ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, November 26, 2016

KAULI YA RAIS MAGUFULI KUHUSU WANAOJENGA KATIKA HIFADHI YA BARABARA.

Rais John Magufuli amesema serikali haitasita kumchukulia hatua mtu yeyote atakayejenga katika hifadhi ya barabara.

LIVERPOOL YAPAA KIBISHI KWA GHARAMA YA MAUMIVU KWA COUTINHO.

Shabiki toka Igombe wilayani Ilemela jijini Mwanza.

Liverpool moved back to the top of the Premier League with a win against Sunderland but could face a run of games without Philippe Coutinho who was taken off on a stretcher at Anfield.

The Brazillian clutched his ankle after a challenge from Didier Ndong late in a first half where Liverpool failed to turn 80% possession into clear chances.
Sunderland threatened briefly in each period, with Steven Pienaar and Duncan Watmore taking heavy touches when presented with openings.
But as Jurgen Klopp's side continued to press, it was Coutinho's replacement, Divock Origi, who found the net with what appeared to be a right-foot cross from the left side of the area.
It sparked relief at Anfield and when Ndong felled Sadio Mane in the box, James Milner converted a spot-kick to make it 14 games unbeaten in all competitions for the Reds.
Chelsea will move back to the top of the table should they beat Tottenham in Saturday's late kick-off but Liverpool have clear momentum and last tasted defeat in the Premier League in August.

A win at a cost?

How Liverpool deal with a potential lay-off for Coutinho will be critical in whether their momentum can lead to a push for an elusive Premier League title.

His contribution of five goals and six assists in the league sums up the key role he has under Klopp and his all-round displays have seen reports of interest from Barcelona.
Against David Moyes' side Coutinho seemed to be man-marked early on. When he escaped the attentions of Jason Denayer after half an hour he took a heavy touch in the area and felt the full force of Ndong's clearance.
There was no suggestion of a foul but Coutinho's foot took the impact of both the ball and Ndong's follow-through, and he instantly waved to the bench before grimacing during treatment.
Origi's impact points to Liverpool having the resources to deal with any spell out for Coutinho. But with Sadio Mane primed to attend the African Cup of Nations with Senegal in January, Klopp will desperately hope he has not lost arguably his most creative force for long.

AMIRI JESHI MKUURAIS DKT MAGUFULI ATUNUKU KAMISHENI KWA MAAFISA WANAFUNZI KUNDI LA 59/15 IKULU JIJINI DAR ES SALAAM

Amiri Jeshi Mkuu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akitunuku kamisheni kwa Maafisa Wanafunzi wa Kundi la 59/15 wa Jeshi la Wananchi la Tanzania (JWTZ) katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es salaam leo Novemba 26, 2016
Amiri Jeshi Mkuu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akitunuku kamisheni kwa Maafisa Wanafunzi wa Kundi la 59/15 wa Jeshi la Wananchi la Tanzania (JWTZ) katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es salaam leo Novemba 26, 2016
Amiri Jeshi Mkuu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akikagua gwaride la heshima linaloundwa na Maafisa Wanafunzi wa Kundi la 59/15 wa Jeshi la Wananchi la Tanzania (JWTZ) kabla hajawatunuku kamisheni katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es salaam leo Novemba 26, 201
Amiri Jeshi Mkuu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akikagua gwaride la heshima linaloundwa na Maafisa Wanafunzi wa Kundi la 59/15 wa Jeshi la Wananchi la Tanzania (JWTZ) kabla hajawatunuku kamisheni katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es salaam leo Novemba 26, 201
Amiri Jeshi Mkuu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akiweka saini kwenye hati  ya  kamisheni kwa Maafisa Wanafunzi wa Kundi la 59/15 wa Jeshi la Wananchi la Tanzania (JWTZ) kabla hajawatunuku katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es salaam leo Novemba 26, 201
Amiri Jeshi Mkuu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akiweka saini kwenye hati  ya  kamisheni kwa Maafisa Wanafunzi wa Kundi la 59/15 wa Jeshi la Wananchi la Tanzania (JWTZ) kabla hajawatunuku katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es salaam leo Novemba 26, 201
Amiri Jeshi Mkuu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akiongea baada ya kutunuku  kamisheni kwa Maafisa Wanafunzi wa Kundi la 59/15 wa Jeshi la Wananchi la Tanzania (JWTZ) katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam leo Novemba 26, 201
Amiri Jeshi Mkuu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akiongea baada ya kutunuku  kamisheni kwa Maafisa Wanafunzi wa Kundi la 59/15 wa Jeshi la Wananchi la Tanzania (JWTZ) katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam leo Novemba 26, 2016


PICHA NA IKULU

HUAWEI, CLARA BOUTIQUE WAZINDUA DUKA KUBWA KANDA YA ZIWA.

Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Huawei Tanzania, Bruce Zhang (kulia) na Mkurugenzi wa Clara Huawei Smartphone Brand Shop, Clara Mwasa wakikata utepe kuashiria uzinduzi wa Duka hilo uliofanyika mwishoni mwa wiki jijini Mwanza.
Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Huawei Tanzania, Bruce Zhang (kulia) na Mkurugenzi wa Clara Huawei Smartphone Brand Shop, Clara Mwasa wakikata utepe kuashiria uzinduzi wa Duka hilo uliofanyika mwishoni mwa wiki jijini Mwanza.
Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Huawei Tanzania, Bruce Zhang (kulia) ikiwapungia mkono wageni waalikwa mara baada ya uzinduzi wa duka la Clara Huawei Smartphone Brand Shop lililoko jijini Mwanza. Kulia ni Mkurugenzi wa Duka hilo, ClaraMwasa.
Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Huawei Tanzania, Bruce Zhang (katikati) akiwaonyesha wateja walihudhuria uzinduzi wa Duka la Clara Huawei  Smartphone Brand Shop lililozinduliwa rasmi mwishoni mwa wiki jijini Mwanza. Kulia ni Mkurugenzi wa Duka hilo, Clara Mwasa.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI 
Huawei, Clara Boutique  wazindua duka kubwa Kanda ya Ziwa  
Novemba 25, 2016:

Kampuni ya Teknolojia ya Mawasiliano ya Huawei Tanzania kwa kushirikiana na Mfanyabiashara maarufu jijini Mwanza, Clara Salon & Boutique imefungua duka kubwa liitwalo “Clara Smartphone Shop” katika Jiji la Mwanza. Hatua hiyo ni mwendelezo wa Huawei katika kutekeleza moja ya mikakati yake ya kujitanua kibiashara nchini.

Huawei imeona kuwepo wa Duka hili kubwa la Clara, katika Jiji la Mwanza kunatokana na kukua mahitaji ya bidhaa za Huawei nchini na hivyo kutoa fursa ya watumiaji kupata huduma kwa karibu zaidi.

“Tunafahamu watanzania walio wengi wanachohitaji, ndiyo maana leo hii tuko Mwanza. Tunaamini kuwa hii ni fursa pekee kwa wakazi wa Mwanza na miji ya jirani kupata bidhaa zetu zenye ubora na viwango vya hali ya juu. Tunaamini kuwa Clara Salon & Boutique wana jina kubwa katika Jiji la Mwanza na hivyo itatusaidia sisi kutimiza lengo letu, anasema Mkurugenzi huyo.

Mwaka huu kampuni hii ya simu ilijipanga kusambaza huduma yao nchi nzima, sambamba na kufungua maduka kwaajili ya kusogeza huduma zetu kwa wateja. Hali hii imetuongezea wepesi wa utoaji wa huduma zao kwa kufanikiwa kwa kiasi kikubwa kutambua mahitaji muhimu kwa wateja wetu.
  
Tanzania imefaidika na uhusiano mzuri uliopo kati yake na Huawei kwa kuwa na miradi mbalimbali yenye lengo la kuboresha teknolojia ya mawasiliano. Huawei inampango wa kukuza teknolojia ya mawasiliano nchini Tanzania na sasa imeanza kushirikiaba kwa karibu na wazawa kama Clara. Milango iko wazi kwa yeyote anayetaka kutuunga mkono kiabiashara.

Wakati Huawei inazindua duka hilo katika Ukanda wa Kanda ya Ziwa, Mkurugenzi huyo alitangaza uwepo wa simu mpya ya kisasa, Huawei Y3II na nyinginezo, katika soko la simu nchini.

Alisema kuwa simu hiyo ina ubora na kuwataka watanzania kutumia, akifafanua zaidi kuwa ni simu yenye ubora, lakini gharama yake sio kubwa, ikilinganishwa na simu za makampuni mengine.Pia bidhaa nyingine zitaambatana na simu hiyo kama matoleo mangine tofauti Huawei P9, Y3c, Y5II ,Y6II, Y3lite na nyingine nyingi.  

Hizi ndizo faida za kuwa na duka kubwa katika Jiji la Mwanza. Kuanzia sasa wanunuzi wa bidhaa zetu wana fursa ya kupata bidhaa zetu zote kwa wakati. Tunaanza na simu hii ya Huawei Y3II ambayo kwa hakika kila atakayeamua kuitumia ataipenda kwa ubora wake.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi huyo, Kampuni ya Huawei inaendelea na mchakato wake wa kusogeza huduma zake kwa wateja wake, kwa lengo la kutimiza malengo yake ili kupambana na soko la mawasiliano.

HIZI HAPA SIMULIZI ZISIZO SAHAULIKA ZA UKATILI DHIDI YA WANAWAKE NA WATOTO.


Kama umeikosa Stori ya #KAZINANGOMA kupitia JEMBE FM ukiwa na @mansourjumanne + @gsengo 👂Mama Anna amekuwa ndani ya Shirika la Kupambana na vitendo vya ukatili katika jamii toka kuanzishwa kwake mwaka 1999 akipitia matukio mengi aliyoyakabili na mengine kupambana nayo.

Hapa anatupa uzoefu wake wakulitumikia shirika hilo akisimulia mmoja ya matukio ambayo hato yasahau:- Mama aliyekatwa sikio na mumewe na kisha mumewe kuswekwa ndani na baada ya siku chache akafia mahabusu, ndugu wakacharuka na kumnyang'anya mali zote walizovuna na mumewe wakidai kuwa ndiye aliye muua. BOFYA PLAY KUSIKILIZA KISA MKASA.VIPI MIKASA YA UKATILI KWA WATOTO.... 

Mume alitelekeza familia yaani mke na watoto, baba akaenda mbali kuishi na kimada, sasa huyu mke aliyeachwa na watoto alikuwa anajiweza kwa biashara, hivyo maisha yakawa yanaendelea na kusonga kama kawaida huku watoto wakisoma kwa mwendo wa mafanikio.

Baba alivyoona hali hiyo ya viashiria vya mafanikio kwamba baadaye watoto wangepata elimu na kuja kumsaidia mama yao kiuchumi, alichokifanya ni kitendo cha ukatili usiovumilika ...baba akatuma ndugu zake wamvizie yule mtoto akiwa anatoka shule na kumlawiti ambapo walimuambukiza magonjwa ya zinaa. 

BOFYA PLAY KUSIKILIZA KISA KIZIMA.
aaa

SKETI 'FUPI' YAMZUIA KUINGIA DARASANI UGANDA.

Msichana aliyezuiliwa kuingia darasani kutokana na kile kilichotajwa kuwa sketi fupi
Msichana aliyezuiliwa kuingia darasani kutokana na kile kilichotajwa kuwa sketi fupi.
CHANZO: BBC SWAHILI.

Mwanafunzi mmoja nchini Uganda ,Joaninne Nanyange amechapisha ujumbe mrefu katika mtandao wake wa Facebook akilalamika vile alivyozuiwa kuingia katika mlango wa darasa lake la chuo kikuu siku ya Jumatano na wanawake wawili mmoja akiwa amevalia magwanda ya polisi.
Anasema askari huyo alimtaka kuvuta sketi yake chini hadi mwisho.
''Nilicheka kwa sababu ombi lake halikueleweka.Alisisitiza hivyobasi nikamwambia hapo ndipo mwisho na hakuna vile ningeweza kuivuta hadi chini''.
Ni hapo ndipo alipoelezewa kuwa sketi yake ni fupi na kwamba hangeweza kujiunga na wenzake katika darasa la kusomea uwakili.
Hatahivyo kitivo cha uwakili mjini Kampala kimesema kuwa hakijapokea malalamishi rasmi kuhusiana na tuki hilo.
Lakini msemaji wa kituo hicho amesema kuwa kuna maadili ya mavazi na kwamba wanawake wanafaa kuvaa sketi zinazofika magotini.

BREAKING NEWS:- RAIS WA ZAMANI WA CUBA 'FIDEL CASTRO' AFARIKI DUNIA AKIWA NA UMRI WA MIAKA 90.

Aliyekuwa Rais wa zamani wa Cuba mwanamapinduzi wa Kikomunisti Fidel Castro, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 90, hii ni kwa mujibu wa kaka yake.
"Kamanda huyo mwanamapinduzi wa taifa la Cuba alifariki mnamo majira ya saa 22:29 usiku wa tarehe 25 Novemba 2016 (03:29 GMT Saturday)," alisema Rais Raul Castro.
Fidel Castro amekuwa rais wa muda mrefu kuliko wote kwani ameiongoza nchi ya hiyo iliyokuwa ndani ya mfumo wa chama kimoja kwa takribani miaka 50 kabla ya rais wa sasa Bwana Raul ambaye ni kaka yake kuingia madarakani mnamo mwaka 2008. 
Wafuasi wake wamemtaja kuwa alikuwa mtu wa kuirejesha Cuba kwa wananchi yaani Serikali ilikuwa ni mtumishi wa wananchi. Lakini amekuwa akishutumiwa kuukandamiza upinzani. 
Fidel Castro, amekuwa mwanasiasa aliyeitawala Cuba kama Waziri mkuu tangu mwaka 1959 hadi 1976 na baada ya hapo akawa rais tangu mwaka 1976 hadi 2008 alipoachia madaraka baada ya afya yake kudhoofika.


Fidel Castro                                                                               Julius K. Nyerere
IMEANDALIWA NA GSENGO BLOG

Fidel Castro, ni mmoja ya wapigania uhuru na mwanamapinduzi duniani na kiongozi wa namna yake katika utawala, pia amekuwa kiongozi wa namna yake duniani aliye amini kuwekeza katika nguvu za kivita na afya nchini Cuba.

Alikuwa ni rafiki mkubwa wa Mwalimu J.K Nyerere enzi za utawala wake mnamo mwaka 1977, ambapo alikuja hapa nchini petu Tanzania kuonana na Mwalimu katika kuangaia namna ya kuendeleza suala la kilimo na tiba ambapo pia alitoa nafasi ya wataalamu wa Tanzania kupata mafunzo ya kilimo nchini Cuba.

Tangu mwaka 2006 alianzkupata maradhi na mwaka 2008 akang'atuka na kukabidhi madaraka kwa Raul Castro.

PUMZIKA KWA AMANI MPIGANAJI MWAMBA WA DUNIA FIDEL CASTRO.

Friday, November 25, 2016

MWANZA YASISIMKA "YASIMAMA SAA KADHAA KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA KWA WANAWAKE"

Maandamano ya kusisimua yamefanyika hii leo asubuhi ndani ya jiji la Mwanza ikiwa ni sehemu ya moja ya mikoa hapa nchini ambapo Tanzania imeungana na jamii ya kimataifa kuadhimisha siku kumi na sita za kupinga ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake huku ndoa za utotoni zikibakia kuwa kikwazo kikubwa kwa mafanikio ya mtoto wa kike ndani ya jamii
Wadau wa kikosi cha Usalama barabarani toka jeshi la polisi mkoa wa Mwanza wameshiriki kikamilifu kuhakikisha zoezi la maandamano toka viwanja vya Ghand Hall hadi uwanja wa Polisi Mabatini linafanikiwa kwa nia ya kuwasilisha ujumbe kwa jamii.
Madereva bodaboda msafarani Maandamano ya Maadhimisho yaliyobeba kauli mbiu FUNGUKA Pinga Ukatili wa Kijinsia Elimu salama kwa wote .
Wadau ndani ya maandamano.
Mwanza imesisimka na kusimama kwa dakika kadhaa kushangaa muonekano wa kuvutia wa maandamano hayo ya maadhimisho ya Siku ya Ukatili Duniani ambapo wadau mbalimbali walijitokeza barabarani wakipiga picha msafara huo. 
 Shirika la Kupinga vitendo vya ukatili kwa Wanawake na Watoto na jamii kwa ujumla KIVULINI ndiyo wamesimamia mpango mzima.
Jeshi la polisi limeonekana kushiriki bega kwa bega kufanikisha dhamira iliyo wekwa.
Wakati maadhimisho haya yakifanyika jijini Mwanza tayari Serikali kupitia wizara ya Afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto imeahidi kuifanyia marekebisho sheria ya ndoa ya mwaka 1971bbkwa lengo la kumlinda mtoto wa kike dhidi ya ndoa za utotoni.

Marekebisho hayoyamelenga kumuokoa mtoto wa kike mwenye umri chini ya miaka 18, aliyeko shuleni na ambaye aliyenyumbani dhidi ya ndooa hizo zinazotajwa kuhujumu haki zao za msingi ikiwemo kupata elimu.
'Kikazi zaidi' nia kufanikisha ni Blogger GSengo wa Gsengo Blog.
Taswira.
Wazazi, wanafunzi, wafanyabiashara wadogowadogo na wakubwa wameungana kwa hili.
FICHUA UKATILI WA KIJINSIA UFIKIE MALENGO YAKO YA MAISHA.
Wadau wakitinga viwanja vya kusanyiko.
Kuwa Mwanaume anayempenda na kumjali Mwanamke.
Umoja wa Mataifa pia unatambua umuhimu wa wanawake katika kuwa na sauti sawa kwenye vyombo vya habari. Kwa mujibu wa maazimio ya Mkutano wa Nne wa Wanawake wa Beijing wa Umoja huo wa mwaka 1995, wanawake wanapaswa kuwa na ushiriki kamili na wa usawa katika vyombo vya habari, ikiwa ni pamoja na menejimenti, uandaaji wa vipindi, elimu, mafunzo na utafiti. Kwa mujibu wa maazimio hayo, kuendelea kuandika au kuonyesha mambo mabaya ya wanawake na picha zinazowadhalilisha katika vyombo vya habari kunapaswa kukomeshwa.  

Utafiti pia unasema wanaume wanaongoza kutoa sauti zao katika vyombo vya habari vya Tanzania, wakiwa ni asilimia 79 ya vyanzo vyote vya habari huku wanawake wakishika asilimia 21 tu. Katika suala la ajira katika vyombo vya habari, utafiti unaonyesha kuwa wanawake ni asilimia 36 ya wafanyakazi katika vyombo vya habari, lakini wanashika asilimia 30 tu ya nafasi za juu za utoaji wa maamuzi. 
"Asilimia 57 ya wanawake waliopo kwenye mahusiano wamewahi kutendewa ukatili wa kimwili ndani ya mahusiano hayo na asilimia 18 waliotendewa ukatili wa kingono ndiyo huenda kutafuta msaada wengine wanaona aibu, idadi ni kubwa lakini kunasababu nyingi zinazowafanya kutojitokeza"

"Ukiichukua Kanda ya Ziwa asilimia 50.4 ya wanawake ambao wamewahi kutendewa ukatili wa kimwili wamefanyiwa ukatili huo wakiwa na umri wa miaka 15, Idadi kubwa ya wasichana wanaomaliza darasa la saba kwa Kanda ya Ziwa huishia kutoendelea na elimu ya sekondari na matokeo yake huishia kwenye ndoa za utoto ni au mahusiano ambayo huanza kufanyiwa vitendo vya ukatili wakiwa na umri wa chini"......... By.  Mkurugenzi wa Mtendaji wa Shirika la KIVULINI Yasin Ally akizungumza na wadau walijitokeza viwanja vya Polisi Mabatini Mwanza.


















Polisi Konstebo Oscar Masuya ofisi ya RPC Kitengo cha Dawati la Jinsia akitoa taarifa ya Jeshi la polisi kuhusu vitendo vya uhalifu mkoa wa Mwanza ambapo jeshi hilo limekuwa likitoa msaada kwa waathirika wa vitendo vya ukatili.
Maswali na majibu.
Wanafunzi wa shule mbalimbali jijini Mwanza wamejitokeza wakiwa na hamasa kubwa.
Ngoma.




Fungua akili.
Wimbo uliovutia ulitoka kwaya hii....
Meza kuu.
Shairi bora.
Takwimu zinaonyesha kuwa kipindi cha mwaka 2016 kuanzia mwezi January hadi mwezi September yameripotia matukio ya ukatili polisi jumla ya makosa 973 ikilinganishwa na mwaka 2015 kipindi kama hicho ambapo yameripotiwa jumla ya makosa 461 tu hivyo kupelekea kuongezeka jumla ya makosa 512 ya kipindi cha mwaka 2016.

Katika kipindi cha mwaka 2016 yapo makosa ambayo yameripotiwa zaidi ukilinganisha na waka 2015, makosa hayo ni ya kulawiti kubaka, kumpa mimba mwanafunzi, kumtorosha mwanafunzi na wazazi au mzazi kutelekeza familia. 

Kuongezeka kwa takwimu kumekuja baada ya juhudi za kutoa elimu kwa wananchi kuongezeka ambapo jeshi la polisi kwa kishirikiana na asasi ya KIVULINI  limeweza kwenda maeneo mengi mkoani Mwanza na kuhamasisha wananchi katika kudhibiti vitendo vya ukatili nao wananchi wakahamasika kutoa taarifa bila shaka.

Bado kuna changamoto nyingi zinazo kabili vita ya kupinga ukatili kwa mkoa wa Mwanza na Kanda ya Ziwa kwa ujumla:- 

1. Jeshi la polisi kutokuwa na ofisi maalum.
2. Kukosekana kwa vitendea kazi ofisi zikihitaji vifaa vya kiofisi vikiwemo vifaa vya kutunzia kumbukumbu kama Computer, kwani taarifa nyingi zinahifadhiwa kwenye mafaili ambayo nayo mara nyingine hupotea au upatikanaji wake wakati wa kufuatilia kesi unakuwa wa kiusumbufu.
3. Mafunzo kwa askari wanaosimamia dawati la jinsia.
4.Kushindwa kutolewa taarifa za ukatili wa kijinsia kwa wakati hivyo kuwa na shaka shaka za kupata ushahidi sahihi.
5. Watu wengi ambao wamekuwa wakitoa taarifa za ukatili wanaporejea nyumbani huamua kurudi nyuma na kumalizana na wahalifu wao kimyakimya nazo kesi kufutwa kienyeji, hali ambayo hulirudisha nyuma jeshi la polisi katika harakati zake za kupambana na uhalifu.
6.Jamii bado haina elimu juu ya vitendo vya ukatili.
7. Wanasheria kuwa yuma katika kusimamia.