Baadhi ya wakazi wa jiji la MWANZA wameamka na kuanza kuchukua hatua na tahadhari ya kujikinga na maambukizi ya virusi vya ugonjwa wa korona hususani ni wafanyabiashara. Hatua hiyo imekuja kufuatia Serikali kupitia Wizara ya afya kuueleza umma kuwepo kwa wagonjwa wawili waliogundulika kuwa na virusi vya ugonjwa wa corona nchini na kuwataka wananchi kuchukua tahadhari.
Dkt. Phills nyimbi ni Mkuu wa wilaya ya Nyamagana anafanya ukaguzi kwenye maeneo yote ya huduma muhimu yenye huduma za mikusanyiko ikiwemo mashule,maduka ya bidhaa mbalimbali, mahoteli, hospitali ya mkoa na mahoteli jijini Mwanza kujionea utekelezaji wa agizo la serikali.
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.