ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, June 7, 2014

TGNP YAFANYA MJADALA WA WAZI JUU YA UBORESHAJI NA UWAJIBIKAJI

Moses Iriria, kutoka ANSAF (Mtafiti) akiwasilisha mada katika mjadala huo.
Moses Iriria, kutoka ANSAF (Mtafiti) akiwasilisha mada katika mjadala huo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Sikika, Irenei Kiria akiwasilisha mada wa washiriki.
Mkurugenzi Mtendaji wa Sikika, Irenei Kiria akiwasilisha mada wa washiriki.
Aliyekuwa Mkurugenzi wa TGNP Matandao, Bi. Usu Mallya akiendesha majadiliano kwa washiriki.
Aliyekuwa Mkurugenzi wa TGNP Matandao, Bi. Usu Mallya akiendesha majadiliano kwa washiriki.
Ofisa Miradi wa TAWJA, Asha Komba ikiwasilisha mada yake katika mjadala wa wazi.
Ofisa Miradi wa TAWJA, Asha Komba ikiwasilisha mada yake katika mjadala wa wazi.
Baadhi ya washiriki wa mjadala huo wa wazi.
Baadhi ya washiriki wa mjadala huo wa wazi.
Sehemu ya washiriki wa mjadala huo wa wazi.
Sehemu ya washiriki wa mjadala huo wa wazi.
Pichani juu ni baadhi ya washiriki wa mjadala huo wakichangia mada anuai.
Pichani juu ni baadhi ya washiriki wa mjadala huo wakichangia mada anuai. 
Pichani juu ni baadhi ya washiriki wa mjadala huo wakichangia mada anuai.
Pichani juu ni baadhi ya washiriki wa mjadala huo wakichangia mada anuai.
Mwanaharakati Badi Darusi akiwasilisha mada yake.
Mwanaharakati Badi Darusi akiwasilisha mada yake
Baadhi ya washiriki wa mjadala huo wa wazi.
Baadhi ya washiriki wa mjadala huo wa wazi.
      .  
 Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam MTANDAO wa Jinsia nchini (TGNP Mtandao) umefanya mjadala wa wazi ulioshirikisha taasisi mbalimbali zisizo za Serikali (NGO's) pamoja na wadau wa masuala ya kijinsia juu ya uboreshaji wa uwajibikaji kwa kuzingatia mgawanyo wa rasilimali kijinsia kwa huduma bora za kijamii nchini Tanzania. 

 Mjadala huo wa wazi uliofanyika leo jijini Dar es Salaam katika Hotel ya Blue Pearl, pamoja na mambo mengine lengo kuu ilikuwa ni kuimarisha sauti ya pamoja kudai uwajibikaji kwa watunga sera kwa kuzingatia mgawanyo wa rasilimali kijinsia, kupiga vita rushwa na kuboresha utoaji huduma za kijamii. 

 Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mara baada ya kumalizika kwa mjadala huo, Kaimu Meneja wa Habari na Mawasiliano wa TGNP Mtandao, Bi. Kenny Ngomuo alisema malengo mahususi ya mjadala ni pamoja na kukuza uelewa wa muktadha wa kimataifa, kitaifa na kijamii na athari zake kwa maisha ya wanawake walioko pembezoni.

 Alisema lengo lingine ni kwa washiriki kubadilishana uzoefu na mafanikio ya harakati mbalimbali kuhusu uchambuzi wa bajeti na ufuatiliaji wa utendaji katika ngazi za jamii hadi taifa na pia kuweka mikakati ya kuendeleza mapambano zidi ya rushwa, kukuza utawala bora ili kuboresha utoaji wa huduma kwa jamii. "...Malengo mengine mahususi kwa washiriki wa mjadala huu ilikuwa kuweka kumbukumbu za mafanikio yanayohusiana na mapambano dhidi ya rushwa ikiwa ni pamoja na kupigania bajeti ya kijinsia na ufuatiliaji. 

Kuimarisha mitandao na ujenzi wa nguvu za pamoja juu ya masuala ya bajeti ya kijinsia, vita dhidi ya rushwa na huduma bora kwa jamii," alisema Bi. Ngomuo. 

 Kabla ya kuanza kwa mjadala huo mada mbalimbali ziliwasilishwa kwa washiriki, ambazo ziligusa maeneo anuai ya huduma za kijamii, rushwa na changamoto nyingine zinazoikabili jamii kabla ya wajumbe kupata fursa ya kujadiliana kwa pamoja.

 Takribani washiriki 130 kutoka Dar es Salaam na mikoa ya jirani ikiwemo Morogoro na Pwani wameshiriki mjadala huo.

Friday, June 6, 2014

AJALI MBAYA YAWAKUMBA NEW HABARI MWANZA WAKATI WAKIMKWEPA TEMBO: GARI NYANG'ANYANG'A WADAU WASALIMIKA

Ajali mbaya imetokea juzi usiku katika moja ya maeneo mto Rubana wilayani Bunda kuingia mbuga ya Serengeti ikihusisha watu wanne baadhi yao wakiwa ni waandishi wa Habari. 

Napata fursa yakufanya mahojiano na mmoja wa majeruhi katika ajali hiyo Fredrick Katulanda mwandishi wa habari wa gazeti la Mtanzania ambaye alisema kuwa ajali hiyo ilitokana na kumkwepa tembo aliyejitokeza ghafla akivuka barabara. . ZAIDI BOFYA PLAY KUSIKILIZA.

ALICHOSEMA KOMBA LEO KWENYE PB MARA BAADA YA PICHA ZA KUCHAFULIWA MITANDAONI.

Imekuwa ni siku ngumu leo kwa Mhe. Komba, hali iliyosababisha kiongozi huyo ambaye ni mbunge wa jimbo la Mbinga Magharibi kushindwa kabisa hii leo kuhudhuria vikao mbalimbali vya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania vinavyoendelea mjini Dodoma.

Hali hiyo imekuja mara baada ya picha mbalimbali chafu kusambazwa kwenye mitandao zikimuonyesha kiongozi huyo akijiachia katika hali ya kingono na binti mmoja ambaye hata hivyo jina lake halijajulikana.

Power Break Fast ya Clouds Fm hii leo kupitia mwakilishi wake mjini Dodoma (Special kwa masuala ya Bunge) Simon Simalenga, imefanya juhudi hatimaye kufanya mahojiano na kiongozi huyo kupata maoni yake juu ya shutuma hizo nzito dhidi yake.
IFUATAYO NI SAUTI YA MHE. KOMBA (BOFYA PLAY KUSIKILIZA) 

TUZO NYINGINE KWA TBL KUPITIA NDOVU SPECIAL MALT

Meneja wa Bia ya Ndovu Special Malt, Pamela Kikuli akiwasili katika Uwanja wa Kimataifa wa Julius Nyerere akitoka Ufaransa kuchukua tuzo ya Ubora wa Kimataifa (Ndovu High International Quality Trophy) iliyoshinda hivi karibuni kutoka katika taasisi ya Kimataifa ya Monde Selectionnchini Ufaransa. Nyuma ni Mpishi wa bia wa Kampuni ya bia nchini(TBL), Cavin Nkya.
Meneja wa Bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo akiwasili katika Uwanja wa Kimataifa wa Julius Nyerere akitoka Ufaransa kuchukua tuzo ya Ubora wa Kimataifa(Safari Lager High International Quality Trophy iliyoshinda hivi karibunikutoka katika taasisi ya Kimataifa ya Monde Selectionnchini Ufaransa.
Picha ya Pamoja mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Kimataifa wa Julius Nyerere akitoka Ufaransa kuchukua tuzo ya Ubora wa Kimataifa(Ndovu High International Quality Trophy) iliyoshinda hivi karibunikutoka katika taasisi ya Kimataifa ya Monde Selectionnchini Ufaransa.
Picha ya Pamoja mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Kimataifa wa Julius Nyerere akitoka Ufaransa kuchukua tuzo ya Ubora wa Kimataifa(Safari Lager High International Quality Trophy) iliyoshinda hivi karibuni kutoka katika taasisi ya Kimataifa ya Monde Selection nchini Ufaransa
Meneja wa Bia ya Ndovu Special Malt, Pamela Kikuli (kulia) akimkabidhi Meneja wa Kiwanda cha Bia cha Dar es Salaam, Calvin Martin tuzo iliyopata bia ya Ndovu Special Malt mara baada ya kuwasili kutoka nchini Ufaransa(Ndovu High International Quality Trophy) Dar es Salaam jana.
Mpishi wa bia wa Kampuni ya bia nchini(TBL), Cavin Nkya(katikati) akimkabidhi Meneja wa Kiwanda cha Bia cha Dar es Salaam, Calvin Martin tuzo iliyopata bia ya Safari Lager mara baada ya kuwasili kutoka nchini Ufaransa(Safari Lager High International Quality Trophy) Dar es Salaam jana.Kushoto ni Meneja wa Bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo.
Meneja wa Bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo akigonga chiazi na baadhi ya wafanyakazi wa Kapuni ya bia nchini(TBL) wakati wa hafla ya kujipongeza kwa kupata tuzo za ubora wa kimataifa kwa Safari Lager na Ndovu Special Malt Dar es Salaam jana.
Meneja wa Bia ya Ndovu Special Malt, Pamela Kikuli akigonga chiazi na baadhi ya wafanyakazi wa Kapuni ya bia nchini(TBL) wakati wa hafla ya kujipongeza kwa kupata tuzo za ubora wa kimataifa kwa  Ndovu Special Malt  na Safari Lager Dar es Salaam jana.
Baadhi ya wafanyakazi wa TBL wakijipongeza kwa kushinda tuzo mbili kwa pamoja.

JULIAS KISARAWE KUMVAA MOROBEST JUN 7

Julias Kisarawe na Morobest wakinyanyuliwa mikono juu kuashiria wamekubalika kuzipiga baada ya kupima na kwenda sawa
Bondia Julias Kisarawe kesho anategemea kupanda ulingoni kuzipiga na Hassan Kiwale "Morobest" .katika ukumbi wa Friends Corner Manzese katika pambano la round nane. 

Akizungumza na vyanzo habari hizi muandaaji Sempai Gola na ofisa wa ngumi za kulipwa nchini Pembe Ndava walisema maandalizi yote yapo kamili, na mabondia wapo katika hali nzuri ukiondoa kasoro ndogo iliojitokeza kwa Moro Best alikuwa acheze na fadhili majia na sasa atacheza na Julias Thomas Kisarawe ambae ni mbadala mkali kwani Kisarawe hajapoteza mchezo katika michezo yake kumi na mbili aliyocheza.mpambano unategemewa kuanza jioni mida ya saa kumi na kutakuwepo na mapambano mengi mno ya utangulizi.

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL ATEMBELEA KIWANDA CHA COCACOLA MWANZA KATIKA MAADHIMISHO YA KILELECHA MAZIGIRA DUNIANI.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiongozana na baadhi ya viongozi wa Mkoa wa Mwanza na wa Kiwada cha Cocacola, wakati alipowasili kwenye Kiwanda hicho kwa ajili ya kutembelea na kujionea mazingira ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Kilele cha Siku ya Mazingira Duniani, zilizofanyika Kitaifa Mkoani Mwanza katika Viwanja vya Furahisha, jana Juni 5, 2014.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiongozana na baadhi ya viongozi wa Mkoa wa Mwanza na wa Kiwada cha Cocacola, wakati alipowasili kwenye Kiwanda hicho kwa ajili ya kutembelea na kujionea mazingira ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Kilele cha Siku ya Mazingira Duniani, zilizofanyika Kitaifa Mkoani Mwanza katika Viwanja vya Furahisha, jana Juni 5, 2014.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kiwanda cha Cocacola Mwanza, Christopher Gachuma, akizungumza machache kabla ya kumkaribisha Makamu wa Rais Dkt. Bilal, kuzungumza na wafanyakazi wa kiwanda hicho, wakati alipowasili kwenye Kiwanda hicho kwa ajili ya kutembelea na kujionea mazingira ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Kilele cha Siku ya Mazingira Duniani, zilizofanyika Kitaifa Mkoani Mwanza katika Viwanja vya Furahisha, jana Juni 5, 2014
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na wafanyakazi wa Kiwanda cha Cocacola, (hawapo pichani) wakati alipowasili kwenye Kiwanda hicho kwa ajili ya kutembelea na kujionea mazingira ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Kilele cha Siku ya Mazingira Duniani, zilizofanyika Kitaifa Mkoani Mwanza katika Viwanja vya Furahisha, jana Juni 5, 2014.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Msimamizi Mkuu wa ubora wa Mazingira na Usalama Kazini, Peter Simon, kuhusu jinsi wanavyo tunza mazingira kwa kutotupa maji machafu ambayo hutengenezwa na kuwa masafi  na kutumika upya kwa baadhi ya shughuli za kiwandani hapo kama kumwagia bustani, kuoshea magari na n.k,  wakati alipowasili kwenye Kiwanda hicho kwa ajili ya kutembelea na kujionea mazingira ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Kilele cha Siku ya Mazingira Duniani, zilizofanyika Kitaifa Mkoani Mwanza katika Viwanja vya Furahisha, jana Juni 5, 2014.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Msimamizi Mkuu wa ubora wa Mazingira na Usalama Kazini, Peter Simon, kuhusu jinsi wanavyo tunza mazingira kwa kutotupa maji machafu ambayo hutengenezwa na kuwa masafi  na kutumika upya kwa baadhi ya shughuli za kiwandani hapo kama kumwagia bustani, kuoshea magari na n.k,  wakati alipowasili kwenye Kiwanda hicho kwa ajili ya kutembelea na kujionea mazingira ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Kilele cha Siku ya Mazingira Duniani, zilizofanyika Kitaifa Mkoani Mwanza katika Viwanja vya Furahisha, jana Juni 5, 2014.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Msimamizi Mkuu wa ubora wa Mazingira na Usalama Kazini, Peter Simon, kuhusu jinsi wanavyo tunza mazingira kwa kutotupa maji machafu ambayo hutengenezwa na kuwa masafi  na kutumika upya kwa baadhi ya shughuli za kiwandani hapo kama kumwagia bustani, kuoshea magari na n.k,  wakati alipowasili kwenye Kiwanda hicho kwa ajili ya kutembelea na kujionea mazingira ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Kilele cha Siku ya Mazingira Duniani, zilizofanyika Kitaifa Mkoani Mwanza katika Viwanja vya Furahisha, jana Juni 5, 2014.
Makamu akiagana na wafanyakazi wa kiwanda hicho baada ya ziara yake.
Picha ya pamoja 

ASILIMIA 25 TU YA KAYA NCHINI HUTUMIA VYOO BORA VYA KISASA

Waziri wa Wizara ya Afya Ustawi wa Jamii Dkt. Seif Rashid.
WAZIRI  wa Wizara ya Afya Ustawi wa Jamii Dkt. Seif Rashid (MB) amesema kwamba Wizara yake ilifanya utafiti katika Halmashauri 112 nchini mwaka 2013 ambapo matokeo yanaonyesha asilimia 25 tu ya Kaya kutumia vyoo bora.

Dkt. Rashidi alisema hayo jana wakati wa kilele cha Siku ya Maadhimisho ya Mazingira Duniani yaliyofanyika jijini Mwanza kitaifa, ambapo utafiti huo matokeo yake yanaonyesha kuwa ni asilimia 29.6  hazina vyoo kabisa huku asilimia 9 kuna vifaa maalum kwa ajili ya kunawa mikono jambo ambalo ni hatari kubwa kwa afya kutokana na wananchi wengi kuwa na mwitikio mdogo wa kujenga vyoo vya bora vya kisasa.
Hakuna matengenezo pale uharibifu unapotokea.
“Takwimu hizo ni kielelezo cha kuwepo kwa magonjwa ya kuhara  na vile vile zinaonysha kuwa bado tupo nyuma ikilinganishwa na lengo la kitaifa tulilojiwekea la kufikia asilimia 53 ya kaya zenye vyoo bora ifikapo mwaka 2016,”alisema .

Rashidi alisema pia Wizara hiyo  ilizindua Kampeni ya kitaifa ya usafi na mazingia ya miaka minne  iliyozinduliwa na mwaka 2012 iliyolenga kuwezesha kaya milioni 1,520,000 kupata huduma bora za vyoo nchini ifikapo mwaka 2015 ambpo hadi sasa kampeni hiyo imefanikisha kaya 312,528  kujenga vyoo bora sawa na asilima 56.4 ya lengo hilo.
Hakuna milango kwaajili ya kujisitiri, hakuna dawa wala usafi siyo suala la kuzingatiwa ni hali ya vyoo kwa baadhi ya shule zetu nchini.
Choo si sehemu inayopewa kipaumbele na huchukuliwa kama sehemu chafu hivyo huwekwa mbali na makazi.
Aidha kaya 204, 213 zina vifaa maalumu vya kunawa mikono baada ya kutoka chooni na kwamba  vitongoji  9,120 vimesaini makubaliano ya kuboresha hali ya usafi wa mazingira katika maeneo yao ikiwa ni utekelezaji wake.

Waziri Dkt. Rashid alitangaza washindi wa tuzo za mashindano ya Afya na Usafi wa Mazingira kwa mwaka 2014, kundi la kwanza lilihusisha Halmashauri za Majiji manne ya Tanga, Mbeya, Mwanza na Dar esalam ambapo Jiji la Mwanza limeibuka kuwa mshindi kwa asilimia 75 ikiwa ni mara ya tisa mfurulizo, Halmashauri za Mikoa mshindi ni Manispaa ya Kinondoni ilibuka kwa asilimia 55.7 kwa mshindi mmoja.

Kundi jingine la tatu lilishirikisha Halmashauri za Manispaa 15 ambapo mshindi wa kwanza ni Manispaa ya Iringa kwa asilimia71.3, mshindi wa pili Manispaa ya Moshi kwa asilimia 68.1 na mshindi wa tatu ikichukuliwa na Manispaa ya Morogoro kwa asilimia 67, kundi la nne ni Halmashauri za Miji ambapo washindi asilimia zao kweny mabano kuwa ni Mji wa Njombe (67.1), Kahama (63.2)  na Mpanda (60.2).

Wito wangu ni kuikumbusha jamii juu ya ungonjwa hatari wa Dengue ambao umetokea mlipuko wa wagonjwa 1,119 kupatwa na kutokea vifo vya watu wanne, kufatia kuumwa na mbu aina ya “Aedes” ambaye hupata mazalia katika maeneo ambayo si safi akitolea mfano vifuu vya nazi , makopo, vyungu vilivyotupwa hovyo, matairi ya magari na maji ya bafuni hivyo kuwataka kuchukua hatua ya kuweka mazingira katika hali ya usafi.

Thursday, June 5, 2014

MZIGO HuoooO KATIKATI YA JIJI LA MIAMBA.

Msaada kwenye tuta. Plate namba inasomekaje wadau?
Mdogo mdogo...
Mzigo mwingine huo nyuma ya bata.....
Bata mbele ya bata na bata nyuma ya bata! Jeh unaona bata wangapi?
Ile ile kwenye kona shaaaaaa....Wabhejha sana!!

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AADHIMISHA KILELE CHA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI KITAIFA MKOANI MWANZA, ATOA TUZO ZA WASHINDI WA USIMIAJI USAFI WA MAZINGIRA.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwasili kwenye Viwanja vya Furahisha jijini Mwanza Wilaya ya Ilemela, kwa ajili ya kuhudhuria sherehe za Kilele cha Siku ya Mazingira Duniani, zilizofanyika Kitaifa Mkoani Mwanza leo, Juni 5, 2014. Katika Kilele hicho Makamu wa Rais alitoa tuzo na kukabidhi vyeti kwa washindi wa Usafi wa Mazingira kuanzia Vjiji hadi Halmashauri za mikoa mbalimbali ya nchini. 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, Kikombe cha mshindi wa kwanza wa usafi wa Mazingira kwa Majiji makubwa, Mstahiki Meya wa Jiji la Mwanza,  Stanslaus Mabula, wakati wa sherehe za Kilele cha maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani, zilizofanyika Kitaifa Mkoani Mwanza katika Viwanja vya Furahisha, leo Juni 5, 2014. 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi mfano wa Hundi yenye thamani ya Sh. milioni 10, mshindi wa jumla katika kutunza na kuhidhadhi Mazingira, Leon Nombo, mkazi wa Wilaya ya Mbinga, wakati wa sherehe za Kilele cha maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani, zilizofanyika Kitaifa Mkoani Mwanza katika Viwanja vya Furahisha, leo Juni 5, 2014.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi Ngao, mshindi wa jumla katika kutunza na kuhidhadhi Mazingira, Leon Nombo, mkazi wa Wilaya ya Mbinga, wakati wa sherehe za Kilele cha maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani, zilizofanyika Kitaifa Mkoani Mwanza katika Viwanja vya Furahisha, leo Juni 5, 2014
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, Kikombe cha mshindi wa kwanza wa usafi wa Mazingira kwa Manispaa za Jiji la Dar es Salaam, Naibu Meya wa manispaa ya Kinondoni, Songolo Mnyonge, wakati wa sherehe za Kilele cha maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani, zilizofanyika Kitaifa Mkoani Mwanza katika Viwanja vya Furahisha, leo Juni 5, 2014.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akifurahia ujumbe wa siku ya mazingira kutoka kwa wanamuziki wa bendi ya Mjomba, wakati wa sherehe za Kilele cha maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani, zilizofanyika Kitaifa Mkoani Mwanza katika Viwanja vya Furahisha, leo Juni 5, 2014.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Maji wa Wizara ya Maji, Hamza Sadiki, wakati alipotembelea katika Banda la Wizara ya Maji katika maonyesho ya Kilele cha maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani, zilizofanyika Kitaifa Mkoani Mwanza katika Viwanja vya Furahisha, leo Juni 5, 2014.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Mwenyekiti wa Mtandao wa Kinamama kutoka Halmashauri 43 za Tanzania, Paulina Kajura, kuhusu utengenezaji wa Mkaa kwa kutumia Taka wakati alipotembelea katika banda la Kinamama hao katika maonyesho ya Kilele cha maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani, zilizofanyika Kitaifa Mkoani Mwanza katika Viwanja vya Furahisha, leo Juni 5, 2014. 


Makamu wa rais Dkt. Bilal akizungumza wakati wa Kilele cha maadhimisho ya sherehe hizo kwenye Viwanja vya Furahisha jijini Mwanza leo, Juni 5
HOTUBA YA MHE. DKT. MOHAMMED GHARIB BILAL,  MAKAMU WA RAIS WA JAMHURI YA  JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, KWENYE KILELE CHA MAADHIMISHO YA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI,
TAREHE 5 JUNI, 2014 MKOANI MWANZA
Kwanza kabisa nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema, kwa kutujaali uzima na afya njema, na kutuwezesha kukusanyika hapa, kushuhudia tukio hili adhimu.

Nitumie nafasi hii kuushukuru uongozi wa Mkoa wa Mwanza, mikoa jirani, na wadau mbalimbali walioshiriki kwa njia moja ama nyingine, kufanikisha Maadhimisho haya, ambayo yamefana sana.  Hongereni sana! Niwashukuru pia kwa mapokezi makubwa na moyo wa ukarimu, mliouonesha kwangu na ujumbe wangu, tangu tulipowasili hapa. Asanteni sana!

Ndugu Wananchi;
Mabibi na Mabwana;
Leo Watanzania tunaungana na jamii ya kimataifa duniani kote kuadhimisha kilele cha Siku ya Mazingira Duniani. Siku hii muhimu huadhimishwa kwa lengo la kukumbushana na kuelimishana kuhusu umuhimu wa mazingira na wajibu wa jamii katika kuyatunza kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo.

Ujumbe wa Siku ya Mazingira Duniani mwaka huu ni: ”Chukua Hatua Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi” (Raise Your Voice, Not the Sea Level). Kitaifa, kaulimbiu inayoongoza maadhimisho haya ni “Tunza Mazingira ili Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi”. Kaulimbiu hii inatukumbusha kuchukua hatua na wajibu tulionao wa kukabiliana na  athari za Mabadiliko ya Tabianchi.

Ndugu Wananchi;
Tunafahamu kwamba, mabadiliko ya tabianchi yanachangiwa na mrundikano wa hewa ukaa inayotokana na shughuli za maendeleo inayofanywa na binadamu kama vile viwanda, kilimo, usafirishaji n.k. Sehemu kubwa, yaani asilimia 97, inachangiwa na nchi zinazoendelea. Ingawa mrundikano uliopo sasa umesababishwa na nchi zilizoendelea. Nchi masikini kama Tanzania ndizo zinazoathirika kwa kiwango kikubwa.

Athari za mabadiliko ya tabianchi sasa ni dhahiri katika maeneo mengi duniani kote. Tumeshuhudia ukame uliokithiri, majira ya mvua yasiyotabirika, mafuriko, kuongezeka kwa joto duniani, kuongezeka kwa kina cha bahari  na kuzama kwa baadhi ya visiwa vidogo; kukauka kwa vyanzo vya maji na kupungua kwa kina cha maziwa. Wananchi wanaoishi katika maeneo hayo, ni wahanga na mashuhuda wa matukio hayo ya kusikitisha. Katika baadhi ya maeneo maisha ya watu, mifugo na mali zao, vimepotea kutokana na athari hizo.

Ndugu Wananchi;
Nchi yetu imeshuhudia athari za mabadiliko ya tabianchi katika sekta zote za uchumi. Baadhi ya sekta za uchumi zinazoathirika zaidi kutokana na mabadiliko ya tabianchi ni Sekta ya Kilimo, Nishati, Maji, Miundombinu, Mifugo, Afya na Maliasili. Nitafafanua  kama ifuatavyo:- 

Sekta ya Kilimo: Sekta hii imeathirika sana kutokana na ukosefu wa mvua za uhakika na ukame wa mara kwa mara unaosababisha uzalishaji hafifu wa mazao ya kilimo hivyo kuchochea tatizo la njaa nchini na kulazimisha Serikali kuwapa chakula wananchi ambao wana uwezo wa kuzalisha na kujilisha wenyewe.

Sekta ya Nishati: Sote tunatambua kuwa nchi yetu imekuwa ikitegemea zaidi nishati ya umeme unaotokana na nguvu za maji kwa miaka mingi. Kutokana na mabadiliko ya tabianchi, vina vya maji katika mabwawa ambayo ni vyanzo vikuu vya nishati ya umeme, vimekuwa vikishuka hadi kufikia chini ya viwango hususan katika msimu wa kiangazi, hivyo kuathiri upatikanaji umeme katika maeneo mengi nchini.

Miundombinu: Katika miaka ya hivi karibuni kumekuwa na matukio mengi ya mafuriko. Kwa mwaka huu, mafuriko yamegharimu maisha ya Watanzania wenzetu na kuharibu miundombinu na makazi ya watu huku yakiacha madhara makubwa katika mashamba yao. Kwa mfano katika Jiji la Dar es Salaam, zaidi ya Shilingi Bilioni 20 zitahitajika kurejesha miundombinu ya barabara. Aidha, mafuriko yaliyotokea Morogoro mwaka huu yameleta hasara kubwa kwa Taifa.

Sekta ya Mifugo:  Taifa limeshuhudia kuongezeka ukame mara kwa mara ulioleta maafa makubwa kwa jamii za wafugaji katika mikoa ya Kaskazini mwa nchi yetu kwa mifugo mingi kufa kwa kukosa maji na malisho, tatizo ambalo limesababisha hata migongano kwenye matumizi ya ardhi. Kutokana na ukame uliotokea mwaka 2006, Serikali ilibidi kuwafidia na kuwapa ruzuku wananchi waliopoteza mifugo yao yote.

Sekta ya Afya: Athari za kiafya zinazohusiana na mabadiliko ya tabianchi, zimeripotiwa nchini ikiwa ni pamoja na ugonjwa wa malaria ambao umesambaa katika maeneo yenye baridi hususan maeneo ya miinuko (Nyanda za Juu Kusini, Kilimanjaro, Arusha na Lushoto) ambayo awali hayakuwa na ugonjwa huu. Kwa takribani mwezi mmoja sasa, nchi yetu inakabiliana na ugonjwa wa “Dengue” unaosabishwa na virusi vinavyoenezwa na mbu aina ya “Aedes.” Mbu hawa huzaliana kwa wingi katika vipindi vya mvua nyingi.

Sekta ya Maji: Kutokana na mabadiliko ya tabianchi, vyanzo vingi vya maji nchini vimekuwa vikipungua kwa kasi kubwa. Kwa mfano, tangu mwaka 1972 kiasi cha maji katika mto Mara, kimeshuka kwa asilimia 68 hususan, katika msimu wa kiangazi, ikiashiria uwezekano wa kuathiri idadi ya wanyama wanaotegemea mto huo katika mifumo Ikolojia ya Serengeti. Aidha, kiasi cha maji katika mito ya Kilombero na Rufiji kimepungua kwa asilimia 8 tangu mwaka 1972. Vile vile, vina vya maji katika Ziwa Victoria, Tanganyika, Manyara, Rukwa na Jipe, vimeendelea kupungua kwa kasi kubwa.

Sekta ya Maliasili: Sote tunafahamu, Tanzania ina maliasili nyingi katika misitu, mapori na maji. Katika maeneo haya kuna mimea, wanyamapori, samaki, wadudu, na viumbe wengine wa majini na nchi kavu. Baadhi ya mimea, wanyamapori na viumbe wengine ni wachache na hawapatikani popote duniani isipokuwa hapa nchini kwetu. Viumbe wengi hawa, sasa wako hatarini kutoweka kutokana na uharibifu wa mazingira na athari za mabadiliko ya tabianchi.
  
Ndugu Wananchi;
Mabibi na Mabwana;
Ili kupunguza au kudhibiti athari hizi za mabadiliko ya tabianchi, zinazotishia jitihada zetu za kujiletea maendeleo, ni muhimu tuchukue hatua za kuhakikisha tunatunza na kuhifadhi mazingira yetu. Tupande miti na kutunza misitu yetu ili itusaidie kunyonya hewa ukaa zinazosababisha mabadiliko ya tabianchi. Katika ngazi ya Kimataifa, tutaendelea kuzishinikiza nchi zilizoendelea, kuchukua hatua mahsusi za kupunguza uzalishaji wa gesijoto na kusaidia nchi zinazoendelea kuhimili na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

Ndugu Wananchi;
Pamoja na kwamba Kitaifa, Maadhimisho haya yanafanyika hapa Mwanza, Watanzania kote nchini, katika Mikoa na Wilaya hadi Vijijini, wameungana nasi katika kuadhimisha siku hii kwa lengo lile lile la kuelimishana na kuhamasishana juu ya umuhimu  wa utunzaji wa mazingira, utunzaji wa  vyanzo vya maji ikiwa ni pamoja na misitu, milima, uoto wa asili, maziwa, mabwawa, mito, visima na vijito. Aidha, kwa upande wa uvuvi, shughuli za uvuvi zifuate misingi na kanuni za uvuvi endelevu inayopiga marufuku matumizi ya sumu na vifaa vya uvuvi visivyozingatia uvuvi endelevu kama vile makokoro, baruti na nyavu zisizoruhusiwa.

Ndugu Wananchi;
Pamoja na athari za mabadiliko ya tabianchi, mazingira ni sehemu ya maisha ya binadamu, na ndio uhai wa Taifa lolote lile. Binadamu hawezi kuishi bila ardhi, maji, mimea na hewa. Hata hivyo pamoja na umuhimu huo, tunaendelea kushuhudia uharibifu mkubwa wa mazingira katika nchi yetu kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo; Kilimo kisichoendelevu  kinachofanyika katika maeneo ya vyanzo vya maji, kwenye vilele na miteremko mikali ya safu za milima;  Matumizi mabaya ya dawa za kilimo, mifugo na za viwandani; Kilimo cha umwagiliaji kisichoendelevu; Matukio ya moto na uchomaji moto misitu; Uchimbaji madini usioendelevu na mrundikano wa taka katika maeneo ya miji na makazi yetu. Vilevile, wingi wa mifugo inayozidi uwezo wa malisho, husababisha upungufu wa maji na malisho, hivyo kuchangia  migongano baina ya wadau mbalimbali katika matumizi ya ardhi. 

Ndugu Wananchi;
Mabibi na Mabwana;
Sote kwa pamoja tunao wajibu wa kutafuta ufumbuzi wa kudumu wa matatizo haya, kila mmoja kwa nafasi yake. Yako mambo mengi ambayo yanahitaji mikakati ya kudumu ili kuhakikisha kwamba shughuli za maendeleo ya kiuchumi haziathiri mazingira.  Mambo haya ni pamoja na:-
     i)        Kuhifadhi ardhi na kupanda miti;
    ii)        Kudhibiti uchomaji moto ovyo;
  iii)        Kuhifadhi vyanzo vya maji, milima na misitu ya asili;
  iv)        Kudhibiti uchafuzi wa mazingira katika maeneo ya makazi na viwandani;
    v)        Ujenzi na matumizi ya vyoo bora;
  vi)        Kudhibiti kilimo na uchimbaji madini usioendelevu;
 vii)        Kudhibiti matumizi  mabaya ya dawa za mifugo na kilimo;
viii)        Kuimarisha vikundi vya usimamizi wa uvuvi;
  ix)        Kuanzisha au kuimarisha kamati za mazingira katika ngazi zote;
    x)        Kusimamia uzalishaji bora usiochafua mazingira kwenye viwanda vyetu; na
  xi)        Kulinda mazingira ya maeneo ya pwani, bahari, mito, maziwa na mabwawa.

Ndugu Wananchi;
Kazi ya kuhamasisha na kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa hifadhi ya mazingira, inahitaji juhudi za vyombo mbalimbali katika ngazi zote. Niombe vyombo vya habari, taasisi zote za Serikali na asasi za kiraia, tusaidiane katika hili.

Hatuna budi kushirikiana ili kutekeleza Sheria na Kanuni za hifadhi ya mazingira katika kila ngazi ya uongozi kote nchini.  Aidha, katika kila ngazi hizo,  pawe na mipango ya matumizi bora ya ardhi; mikakati bora ya kudhibiti uvuvi haramu na ufugaji usio endelevu. Wizara na taasisi husika kwa kushirikiana na jamii yote, ziendeleze mafanikio yaliyokwishapatikana kwa kusimamia ipasavyo Sheria na Kanuni zilizopo.

Aidha, Kampeni ya Kitaifa ya Upandaji Miti iendelezwe na juhudi zielekezwe katika kuitunza na kuihudumia miti iliyopandwa. Ningependa kusisitiza kwamba utamaduni tuliouanza wa kupanda miti, kutunza misitu na uoto wa asili, tuuendeleze na kuudumisha. Nitumie fursa hii, kupongeza mikoa iliyovuka malengo ya upandaji miti Milioni 1.5 kwa kipindi cha mwaka 2012/2013.  Mikoa hiyo ni Kagera, Mbeya, Njombe, Ruvuma, Iringa na Tanga.

Ndugu Wananchi;
Katika Maadhimisho haya, tuzo zimetolewa kwa washindi wa ngazi ya Kitaifa, waliojitokeza katika Mashindano ya Tuzo ya Rais ya Kuhifadhi Vyanzo vya Maji, Kupanda na Kutunza Miti, ambayo hutolewa kila baada ya miaka miwili. Nitumie fursa hii, kupongeza mikoa 17 iliyoshiriki katika mashindano haya. Mikoa hiyo ni:- Dodoma, Iringa, Kagera, Katavi, Kilimanjaro, Lindi, Manyara, Mara, Mbeya, Morogoro, Mwanza, Mtwara, Pwani, Ruvuma,  Shinyanga, Simiyu na Tanga.  Natoa wito kwa Mikoa ambayo haikushiriki, wahakikishe wanahamasisha wananchi wao kushiriki mashindano haya.

Nitumie fursa hii kuwapongeze washindi wa Tuzo hii, kwa juhudi kubwa walioifanya katika kuhifadhi vyanzo vya maji, kupanda na kutunza miti. Washindi hawa wawe mfano wa kuigwa na jamii yote ya Watanzania. Vilevile, niwapongeze wale wote waliojitokeza kushiriki mashindano haya, hata kama hawakuibuka washindi, ujasiri mliouonesha ni kielelezo tosha kuwa ni wana mazingira nambari moja.  Natoa wito kwa wananchi kote nchini kujitokeza kwa wingi kushiriki mashindano ya Tuzo hii itakayotolewa tena tarehe 5 Juni, 2016, Mwenyezi Mungu akitujalia uzima. 

Ndugu Wananchi;
Wageni Waalikwa;
Mabibi na Mabwana;
Kabla ya kuhitimisha hotuba yangu, kwa mara nyingine, napenda  kuushukuru na kuupongeza Uongozi wa Mkoa wa Mwanza kwa maandalizi mazuri ya Maadhimisho ya Siku ya Mazingira nchini.  Nizipongeze tena taasisi, vikundi na watu binafsi kwa ushirikiano wao katika kufanikisha maadhimisho haya.  

Napenda niwakumbushe jambo moja muhimu sana, katika kufanikisha suala zima la Uhifadhi na Utunzaji wa Mazingira yetu; Ili tufanikiwe katika jambo hili;  Lazima tuifanye kila siku kuwa Siku ya Maadhimisho ya Mazingira Duniani. Tuchukue Hatua Kutunza Mazingira yetu ili Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi.

Mwisho kabisa, Kwa heshima kubwa na taadhima  natamka kwamba; Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani yamefikia Kilele.


Ahsanteni  sana kwa kunisikiliza.