ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, May 17, 2019

FAWE YAJIZATITI KUWANUSURU WANAFUNZI NA MKUMBO WA KUIPA KISOGO ELIMU


Wadau wa Maendeleo Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sayansi na Utamaduni UNESCO na FAWE TZ kupitia ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Korea ya Kusini (KOICA) wanaendesha mafunzo ya Malezi na Unasihi katika shule mbalimbali wilayani Sengerema Mkoani Mwanza ambapo siku ya Alhamisi ya tarehe 16 mwezi Mei 2019 walikuwa katika Shule ya Msingi Iyogelo.

Jeh wanafunzi wananufaika vipi na mpango huo?

Thursday, May 16, 2019

CHAMA CHA WATAALAMU WALIOBOBEA KUPAMBANA NA UFISADI WAKUTANA KUJADILI NJIA ZA KUMALIZA KABISA UFISADI.

 picha15 ikionyesha ,Rais wa chama cha wataalam waliobobea katika kupambana na ufisadi ( ACFE) ,Emanuel Johanness akiongea na waandishi wa habari

picha ikionyesha washiriki wa mkutano huo wakiendelea kufuatilia kwa makini 
Na Woinde Shizza,Arusha
CHAMA cha wataalamu waliobobea katika kupambana na Ufisadi duniani (ACFE)kimejipanga kuanza kutumia teknolojia za kisasa  katika kubaini na kuchunguza uhalifu huo unaoonekana kushika kazi katika nchi mbalimbali duniani.
Akiongea na waandishi wa habari leo katika mkutano mkuu wa chama hicho,unaofanyika tawi la Tanzania, jijini Arusha  ,Rais wa ACFE ,Emanuel Johanness  alisema lengo kubwa la mkutano huo ni kuangalia mapambano ya ufisadi katika siku za usoni kutokana na aina ya ufisadi kuhamia kwenye kiteknolojia zaidi.
Alisema taarifa  yao ya mwaka jana 2018 imeonyesha kuwa katika kesi  2690 za ufisadi zilizoripotiwa  kutoka nchi  125 duniani katika sekta mbalimbali 23, imeonyesha kuwa kiasi cha dolla za kimarekani billion 7 zimepotea kutokana na ufisadi unaofanyika kwenye taasisi za umma ,makampuni na sekta binafsi.
Alisema kuwa njia sahihi inayotumika kwa sasa  kubaini ufisadi ni pamoja na kupewa taarifa za siri kutoka kwa wananchi wazalendo ,ambapo pamoja na mafanikio hayo  ipo haja kwa chama hicho kupeana mbinu mbadala ikiwemo matumizi ya teknolojia za kisasa kubaini ufisadi.
“Kadri siku zinavyozidi kwenda ndivyo wahalifu hawa wanavyozidi kugundua mbinu mpya za kufanya ufisadi,na ndio maana katika mkutano huu tumealika mwenzetu kutoka nchi ya Afrika kusini kuja kutupatia uzoefu wa namna wao wanavyopambana na ufisadi kwani nchi yao imefanikiwa kwa kiwango kikubwa zaidi na mapambano hayo na walianza mda mrefu kupambana na wahalifu hawa”alisemaJohaness
Akizungumzia kasi ya ufisadi hapa nchi alisema bado ni kubwa na alibainisha kuwa ufisadi  mkubwa unaoongoza hapa nchi ni pamoja na rushwa,ubadhilifu wa fedha na kughushi na kwamba hatua ya serikali kuanzisha mahakama ya mafisadi itasaidia sana kupunguza uhalifu huo na kuokoa fedha za serikali kutokana na baadhi ya waalifu kukutwa na hatia na mali zao  kutaifishwa .
Hata hivyo chama hicho  kwa upande wa tawi la Tanzania kimefanikiwa kwa kiasi kikubwa kubaini matukio ya ufisadi kutokana na wanachama wake zaidi ya 200 kutoka katika sekta nyeti hapa nchini jambo ambalo limefanikisha kupata taarifa za siri na kuzifanyia uchunguzi haraka.
Kwaupande wake mmoja wa washiriki kutoka mamlaka ya mapato Tanzania TRA Salum Kessy alisema kuwa serikali ilivyoanzisha  mahakama ya ufisadi  ni miongoni mwa hatua nzuri kwani  hata wao wanavyofanya uchunguzi ukikamilika wanapata pa kuwapeleka  wahalifu hao.

Alisema kuwa iwapo watanzania tutaungana kwa pamoja zikiwemo taasisi za kiserikali pamoja na binafsi kukemea ufisadi basi tutapunguza kwa kiasi kikubwa tatizohili  na sio kupunguza tu bali tunaweza kulimaliza kabisa tatizo hili.
Mkutano huo mkuu unafanyika kwa siku tatu hapa nchini na unashirikisha wataalamu kutoka nchi tano za afrika ambazo ni Kenya ,Nigeria ,Afrika kusini ,Uganda,Zambia na wenyeji Tanzania na kwamba chama hicho cha  wataalamu waliobobea katika kupambana na ufisadi kina wanachama toka nchi zaidi 160 duniani na mkutano huo unatarajia kutoka na jibu moja utakaotoka na mbinu itakaomaliza ufisadi katika nchi mbalimbali duniani.

TANZANIA YAPONGEZWA KWA UKUAJI MZURI WA UCHUMI, RAIS MAGUFULI AZUNGUMZA.


Rais wa Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB) Mhe. Dkt. Akinwumi Adesina apongeza ukuaji mzuri wa uchumi wa Tanzania wa wastani wa asilimia 7 kwa mwaka.


MKOA WA KWANZA KUTOKOMEZA MIFUKO YA PLASTIKI KUPATIWA Tsh. MILIONI 40


Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais - Mazingira na Muungano, Januari Makamba amesema watatoa motisha kwa mikoa itakayotokomeza kabisa mifuko ya plastiki itakapofika Julai Mosi mwaka huu kwa kuwapatia Tsh. Milioni 40 kwa mshindi wa kwanza huku mshindi wa pili akijinyakulia Tsh. Milioni 30 na watatu atakabidhiwa Tsh. Milioni 10.

Waziri Makamba amesema kuwa nchi ya Tanzania inaweza kufanikiwa azma hiyo kwa kuwa inazalisha mifuko mbadala ya karatasi ambayo hutumiwa kwa kiasi kikubwa na nchi jirani za Rwanda na Kenya kutoka Kiwanda cha Karatasi cha Mufindi.


ALICIOUS NA RUMBA YAKE YA UKWELI ILIYOTIKISA JIJI LA MWANZA 2019



Hivi ndivyo ilivyokuwa siku ya sikukuu ya Pasaka Mwanza pale ambapo Villa Park Resort ya jijini Mwanza ikishirikiana na Kipindi cha Saturday Xpress toka Jembe Fm ilikuwa ni burudani ya muziki wa Live Band toka kwa Bendi maarufu inayotikisa Kanda ya Ziwa Super Kamanyola pamoja na mwanadada Alicious, Mkongo anayeishi nchini Kenya.

TANZIA BARAZA LA MAASKOFU KATOLIKI TANZANIA LATANGAZA KIFO CHA ASKOFU MSTAAFU MMOLE.


Askofu Mstaafu marehemu Gabriel Mmole
Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania limetangaza kifo cha Mhashamu,Askofu Mstaafu wa Jimbo katoliki la Mtwara,Gabriel Mmole aliyefariki dunia siku ya jana, Mei 15 Saa 10 alfajiri.

SERIKALI YAELEZA SABABU YA KUACHANA NA KAMPUNI YA KUNUNUA KOROSHO KUTOKA KENYA.




Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limepitisha Bajeti ya Wizara ya Viwanda na Biashara kwa mwaka wa fedha 2019/2020 jumla ya Shilingi Bilioni 100.3

Akihitimisha hoja bungeni, Waziri wa Viwanda na Biashara, Joseph Kakunda amezungumzia suala la kampuni ya Indo-Power iliyopaswa kununua Korosho akieleza kuwa kampuni hiyo ni halali na ilikaguliwa na Balozi wa Tanzania nchini Kenya.

Ameeleza kilichofanya serikali kuamua kuchana na kampuni ni kutokana na ilichelewa kutekeleza baadhi ya vipengele katika mkataba. Amesisitiza kuwa Serikali itauza korosho hivi karibuni tofauti na watu wengi wanavyofikiria

Wednesday, May 15, 2019

MAGARI YAGONGANA USO KWA USO, MMOJA AFARIKI.

Mwanafunzi wa shule ya msingi Silver Mjini Babati Mkoani Manyara, Osiligi Paul mwenye umri wa miaka mitatu na miezi sita amefariki dunia baada ya kutokea ajali mbaya.

Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Manyara, Augostino Senga amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo iliyohusisha basi la kampuni ya Mtei kugongana na basi dogo aina ya Hiace eneo la Himiti mjini Babati




.

SAFARI YA ANTOINE GRIEZMANN KWENDA BARCELONA IMEKWIVA.


Katika ujumbe wake wa kuthibitisha kuondoka mwisho wa msimu huu na kuwaaga mashabiki wa klabu hiyo amesema "Imekuwa miaka mitano bora, asanteni kwa kila kitu, nimewaweka moyoni mwangu."

Mchezaji huyo mwenye miaka 28 amekuwa akihusishwa na uhamisho wa kwenda Barcelona tangu msimu uliopita na tetesi hizo zimeshika hatamu baada ya timu hiyo kupokea kipigo cha goli 4-0 kutoka kwa Liverpool.

Inadaiwa kuwa Barcelona ambao ni mabingwa wapya wa Ligi Kuu msimu huu nchini Uhispania, imeandaa kitita cha Paundi Milioni 108(Tsh. 321,442,041,276) ili kumsajili

Mchezaji huyo aliyejiunga Atletico mwaka 2014 akitokea Real Sociedad ameichezea timu hiyo michezo 256 na kufunga magoli 133 lakini pia amepiga pasi 50 zilizozaa magoli.

Ameiwezesha timu hiyo kushinda makombe ya Spanish Super Cup (2014-15), Europa League (2017-18) na UEFA Super Cup (2018-19).

WhatsApp si salama, fanya haya uwe salama

WhatsApp , salama, fanya , uwe ,salama,wadukuzi,hackers, AFP,


Dar es Salaam. Kama unapendelea kutuma taarifa muhimu na nyeti kwa kutumia mtandao wa WhatsApp, kutuma picha au video, sasa unapaswa kuuhuisha (update) katika simu yako ya mkononi baada ya wadukuzi kufanikiwa kujipenyeza.

Kutokana na kile kilichokuwa kikielezwa kuwa haikuwa rahisi kwa mtu kudukua mawasiliano ya WhatsApp, wengi wamekuwa wakivutiwa na mtandao huo na kuutumia kutuma taarifa muhimu na mazungumzo ya faragha.

Lakini jana, wamiliki wa mtandao huo wametahadharisha kuwa kuna hatari ya kudukuliwa kutokana na kuwepo na taarifa za maharamia wa kimtandao (hackers) waliovamia mtandao huo ambao una watumiaji zaidi ya bilioni 1.5 ulimwenguni kote.

“WhatsApp inahamasisha watu kuhuisha toleo la mwisho la programu katika simu zao sanjari na kuhuisha mfumo wa simu zao ili kuepuka mpango wa udukuzi uliopangwa dhidi yao, lakini pia kulinda taarifa zao binafsi,” imeeleza taarifa iliyonukuliwa na AFP.

Hata hivyo, WhatsApp hawajabainisha idadi ya watu walioathirika na udukuzi huo, lakini virusi hivyo vinaweza kuingia katika simu aina ya Android, iPhone na vifaa vyote vinavyotumia WhatsApp.

Taarifa za mwanzo za kuwepo kwa hofu ya kudukuliwa kwa mtandao huo ziliripotiwa na tovuti ya Financial Times ambayo ilieleza kuwa mbinu inayotumika ni mlengwa kupigiwa simu au kutumiwa ujumbe ambapo utaambatana na virusi ambavyo vitasaidia udukuzi huo.

Financial Times ilisema virusi hivyo vimetengenezwa na kampuni ya Kiisraeli ijulikanayo kama NSO Group ambayo imekuwa ikituhumiwa kwa kushirikiana na Serikali mbalimbali kukabiliana na wanaharakati na waandishi wa habari.

Pia wachunguzi wa usalama wamesema virusi hivyo vinaonekana kufanana na teknolojia mbalimbali zilizowahi kutengenezwa na NSO, hiyo ni kwa mujibu wa mtandao wa New York Times.

Hata hivyo, jana taarifa ya NSO ambayo imewahi kutuhumiwa kushiriki tukio la udukuaji wa taarifa za mwanaharakati wa Umoja wa Falme za Kiarabu mwaka 2016, imeeleza kuwa leseni yake ni kutengeneza mifumo ya kuisaidia Serikali kupambana na uhalifu.

“Tunachunguza madai yote ya kuaminika ya matumizi mabaya ya mtandao. Kama kuna haja tunachukua hatua ikiwa ni pamoja na kuzima mfumo husika,” inaeleza taarifa ya kampuni hiyo bila kukubali wala kukataa kuhusikia na udukuzi wa WhatsApp. 

CHANZO:- GAZETI LA MWANANCHI  

Tuesday, May 14, 2019

UTATA JUU YA TAARIFA YA KUJIRUSHA TOKA GHOROFANI HADI KUFA MWANZA



JIJI la Mwanza Jumatatu ya tarehe 13 Mei 2019 kumekucha na tukio la kustusha, pale ambapo umati wa wananchi ulipokushanyika mbele ya hoteli maarufu jijini hapa ya Gold Crest iliyo kwenye Jengo la PPF Plaza, lenye ghorofa nane, umati huo ulikuwa ukimwangalia jamaa anayetajwa kufariki dunia nayo sababu kubwa toka kwa baadhi ya tuliozungumza nao wakisema kuwa mtu marehemu huyo wanahofia kuwa amejirusha toka juu ghorofani hapo.

Kamanda wa Jeshi la polisi mkoa wa Mwanza Jumanne Muliro amesema kuwa uchunguzi kwa hatua za awali unaonesha kauli za wananchi kukinzana na uchunguzi wa awali walioufanya.

Monday, May 13, 2019

UWT IRINGA DC WAUNGA MKONO KAZI INAYOFANYWA NA RAIS DAKTARI JOHN MAGUFULI

 Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Iringa Lena Hongole akiongea kwenye kongamano hilo lilofanyika katika kijiji cha Kisinga' kata ya Kising'a lakini pia viongozi mbalimbali walishiriki kongamano hilo.
 Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa Daktari Abery Nyamahanga akitoa neno kwa UWT wakati wa kongamano la kumpongeza Rais Daktari John Joseph Magufuli ambaye ni mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa.
Baadhi ya madiwani wa chama cha mapinduzi wakiwa wameshiriki katika kongamano hilo la UWT la kupongeza
Rais Daktari John Joseph Magufuli ambaye ni mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa.
Hii ndio ya pongezi iliyotolewa na UWT Iringa Dc kwa
Rais Daktari John Joseph Magufuli ambaye ni mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa.

NA FREDY MGUNDA,IRINGA.
 
Umoja wa wanawake wa CCM (UWT) Wilaya ya Iringa wamefanya kongamano la kuunga mkono juhudi na kazi zinazofanywa na Rais Daktari John Joseph Magufuli ambaye ni mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa.

Akizungumzia malengo ya kongamano hilo Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Iringa Lena Hongole amesema kuwa Rais amekuwa akifanya kazi kubwa ya kuleta maendeleo kwa wananchi waliomchagua 2015.

“Sisi wanawake wa wilaya ya Iringa tunampongeza sana Rais Daktari John Joseph Magufuli kwa kazi kubwa ya kuleta maendeleo wananchi waliomchagua kwa kipindi hiki kifupi tangu aingie madarakani”alisema Hongole

Hongole alisema kuwa Tanzania inakuwa kimaendeleo kwa kasi kubwa kutokana na uongozi wa Rais ambapo amefanikiwa kuwajenga watanzania kuwa wazalendo kwa kufanya kazi na kujituma kuhakikisha wanapata maendeleo.

“Mafanikio yenye tija tunayaona hivi sasa hivyo sisi kama wanawake hatuna haja ya kushindwa kumpongeza Rais wetu ambaye amekuwa kiungo muhimu cha maendeleo ya nchi hii hivi sasa” alisema Hongole

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa Daktari Abery Nyamahanga amewapongeza wanawake hao kwa kuunga mkono juhudi za Rais.

“Nyinyi akina mama mmekuwa mstari wa mbele kuunga mkono juhudi hizi ambazo zinazaa matunda ya kuleta maendeleo ndio maana tunaiona hata iringa inazidi kupata maendeleo kila kukicha tunaona sura mpya ya maendeleo ya nchi” alisema Nyamahanga

Nyamahanga alisema kuwa Rais Daktari John Joseph Magufuli amefanya mambo makubwa kwa kipindi kifupi kwa kuboresha sekta ya afya ,sekta ya elimu,uchumi,miundombinu  na utalii na kufanikisha maendeleo haya tunayoyaona hivi sasa.

“Hakuna mtanzania ambaye haoni nini kinafanyika katika nchi hii kwa kila mtu mwenye macho na masikio anajionea na kusikia maana hakuna ubishi kuwa Rais huyu amekuwa mzalendo kweli kweli katika nchi yetu hii” alisema Nyamahanga

Nyamahanga aliwataka wanawake hao UWT kukumbuka juu ya chaguzi zinazokuja hivi karibuni kuhakikisha wanakuwa na Wagombea ambao wanakubarika katika jamii ili kuhakikisha CCM wanashinda kwa kishindo.

“Wakina mama hakikisheni kama mnasifa ahakikisheni mnajitokeza kwa wingi kushika nyadhifa mbalimbali kwenye chaguzi hizi zinazokuja na kuhakikisha tunamuunga mkono mgombea wa CCM na sio kutoka nje ya chama chetu” alisema Nyamahanga

Naye Diwani wa kata ya Kising’a Bi Ritta Mlagala amesema toka mwaka 2015 hadi sasa wamefakiwa kuboresha sekta ya afya na elimu kwa kutekeleza ilani ya CCM ya 2015 hadi 2020.

“Tumefanikiwa kujenga kituo cha afya,kuendelea kujenga majengo mapya ya shule ya sekondari ya Ilambilole iliyopo kata ya Kising’a na tumejenga madarasa manne na ofisi mbili katika shule msingi kising’a hivyo hayo ndio maendeleo yanayofanywa na serikali ya awamu ya tano” alisema Mlagala

Aidha Mlagala alisema kuwa wameanza kujenga zahanati ya kijiji cha Mkungugu  na nyumba ya waaguzi ambazo zote zinatarajia kukamilika hizi karibuni licha ya kuwa na changamoto kadhaa ambazo zinatusukuma kuhakikisha tunatafuta wadau watuunge mkono kumalizia.

Sunday, May 12, 2019

LEO NI LEO - NANI KUTWAA TAJI LA EPL?


Bingwa wa Ligi Kuu England (EPL) kupatikana leo pale Liverpool na Manchester City watakaposhuka dimbani majira ya saa 11 jioni. 

Liverpool watacheza na Wolverhampton Wanderersm, huku Manchester City wakicheza na Brighton & Hove Albion. 

Endapo, Man City na Liverpool zote zitatoka suluhu au sare, basi Man City atakuwa bingwa. Endapo, Man City itafungwa na Liverpool kushinda, basi Liverpool watakuwa Mabingwa wa EPL na kukata kiu ya miaka 29 bila taji.

Endapo, Man City atashinda na Liverpool kushinda, maana yake Man City atakuwa Bingwa kwa tofauti ya pointi moja kama ilivyo sasa kwenye msimamo na endapo, Man City itatoa sare na Liverpool ikashinda, basi Liverpool watakuwa Mabingwa.

RAIS MAGUFULI ATEKELEZA AHADI YAKE KWA WAKAZI WA SENGEREMA


Ahadi ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa wakazi wa Kata ya Nyampande, Wilaya Sengerema mkoani Mwanza ya kuwaondolea adha ya upatikanaji wa maji imeanza kutekelezwa, baada ya Serikali kusaini mkataba na mkandarasi ili kutandaza mtandao wa maji ya bomba katika Kata hiyo.

Mkataba huo wa zaidi ya shilingi bilioni moja umesainiwa Mei 09, 2019 baina ya Serikali kupitia Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira mkoani Mwanza (MWAUWASA) pamoja na mkandarasi kampuni ya HALEM ya jijini Dar es salaam mbele ya Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella.
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira mkoani Mwanza (MWAUWASA), Mhandisi Antony Sanga (kulia) pamoja na Mkurugenzi wa kampuni ya HALEM Construction ya jijini Dar es salaam, Mhandisi Happy Lebe (kushoto), wakisaini mkataba wa utekelezaji mradi wa maji Nyampande wilayani Sengerema. Aliyesimama upande wa kulia ni Mwanasheria wa MWAUWASA, Oscar Twakazi na kushoto ni Meneja Vifaa kampuni ya HALEM, Steven Malima.
Mkurugenzi wa MWAUWASA, Mhandisi Antony Sanga (kulia) pamoja na Mkurugenzi wa kampuni ya HALEM, Mhandisi Happy Lebe wakikabidhiana mkataba wa utekelezaji wa mradi wa maji Nyampande wilayani Sengerema baada ya pande zote mbili kuusaini.

LIVE:- WAZIRI MKUU AMUWAKILISHA JPM IBADA YA KUMSIMIKA ASKOFU MKUU JIMBO KUU KATOLIKI LA MWANZA


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa   anamuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika Ibada ya Kumsimika Askofu mkuu wa Jimbo kuu katoliki la Mwanza Mhashamu Baba Askofu Mkuu Renatus Leonard Nkwande  katika eneo la Kawekamo Jimbo kuu Katoliki la Mwanza .Mei 12,2019.

MKANDARASI ASAINI MKATABA MRADI WA MAJI NYASHIMO WILAYANI BUSEGA.

Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Serikali kupitia Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira jijini Mwanza (MWAUWASA) imesaini mkataba na mkandarasi kampuni ya BENNET Contractors, kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa maji kwa wakazi wa Kata ya Nyashimo, Wilaya Busega mkoani Simiyu.

Mkataba huo umesainiwa Mei 10, 2019 na kushuhudiwa na wananchi pamoja na viongozi mbalimbali akiwemo Mkuu wa Mkoa Simiyu, Antony Mtaka aliyebainisha kwamba kukamilika kwa miradi mbalimbali ya maji wilayani Busega, kutaongeza idadi wananchi wanaofikiwa na mtandao wa maji safi na salama kutoka asilimia 39 za sasa hadi asilimia 79.

Mkurugenzi wa MWAUWASA, Mhandisi Antony Sanga amesema utekelezaji wa mradi huo wenye thamani ya shilingi bilioni 1.8 ni sehemu ya ahadi ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli aliyoitoa wakati akizungumza na wakazi wa Kata ya Nyashimo.

Naye Mkurugenzi wa kampuni ya BENNET Contractors, Sabatho Boaz ameahidi kukamilisha mradi huo kwa ubora na kwa muda wa miezi 15 kama mkataba unavyoelekeza ili kuwaondolea wananchi wa Kata ya Nyashimo adha ya upatikanaji wa maji safi na salama.
Mkurugenzi Mtendaji wa MWAUWASA, Mhandisi Antony Sanga (kushoto) pamoja na Mkurugenzi wa kampuni ya BENNET Contractors, Sabatho Boaz (kulia) wakisaini mkataba wa utekelezaji mradi wa maji ya bomba katika Nyashimo wilayani Busega. Wanaoshuhudia ni viongozi mbalimbali akiwemo Mkuu wa Mkoa Simiyu, Antony Mtaka.
Mkurugenzi Mtendaji wa MWAUWASA, Mhandisi Antony Sanga (kushoto) pamoja na Mkurugenzi wa kampuni ya BENNET Contractors, Sabatho Boaz (kulia) wakibadilishana mkataba wa utekelezaji mradi wa maji ya bomba katika Kata ya Nyashimo wilayani Busega.
Mkuu wa Mkoa Simiyu, Antony Mtaka (katikati), akimpongeza Mkurugenzi Mtendaji wa MWAUWASA, Mhandisi Antony Sanga (kushoto) baada ya kusaini mkataba wa mradi wa maji Nyashimo wilayani Simiyu. Kulia ni Mkurugenzi wa kampuni ya BENNET Contractors, Sabatho Boaz .
Mkuu wa Mkoa Simiyu, Antony Mtaka akizungumza kwenye zoezi hilo la kusaini mkataba wa mradi wa maji Nyashimo wilayani Busega.
Mkuu wa Wilaya Busega, Tano Mwera amesisitiza mradi huo kukamilika kwa wakati ndani ya kipindi kilichopangwa.
Makamu Mwenyekiti Bodi ya MWAUWASA, Edith Mdogo akitoa salamu zake wakati wa zoezi la kusaini mkataba huo.
Mbunge wa Jimbo la Busega, Dk Raphael Chegeni (CCM), ameishukru Serikali kupitia Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kutoa fedha kutekeleza mradi wa maji Nyashimo.
Diwani wa Kata ya Nyashimo wilayani Busega, Mickness Mahela akitoa salamu zake kwenye wakati wa zoezi la kusaini mradi wa maji Nyashimo.
Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Mkoa Mwanza, Hellen Bogoye akitoa salamu zake kwenye zoezi hilo la kusaini mradi wa maji Nyashimo wilayani Simiyu utakaosaidia kumtua mama ndoo kichwani.
Viongozi mbalimbali akiwemo Mkurugenzi Mtendaji wa MWAUWASA, Mhandisi Antony Sanga (wa pili kushoto) wakiwa kwenye zoezi hilo.
Baadhi ya wakazi wa Kata ya Nyashimo wilayani Busega wakifuatilia zoezi hilo.
Tazama Vidio hapa chini