWANZA

NA ALBERT G.SENGO/MWANZA 

Serikali imetangaza mpango wa kujenga eneo changamani la michezo litakalokuwa kubwa zaidi nchini, litakalojengwa jijini Mwanza.

Akizungumza hii leo na waandishi wa habari, katika ukumbi wa juu ndani ya MV New Mwanza, Msemaji Mkuu wa Serikali Gerson Msigwa amesema Serikali imeomba takribani hekari elfu moja katika eneo la Wilaya ya Ilemela District kwa ajili ya ujenzi wa mradi huo.

Eneo hilo linatarajiwa kujumuisha uwanja mkubwa wa mpira wa miguu, uwanja wa riadha, viwanja vya michezo ya ndani (indoor arena) kwa michezo kama mpira wa kikapu na mpira wa wavu, pamoja na miundombinu ya mafunzo na kukuza vipaji vya wanamichezo.