ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, September 17, 2016

BATA ZA DEBE NA JEMBE FM USO KWA USO NA DJ CREME DE-LA CREME.

CEO wa Jembe Media Group Dr. Jembe (Right) akionesha kukubali kazi ya Dj Creme De-la Creme akika usiku wa burudani na Jack  Daniels ndani ya Regency Park jijini Dar es salaam.
Dj Creme De-la Creme na mizuka yake.....
Dj Creme De-la Creme aki-show love kwa photo na Montana.
In na de area.
We mba-ya....!!!!
Hatariiiiiiiiiiii.....
With flowers....
TMC za Dar.
SwagZ.
African dance ni afya .....
style.....
Kutoka Jembe DJz wakuitwa Dj Mike Beatz akiteta jambo na Dj Creme De-la Creme toka nchini Kenya.
What......!!!!?
Stimu zimelipiwa.....
Me, my Boss and them.
DjZ.
We....
Pamoja sana.

JOGGING SIO UHUNI,KUNA WATU WALITAKA KUPENYEZA MAMBO YAO NA KUTAKA KUICHAFUA JOGGING- DC ILALA

Mkuu wa wilaya ya Ilala Mh Sophia Mjema (pili kulia) akiwa sambamba na Katibu Tawala wa wilaya hiyo Edward Mpogolo (tatu kushoto) wakishiriki mazoezi ya pamoja ya kikundi cha klabu ya Mazoezi cha New Life Jogging,na vikundi vingine mbalimbali vya mazoezi , mapema leo asubuhi katika viwanja vya Kimanga,Tabata Mawenzi,jijini Dar,ambapo Mkuu wa Wilaya alialikwa kuwa mgeni rasmi kwenye hafla fupi ya kikundi cha New Life Jogging kilipokuwa kinatimiza mwaka mmoja tangu kuanzishwa kwake.PICHA NA MICHUZI JR-MMG.
Mkuu wa wilaya ya Ilala Mh Sophia Mjema akikabidhiwa Risala na Mwenyekiti wa kikundi cha Newa Life Jogging,Baraka Urio akiwa ameambatana na wanachama wa kikundi hicho,mara baada ya kuisoma na kuelezea changamoto na fursa mbalimbali zilizopo ndani ya kikundi hicho.Kikundi hicho chenye makazi yake Tabata Mawenzi leo kimetimiza mwaka mmoja tangu kuanzishwa kwake.
Mkuu wa wilaya ya Ilala Mh Sophia Mjema akizungumza mbele ya vikundi mbalimbali vya mazoezi (havipo pichani),vilivyoshiriki kwenye hafla hiyo fupi ya kutimizwa mwaka mmoja wa kikundi cha New Life Jogging.Mh.Mjema aliwataka viongozi wa vikundi hivyo kuelezea changamoto zao walizo nazo ikiwemo na fursa zilizopo ili serikali kupitia Ofisi yake ziweze kufanyiwa kazi kwa wakati.Mh Mjema alisema kuwa Jogging sio uhuni,isipokuwa kuna watu walitaka kupenyeza mambo yao katika Jogging.

"Lakini wale waliotaka kuyapenyeza hayo,waliotaka kuingiza uhalifu,waliotaka kupenyeza madawa ya kulevya ,waliotaka kuingiza siasa,waliotaka kuingiza Panya rodi washindwe na walegee,hatutaki Jogging zetu zichafuke,tunataka Jogging zitumike kuona fursa zilizopo",alisema Mh Mjema.
Katibu Tawala wilaya ya Ilala,Ndugu Edward Mpogolo akiwasalimia na kuwatia moyo vikundi hivyo vya Jogging,ambaye pia aliwaeleza kuwa wakati wa kujituna na kufanya kazi ni sasa,hivyo amewaomba viongozi wa vikundi hivyo kukutana nao ili kuhakikisha fursa na changamoto walizozieleza katika risala yao zinafanyiwa kazi kwa wakati.
Mkuu wa wilaya ya Ilala Mh Sophia Mjema akikabidhiwa jezi na Mwenyekiti wa kikundi cha New Life Jogging,Baraka Urio,pichani kati ni Katibu Tawala wilaya ya Ilala,Ndugu Edward Mpogolo na wadau wengine wakishuhudia tukio hilo.
Mgeni rasmi,Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mh.Sophia Mjema na viongozi wengine waandamizi kutoka ofisi ya Mkuu wa wilaya wakiwa katika picha ya pamoja na Kikundi cha New Life Jogging,ambacho leo kinasherehekea kutimiza mwaka mmoja tangu kuanzishwa kwake.
Vikundi mbalimbali vilishiriki kwenye mazoezi hayo ya pamoja.

MAGAZETI YA LEO:- KACHERO WA POLISI AHUKUMIWA KIFO, MBONGE AIBWAGA NHC KORTINI, NEEMA YAWASHUKIA WAATHIRIKA BUKOBA

Neema yawashukia waathirika Bukoba,kachero wa polisi ahukumiwa kifo, Mbowe aibwaga  NHC kortini, mawaziri watoro bungeni sasa kushitakiwa. Pata dondoo za magazeti ya leo hapa. 

Uhai wa Bageni sasa mkononi mwa JPM, Lowassa, Maalim Seif kutinga mechi ya Simba na Yanga, NHC wakwama tena kesi ya Mbowe.Pata dondoo za magazeti ya leo hapa.

BENKI YA CBA YAJA NA HUDUMA ZA KISASA ZA KIBENKI

Afisa Mtendaji Mkuu wa benki ya CBA Tanzania, Dk Gift Shoko akizungumza na wateja mashuhuri wa benki hiyo katika uzinduzi wa huduma ya ‘Private Banking’ uliofanyika jinni Dar es Salaam hivi karibuni. Kufuatia uzinduzi wa huduma hiyo ya ‘Private Banking’, sasa wateja wa benki ya CBA watapata huduma za kipekee na murua zenye kuwawezesha kufanya miamala kwa ufanisi, haraka na mazingira mwanana. Picha zote na Cathbert Angelo Kajuna wa Kajunason Blog. Mgeni rasmi na Mwenyekiti wa CEO Round Table nchini, Ali Mufuruki akizungumza na wateja mashuhuri wa benki ya CBA Tanzania katika uzinduzi wa huduma ya ‘Private Banking’ uliofanyika jinni Dar es Salaam hivi karibuni. Kufuatia uzinduzi wa huduma hiyo ya ‘Private Banking’, sasa wateja wa benki ya CBA watapata huduma za kipekee na murua zenye kuwawezesha kufanya miamala kwa ufanisi, haraka na mazingira mwanana. Mwenyekiti wa Tanzania CEO Roundtable, Ali Mufuruki akipokea zawadi kutoka kwa Afisa Mtendaji Mkuu wa benki ya CBA, Dk. Gift Shoko wakati wa uzinduzi wa huduma ya ‘Private Banking’ jijini Dar Es Salaam hivi karibuni. Mufuruki alikuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo. Kufuatia uzinduzi wa huduma hiyo ya ‘Private Banking’, sasa wateja wa benki ya CBA watapata huduma za kipekee na murua zenye kuwawezesha kufanya miamala kwa ufanisi, haraka na mazingira mwanana. Wageni waalikwa. ---
Benki ya CBA yaja na huduma za kisasa za kibenki 

Katika mkakati wake wa kuendelea kuboresha huduma zake nchini,Benki ya CBA imezindua huduma mpya kwa wateja wake binafsi zitakazowawezesha kupata huduma za kibenki kwa njia ya teknolojia ya kisasa  ya kupata huduma za kibenki kimtandao kupitia simu zao za mkononi. 

Akiongea wakati wa uzinduzi wa huduma hii mpya,Afisa Mtendaji Mkuu wa CBA Tanzania,Dk.Gift Shoko,alisema kuwa huduma hizi zimelenga kuwarahisishia maisha wateja na kuwawezesha kupata huduma za kibenki kulingana na matakwa yao na kwenda sambamba na mtindo wa maisha wanaoishi. 

Alisema pia wateja wa CBA Tanzania kuanzia sasa wanaweza kutumia kadi za kimataifa za kufanya mihamala ya malipo za Visa Platinum Debit Card na Visa Gold Credit Card kwa fedha za kitanzania na Dola za Kimarekani ambazo zinawawezesha kupata huduma mbalimbali wakiwa katika uwanja wa ndege wa JKIA kwenye sehemu ya kupita watu maarufu (VIP lounge).Alisema huduma hii itawawezesha wateja wa kundi hili kufanya mihamala wakiwa katika viwanja vya ndege 600 kwenye nchi 1,000 na miji mikubwa  ipatayo 300 duniani kote. 

“Tunazidi kurahisisha huduma za kibenki kwa wateja ili wazipate popote na kwa wakati wowote watakapokuwa bila kupoteza muda kama ilivyokuwa hapo awali”.Alisema. 

Kitengo cha kuhudumia wateja watakaojiunga na huduma hii kwa kuanzia itapatikana jijini Dar es Salaam katika matawi yaliyopo  kwenye mitaa ya Ohio na Samora vilevile katika tawi la Arusha. 

Benki ya CBA Tanzania ambayo ni moja ya Benki kubwa  zinazoongoza kwa ubunifu wa huduma mbalimbali za kibenki kwa wateja wake ,moja ya huduma ambayo imeianzisha na kuleta mapinduzi makubwa katika sekta ya makazi ya kutoa mikopo ya nyumba inayolipwa hadi kufikia kipindi cha miaka 20. 

Benki ya CBA Tanzania hadi kufikia sasa inayo matawi 11 nchini kote ambapo 5 yapo jijini Dar es Salaam na mengine katika miji ya  Mbeya, Tunduma, Mtwara, Moshi, Mwanza, na Arusha.Pia benki ipo katika nchi nyingine za Afrika Mashariki za Kenya,Uganda na Rwanda ambazo ziko chini ya mwamvuli wa CBA GROUP. 

Thursday, September 15, 2016

JPM ATEUA MWENYEKITI WA BODI NA MKURUGENZI ATCL

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, leo tarehe 15 Septemba, 2016 amemteua Mhandisi Emmanuel Korosso kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL).

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi, imeeleza kuwa uteuzi wa Mhandisi Emmanuel Korosso unaanza mara moja.

Mhandisi Emmanuel Korosso anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Salim Msoma ambaye alimaliza muda wake.

Wakati huo huo, Rais Magufuli amemteua Mhandisi Ladislaus Ernest Matindi kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL).

Kabla ya uteuzi huu Mhandisi Ladislaus Ernest Matindi alikuwa Mkurugenzi katika Shirika linaloshughulikia masuala ya usafiri wa anga Barani Afrika (EGNOS-Africa Joint Programme Office) lenye makao yake nchini Senegal.
Uteuzi huu unaanza mara moja.

MADEREVA WA TANZANIA WATEKWA NA WAASI DRC


VISIMA 7 KUPUNGUZA TATIZO LA MAJI KISHAPU

Mkurugenzi wa Halimashauri ya Wilaya Kishapu Bwana. Stephen M Magoiga akizindua moja kati ya Visima saba.
Afisa Mradi Mwandamizi Mama Tina Mosha Akimtwisha maji Moja ya wanakiji wa IKONDA.
Moja visima vilivyokuwa vikitumiwa na wananchi kabla ya ujenzi wa visima vya kisasa.
Vijana wa Youth CAN wakitoa elimu ya Mazingira, Majina Afya kwa njia ya Nyimbo Kijijini Ikonda.
Vijana wa Youth CAN wakitoa elimu ya Mazingira, Majina Afya kwa njia ya Nyimbo Kijijini Ikonda.
Nizar Selemani Mratibu wa shuguli za vijana katika shirika la NCA na Baraka Chedego ambae ni Mratibu wa Youth CAN wakizungumza jambo wakati wa mkutano na wanakijiji cha Ikonda.
Vikundi Mvalimbali vya sanaa kutoka Kishapu vikitoa burudani wakati wa Mkutano.
Wananchi wa Kishapu wakifatilia mkutano kwa Umakini Mkubwa.
Wananchi wa Kishapu wakifatilia mkutano kwa Umakini Mkubwa.


MSAFARA WA VIJANA WATOA ELMU YA MAZINGIRA NA AFYA KISHAPU
Youth Climate Activist Network (YouthCAN) Tanzania Ni mtandao wa vijana wanaotoka kwenye taasisi za dini mbalimbali wanaofanya shuguli mbalimbali za mazingira na afya kwa ujumla kwa kujitolea chini ya Shirika la Norwegian Church Aid (NCA)
Kuanzia Tarehe 11/9 /2016 vijana hawa walianza masafara wa Kutembelea baadhi ya maeneo yaliyoathirika sana na mabadiliko ya tabia nchi. 

Ilikutoa elimu ya Utunzaji wa mazingira, vyanzo vya maji na usafi baada ya kutoa elimu hiyo Halmashauri ya wiliya Kishapu Mkoani Shinyanga wanatarajia kwenda Kutoa elimu hiyo Mkoani Manyara kwenye baadhi ya vijiji vilivyopo Hanang. Hydom na Mbulu.

Licha ya kutoa elimu juu mazingira, Maji ana afya vijana hawa watapata nafasi ya kuzindua baadhi ya Visima vya maji vilivyojengwa na Shirika la Norwegian Church Aid (NCA) kwa kushirikiana na Washirika wake.

Ambapo kwa kuanza wamepata fursa ya kushiriki uzinduzi wa visima 7 vilivyojengwa kwa msaada wa watu wa Norway visima hivyo vitasaidia kutatua tatizo la maji safi na salama katika vijiji vi 3 wiliyani Kishapu ambavyo ni IKONDA A,UBATA na MWAWEJI.


Picha zote na IMANI SELEMANI NSAMILA.