ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, November 20, 2015

MBUNGE WA JIMBO LA NYAMAGANA, MABULA ATAKA UONGOZI KUSITISHA ZOEZI LA KUWAONDOA NA KUWAZUIA WAFANYABIASHARA JIJINI HUMO

Stanslaus Mabula 
DODOMA.


MBUNGE wa Jimbo la Myamagana mkoani Mwanza, Stanslaus Mabula (CCM) ameutaka uongozi wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza kusitisha tamko na zoezi la kuwaondoa na kufanya shughuli zao wafanyabiashara wa mbogambonga, matunda, majisafi, juisi na mamalishe jijini humo kwa madai kuwepo ugonjwa wa kipindupindu na badala yake kuwaelimisha kufuata kanuni bora za afya.



Mbunge Mabula amesema hayo akiwa Mjini Dodoma kwenye shughuli za Bunge zinazoendelea baada ya kupokea taarifa kutoka kwa wananchi wa jimbo hilo waliompigia  simu  kumpatia taarifa ili awasaidie  juu ya tamko na zoezi linalofanywa na Halmashauri kupitia Idara ya Afya ya Jiji hilo kuwazuia kufanya biashara katika maeneo mbalimbali ya mitaa ya Kata 18 kutokana na tishio la kutokea kwa mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu  jambo ambalo wamedai linawaathili katika kujitafutia kipato.



Mabula akizungumza na Blog hii ameutaka uongozi wa Jiji hilo chini ya Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza, Tito Mahinya, kusitisha tamko na zuio hilo la na badala yake wawaelimishe kwanza wananchi kupitia Idara yake ya Afya kwa kuwaeleza wafanyabiashara wa mbogamboga, matunda, maji juisi na vyakula vingine kuepuka kupanga dhidhaa zao sehemu zilizo safi na mamalishe watoe huduma ya chakula katika mazingira bora na yaliyo safi kwa  kufuata kanuni bora za afya zilizopo.



“Wananchi hao wanatakiwa kupewa elimu na kuelimishwa juu ya madhala ya ugonjwa wa kipindupindu uliolikumba jiji letu kwa wiki tatu ambapo  taarifa zilieleza watu saba walipatwa na ugonjwa huo na walitibiwa na jana wameruhusiwa baada ya kuthibitika kuwa wamepona, jambo hili likifanyika kwa kuwaeleza wananchi kutaondosha dhana na madai ya kuonewa ikiwemo kuondolewa katika maeneo yao ya kufanyia shughuli zao za kujiingizia kipato,”alisema.



Mabula alieleza kwamba kufatia hali hiyo amewasiliana na Kaimu Mkurugenzi Mahinya  kusitisha zoezi haraka na badala yake kupitia Idara ya Afya kupita na kutangaza kwa wananchi kanuni bora za kuepuka mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu kwa kutoa elimu kwa wananchi hao jinsi ya kuzifuata ikiwa ni kuuza matunda, mbogamboga, vyakula sehemu zilizo safi na wasipange kwenye majimaji na mazingira safi.



“Mamalishe ambao wanahangaika kujitafutia kipato waelimishwe kwani wamekopa fedha za mitaji na kuanzisha biashara zao ni vyema wakapewa elimu kuzifuata kanuni bora za usafi katika mazingira ya tishio la kipindupindu kwa kutengeneza chakula na kukiuza kwa wateja wao katika mazingira safi na salama ikiwemo kuhakikisha vyakula saa zote vinakuwa vya moto, kuwepo na jiko lenye sufuria la maji ya moto ambapo ndani yake kutawekwa sahani, vijiko na vikombe ambavyo mamalishe watavitumia kuwapatia wateja wao chakula na siyo kuwaeleza wasitishe na kuondoka kama ilivyotangazwa ,”alisema.



Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi, Mahinya alieleza kuwa kutokana na kubainika kuwepo ugonjwa wa kipindupimdu na watu saba kugundulika kupata ugonjwa huo waliochukua hatua za kuwazuia wananchi hasa wafanyabiashara wa matunda, mbogamboga na vyakula kupanga bidhaa zao chini sehemu zenye majimaji, lakini pia kuwazuia mamalishe kuendelea kuuza chakula kwenye vibanda na masoko ya jioni yaliyo kwenye mazingira machafu.



“Tumezungumza na Mbunge Mabula baada ya kupigiwa simu na kupewa taarifa na wananchi kuwa uongozi wa Halmashauri umewazuia kufanya biashara, lakini nimemuelewesha na tumekubaliana kuwa tutatumia gari la matangazo kupita tena kuwaeleza wananchi jinsi ya kufuata kanuni bora za mamalishe kutoa huduma ya chakula kwa wateja ili kuepuka kuambukizwa ugonjwa wa kipimdupimdu na wauzaji wengine kufanya usafi na kuacha kupanda vyakula chini  kwenye majimaji,”alisema.



Mahinya amewataka wananchi kuzingatia taratibu na kanuni za afya ili kuepuka kupatwa na ugonjwa wa mlipuko pia wadumishe utamaduni wa kufanya usafi na utunzaji mazingira ili kuendelea kuliweka jiji katika taswila ma muonekano wa usafi badala ya kukimbilia kulalamikia Halmashauri inapochukua hatua za kusitishwa utolewawaji huduma kwenye mazingira hatarishi na yasiyo salama kwa wateja na watumiaji kwenye baadhi ya maeneo ya masoko na vibanda vinavyotumiwa na mamalishe.

RAIS MAGUFULI AZINDUA BUNGE KWA HOTUBA YENYE HISIA: ARUDIA AHADI ALIZOZITOA KAMPENI ZA UCHAGUZI AKIMAANISHA ANA DENI KWA WATANZANIA

VIPAUMBELE NILIVYONASA BUNGENI DOM:- *Dawa za kulevya ni janga linaloathiri vijana wengi ameahidi kushughulikia mtandao huo na wakubwa wanao husika.

*Mapambano ya rushwa na ufisadi ameahidi kwa wananchi na kilichobaki utekelezaji. 

*Nimeahidi kuunda mahakama ya Rushwa na ufisadi naamini hawataniangusha katika hili sitakuwa na kigugumizi. 

*Wafanyakazi wazembe... Hatuwezi kulea watu ambao wanalipwa mishahara tu wakati hawafanyi kazi yeyote.

*Nitadhibiti warsha ambazo hazina umuhimu katika Serikali yetu wala kuongeza ufanisi kwa wafanyakazi.

*Naahidi kudhibiti Safari za nje ambazo zimekuwa zikigharimu Serikali Fedha nyingi ambazo zingeweza kutumika katika shughuli mbalimbali za kimaendeleo..

*Serikali ya awamu ya 5 itaongeza wigo katika ukusanyaji wa mapato ukizingatia kuwa kodi ni kitu muhimu na nilazima zikusanywe.

KATIBU MKUU WIZARA YA ELIMU ANOGESHA MAHAFALI YA 10 YA CHUO CHA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE DAR ES SALAAM LEO

Mkurugenzi wa Elimu ya Ufundi na Ufundi Stadi Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Thomas Katebalilwe akihutubia kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Sifuni Mchome, aliyekuwa mgeni rasmi katika mahafali ya 10 ya Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Dar es Salaam leo asubuhi.
 Mkuu wa chuo hicho, Profesa Shadrack Mwakalila akielezea mafanikio ya chuo.
 Mkurugenzi wa Elimu ya Ufundi na Ufundi Stadi Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Thomas Katebalilwe (wa pili kushoto), akimkabidhi cheti kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Sifuni Mchome, mwanafunzi, Benard Nyoni, aliyefanya vizuri katika masomo yake wakati wa sherehe za mahafali ya 10 ya Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere (MNMA), Dar es Salaam leo. Kutoka kushoto ni Mkuu wa chuo hicho, Profesa Shadrack Mwakalila na  Kaimu Mwenyekiti ya Bodi ya chuo, Evelyne Makalla.
 Mkurugenzi wa Elimu ya Ufundi na Ufundi Stadi Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Thomas Katebalilwe (wa pili kushoto), akimkabidhi cheti kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Sifuni Mchome, mwanafunzi, Godfrey Nchimbi aliyefanya vizuri katika masomo yake wakati wa sherehe za mahafali ya 10 ya Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere (MNMA), Dar es Salaam leo asubuhi. Kutoka kushoto ni Mkuu wa chuo hicho, Profesa Shadrack Mwakalila, Kaimu Mwenyekiti ya Bodi ya chuo, Evelyne Makalla na Rais wa Serikali ya Wanafunzi (MASO), Elias Kumanya. 
 Wahitimu wa ngazi ya cheti, stashahada na shahada ya kwanza waliofanya vizuri katika masomo yao wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kukabidhiwa vyeti na Mkurugenzi wa Elimu ya Ufundi na Ufundi Stadi Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Thomas Katebalilwe kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Sifuni Mchome, wakati wa sherehe za mahafali ya 10 ya Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere (MNMA)
 Meza kuu ilivyokuwa ikionekana kwenye mahafali hayo.
 Mkurugenzi wa Elimu ya Ufundi na Ufundi Stadi Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Thomas Katebalilwe (katikati), akiwa katika picha ya pamoja na  Mkuu wa chuo hicho, Profesa Shadrack Mwakalila (kushoto),  na Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya chuo, Evelyne Makalla katika mahafali hayo.
   Brass Bendi ya Magereza ikiongoza maandamano wakati wa mahafali hayo.
 Mgeni rasmi na viongozi wengine wakiongoza maandamano kuelekea eneo la sherehe.
 Wahitimu wa ngazi ya cheti, stashahada na shahada ya kwanza wakiwa katika sherehe za mahafali ya 10 ya Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere (MNMA), yaliyofanyika Dar es Salaam.
 Wanafunzi wenzao wakiwapongeza watangulizi wao kwa kuhitimu.
 Brass Bendi ya Magereza ikitoa burudani katika mahafali hayo.
 Wahadhiri wa chuo hicho wakiwa katika mahafali hayo.
 Wageni waalikwa wakijumuika katika sherehe hiyo.
 Hapa ni kazi tu
 Wadau mbalimbali wakiwa kwenye mahafali hayo.
 Wahitimu wakiwa kwenye mahafali hayo.
 Wahitimu wakiwa kwenye mahafali hayo.
 Wahitimu wakiwa kwenye mahafali hayo.
 Wahitimu waliofanya vizuri masomo yao wakiwa katika icha ya pamoja na meza kuu.
 Wahitimu wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi.

SHEREHE ZA KUAPISHWA WAZIRI MKUU WA AWAMU YA TANO VIWANJA VYA IKULU NDOGO CHAMWINO MJINI DODOMA.

WAZIRI MKUU AAPISHWA RASMI LEO MJINI DODOMA.


Mhe kassim majaliwa ala kiapo rasmi new

Hatimaye Mhe Kassim Majaliwa ala kiapo cha uaminifu na kuahidi kuhifadhi na kulinda katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

JAMESON YAANDAA PRE-PART GEORGE AND DRAGON DAR kuelekea Jameson Live Party itakayofanyika Nairobi.


  • Mshindi mmoja kujishindia tiketi ya watu wawili kwenda Kenya kwenye party ya Jameson itakayotumbuizwa na B.O.B

Jameson inaandaa pre-party itakayofanyika tarehe 21 ya mwezi huu katika bar ya George and Dragon jijini Dar es Salaam.
Watumiaji wa Jameson watakaonunua chupa ya kinywaji hicho watafanikiwa kuingia moja kwa moja kwenye droo ya kushinda tiketi ya kwenda Kenya kushuhudia party ya Jameson itakayofanyika hapo tarehe 12, December.
Jameson Live 2015 Party, inamleta msanii wa hiphop kutoka Marekani, Bobby Ray Simons, maarufu kama B.O.B, ambayo itafanyika Ngong Racecourse hapo tarehe 12 December.
Rapa huyo mzaliwa wa Atlanta amezungumzia kuhusu show yake hiyo ya Nairobi katika ukurasa wake wa Facebook, akiwataka mashabiki wake wajiandae kwa show kali.
B.O.B ambaye alitambulika katika ulimwengu wa muziki kupitia kupitia mixtape yake ya Cloud 9, amefanikiwa kufanya show sehemu mbalimbali duniani huku wimbo wake wa ‘Airplanes’ na ‘Nothing on You’ aliyomshirikisha Bruno Mars zikiongoza chati mbalimbali za mziki duniani.
Nyimbo zake za hivi karibuni kama ‘So Good’ na ‘Headband’ nazo zimefanikiwa kumfanya B.O.B kuwa mmoja ya wanamuziki wakubwa duniani.

Huku akiwa ameshinda tuzo mbalimbali za BET, MTV pamoja na Teen Choice na huku akifanikiwa kuchaguliwa kuwania tuzo za Grammy zaidi ya mara sita, B.O.B ameshawahi kufanya show na wanamuziki mahiri kama Janelle Monae, Eminem, Linkin Park, Kanye West, Drake, Usher, Paramore na wengine wengi.

Jameson wamejipanga kukuza viwango vya burudani kwa nchi za Afrika Mashariki na awamu hii wamejipanga kwa kuwapa burudani ya pekee mashabiki watakaohudhuria burudani hiyo huku wakizidi kuwekeza zaidi katika kuwaleta wasanii wa kimataifa.
                                                                                            
Mwaka 2014 Jameson ilifanikiwa kuandaa matamasha mawili makubwa nchini Kenya ambayo yote tiketi zake zilimalizika kabla huku la kwanza burudani ikitolewa na wasanii wa ndani, na la pili burudani ilitolewa na msanii 2 Chainz huku balozi mashuhuri wa Afrika Akon akihudhuria pia.

Akizungumzia kuhusu show hiyo, Balozi wa Jameson, Antony Owich amesema party ya mwaka huu itazidi kuwa kubwa na bora kuliko miaka iliyopita.

‘Jameson imejikita katika kuwapa kumbukumbu za kipekee mashabiki wake na kwa mwaka huu inawaahidi kuwapa burudani ya pekee kabisa na watu wasikose kuhudhuria’ alisema Owich.







MAGAZETI NOV 20 TBC


Magazeti Nov 20 TBC

Mh.Majaliwa asema hakutegemea, aahidi kutumikia wote bila ubaguzi. Dk.Tulia achaguliwa kuwa Naibu Spika Bunge la 11.

JAMBAZI LAUAWA: Singida

Mtu mmoja anayesadikiwa kuwa jambazi ameuawa kwa kupigwa risasi mkoani Singida wakati akijaribu kumpora polisi silaha;

MACHIMBO YA NYANGARATA YAFUNGWA KWA MUDA

Na Emmanuel Mlelekwa,
Novemba 19,2015.
KAHAMA
Wizara ya Nishati na madini imesitisha shughuli za uchimbaji katika machimbo ya Nyangarata yaliyopo wilayani kahama hadi hapo serikali itakaporuhusu shughuli za uchimbaji kuendelea.

Kauli hiyo imetolewa na Naibu Kamishina wa Madini Nchini Mhandisi Ally Samage katika kikao  cha tahmini baada ya kuopoa maiti ya mtu mmoja aliyekuwa amefukiwa na kifusi katika machimbo ya Nyangarata.

Amesema serikali imelazimika kufanya hivyo ili kufanya upembuzi wa namna ya kuendesha machimbo baada ya mtu mmoja kufariki na wengine 15 kuopolewa kwa nyakati tofauti tangu kutitia kwake Oktoba 6 mwaka huu.

Insert…..Kamishina 1

Aidha amesema serikali imekuwa ikishirikiana na wachimbaji hivyo kutokana na majanga ya namna kama ilivyotokea katika machimbo ya Nyangarata yanatakiwa kuepukika kwa kuzingatia usalama wa shughuli za uchimbaji.

Insert……Kamishina 2

Kwa upande wake mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na Usalama wilaya ya Kahama ambaye pia ni Mkuu wa wilaya hiyo Vita Kawawa amesema tayari kamati yake imefanikiwa kuuopoa mwili wa marehemu aliyefarikina kuukabidhi kwa ndugu zake.

Hata hivyo amesema kuwa jukumu la Serikali ni kuhakikisha afya za wahanga zinaimarika na zirejee katika hali zao za awali na kupata uwezo wa kufanya kazi ili kuendeleza familia zao,jamii na taifa kwa ujumla.
 Insert….DC



KAHAMA

Mahakama ya Mwanzo wilayani Kahama Mkoani Shinyanga imewahukumu Watu wawili Vifungo vya miezi 6 baada ya kukutwa na makosa ya wizi wa Beteri za minara mali ya Kampuni ya Simu za Mkononi ya HALOTEL

Katika hukumu ya kwanza  hiyo iliyotolewa Novemba 17 mwaka huu, Hakimu mfawidhi wa mahakama hiyo  Herman Byalugaba amesema mahakama imetoa adhabu hiyo baada ya kuridhika na ushahidi uliotolewa na upande wa mashitaka ambao ni Kampuni ya Halotel 

Awali mwendesha mashitaka kutoka kampuni hiyo Bw.Stephen Chacha  amemtaja mshitakiwa kuwa ni  Emmanuel Charles ambaye  amekutwa na hatia ya wizi wa Betri 3 zenye thamani ya shilingi milioni mbili laki saba katika kosa hilo lililotendeka Oktoba 30 mwaka huu

Hukumu ya pili imetolewa na  Hakimu Leah Kyomushula dhidi ya mtuhumiwa Humphrey Silvesta kifungo cha nje miezi 6baada ya kukutwa na hatia ya wizi wa betri 4 zenye thamani ya shilingi milioni moja na laki saba uliofanyika Oktoba 30 mwaka huu.

Thursday, November 19, 2015

WAZIRI MKUU SERIKALI YA HAPA KAZI TU NI MAJALIWA KASSIM MAJALIWA.

Mh Kassim Majaliwa Ateuliwa Kuwa Waziri Mkuu.

Kitendawili cha Rais Magufuli hatimaye chateguliwa, amteua Mh.Kassim Majaliwa kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania. BOFYA VIDEO KUSIKIA KILICHOJIRI HAPA BUNGENI DODOMA LEO.
Mbunge wa Jimbo la Sumve Mhe. Richard Ndassa akizungumza na Mwakilishi wa Jembe Fm 93.7 Albert G. Sengo pamoja na mwanahabari James George wa Star Tv kutoka katika viwanja vya Bunge mjini Dodoma.
Waheshimiwa wabunge wakitete na mdau wa Habari mkongwe ambaye pia ni Blogger maarufu Afrika Issa Michuzi wa Michuzi Jr. 
Waheshimiwa wakiteta.

Wednesday, November 18, 2015

CCM YAPITISHA JINA LA Dkt. TULIA ACKSON MWANSASU KUWANIA UNAIBU SPIKA: KUCHAGULIWA KESHO.

Mbunge mteule Mhe. Dkt Tulia Ackison Mwansasu aliyepitishwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwania nafasi ya Naibu Spika wa Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambapo kesho kunatarajiwa kufanyika kwa uchaguzi huo ndani ya ukumbi wa Bunge Mjini Dodoma hapa akiomba kura kwa Mhe Vicky Kamata (Vitimaalum CCM) katika Hoteli ya New Dodoma leo

 Pitia sifa za mgombea huyu kijana katika nasafi ya Naibu Spika Dkt Tulia A Mwansasu mtaalamu wa Sheria

 Mhe. Shanif Hillan Mansoor (Jimbo la Kwimba) akiwa na Albert G Sengo mtangazaji wa Jembe FM na miliki wa Blog hii akijianda kufanya mahojiano baada ya kuapishwa kuzungumzia kero na changamoto za wananchi anazotaraji kuanza kuzifanyika kazi kama alivyowaahidi wananchi jimboni mwake.
 Mhe Dkt Tulia hongera kwa kupitishwa na Chama kuwania Unaibu Spika unafaa na kazi ni moja tu kuanzia sasa kuomba kura kwa waheshimiwa wenzako ni moja wa Makada wa CCM akimpatia neno hilo(wa pili kushoto) Albert G Sengo akisikiliza na Mhe Mansoor akifikiria neno la kusema kwa Mhe Dkt Tulia
 Mhe Mansoor akisema neno kwa Mhe Dkt Tulia kwamba tayari wewe ndo Naibu Spika tunasubilia kesho Wabunge kukupigia kura ili uibuke mshindi kwa kishindo hatuna shaka juu ya nafasi hiyo
 Wakati wa Waheshimiwa Wabunge kujumuika na familia, ndugu, jamaa na marafiki baada ya kuapishwa na hapa ni Mhe Kamata akifurahia na ndugu zake
 Mhe Dkt Tulia A Mwansasu (katikati) akisikiliza kwa makini ushauri wa Mhe Mbunge (kulia) na Mhe Richard Ndassa (Jimbo la Sumve) akisikiliza kwa makini alipowaomba wampigie kura kesho.
 Mhe Andrew Chenge aliyekuwa Mwenyekiti wa Mkutano wa kumchagua Spika Job Ndugai wa Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jana alipopiga picha na jamaa leo katika viwanja vya Bunge mjini Dodoma.
Mhe Kemilembe Julias Lwwota (Vitimaalum CCM) akiwa na ndugu na marafiki nje ya ukumbi wa Bunge baada ya kuapishwa leo mjini Dodoma
Mhe Kemilembe Julias Rwota akiwa na ndugu na marafiki nje ya ukumbi wa Bunge baada ya kuapishwa leo mjini Dodoma