ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, August 25, 2012

SIKILIZA ALICHOKISEMA MASHA LEO WAKATI AKICHUKUWA FOMU KUGOMBEA NAFASI UJUMBE WA NEC WILAYA YA NYAMAGANA

Mh. Lawrance Masha akichukuwa fomu kugombea nafasi ya U-NEC Wilaya ya Nyamagana kwa Katibu wa CCM Wilaya ya Nyamagana Deogratius Lutta tukio hilo limefanyika leo katika ofisi za CCM Nyamagana jijini Mwanza.

Mh. Lawrance Masha akisaini kwenye daftari la waliochukuwa fomu kugombea nafasi ya U-NEC kupitia Wilaya ya Nyamagana mbele ya Katibu wa CCM Wilaya ya Nyamagana Deogratius Lutta (aliyeshika kichwa) sambamba na wadau wengine walio msindikiza kukamilisha zoezi hilo.
Mchakato wa kugombea nafsi ya U-NEC wilaya ya Nyamagana ni pamoja na Bw. Emmanuel Masalu Ngofilo, Mwenyekiti wa CCM Kata ya Mahina Bw. James Bwire, Bw. Bakari Kimwaga, Afisa Uhusiano wa MWAUWASA Bw. Robert Maswanya na Othman Ally.

Wengine ni Faraj S Faraj, Moric Deya, James Joseph Nyamasiriri na Lawrance Masha aliyechukuwa leo.

Mh. Lawrance Masha

Sikiliza hapa wakati akizungumza na waandishi wa habari. (Bofya Play)

MAMBO YA SERENGETI FIESTA 2012, TANGA.


 Watangazaji wa Clouds Fm Adam Mchomvu akiongea na wakazi wa jiji la Tanga na vitongoji vyake juu ya ujio wa tamasha la Serengeti Fiesta 2012 linalotarajia kulindima kesho Jumapili Uwanja wa Mkwakwani na kupabwa na wasanii mbali mbali ikiongozwa na Prezzo kutoka Kenya. Kiingilio cha shilingi elfu tano (5,000).

Gari la kurusha matangazo live bila chenga likiwa eneo la Komesho, Tanga ambapo matangazo yalikuwa yanarushwa moja kwa moja kutoka Tanga.
 Kila kijana alipata nafasi ya kuonyesha kipaji chake.

 Gossip Cop TZ, Sudi Brown akionyesha manjonjo yake katika staili yake ya ninja.

Katika burudani ya nje, hakuna aliyetaka kupitwa.
Wananchi wakifuatilia kwa makini.
 ...haya twendeee

 Show love nayo ilikuwepo.

Mwanadada akionyesha umahili wake wa kudata na biti hadi Mtangazaji wa Clouds Fm Adam Mchomvu akamkubali.

Wameng'aa.

 Mama kafurahi baada ya kupewa t-shirt.


Na ming'aro ya kutosha.
Nyomi ya kutosha.

MASHABIKI ARSENAL WAMTEMEA MOTO ROBIN VAN PERSIE

Urban Pulse na Freddy Macha waweletea habari moto moto siku moja baada ya kutangazwa kuhama kwa mshambuliaji na nahodha wa Arsenal, Robin Van Persie kwenda Manchester United  adui  wake mkubwa. Mahojiano yalifanywa kando kando ya uwanja maarufu wa Emirates ambapo washabiki walikuwa wakielekea kufurahia mechi ya kwanza ya ligi (2012-2013) baina ya Arsenal na Sunderland.

FROM MOSHI KITU LIVE KWA CLOUDS TV USIKU HUU

Kama unafuatilia kupitia luninga yako bila shaka unainjoi vilivyo...... usiku huuu.......

Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,Mh Leonidas Gama akimtaja mshindi aliyejinyakulia gari aina ya Vits iliyokuwa ikinadiwa kwenye tamasha la Serengeti Fiesta 2012,maara baada ya kuchezeshwa droo usiku huu,pichani mwanzo kulia ni Mkurugenzi wa Masoko kampuni ya bia ya Serengeti,Ephraim Mafuru,Muwakilishi kutoka michezo ya bahati nasibu ya Taifa,Abdallah Mohamed akishuhudia tukio hilo,na mwisho kushoto ni Mkurugenzi wa kampuni ya Clouds Media Group,Joseph Kusaga pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Moshi Mjini,Mh Dr Msengi wakishuhudia tukio hilo usiku huu ndani ya uwanja wa chuo cha ushirika.

Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,Mh Leonidas Gama sambamba na Mkuu wa Wilaya ya Moshi Mjini,Mh Dr Msengia wakiingia kwa shangwe kwenye jukwaa la Serengeti Fiesta 2012 usiku huu kwa ajili ya kulizindua tamasha hilo ambalo limepokelewa vyema kwa wakazi wa mji huo na vitongoji vyake.Pichani kulia ni Dj Zero akikamua vilivyo.

Dj Pq kutoka Clouds FM akikamua vilivyo kwenye mashine,kati ni mtangazaji wa Clouds FM B Dozen na mdau mwingine wakifuatilia kwa makini makamuzi yanayoendelea usiku huu,ambapo washabiki kibao wamejitokeza ndani ya uwanja wa chuo cha ushirika.

Sanaa ya home na asili.

Pichani shoto ni msanii kutoka THT,Recho sambamba na wacheza shoo wake wakitumbuiza jukwaani usiku huu ndani ya tamasha la Serengeti Fiesta 2012.

Moja ya kikundi mahiri  kutoka THT kkikionesha mbwembwe zake jukwaani.

THT na mbwembwe zaidi.

Dj Zero akikamua vilivyo.

Moja ya kikundi cha  THT kikiwa katika picha ya pamoja.

Baadhi ya wakazi wa mji wa Moshi na vitongoji vyake waliojitokeza kwenye tamasha la Serengeti Fiesta usiku huu ndani ya Uwanja wa chuo cha Ushirika mjini Moshi.

Recho's dance.

Ze colour.

Baadhi ya wasanii nyota wa filamu nchini nao wakishuhudia tamasha la Serengeti Fiesta usiku huu.

Hapatoshi usiku huu.
Moshiiiii hapatoshiiiii.
Msanii wa kizazi kipya Sheta akiwaimbisha washabiki wake waliojitokeza kwa wingi usiku huu ndani ya tamasha la Serengeti.

Ze pipoz usiku huu ndani ya tamasha la Serengeti.

Back side...

MATONYA AFARIKI DUNIA, MAKAMBA AMLILIA



Mzee Paulo Mawezi maarufu kama Matonya akiwa na mwanae Elizabath wakiwa katika Kijiiji cha Mpamantwa Tarafa ya Bahi Mkoani Dodoma. Picha hii ilipigwa 2010 wakati alipokwenda kwa mapumziko ya sikukuu ya Krismas. Picha na Maktaba
Habel Chidawali, Bahi
LICHA ya umaarufu mkubwa aliokuwa nao na kufahamika katika miji mingi nchini, ombaomba Paul Mawezi maarufu kwa jina la Mzee Matonya, amefariki dunia na kuzikwa katika mazingira ya ufukara mkubwa.
Matonya alizikwa jana kijijini kwake Mpamantwa, Wilaya ya Bahi, Dodoma akiwa amevishwa nguo moja nyeusi, huku mwili wake ukibebwa na watu wasiozidi 20, waliotumia ngozi kuu kuu ya ng’ombe.

Matonya aliyekuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa kikohozi tangu Mei mwaka huu, alifariki dunia juzi usiku na kuzikwa jana saa saba mchana mita tatu kutoka katika nyumba yake ya tembe alimokuwa akiishi.

Ndugu na jamaa zake wa karibu walisema Matonya ambaye umri wake unakadiriwa kuwa zaidi ya miaka 90, hakuwahi kwenda kutibiwa hospitali kutokana na ukosefu wa fedha.

Mwandishi wetu alishuhudia idadi ndogo ya waombolezaji nyumbani kwa Matonya, huku watoto wake watatu waliokuwapo msibani hapo kati ya watano aliowaacha hai, wakisema kuwa baba yao amefariki kutokana na umaskini na ufukara.

“Hatukuweza kumpeleka hata hospitali kupata vipimo kwani hatukuwa na uwezo wa kwenda mjini Dodoma kutokana na kukosa hata nauli, ndiyo maana tumekuwa kimya hadi Mungu alipomchukua,’’ alisema mmoja wa watoto hao, David Paulo.

Umaarufu wa Matonya
Umaarufu wa Matonya ulitokana na staili yake ya kuomba kwa kulala chali barabarani, huku akiwa ameinua kopo juu bila ya kujali jua au mvua.

 Kwa nyakati tofauti alipinga mpango wa Serikali wa kumrejesha kwao Bahi na mara kadhaa alimweleza aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Yusufu Makamba kuwa yeye ni mtoto wa mjini hivyo asingemuweza. Aliingia Dar es Salaam kwa mara ya kwanza Desemba 7, 1961.

Katika siku za karibuni, alikuwa gumzo kwa Serikali na viongozi huku akipachikwa jina la Komandoo na Kiboko ya Makamba.

Baada ya kuondolewa Dar es Salaam, aliweka makazi yake mapya ya kuomba mkoani Morogoro hususan eneo la Darajani, ambako aliendeleza staili ya kuomba akiwa amelala chali na kuinua kopo juu kwa muda mrefu bila kuchoka.
Iliwahi kuvuma kwamba ombaomba huyo alikuwa na utajiri mkubwa, jambo ambalo mtoto wake mkubwa, Elizabeth Paulo alilipinga na kusema kwamba halina ukweli na hakuacha chochote.

Mke wa Marehemu Paulina alisema walitengana na Matonya zaidi ya miaka 37 iliyopita na wakati huo alikuwa na mali nyingi (ng’ombe). “Tulipotengana tu, mimi nilirudi kwetu na watoto wangu walikuwa bado wadogo na bahati mbaya mdogo wake aliyekuwa akitunza ng’ombe (wa Matonya) alifariki dunia na huo ukawa ndiyo mwanzo wa kumaliza mifugo yote kwani watu waliwaiba wote,’’ alisema Paulina.

Matonya alirudi kijijini kwake Mpamantwa kwa ajili ya mapumziko ya Krismasi Novemba, 2010 akitokea Morogoro kama ilivyokuwa kawaida yake na tangu wakati huo hakurudi tena.

Makamba amlilia
Akizungumzia msiba huo, Makamba ambaye alifanikisha mpango wa kumwondoa Matonya Dar es Salaam, alisema amesikitishwa na kifo hicho cha mtu aliyemtaja kuwa alikuwa rafiki yake mkubwa

CHANZO: MWANANCHI

UMOJA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA MKOA WA MWANZA WAGOMEA SENSA.


Makamu Mweneyekiti wa Umoja wa Wenyeviti wa serikali za mitaa mkoa wa Mwanza Hamza Yusuph Shido akitoa tamko la Umoja huo kutoshiriki SENSA ya watu na makazi, pembeni yake ni Mwita Marwa Meteti ambaye ni katibu mkuu wa umoja huo.
Sikiliza tamko lao kwa ufupi. (Bofya play)
Makamu Mweneyekiti wa Umoja wa Wenyeviti wa serikali za mitaa mkoa wa Mwanza Hamza Yusuph Shido (katikati) akitoa tamko la Umoja huo kutoshiriki SENSA ya watu na makazi, kulia ni Mwita Marwa Meteti ambaye ni katibu mkuu wa umoja huo na kushoto ni naibu katibu wa umoja huo Kipara Mc, Mlemela, Tamko hilo limetolewa ndani ya ukumbi wa ofisi za MPC jana jioni.
BAADHI YA MALALAMIKO YAO.
-Wakanusha makarani wa SENSA kutokea mitaa yao: wengi hawawafahamu.
-Wadai kuwa vijana hawakuchaguliwa badala yake waliopewa ni ndugu za wafanya mchujo.
-Wameamua kususia zoezi la kusimamia SENSA kwani wanafanyishwa kazi katika mazingira magumu hawalipwi posho, wametelekezwa, walaumu kutohusishwa katika uwezeshwaji tokea awali kwenye michakato.
Walioketi mezani mbele ni sehemu ya Wanaumoja wa Wenyeviti wa serikali za mitaa mkoa wa Mwanza waliohudhuria mkutano huo wa kutoa tamko mbele ya waandishi wa habari.

Sehemu ya kusanyiko hilo.

Friday, August 24, 2012

WASANII NYOTA BONGO MOVIE WAVAMIA MJI WA MOSHI KUSHANGWEKA NA FIESTA YA KWANZA MWAKA 2012

Mmoja wa wasanii mahiri katika fani ya uigizaji hapa nchini,Wema Sepetu akifanya mahojiano mafupi na Millard Ayo wa Clouds FM mapema leo kwenye amsha amsha ya tamasha la Serengeti Fiesta ambalo linafanyika jioni ya leo mpaka lyamba ndani ya uwanja wa chuo cha Ushirika,ndani ya mji wa Moshi,ambapo katika tamasha hilo kiingilio kimepangwa kuwa ni nusu mnyama tu a.k.a 5,000/= kwa kila kichwa.

Wema Sepetu pia akizungumzia ujio wao ndani ya mji wa Moshi,kuwa wao kama Wasanii Nyota wa Filamu wamewasili mkoani humo kusaka vipaji vipya mbalimbali vya filamu,usahili huo unafanyika kwenye ukumbi wa Mr Price,ulioko mtaa wa Malindi.

Mtangazaji wa Clouds FM,Millard Ayo akiwa Live mapema leo mtaa wa Malindi katika mpango mzima wa amsha amsha kwa wakazi wa Moshi kuhusiana na tamasha la Serengeti Fiesta 2012,ambapo pia katika tamasha hilo kutatolewa zawadi mbalimbali ikiwemo gari ndogo aina ya Vits kama uinavyo pichani ikinadiwa vilivyo.

Kawa kawa amsha amsha ya tamasha la Serengeti Fiesta pia linatoa mafuta kwa magari daladala,pikipiki sambamba na baji lita 10 ama tano kutoka kampuni ya Gapco ambao pia ni sehemu ya wadhamini wa tamasha hilo.

Msanii mwingine nyota katika tasnia ya filamu,Aunt Ezekiel akielezea ni namna tamasha la Serengeti Fiesta lilivyowambamba wakazi wa mji wa Moshi na vitongoji vyake,na pia ujio wao kuwatafuta wasanii wapya chipukizi katika tasnia hiyo ambayo imekuwa ikikua siku hadi siku.

Wema Sepetu katika pozi na washabiki wake mapema mchana huu.

Mastaa wetu wa filamu hapa nchini,wametokelezeaje sasaaa.

Kiongozi wa msafara wa tamasha la Serengeti Fiesta 2012,Mully B akiwa na mastaa wa filamu,Wema Sepetu na Aunt Ezekiel afu fulllll BBM kama kawa.

Millard Ayo akifanya mahojiano na Ray a.k.a Vincent Kigosi kuhusiana na ujio wao ndani ya  mji wa Moshi

Kutoka kushoto ni Mr Hatman,Steve Nyerere,Bonge pamoja na Millard Ayo katika shoo love ya pamoja.

Wema Sepetu akijiweka sawa.

Wakiwa katika mazungumzo yao ya hapa na pale.

Kila mmoja ana haki ya kupata habari na kuhabarishwa.

Ha-ha-ha-ha....
Pichani ni Gari aina ya Vits itakayotolewa jioni ya leo kwenye tamasha la Serengeti Fiesta 2012,kwa mshindi atakaejishindia kwenye droo itakayofanyika katika uwanja wa chuo cha ushirika,ambako tamasha hilo litarindima mpaka majogoo.

Jacob Steven a.k.a Steven akifafanua jambo mapema leo mtaa wa Malindi kuhusiana na suala zima la wasanii hao kulivamia jiji la Moshi