ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, March 21, 2020

BURIANI NYOTA WA COUNTRY KENNY ROGERS.


KUTOKA Los Angeles, Marekani. Nyota wa muziki wa country, Kenny Rogers, ambaye amekuwa katika muziki kwa miaka 60, amefariki akiwa na umri wa miaka 81, familia yake ilisema jana jioni.
"Rogers amefariki kwa amani akiwa nyumbani kwake na kifo chake ni cha kawaida. Amefariki akiwa chini ya uangalizi na akiwa amezungukwa na familia yake," imesema taarifa ya familia.
Mwimbaji huyo mzaliwa Texas alijulikana kwa nyimbo zake zilizotamba duniani kama "The Gambler," "Lucille" na "Islands in the Stream."
Familia ilisema ilikuwa inapanga kuwa na mazishi ya kifamilia kutokana na taifa la Marekani kuwa katika hali ya dharura baada ya mlipuko wa virusi vya corona.
 Rogers, ambaye amewahi kutwaa tuzo za Grammy mara tatu, alilazimika kufuta ziara za mwisho za kuaga mashabiki kutokana na tatizo la afya mwaka 2018.
Rogers alianza muziki mwishoni mwa miaka ya hamsini na hakuchukua muda akaanza kuwa maarufu katika muziki wa rock, jazz na aina nyingine ambazo aliziingiza katika nyimbo zake za country.

Aliendelea kutamba na vibao vyake 24 vilishika nafasi ya kwanza katika chati za muziki, akishinda mara sita katika Tuzo za Muziki wa Country na kuingizwa katika Country Music Hall of Fame.

Mashairi yake mepesi ya mapenzi na kufanya ziara mara kwa mara vilimfanya apendwe na wengi.
Rogers pia alizidisha umaarufu wake aliposhirikiana na mwanamuziki nyota wa kike, Dolly Parton na kuonekana katika vipindi vya televisheni, kikiwemo cha "The Muppet Show."

VIWANDA 50 PWANI, MTWARA NA DAR KUUNGANISHWA NA NISHATI YA UMEME WA GESI ASILIA


Naibu Waziri wa Nishati Subira Mgalu alisema kwamba katika kutimiza azma ya Tanzania kuwa na uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025 serikali imedhamilia kusambaza na kuwaunganishia nishati ya umeme wa gesi asilia katika viwanda vipya vipatavyo 50 ambavyo vimepitiwa na bomba la gesi ikiwemo Mkoa wa Dar es Salaam Pwani pamoja na Mtwara na kuongeza gharama za umeme zitashuka pindi mradi wa bwawa la umeme mwalimu nyerere utakapomalika Juni 2022 na kuzalisha mega wati 2115. Mgalu ameyasema hayo wakati wa ziara ya kikazi ya kamati ya kudumu ya bunge ya nishati na Madini ambayo yameifanya kwa lengo la kutembelea baadhi ya viwanda vilivyopo Wilayani Mkuranga Mkoa wa Pwani ambavyo vinajiendesha kwa kutumia nishati ya umeme ikiwa pamoja na kuzungumza na wawekezaji ili kubaini changamoto wanazokabiliana nao na kuzitafutia ufumbuzi. Aidha Naibu Waziri huyo amebainisha kwamba kwa sasa Serikali ya awamu ya tano mpango wake mkubwa ni kuhakikisha inasambaza na kuviunganishia viwanda mbali mbali nishati ya umeme ili viweze kutimiza malengo ya azma y serikali ya kuwa na uchumi wa kati pamoja na kutoa fursa mbali mbali za ajira kwa vijana ambao ni wazalendo lengo ikiwa waweze kujikwamua na wimbi la umasikini.

MAGEREZA KUANZISHA KIWANDA CHA MIKATE.

 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene akiongoza Kikao cha Makadirio ya Mapato, Matumizi na Miradi ya Maendeleo ya Jeshi la Magereza kilichofanyika leo katika Ukumbi wa Makao Makuu ya wizara, jijini Dodoma.Aliyesimama ni Mkuu wa Kitengo cha Mipango wa Jeshi la Magereza, Kamishna Msaidizi Mwandamizi, Ambayuu Kitiku.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Christopher Kadio, akizungumza wakati wa Kikao cha Makadirio ya Mapato, Matumizi na Miradi ya Maendeleo ya Jeshi la Magereza kilichofanyika leo katika Ukumbi wa Makao Makuu ya wizara, jijini Dodoma.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
 Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, Suleiman Mzee akizungumza wakati wa Kikao cha Makadirio ya Mapato, Matumizi na Miradi ya Maendeleo ya Jeshi la Magereza kilichofanyika leo katika Ukumbi wa Makao Makuu ya wizara jijini DodomaKushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Christopher Kadio.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
 Mkurugenzi wa Sera na Mipango wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi,Wanja Mtawazo akizungumza mbele ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene (kulia), wakati wa Kikao cha Makadirio ya Mapato, Matumizi na Miradi ya Maendeleo ya Jeshi la Magereza kilichofanyika leo katika Ukumbi wa Makao Makuu ya wizara, jijini Dodoma.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Mkuu wa Kitengo cha Mipango wa Jeshi la Magereza, Kamishna Msaidizi Mwandamizi, Ambayuu Kitiku akimpitisha katika randama Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene wakati wa Kikao cha Makadirio ya Mapato, Matumizi na Miradi ya Maendeleo ya Jeshi la Magereza kilichofanyika leo katika Ukumbi wa Makao Makuu ya wizara, jijini Dodoma. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi  
Na Mwandishi Wetu, Dodoma
Jeshi la Magereza nchini limedhamiria kuanzisha Kiwanda cha Mikate kitakachojengwa katika Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji Ukonga ili kwenda sambamba ya dhana ya Viwanda ya Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt.John Pombe Magufuli.
Hayo yamesemwa leo Machi,20  na Mkuu wa Kitengo cha Mipango wa Jeshi hilo, Kamishna Msaidizi Mwandamizi, Ambayuu Kitiku wakati akiwasilisha maelezo ya Randama kuhusu Makadirio ya Mapato, Matumizi ya Kawaida na Miradi ya Maendeleo kwa mwaka 2020/2021 mbele ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene wakati wa kikao kilichofanyika jijini Dodoma.
“Katika mpango wa bajeti wa mwaka 2020/2021 Jeshi limeweka vipaumbele katika maeneo ya ajira na maendeleo ya watumishi, utawala wa magereza, uboreshaji miundombinu ya majengo ya magereza, kuimarisha shughuli za kilimo ili kujitosheleza kwa chakula, kuimarisha shughuli za Shirika la Magereza na kuimarisha shughuli za Viwanda ikiwepo Ujengaji wa Kiwanda cha Mikate kitakachojengwa katika Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji Ukonga kilichopo jijini Dar es Salaam” alisema SACP Kitiku
Akizungumza wakati akichangia hoja hiyo Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene aliwataka Jeshi la Magereza pindi mradi huo utakapoanza watengeneze mkate bora wakizingatia suala nzima la masoko, teknolojia bora ikiwepo ladha ya mkate huo, vifungashio vyake ili waweze kwenda sambamba na hitajio la mtumiaji wa mwisho
“Ni wazo zuri kwa mlichopanga kwani mtakapofanikiwa mtakua mmeongeza kipato na ile dhana ya jeshi la magereza kujitegemea itakua sasa imeingia kwenye utekelezaji sambamba na kujitosheleza kwa chakula cha kulisha wafungwa, lakini katika mpango huo lazima baadhi ya mambo muyafanyie utafiti ikiwepo soko linataka nini, teknolojia mtakayotumia muhakikishe ni nzuri itakayowafanya mpate bidhaa yenye ladha nzuri sambamba na kifungashio cha bidhaa hiyo, ni vizuri mmeliweka wazo wazi mapema nadhani mtapata michango ya kuliboresha” alisema Simbachawene
Jeshi la Magereza limeomba kuidhinishiwa kiasi cha Shilingi 201,251.298,000/- katika mwaka wa fedha 2020/2021 kwa ajili ya matumizi mbalimbali ikiwemo miradi ya maendeleo huku likiweka lengo la kukusanya maduhuli ya Shilingi 2,000,000.000/- kwa mwaka wa fedha wa 2020/2021.

Friday, March 20, 2020

VIDEO- WANAHAMIAJI HARAMU 51 RAIA WA ETHIOPIA WAKAMATWA WILAYANI BAGAMOYO


NA VICTOR MASANGU
Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na usalama wa Wilaya ya Bagamoyo Zainabu Kawawa alisema, wahamiaji hao wamekutwa katika pori wakiwa katika harakati za kutafuta usafiri kuelekea Mikoa ya Nyanda za juu Kusini ili waweze kuendelea  na safari yao hadi Afrika Kusini.

Kawawa lisema, Wahamiaji hao walikuwa wanaotokea nchini Ethiopia, ambao katika mahojiano ya awali walikiri kuingia Nchini kwa kupitia Pwani ya Bagamoyo, wakitumia majahazi. 

Alisema, Wahamiaji hao walichukuliwa hadi katika kituo cha Afya Matimbwa (Bagamoyo) ili kupimwa kama Wana maambukizi ya Virusi vya Corona.

Kituo hicho kilichotengwa na Halmashauri kwa ajili ya kuhudumia wagonjwa wa Corona wanaoweza kujitokeza siku za usoni, .

MWANZA KILA KONA NI MAPAMBANO YA CORONA


Baadhi ya wakazi wa jiji la MWANZA wameamka na kuanza kuchukua hatua na tahadhari ya kujikinga na maambukizi ya virusi vya ugonjwa wa korona hususani ni wafanyabiashara. Hatua hiyo imekuja kufuatia Serikali kupitia Wizara ya afya kuueleza umma kuwepo kwa wagonjwa wawili waliogundulika kuwa na virusi vya ugonjwa wa corona nchini na kuwataka wananchi kuchukua tahadhari.

Dkt. Phills nyimbi ni Mkuu wa wilaya ya Nyamagana anafanya ukaguzi kwenye maeneo yote ya huduma muhimu yenye huduma za mikusanyiko ikiwemo mashule,maduka ya bidhaa mbalimbali, mahoteli, hospitali ya mkoa na mahoteli jijini Mwanza kujionea utekelezaji wa agizo la serikali.

RAIA 51 WA KIGENI WANASWA KICHAKANI WILAYANI BAGAMOYO MKOANI PWANI

 Baadhi ya wahamiaji haramu 51 ambao ni raia wa Ethiopia ambao wamekamatwa kwa kos ala kuingia nchini bila ya kibali wakiwa wamekamatwa wakiwa wamejificha katika kichaka ambacho kipo karibu na pembezoni mwa ufukwe wa bahari ya hindi(Picha na Victor Masangu)

Baadhi ya wahamiaji haramu 51 ambao ni raia wa Ethiopia ambao wamekamatwa kwa kos ala kuingia nchini bila ya kibali wakiwa wamekamatwa wakiwa wamejificha katika kichaka ambacho kipo karibu na pembezoni mwa ufukwe wa bahari ya hindi(Picha na Victor Masangu)

Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Bi. Zainabu Kawawa akiwa ananawa mikono baada ya kutoka kuwaangalia wahamiaji haramu  wapatao 51 ambao wamekamatwa kwa kuingia nchini bila ya kuwa na kibali maalumu katika maeneo ya kichaka kimoja kilichopo ufukweni mwa bahari ,(Picha na Victor Masangu)
 Baadhi ya wahamiaji haramu raia wa Ethiopia ambao wamekamatwa kutokana na kuingia  nchini bila ya kuwa na kibali wakiwa katika moja ya kituo cha afya kwa ajili ya kuangaliwa afya zao ikiwemo kuwapima kama wanamaambukizi ya magonjwa mbali mbali ikiwemo ugonjwa wa Corona.(Picha na Victor Masangu)
 Mwonekano wa basi ambalo limewabeba wahamiaji hao haramu wapatao 51 ambao wamekamatwa kwa kosa la kuingia nchini bila ya kuwa na kibali ambao serikali ya Wilaya ya Bagamoyo chini ya Mwenyekiti wake Zainabu Kawawa imeamua kuwapeleka katika eneo maalumu ili kuepukana kama watakuwa na maambukizi wa ugonjwa wa Corona.(PICHA Victor Masangu)
NA VICTOR MASANGU, BAGAMOYO

JESHI la Polisi Mkoa wa Pwani limewakamata Wahamiaji haramu 51 walioingia nchini kupitia bandari bubu ya ya Makurunge Tarafa ya Yombo Wilayani Bagamoyo Mkoani hapa.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani  Wankyo Nyigesa alithibitisha kutokea kwa tukio hilo, ambapo alisema wahamiaji hao walikamatwa  majira ya saa 11 alfajiri Mach 19.

Wankyo alisema, watuhumiwa hao walikabidhiwa kwa vyombo vingine vya dola kwa taratibu za kisheria  waweze kuchukuliwa hatua.

Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na usalama wa Wilaya ya Bagamoyo Zainabu Kawawa alisema, wahamiaji hao wamekutwa katika pori wakiwa katika harakati za kutafuta usafiri kuelekea Mikoa ya Nyanda za juu Kusini ili waweze kuendelea  na safari yao hadi Afrika Kusini.

Kawawa lisema, Wahamiaji hao walikuwa wanaotokea nchini Ethiopia, ambao katika mahojiano ya awali walikiri kuingia Nchini kwa kupitia Pwani ya Bagamoyo, wakitumia majahazi. 

Alisema, Wahamiaji hao walichukuliwa hadi katika kituo cha Afya Matimbwa (Bagamoyo) ili kupimwa kama Wana maambukizi ya Virusi vya Corona.

Kituo hicho kilichotengwa na Halmashauri kwa ajili ya kuhudumia wagonjwa wa Corona wanaoweza kujitokeza siku za usoni, .

Wahamiaji hao, wamefikishwa katika kituo hicho ili kufanyiwa vipimo vya awali kujiridhisha kama hawana maambukizi ya ugonjwa wa Corona,  kabla ya kupelekwa katika gereza la Kigongoni  Wilayani Bagamoyo wakisubiri kusomewa mashtaka yao ya kuingia Nchini bila kibali


Wakati huo huo, Jeshi la Polisi Mkoani Pwani linawashikilia watu watatu kwa tuhuma za kuhusika na mauaji na kufukia mwili wa marehemu..

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani Wankyo Nyigesa alisema, watuhumiwa hao walikamatwa Machi 19 huko Kibindu Wilaya ya Bagamoyo wakituhumiwa kuua na kuzika mwili wa marehemu (jina linahifadhiwa)katika shamba la mahindi.

Wankyo alisema, Machi 3, majira ya saa nane mchana huko Kibindu mtuhumiwa Chacha Machangu (27) alimfumania mke wake akiwa na mwanaume mwingine .

Kamanda alisema, Machangu alimshambulia mke wake kwa kumkata na panga maeneo mbalimbali ya mwili wake na kumsababishia majeraha yaliyopelekea kifo.

Wankyo alisema, Machangu kwa kushirikiana na ndugu zake Emmanuel Machangu (19) na Hamis Machangu (22 walichimba shimo kwenye shamba la mahindi na kufukia mwili wa marehemu.

Kamanda alibainisha kuwa, Machi 19 Jeshi la Polisi lilipata taarifa kutoka kwa wasamaria wema ambapo lilifanikiwa kuwakamata watuhumiwa hao watatu ambao walionyesha shimo lilipo na lilipofukuliwa mwili wa marehemu ulipatikana.

Alisema, mwili wa marehemu ulifanyiwa uchunguzi na daktari na kufanyiwa mazishi kwa kufuata taratibu.

Jeshi hilo limesema, bado linaendelea kuwasaka watuhumiwa wengine wanaodaiwa kushiriki katika tukio hilo.

BITEKO AWATAKA WACHIMBAJI MADINI KUCHUKUWA TAHADHARI DHIDI YA CORONA.

Baadhi ya wachimbaji wadogo wa Almasi katika Kata ya Magazo Wilaya Kishapu mkoani Shinyanga (kulia), wakisalimiana na Waziri wa Madini, Doto Biteko (wa kwanza kushoto) alipotembelea eneo la kuchenjulia mabaki ya mchanga wa almasi (makinikia) kutoka mgodi wa Mwadui/ Williamson Diamonds Ltd. Wachimbaji hao wamechukua tahadhari ya kujikinga na maambukizi ya virusi vya Corona kwa kuvaa vikinga pua na mdomo (mask).
Waziri wa Madini, Doto Biteko (kulia) akisalimiana na baadhi ya viongozi wa mgodi wa Mwadui/ Williamson Diamonds Ltd (kushoto) alipotembelea mgodi huo kujionea zoezi la utoaji nje mabaki ya mchanga wa almasi (makinikia) kwa ajili ya kuchenjuliwa upya na wachimaji wadogo.
 Mkuu wa Wilaya Kishapu mkoani Shinyanga, Nyabaganga Talaba (katikati) akionesha namna sahihi ya kutakasa mikono kwa kutumia sabuni maalum (hand sanitizer) ili kujikinga na maambukizi ya virusi vya Corona.
 Waziri wa Madini, Doto Biteko akiwa ameambatana na viongozi mbalimbali wilayani Kishapu kukagua eneo la mchanga wa almasi uliotolewa na mgodi wa Mwadui (Williamson Diamonds Ltd).
 Waziri wa Madini, Doto Biteko akiwa ameambatana na viongozi mbalimbali wilayani Kishapu akitoka kukagua eneo la mabaki ya mchanga wa almasi uliotolewa kwa wananchi na mgodi wa Mwadui (Williamson Diamonds Ltd) ili kuchenjuliwa upya.
Waziri wa Madini, Doto Biteko akikagua vizimba vilivyoandaliwa kwa ajili ya shughuli ya kuchenjua mabaki ya machanga wa almasi (makinikia) katika eneo la Maganzo wilayani Kishapu. 
Zoezi la utoaji mabaki ya mchanga wa almasi (makinikia) kwa ajili ya kuchenjuliwa upya na wananchi katika eneo la Maganzo limeanza Machi 19, 2020.
 Waziri wa Madini, Doto Biteko akiwa ameambatana na viongozi mbalimbali wilayani Kishapu akikagua eneo ambalo wananchi watakuwa wakitakasa mikono yao kwa sabuni maalum (hand sanitizer) kabla ya kuingia eneo la kuchenjulia mabaki ya mchanga wa almasi (makinikia) ikiwa ni tahadhari dhidi ya virusi vya Corona.
 Waziri wa Madini, Doto Biteko (kulia) akikagua vifaa vya kupima ubora wa almasi katika eneo la mnada wa uuzaji madini hayo lililopo katika mgodi wa Mwadui unaomilikiwa na kampuni ya Williamson Diamonds Ltd.
Meneja Mkuu wa Mgodi wa Mwadui/ Williamson Diamonds Ltd, Ayound Mwenda (kushoto) akitoa ufafanuzi kuhusu vifaa vya kupimia ubora wa alamsi mgodini hapo.

Na George Binagi-GB Pazzo, Shinyanga
Waziri wa Madini, Doto Biteko amewataka wachimbaji wa madini nchini Tanzania kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya maambukizi ya ugonjwa wa mafua, kikohozi na homa kali ya Corona ambao umesababisha athari ikiwemo vifo katika mataifa mbalimbali duniani.

Biteko alitoa tahadhari hiyo Machi 19, 2020 alipotembelea eneo la kuchenjulia mabaki ya mchanga wa almasi (makinikia) uliotolewa na mgodi wa Mwadui (Williamson Diamonds Ltd) kwa wachimbaji wadogo ambapo alifurahishwa na matayarisho mazuri ya eneo hilo ikiwemo tahadhari dhdi ya virusi vya Corona kabla ya zoezi la kuchenjua mchanga huo halijaanza rasmi.

“Tuendelee kujikinga na maambukizi ya virusi vya Corona kwa kuepuka kushikana mikono ovyo, lakini pia tuzingatie matuzi sahihi ya viziba pua na mdogo (mask) pamoja na kutakasa mikono kwa kutumia sabuni maalum (hand sanitizer)” alisisitiza Biteko wakati akisalimiana na baadhi ya wachimbaji wadogo wa almasi katika eneo la Maganzo.

Aidha Biteko aliwakumbusha wafanyabishara na wachimbaji wadogo wa almasi kufanya shughuli zao kwa kuzingatia sheria na kanuni za madini ikiwemo kuuza madini yao kwenye masoko huku wakijiepusha na utoroshaji madini kwani yeyote atakayeshindwa kufanya hivyo ataangukia mikononi mwa sheria na kuishia kufungwa jambo ambalo asingependa litokee.

“Ni marufuku kutunza kinyemera madini nyumbani kwako bila kuwa na nyaraka kutoka kwa maafisa wetu wa madini, sisi tukikukamata hayo madini yatakuwa mali halali ya Serikali” Biteko aliwatahadharisha wafanyabishara na wachimbaji wa almasi.

Awali akizungumzia zoezi la utoaji nje mchanga wa almasi, Katibu Mkuu wa Chama cha Wachimbaji Madini Mkoa Shinyanga (SHIREMA), Greygory Kabusi alisema maandalizi yamekamilika na vikundi 700 vya wachimbaji wadogo wa almasi vyenye wanachama 10 kila kimoja vinatarajiwa kuanza shughuli ya kuchenjua mchanga huo na hivyo kujipatia kipato.

Naye Mkuu wa Wilaya Kishapu, Nyabaganga Talaba alisema Serikali inafuatilia kwa ukaribu zoezi la uchenjuaji mchanga huo ili kuchukua tahadhari za kiusalama hususani katika kipindi hiki cha maambukizi ya virusi vya Corona.
Tazama video hapa chini

MWANAMUZIKI MKONGWE AURLUS MABELE AFARIKI KWA CORONA.

Mwanamuziki mkongwe wa miondoko ya Soukous Aurlus Mabele amefariki dunia jijini Paris nchini Ufaransa.

Kwa mujibu wa NationBreaking kifo cha Mabele kimetokana na kiharusi na homa ya Covid-19.


Taarifa hiyo imetolewa na msanii mwenzake wa LOKETO Nyboma Mwandido.



ENZI ZA UHAI WAKE.

Thursday, March 19, 2020

BOT YATOA NENO KUHUSU CORONA.

Benki Kuu ya Tanzania inapenda kuutarifu umma kwamba noti zetu zimetengenezwa kwa namna ambayo zinaweza kuzuia vimelea kusalia kwenye noti. Hata hivyo, kwa kuwa noti hizo zinapita katika mikono mingi, tunawashauri wananchi kuzingatia miongozo mbalimbali inayotolewa na mamlaka zenye dhamana ya afya ya jamii, ikiwa ni pamoja na kunawa mikono mara kwa mara kwa kutumia maji yanayotiririka na sabuni au kutumia vitakasa mikono (sanitizers). Kufanya hivyo kutasaidia kuua vimelea kwenye mikono.

Aidha, tunawashauri wananchi kufanya miamala kwa kutumia njia mbadala za malipo kama vile simu za mkononi, intaneti na kadi bila kulazimika kufika kwenye kaunta za benki au ATM kuchukua noti.


Kama ilivyotangazwa na Shirika la Afya Duniani (WHO), Ugonjwa wa Corona ni tishio duniani kote na tayari umeingia nchini tangu Jumatatu Machi 16, 2020 kwa mgonjwa wa kwanza kupatikana mkoani Arusha na wagonjwa wengine wawili mmoja huko Zanzibar na mwingine jijini Dar es Salaam ambao walitangazwa jana na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, na hivyo kufanya jumla ya wagonjwa wa Corona (COVID-19) hapa nchini kufikia watatu.

Tunawasihi wananchi katika kipindi hiki ambacho taifa liko katika mapambano dhidi ya COVID-19 kuzipuuza taarifa zinazozagaa mitandaoni ambazo hazina vyanzo vya uhakika, zinazozihusisha noti zetu na usambazaji wa virusi vya corona

UDSM WATOA SAA 48 WANAFUNZI KUONDOKA .

Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) nchini Tanzania kimewataka wanafunzi wote kuhakikisha ifikapo Ijumaa Machi 20, 2020 wawe wameondoka kurejea nyumbani.
UDSM imetoa taarifa hiyo leo Jumatano Machi 18,2020 ikiwa ni saa chache kupita tangu Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa atangaze kuvifunga vyuo vyote kutokana na kujikinga na virusi vya ugonjwa wa corona (CODIV-19).

Agizo hilo la Majaliwa amelitoa baada ya wagonjwa wawili zaidi raia wa kigeni kubainika kuwa na virusi vya corona wakiwa Dar es Salaam na Zanzibar hivyo kufikisha idadi ya waliobainika nchini humo kuwa watatu.

Katika taarifa ya Makamu mkuu wa UDSM, Profesa William Anangisye imesema katika kutekeleza maelekezo na ushauri wa Serikali kwa lengo la kudhibiti kuenea kwa ugonjwa huo, shughuli zote za masomo chuoni hapo zimesitishwa kuanzia leo Machi 20 2020 hadi hapo itakapotangazwa vinginevyo.

“Kutokana na masomo kusitishwa, wanafunzi wote, wa programu zote, walioko likizoni wanatakiwa kubaki nyumbani huko waliko, hadi hapo watakapotaarifiwa kurejea chuoni,” amesema Profesa Anangisye

Makamu mkuu huyo wa chuo amesema, “wanafunzi wote wa programu zote, ambao kwa sababu mbalimbali bado wapo katika kampasi yoyote ya chuo wanatakiwa kuwa wameondoka chuoni ifikapo Ijumaa Machi 20, 2020, kwenda nyumbani hadi hapo watakapotaarifiwa kuwa chuo kimefunguliwa tena.”

NAIBU WAZIRI UTALII AIMWAGIA SIFA APC KWA KUSHIRIKI MAPAMBANO YA UJANGILI, KUHAMASISHA UTALII WA NDANI

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Constantine Kanyasu wa nne kutoka kushoto akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa kamati ya utendaji ya APC pamoja na wafanyakazi wake
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Constantine Kanyasu akimsikiliza Mwenyekiti wa APC Claud Gwandu (Hayupo pichani), alipokuwa akieleza shughuli ambazo zimekuwa zikifanywa na APC kwa ustawi wa wanachama wake pamoja na jamii
Mwenyekiti wa APC Claud Gwandu akimweleza Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Constantine Kanyasu (Haonekani pichani) shughuli ambazo APC imekuwa ikizifanya mara baada ya waziri huyo kutembelea ofisini za APC
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Constantine Kanyasu akisaini kitabu cha wageni alipotembelea ofisi za chama cha waandishi wa habari Mkoa wa Arusha (APC)

Na Seif Mangwangi, Arusha
NAIBU Waziri wa Maliasili na Utalii, Constantine Kanyasu amepongeza uongozi wa Klabu ya waandishi wa habari Mkoa wa Arusha (APC), kwa ushiriki wake katika maendeleo ya uhifadhi nchini ikiwemo mapambano dhidi ya ujangili na uhamasishaji utalii wa ndani.

Kanyasu ameyasema hayo wakati akizungumza na uongozi wa Kamati ya utendaji ya APC alipofanya ziara katika ofisi hizo kwa lengo la kujionea shughuli ambazo zimekuwa zikifanywa na klabu hiyo na kusikiliza changamoto ambazo wamekuwa wakikabiliana nazo.

Amesema Mkoa wa Arusha ni kitivo kikuu cha utalii na wakati wote ambapo amekuwa akifuatilia taarifa za utalii waandishi wa habari wa Arusha wamekuwa wakiongoza kuandika taarifa hizo ambazo matokeo  yake yamekuwa makubwa kwa jamii.

“Arusha mmekuwa na mchango mkubwa sana kwenye suala la maendeleo ya utalii nchini, ukizungumzia ujangili ambao umeshuka kwa asilimia kubwa sana nchini mchango wenu ni mkubwa sana, kwa kweli kama Wizara tunawapongeza sana,”anasema.

Anasema Wizara yake itaendelea kushirikiana na waandishi wa Arusha na wengine wote nchini ili kuendelea kuhamasisha utalii wa ndani pamoja na mapambano dhidi ya ujangili unaofanywa na watu wachache wenye nia mbaya ovu kwa nchi ya Tanzania.

Awali Mwenyekiti wa APC, Claud Gwandu, alimweleza Naibu Waziri kuwa waandishi wa habari wa Arusha wamekuwa wakishirikiana kwa karibu na uongozi wa Mamlaka ya hifadhi za Taifa (TANAPA), katika kutangaza shughuli za utalii.

Amemweleza Naibu Waziri kuwa hivi sasa APC iko kwenye maandalizi ya kuandaa maadhimisho ya siku ya uhuru wa vyombo vya habari duniani, yanayoadhimishwa Mei 3 ya kila mwaka ambapo inatarajia kukutanisha waandishi wote wa Arusha na kujadili changamoto ambazo wamekuwa wakikabiliana nazo mwaka mzima.

Amesema katika maadhimisho hayo APC inatarajia kuzindua televisheni yake (APC Online tv), zpamoja na blogu ambazo mbali ya kutumika kuuhabarisha umma masuala ya kijamii pia zitakuwa na vipindi maalum vya kutangaza utalii.

Wednesday, March 18, 2020

MGALU- VIWANDA 50 PWANI,MTWARA NA DAR KUUNGANISHWA NA NISHATI YA UMEME WA GESI ASILIA

 Naibu Waziri wa Nishati Mh. Subira Mgalu akizungumza jambo kuhusiana na mikakati ya serikali ya awamu ya tano ya kuweka mipango ya kuunganisha nishati ya umeme wa gesi asilia katika viwanda vipya 50 wakati wa ziara ya Kamati ya kudumu ya bunge ya nishati na madini ambayo ilifanya ziara yake ya kikazi ya kutembelea baadhi ya viwanda vilivyopo katika Wilaya ya Mkuaranga.(Picha na Victor Masangu)
 Badhi ya wabunge wanaounda kamati ya nishati na madini wakati wanaingia katika kiwanda cha kuzalishia chuma cha Lodhia ikiwa ni moja ya ziara yao ya kikazi kwa ajili ya kuijionea shughuli mbali mbali zinazofanywa na wawekezaji pamoja na kubaini changamoto zao, wa kati kati ni Mbunge wa Jimbo la Kibaha Vijijini Hamoud Jumaa.(Picha na Victor Masangu)
  Kaimu mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya bunge ya nishati na Madini Vedastus Matayo akipokea maelekezo kutoka kwa mmoja wa viongozi wa kiwanda cha kuzalishia chuma cha Lodhia kilichopo kata ya Kisemvule wakati wa ziara ya kamati hiyo ilipokwenda kwa ajili ya kujionea shughuli mbali mbali za uzalishaji kiwandani hapo (Picha na Victor Masangu)
 Mmoja wa wakurugenzi wa kiwanda cha Lodhia ambacho kinajishighulisha na uzalishaji wa bidhaa mbali mbali ikiwemo chuma, akiwaonyesha wajumbe wa kamati ya bunge ya nishati na madini jinsi ya kiwanda hicho kinavyofanya kazi pamoja na kuwaelezea changamoto mbali mbali zinazowakabili ili kuziwasilisha kwa serikali zifanyiwe kazi.(Picha na Victor Masangu)
 Mwonekano wa mtambo maalumu wa kuzalishia nishati ya umeme wa gesi asilia ambao umefunngwa na  shirika la TPDC katika kiwanda hicho cha kuzalishia chuma pamoja na kutengenezea  mabomba ya maj wakati wa ziara hiyo ya kamati ya bunge ya nishati na madin.(Picha na Victor Masangu)
 Baadhi ya wajumbe wa kamati ya bunge ya nishati na madini wakiwa na viongozi mbali mbali wa kiwanda hicho wakitembezwa katika maeneo mbali mbali ili kuweza kujionea mwenendo mzima wa vyuma chakavu vinavyoyayushwa na kutengenezwa Nondo mpya kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbali mbali ikiwemo ile ya serikali.(Picha na Victor Masangu)
 Mkurugenzi mtendaji wa kiwanda cha Lodhia  Haruni Lodhia ambacho kinajihusisha na uzalishaji wa kutengeneza Nondo pamoja bidhaa zingine mbali mbali akizungumza mbele ya wajumbe  kamati ya bunge ya nishati na madini  hawapo pichani ilipofanya ziara ya kikazi ya kutembelea kiwanda hicho.(Picha na Victor Masangu)
VICTOR MASANGU, MKURANGA
 Naibu Waziri wa nsihati Subira Mgalu alisema kwamba katika kutimiza azma ya Tanzania kuwa na uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025 serikali imedhamilia kusambaza na kuwaunganishia  nishati ya umeme wa gesi asilia  katika viwanda vipya vipatavyo 50  ambavyo vimepitiwa na bomba la gesi ikiwemo Mkoa wa Dar es Salaam Pwani pamoja na Mtwarana kuongeza gharama za umeme zitashuka pindi mradi wa bwawa la umeme mwalimu nyerere utakapomalika Juni 2022 na kuzalisha mega wati 2115.
Mgalu  aliyasema hayo wakati wa ziara ya kikazi ya  kamati ya kudumu ya bunge ya nishati na Madini ambayo yameifanya  kwa lengo la kutembelea baadhi ya viwanda vilivyopo Wilayani Mkuranga Mkoa wa Pwani  ambavyo vinajiendesha kwa kutumia nishati ya umeme ikiwa pamoja na kuzungumza na wawekezaji ili kubaini changamoto wanazokabiliana nao na kuzitafutia ufumbuzi.
Naibu Waziri huyo alibainisha kwamba kwa sasa serikali ya awamu ya tanoi mpango wake mkubwa ni kuhakikisha inasambaza na kuviunganishia viwanda mbali mbali nishati ya umeme ili viweze kutimiza malengo ya azma y serikali ya kuwa na uchumi wa kati pamoja na kutoa fursa  mbali mbali za ajira kwa vijana  ambao ni wazalendo  lengo ikiwa waweze kujikwamua na wimbi la umasikini.
“Mpango wetu wa serikali licha ya kuwa bado kuna baadhi ya maeneo ya viwanda hayajafikiwa na nishati ya umeme lakini kwa sasa kupitia nishati ya gesi asilia tuna mpango wa kuviunganishia viwanda vipya vipatavyo 50 ambavyo vipo katika Mikio ya Dar es Salaam, Mtwara pamoja na Mkoa wa Pwani hivyo juhudi za makusudi bado zinaendelea kwa hiyo viwanda ambavyo vinapitiwa na bomba kubwa la gesi vitaweza kunufaika.
Aidha Naibu Waziri huyo alifafanya kwamba pindi mradi wa umeme wa bwawa la Malimu Nyerere uliopo Wilayani Rufiji utakapokamilika utaweza kuwa ni mombozi mkubwa kwa wawekezaji wa viwanda vidogo, vya kati na vile vikubwa kutoka maenne mbali mbali sambamba na kuwaunganishia wananchi wengine pamoja na taasisi za serikali na sizozo  za serikali.
Katika hatua nyingine Mgalu ameipongeza kamati ya kudumu ya bunge ya nishati na madini kwa kuweza kwenda kutembelea katika kiwanda cha kuzalisha chuma pamoja na mabomba ya maji ili kuweza kubainichangamoto mbali mbali ambazo zinawakabili wawekezaji na hatimaye kuweza kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu ambao utasaidia kutimiza azma ya serikali ya kuwa na uchumi wa kati kupitia viwanda hivyo.
Kwa upande wake  Kaimu mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya bunge ya nishati na Madini Vedastus Matayo alibainisha kwamba ujenzi wa kiwanda hicho utaweza  kuipunguzia serikali gharama kubwa ambazo zimekuwa zikitumia kwa ajili ya kuagiza baadhi ya Nondo kutoka nje ya nchi hivyo amempongeza mwekezaji huyo kwa  kuwekeza katika  Wilaya ya Mkuranga kwani kumesaidia vijana zaidi ya 1 300 kupata fursa ya ajira.
“Sisi kama kamati kwa kweli tunapenda kumpongeza mwekezaji huyo kwa kuweza kuwekeza katika Wilaya ya Mkuranga ambayo ipo katika Taifa letu ya Tanzania hii ni hatua nzuri ambayo ameifanya na kwa sasa anazalisha bidhaa mbali mbali kwa kutumia nishati ya umeme wa gesi asilia hivyo kutaweza kuleta mabadiliko chanya ya kimaendeleo kwa wananchi wenyewe pamoja na wale wawekezaji wa ndani na nje ya nchi,”alibainisha  Matayo
Aidha Matayo katika hatua nyingine alibainisha kuwa Kamati ya bunge ya nishati ya kudumu ya nishati na  madini  ilibaini kuwepo kwa urasimu na ucheleweshaji wa vibali kutoka kwa baaadhi ya mamlaka zinazohusika kwa wawekezaji wa sekta ya viwanda pamoja na gharama ya nishati ya umeme kuwa ni kubwa hivyo hivyo watayachukua mapendekezo hayo kwa ajili ya kuyawasilisha bungeni ili serikali iweze kuyatafutia ufumbuzi wa kudumu.
Pia alisema kuwa mapendekezo pamoja na changamoto mbali mbali ambazo wamekutana nazo katika kiwanda hicho ikiwemo na maeneo mengine ambayo tayari wameshayapitia watayawasilisha serikalini ili yaweze kufanyiwa kazi ikiwemo na kutilia mkazo katika suala la usumbufu mkubwa wanaoupata wawekezaji pindi wanapohitaji kuagiza matilio mbali mbali kutoka nje ya nchi kwa ajili ya kutengeneza bidhaa zao.
Awali  akitoa taarifa mbele ya Kamati ya nishati na madini Mkurugenzi mtendajiwa wa kiwanda hicho cha kuzalisha chuma Haluni Lodhia amebainisha kwamba hapo awali walikuwa wanakabilia na changamoto kubwa ya ukosefu wa nishati ya umeme wa uhakika pamoja na miundombinu ya barabara,ambapo ameipongeza serikali ya awamu ya tano kupitia Shirika la maendeleo ya  Petroli Tanzania (TPDC) kwa litafutia ufumbuzi suala hilo na hatimaye kuanza utekelezaji wa kuzalisha bidhaa mbali mbali, ikiwemo Nondo, mabomba ya maji na bodi za jasi.

Tuesday, March 17, 2020

SERIKALI YA TNZANIA YAFUT WIKI YA MAJI 2020



Waziri wa Afya wa Tanzania, Ummy Mwalimu
Dar es Salaam. Wizara ya Maji nchini Tanzania imetangaza kufuta shughuli zote zilizokua zifanyike kuelekea Siku ya Maji Duniani.

Taarifa iliyotolewa leo Jumatatu Machi 16, 2020 na Kitengo cha Mawasiliano cha wizara hiyo imesema hatua hiyo inatokana na kuchukua tahadhari dhidi ya maambukizi ya Virusi vya Corona.

“Tunasikitika kwa usumbufu utakaojitokeza kwa wadau wote,” ameeleza taarifa hiyo

Kufutwa kwa maadhimisho hayo, kumetolewa ikiwa ni saa chache kupita tangu Waziri wa Afya wa Tanzania, Ummy Mwalimu kutangaza raia mmoja wa nchi hiyo kubainika kuwa na ugonjwa wa Corona.

Raia huyo ambaye ni mwanamke mwenye miaka 46 aliwasili nchini humo jana Jumapili akitokea Ubelgiji.