ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, January 21, 2022

SHAHIDI AELEZA WALIVYOWAKAMATA WATUHUMIWA KESI YA KINA MBOWE.

 


CHANZO:- MWANANCHI
Shahidi wa 11 upande wa mashtaka katika kesi ya ugaidi inayomkabili Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na wenzake watatu ameieleza mahakama alivyoshiriki katika kuwakamata na kuwasafirisha hadi Dar es Salaam watuhumiwa katika kesi hiyo.


Akitoa ushahidi wake leo Ijumaa Januari 21, 2022 Askari mpelelezi Sajenti Goodluck ameleza alivyomkamata mtuhumiwa mwingine aitwaye Halfan Bwire maeneo ya Polisi Chang'ombe Jijini Dar es Salaam.


Soma ushahidi wote hapa


Wakili Kidando: Mheshimiwa Jaji shauri hili linakuja kwa anili ya kusikilizwa kwa leo tuna shahidi mmoja tuko tayati kuendelea


Jaji: Utetezi?


Kibatala: Nasi tuko tayari


shahidi ameitwa na anapanda kizimbani


Jaji: Majina yako


Shahidi: Naitwa H.4347 Detective  Sajent Goodluck


Jaji: Umri wako


Shahidi: miaka 32


Jaji: Dini


Shahidi: Mkristo


Jaji: Kabila lako?


Shahidi:Mchaga


Shahidi anaongozwa na Wakili wa Serikali Mwandamizi Pius Hilla.


Shahidi: Naitwa Detective Sajent Goodluck


Soma zaidi: Kesi ya kina Mbowe kuanza na kiporo cha mapingamizi


Kazi yangu ni Askari Polisi tangu mwaka 2013 na kituo changu cha kazi ni Central Police Arusha, niko hapo tangu mwaka 2014.


Jukumu langu ni Upelelezi wa Makosa ya jinai.


Shahidi: Tarehe 4/8/2020 nilikuwa kazini Polisi Arusha, nikiendelea na majukumu yangu, jioni siku hiyo nilipata taarifa kutoka kwa afande Mahita kuwa tunahitajika kwa Afande RCO, (Mkuu wa Upelelezi mkoa) mimi na Koplo Francis.


Shahidi: Afande Mahita ni Msaidizi wa Afande OC-CID (Mkuu wa Upelelezi Wilaya).


Shahidi: Aliyekuwa RCO kipindi hicho alikuwa ni Afande Ramadhani Kingai


Shahidi: Tulipofika kwa Afande RCO alisema kuwa kuna kazi ya kufanya.


Shahidi: Mimi na Koplo Francis tulikwenda kuchukua silaha, Mimi nilichukua AK47 na mwenzangu pia.


Shahidi: Baada ya kuchukua silaha tulirudi mkoani kwa Afande RCO. Alisema tunatakiwa twende Polisi Usa River Wilaya ya Arumeru.


Shahidi: Muda huo ilikuwa Ni majira ya saa 12 jioni


Shahidi: Safari ya kuslekwa Usa Riva ilihusisha Afande RCO,Mimi, Afande. Mahita, na Koplo Francis.


Shahidi: Baada ya kufika kituo Polisi Usa River tuliingia kituoni tukamkuta OC- CID ambaye alikuwa ni Afande Jumanne. Alikuwa nje ya kituo.


Shahidi: Alitukaribisha ofisini kwake ambapo wote tuliingia.


Shahidi: Tukiwa ofisini Afande RCO alitwambia amepewa maelekezo ya kuandaa timu ya kufanya kazi ambayo ni kazi maalum.


Shahidi: Hakusema alipewa maelekezo na nani.


Shahidi: Alitwambia kuwa amepata taarifa kuna kitu cha watu wamekula njama kufanya vitendo vya kigaidi maeneo mbalimbali.


Soma zaidi:Shahidi augua, kesi ya kina Mbowe yaahirishwa


Shahidi: Alitwambia pia taarifa alizozipata kikundi hicho kuna watu wako Kilimanjaro Moshi.


Shahidi: Kwamba kikundi hicho kimepanga kuwadhuru viongozi akiwemo aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, na kufanya maandamano yasiyokuwa na kikomo.


Shahidi: Pia alitueleza kuwa kikundi hicho kinaratibiwa na mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo, Freeman Mbowe.


Shahidi: Afande Kingai alitwambia kuwa kikundi hicho kimepanga kuchoma vituo vya mafuta na kukata miti magogo kupanga barabarani, ili kuleta tahauruki kwa Wananchi, nchi ionekane haitawaliki


Shahidi: Afande Kingai alitwambia kwamba kwa taarifa alizonazo kuna wengine tayari wako Moshi kwa hiyo tunatakiwa twende Moshi ili kuzuia uhalifu huo usifanyike.


Shahidi: Afande Kingai alitwambia tunatakiwa tuwakamate.


Shahidi: Baada ya maelekezo hayo tuliondoka kuelekwa Moshi.


Shahidi: Safari ya kuelekea Moshi ilihusisha Afande RCO Kingai, Afande Jumanne, Afande Mahita, Koplo Francis pamoja na DC Azoz, here wa Afande RCO.


Shahidi: Baada ya kufika Moshi, tulienda maeneo ya Central Police Moshi.


Shahidi: Afande Kingai alishuka kwenye gari akawa anafanya mawasiliano, baada ya hapo tulienda kuzunguka mjini ili kuwakamata wahalifu hao.


Shahidi: Kazi yetu kwa siku hiyo ilikuwa ni kuwatafuta wahalifu lakini hatukufanikiwa kuwakamata. Tulifanya hivyo hadi majira ya saa tano usiku.


Shahidi: Ilipofika majira ya saa tano kuelekea saa sita, Afande Kingai alisema kwa kuwa hatukufanikiwa kuwakamata kwa taarifa alizokuwa anazipokea yeye alisema tukapumzike.


Shahidi: Tarehe 5 asubuhi Afande Kingai alikuwa anaendelea kupokea taarifa kutoka kwa mtu aliyekuwa anampa taarifa na mpaka majira ya saa sita kuelekea saa saba ndipo Afande Kingai alisema amepata taarifa mahali walipo. Alionyesha mwonekano wao kisha akatuambia tuondoke twende eneo la Rau Madukani.


Shahidi: Kulikuwa na watuhumiwa watatu.


Shahidi: Baada ya Afande Kingai kutueleza hivyo tuliondoka kuelekea maeneo ya Rau Madukani kwa ajili ya kuwakamata wahalifu.


Shahidi: Baada ya kufika Rau Madukani, tulipaki gari na Afande Kingai akampa maelekezo Afande Mahita ashuke kwenye gari aende kuangalia mahali walipokuwa.


Shahidi: Afande Mahita alishuka kwenye gari akaenda kuangalia.


Shahidi: Haikuchukua muda mrefu Afande Mahita alirudi akatwambia kwamba nimewaona wote watatu wamekaa kwenye grocery.


Shahidi: Baada ya taarifa hiyo ya Afande Mahita, Afande Kingai akatoa maelekezo ili twende kuwakamata watuhumiwa. Afande Kingai aligawa timu mbili, moja iliongozwa na Afande Kingai. Afande Jumanne na mimi na nyingine ilikuwa inaongozwa na Afande Mahita, Mimi na Koplo Francis na dereva alibaki kwenye gari.


Shahidi: Timu moja ambayo nilikuwepo mimi ikiongozwa na afande Kingai ilipita kulia na timu ya Afande Mahita ilipita kushoto.


Shahidi: Baada ya Afande Kingai kuwa na timu mbili tulielekea eneo la tukio kwenywe grocery.


Shahidi: Kabla ya sisi kufika kwenye grocery nilisikia sauti ya Afande Mahita akiwaweka watu chini ya ulinzi.


Shahidi: Baada ya kusikia sauti tuliongeza mwendo kuelekea eneo la tukio, tulimkuta Afande  Mahita na Koplo Francis amewaweka watu wawili chini ya ulinzi.


Shahidi: Baada ya kufika mahali walipokuwa watuhumiwa Afande Kingai alijitambulisha kwa watuhumiwa. Baada ya kujitambuliaha aliwauliza watuhumiwa majina yao.


Shahidi: Mtuhumiwa wa kwanza alijitambulisha kwa kina la Adamu Kasekwa na mtuhumiwa mwingine akijitambulisha kwa jina la Mohamed Ling'wenya.


Shahidi: Baada ya utambulisho huo, Afande Kingai alimpa maelekezo Afande Jumanne kuwapekuwa watuhumiwa.


Shahidi: Wakati huo mimi na Koplo Francis tulikuwa tumeimarisha ulinzi.


Shahidi: Afande Jumanne aliwaita mashahidi wawili waliokuwepo karibu, mmoja alikuwa anauza grocery na mwingine alikuwa kwenye bar, mmoja anaitwa Ester na mwingine anaitwa Anitha.


Shahidi: Baada ya mashahidi kufika Afande Jumanne alianza kumpekua mtuhumiwa wa kwanza.


Shahidi: Mtuhumiwa wa kwanza aliyeanza kupekuliwa ni Adamu Kasekwa.


Shahidi: Baada ya kugeuka alianza kumpapasa kuanzia juu alipofika kiunoni alitoa bastola, upande wa kushoto.


Shahidi: Baada ya kutoa bastola aliinyoosha juu kwa mashahidi, akasoma namba zilizokuwa kwenywe bastola A5340. Alisoma jina la ile silaha. Alisema ni Luger.


Shahidi: Baada ya hapo alitoa magazine akahesabu risasi zilizokuwemo.


Shahidi: Risasi alizozitoa kwenye magazine aliIhesabu zilikuwa ni tatu.


Shahidi: Baada ya hapo aliendelea kumpekua mtuhumiwa akatoa kikaratasi ambacho kilikuwa nadawa zinazodhaniwa za kulevya kwenye mfuko wa suruali.


Shahidi: Ile bastola alinikabidhi na zile kete pia alinikabidhi


Shahidi: Afande Jumanne aliendelea kumpekua mtuhumiwa wa pili ambapo alimkuta mfuko na simu aina ya Itel. Alitoa betri akasoma namba za simu. Baada ya kumpekua akiamuru mtuhumiwa akae chini na akinikabidhi ile simu.


Shahidi: Baada ya hapo Afande Jumanne aliniambia nichukue bahasha kwenye gari. Kwa sababu gari ilikuwa imesogea eneo la tukio nilichukua bahasha nikamkabidhi akatoa document kwa ajili ya kujaza.


Shahidi: Baada ya kumkabidhi Afande Jumanne ile bahasha akitoa karatasi akaanza kujaza vile vielelezo kwenye hati ya kukamatia mali.


Shahidi: Nakumbuka alijaza hati mbili. Hati ya kwanza alijaza silaha na zile simu, hati nyingine alijaza madawa yadhaniwayo kuwa ya kulevya.


Shahidi: Baada ya kumaliza kujaza vielelezo, alisaini afande Jumanne, wakasaini mashahidi pamoja na watuhumiwa


Shahidi: Baada ya hapo alimuamuru mtuhumiwa akae chini na alimuamuru mtuhumiwa wa Pili asimame, ni Mohamed Ling'wenya.


Shahidi: Baada ya kumuamuru mtuhumiwa wa pili asimame akamuamuru ageuke na baada ya kugeuka alimpekua kwa kumpapasa kuanzia kichwani, alipofika mfukoni alitoa kete zinazodhaniwa kuwa dawa za kulevya.  


Shahidi: Hizo kete zilikuwa kwenye kimfuko kama paketi za karanga, akizihesabu mbele ya mashahidi na vilikuwa 25.


Shahidi: Baada ya hapo alinipa nizishike. Aliendelea kumpekua mtuhumiwa ambapo alimkuta na simu moja aina ya  Tecno, ilikuwa kwenye mfuko wa suruali.


Shahidi: Alitoa betri akasoma IMEI number na akasoma namba za ile line na akajaza hati ya kukamatia mali vielelezo hivyo. Afande Jumanne alisaini, mashahidi walisaini pamoja na mtuhumiwa mwenyewe alisaini.


Shahidi: Baada ya Afande Jumanne kujaza hati zote za ukamataji mali vile vielelezo nilipewa Mimi. Afande Kingai alielekeza tuelekee kwenye gari baada ya kufika Afande Jumanne aliandaa hati ya makabidhiano ya vielelezo ambayo alikuwa ameiandaa yeye akanikabidhi Mimi pamoja na silaha na simu.


Shahidi: Hati niliyokabidhiana silaha na Jumanne nitaitambua kwa sababu ina jina langu, H4347 Detective Goodluck jina la aliyenikabidhi, Afande Jumanne na vielelezo nilivyokabidhiwa


Shahidi: Wakili anamuonesha nyaraka na anamuuliza Ni nyarakangani na shahidi anajibu.


Shahidi: Ni hati ya makabidhiano mali. Nimeitambua kwa saini yangu, majina yangu, tarehe ya makabidhiano 5/8/200/2020 na vielelezo nivyokabidhiwa.


Shahidi: Kwa mujibu wa hati anayekabidhi ni Afande Jumanne, anayekabidhiwa ni nini H4347 Detective Goodluck.


Shahidi: Kinachokabidhiwa ni bastola aina ya Luger.


Shahidi: Makabidhiano yalifanyika tarehe 5/8/2020.


Shahidi: Baada ya kuitambua hati hiyo wakili Hilla anairejesha kwa karani hati hiyo na anaendelea kumuongoza shahidi.


Shahidi: Baada ya makabidhiano hayo tuliondoka kuelekea kituo cha Polisi Moshi, tukiwa na Afande Kingai, Afande Jumanne, Afande Mahita, Mimi na watuhumiwa Adamu Kasekwa na Mohamed Ling'wenya.


Shahidi: Tulikuwa kwenye gari la Afande Kingai


Shahidi: Koplo Francis alikuwa kwenye gari lingine la RPC Arusha pamoja na mashahidi huru.


Shahidi: Tukiwa tunaelekea kituoni, Afande Kingai aliuliza taarifa tulizo nazo mko watatu mwingine yuko wapi? Watuhumiwa wenyewe wakasema kuwa kweli lakini hawajui mwenzao ameenda wapi  


Shahidi: Kituoni Afande Jumanne walishuka lakini Mimi na Afande Kingai hatukushuka pamoja na watuhumiwa sababu Afande Kingai alisema kuwa tunatakiwa kwenda kumtafuta mtuhumiwa mwingine.


Shahidi: Waliporejea akina Afande Jumanne tuliondoka kwenda kumtafuta mtuhumiwa kwa sababu watuhumiwa walisema atakuwa maeneo ya karibu.


Shahidi: Baada ya kufika eneo la tukio hatukufanikiwa kumkamata lakini watuhumiwa wenyewe walionesha nia ya kusaidia kumpata.


Shahidi: Baada ya kutueleza hivyo, tulichukua hatua ya kuzunguka katika maeneo ambayo watuhumiwa walituongoza.


Shahidi: Walimtaja kwa jina la Lujenge.


Shahidi: Ufuatiliaji wa siku hiyo hatukufanikiwa kumkamata mpaka majira ya saa tano.


Shahidi: Baada ya kutokumkamata mtuhumiwa Afande Kingai alisema kuwa ni wa kuwarudisha watuhumiwa kituoni wakawekwe lockup


Shahidi: Baada ya watuhumiwa kuwekwa lockup tulirudi na kuendelea na ufuatiliaji.


Shahidi: Afande Kingai ndio alikuwa anafanya mawasiliano.


Shahidi: Tarehe 6 /8/2020 majira ya asubuhi saa 11 tukifika kituoni tukawachukua watuhumiwa kwa madhumuni ya ufuatiliaji mtuhumiwa.


Shahidi: Tulienda maeneo mbalimbali Moshi, kama Machame mpaka Aisho Hoteli


Shahidi: Mbali na maeneo hayo pia tulienda Sakina, hatukufanikiwa tukarudi Moshi Police. Afande Kingai akapata maelekezo kwamba watuhumiwa wanatakiwa wapelekwa Dar es Salaam.


Shahidi: Baada kutoka Central Moshi tulipofika njiapanda ya Himo gari ikapata hitilafu, Afande Kingai alifanya mawasiliano ya kupata gari nyingine.  


Shahidi: Baada ya hapo wakati tunasubiria kupata gari nyingine kutoka Moshi Afande Kingai alikuja na chakula, alikuwa amebeba ndizi na nyama tukala


Shahidi: Gari ilitoka Moshi. Baada ya gari ya RPC Moshi kufika tuliwahamisha watuhumiwa tukaendelea na  safari.


Shahidi: Tulifika Dar es Salaam tarehe 7/8/2020 saa 11 alfajiri. Watuhumiwa walikabidhiwa charge room.


Shahidi: Baada ya kukabidhi watuhumiwa Afande Kingai alielekeza tuondoke ili tukanawe uso baada ya hapo turudi saa moja.


Shahidi: Baada ya kurudi kituoni Afande Kingai alinielekeza nikabidhi vielelezo.


Shahidi: Maelekezo hayo niliyatekeleza nilikwenda kwa mtunza vielelezo, nikakabidhi silahà namba A5340.


Shahidi: Nilimkabidhi St/Sgt Nuru.


Shahidi: Muda wote huo silaha nilikuwa nayo kwenye begi.


Shahidi: Vingine nilivyokabidhi ni simu, simu nilimkabidhi Afande Swila, ni Askari wa hapa Dar es Salaam. Nilimkabidhi simu tulizokamata kwa watuhumiwa kule Moshi aina ya Tecno na Itel pamoja na line.


Shahidi: Baada ya kukabidhi vielelezo Afande Kingai akielekeza kuwa tuendelee na ufuatiliaji ni wa taarifa ambazo alizokuwa anazipata na kwamba tuungane na Afande Swila.


Shahidi: Makabidhiano ya vielelezo tulikabidhiana kwa kusaini hati ya makabidhiano. Ilikuwa ni tarehe 7/8/2020.


Shahidi: Hiyo hati ya makabidhiano ya silaha, risasi naweza kuitambua kwa majina yangu, tarehe ya makabidhiano, vielelezo ambavyo tulitoka navyo Moshi pia na jina la mkabidhiwa.


Shahidi: Wakili Hilla anamuonesha shahidi hati ya makabidhiano ya vielelezo na shahidia anasema anaitambua kuwa ndio hati ya makabidhiano aliyoijaza wakati akimkabidhi Sajent Nuru vielelezo.


Shahidi: Naiomba mahakama ipokee kama ushahidi.


Mawaili wa utetezi wanaikagua.




Mawakili wote Nashon Nkungu ( kwa mshtakiwa wa kwanza), John Mallya (kwa mshtakiwa wa Pili), Fredrick Kihwelu ( kwa mshtaiwa wa tatu) na Kibatala kwa mshtakiwa wa nne wanaeleza kuwa hawana pingamizi.


Mahakama imeipokea hati hiyo ya makabidhiano mali baina ya shahidi na Sajenti Nuru kuwa kielelezo cha 36 cha ushahidi wa upande wa mashtaka.


Kisha shahidi anasoma maelezo yaliyomo kwenye Katika hati hiyo ya makabidhiano ya mali


Shahidi: Tarehe 8/8/2020 tulikuwa tunaendela na ufuatiliajibwa watuhumiwa wengine walioko Dar Afande Kingai akituelekeza mimi na Afslande Mahita kuwahamisha watuhumiwa kutoka Police Central kwenda kituo cha Polisi Mbweni, ilikuwa muda wa saa 5 asubuhi. Watuhumiwa tuliowahamisha kutoka Central kwenda Polisi Mbweni ni wstujumiwa tuliotoka nao Moshi ambao ni Adamu Kasekwa na Mohamed Ling'wenya.


Shahidi: Tuliohusika kuwahamisha Ni Afande Jumanne, Afsnde Mahita, Arande Swila pamoja na mimi na dereva.


Shahidi: Baada ya kufika Polisi Mbweni tulishuka na watuhumiwa, chargeroom (chumba cha mashtaka) wakiingia na Afande Jumanne na Afande Mahita kuwakabidhi watuhumiwa.


Shahidi: Baada ya watuhumiwa kukabidhiwa tuliondoka kufuatilia taarifa mbalimbali kuhusiana na watuhumiwa wengine.


Shahidi: 9/8/2020, tulikuwa tunafuatilia taarifa zilizokuwa zinatolewa, tukiwa maeneo mbalimbali ya Dar es Salaam..


Shahidi: Siku hiyo maeneo ya jioni nilikuwa maeneo ya Temeke.


Shahidi: Siku hiyo ya terehe 9 nilifanikiwa kumkamata mtuhumiwa mwingine aitwaye Halfan Bwire. Bwire alimamatiwa maeneo ya Polisi Chang'ombe.


Shahidi: Mazingira ya ukamataji wa Bwire, alikuwa kwenye gari ya abiria daladala, kwa hiyo ilielekezwa kuingia kituo cha Polisi Chang'ombe.


Shahidi: Baada ya gari kuingia kituoni, Mimi na Afande Mahita tulielekezwa kuongia kwenye gari ndipo tukamkamata.


Shahidi: Kwenye upekuzi wa mtuhumiwa tulimkuta na simu mbili, mfukoni katika suruali ya mtuhumiwa.


Shahidi: Baada ya upekuzi mtuhumiwa aliingizwa lockup kituo cha Polisi Chang'ombe.


Shahidi: Sisi Tuliendelea na ufuatiliaji wa taarifa nyingine ambazo tulikuwa nazo.


Wakili Hilla: Mheshimiwa Jaji tunaomba ahirisho kwa ajili health break.


Kibatala: Mheshimiwa, hatujui amebakiza maelezo marefu kiasi gani kama si ndefu tungeomba angemaliza.


Hilla: Mheshimiwa Jaji bado tuna mambo mengi hatuwezi kukadiria muda.


Jaji: Tuna-break mpaka saa 7:45.

Thursday, January 20, 2022

WAFUNGWA 10 DRC WAHUKUMIWA KWA UBAKAJI GEREZANI.


 
Wafungwa kumiwamepatikana na hatia ya kuwabaka makumi ya wafungwa wa kikewakati wa ghasia katika jela moja iliojaa wafungwa kupitia kiasi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC.


Wanawake 37 na msichana mmoja walitoa ushahidi kwamba walibakwa mara kadhaa wakati wa ghasia za siku tatu katika jela ya Kasapa Central Prison karibu na mji wa Lubumbashi 2020.


Baadhi ya wafungwa wa kike walipata uja uzitona kuambukizwa maradhi ikiwemo HIV


Wanaume hao 10 walipigwa faini na kuagizwa kuhudumia miaka mingine 15 jela kila mmoja wao.


Ijapokuwa baadhi ya wafungwa waliogopa kutoa ushahidi , makumi walitoa ushahidi mbele ya kiongozi wa mashtaka wa jeshi kwamba walibakwa wakat iwa ghasia hizo.


Melania Mumbo ambaye ni wakili wa waathiriwa, aliambia AFP News ‘’Tumeridhika na uamuzi baada ya kupigania haki kwa muda mrefu.


Gereza hilo lilitekwa na wafungwa wa kiume kwa siku kadhaa mwezi Septemba 2020. Walichoma eneo la wafungwa wa kike- ikiwemo msichana wa miaka 16- na hivyobasi kuwalazimisha wanawake hao kulała katika eneo jingine la jela hiyo ambapo walibakwa.


Takriban wafungwa 20 na askari jela waliripotiwa kuuawa wakat wa ghasia hizokabla maafisa wa usalama kuchukua udhibiti.


Ubakaji huo uliangaziwa na shirika la haki za kibinadamu la Human Rights Watch , ambao waliarifu watawala kuchunguza unyanyasaji huona kuwahudumia walioathiriwa.


Shirika hilo linasema kwamba jela hiyo iliojengwa kumiliki wafungwa 800 , ilikuwa na karibia wafungwa 2000 wakati wa ghasia hizo.

MHUDUMU WA GESTI AUAWA KWA KUKABWA SHINGO KWA KAMBA YA VIATU CHUMBANI KWA MTEJA



CHANZO: MALUNDE BLOG
MUHUDUMU wa nyumba ya kulala wageni ya Peace Lodge iliyoko katika eneo la Matarawe Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma ambaye jina lake limehifadhiwa anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 23 amekutwa amekufa kwenye moja ya vyumba vya kulala wageni.

Akizungumza na Nipashe jana Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma, Louis Taisamo, alisema tukio hilo limetokea juzi jioni ambako inadaiwa kuwa kwenye nyumba hiyo chumba namba nne mhudumu huyo, mkazi wa Kimoro-Makambi Manispaa ya Songea alikutwa akiwa ameuawa kwa kukabwa shingoni na kamba ya viatu na mtu asiyefahamika kwa jina, ambaye alikuwa ni mpangaji katika chumba hicho.


Alisema inadaiwa kuwa mtuhumiwa huyo alipanga chumba namba nne kwa siku tano kuanzia Januari 6, mwaka huu hadi Januari 10 mwaka huu na baada ya hapo alitoweka na hakuwa analala katika chumba hicho.


Kamanda Taisamo alifafanua kuwa inadaiwa mtuhumiwa huyo alitoweka kwenye nyumba hiyo ya kulala wageni baada ya kuwa na deni la pango Sh. 50,000 ambapo alilazimika kuacha simu yake aina ya Nokia na baadhi ya nguo zake mpaka hapo atakapolipa deni.

Alieleza zaidi kuwa inadaiwa mtuhumiwa huyo alikuwa akifika katika nyumba hiyo ya wageni mara kwa mara kuomba arudishiwe simu na nguo zake na alikuwa akijibiwa na mhudumu (marehemu) kuwa mali zake zipo kwa mmiliki wa nyumba hiyo na kwamba atarudishiwa mali zake baada ya kulipa deni.


Alisema inadaiwa siku ya tukio mtuhumiwa ambaye jina lake halijafahamika, alifika tena kwenye nyumba hiyo na kuwasiliana na mhudumu ambapo baada ya kutekeleza mauaji alitoroka na kufanikiwa kuondoka na vitu vyake ambavyo vilikuwa vimezuiliwa.

 Taisamo alisema mtuhumiwa hajakamatwa, na kwamba Jeshi la Polisi mkoani humo linafanya juhudi za kumtafuta.

Wednesday, January 19, 2022

SHAHIDI AELEZA MAWASILIANO YA MBOWE KATIKA KESI YA UGAIDI.

 


Mtaalamu wa uchunguzi wa uhalifu wa kimtandao wa jeshi la polisi, Innocent Ndowo ameeleza mawasiliano kati ya Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na Luten Denis Urio yalivyokuwa.


Shahidi huyo wa 10 wa upande wa mashtaka katika kesi ya ugaidi inayomkabili  Mbowe na wenzake watatu amedai amebaini ujumbe mfupi uliotoka kwa Urio kwenda kwa Mbowe akitaka atume Sh500,000 kwa ajili ya kuwasafirisha mshtakiwa wa kwanza na wa pili.


Soma ushahidi hapa

Sasa Jaji Tiganga ameingia mahakamani na kesi inatajwa na karani.


Waendesha mashtaka wanajitambulisha wakiongozwa na kiongozi wao Wakili wa Serikali Mwandamizi, Robert Kidando


Jopo la mawakili wa utetezi likiongozwa na Peter Kibatala linajitambulisha.


Jaji anawaita washtakiwa kwa namba zao kuanzia wa kwanza hadi wa nne kujiridhisha Kama wote wako mahakamani nao wanaitika mmoja mmoja.


Wakili wa Serikali Kidando: Mheshiwa Jaji kesi imekuja kwa ajili ya kuendelea kusikilizwa na shahidi tuliyekuwa naye jana amefika na ametutaarifu kuwa hali yake imeimarika na anaweza kuendelea. Tuko tayari kuendelea


Jaji:Utetezi


Kibatala: Mheshimiwa Jaji nasi pia tuko tayari kuendelea


Jaji:Shahidi nakukumbusha uko chini ya kiapo tangu jana.


Wakili wa Serikali  Mwandamizi Pius  Hilla anaendelea kumwongoza shahidi kutoa ushahidi wake kuanzia alipoishia Jana.


Jaji: Anarejea mahali ilipoishia jana kisha wakili anaendelea kumwongoza shahidi naye anaeleza


Shahidi: Ripoti yangu kwenda kwa wapelelezi iliambatana na covering letter kutoka Police Forensic Bureau. Covering letter inaandaliwa na mchunguzi Kisha inakwenda kwa kamishna Msaidizi wake anasaini kwa niaba.


Madhumuni ya covering letter ni kutambulisha kazi iliyofanywa na mchunguzi.


Shahidi: Extracted information zilitokana na vile vilelezo vilivyoletwa maabara yaani simu nane lakini simu nne ndizo zilikuwa na matokeo positive ambazo ya kwanza niliipa alama ya herufi E, kwenye stika ya kijani ambayo ni aina ya Tecno.


Shahidi: Nyingine niliipa alama F kwa mkono wangu ambayo ni aina ya Itel.


Shahidi: Simu ya tatu niliipa alama G, aina ya Tecno


Shahidi: Simu ya nne niliipa alama H, Tecno.


Shahidi: Alama hizi nilikuwa naziweka nyuma ya simu na zile ambazo zilikuwa na cover nilikuwa naweka kwenywe cover na nyuma ya simu.


Shahidi: Nilikuwa naweka alama kwenye simu kwa ajili ya utambuzi wangu wakati nafanya Uchunguzi.


Shahidi: Barua hiyo ya co erring letter nitazitambua kwa nembo ya ofisi, saini ya SACP Naftali Joseph Mwamtamba, mhuri wa Kamishina,


Shahidi: Ripoti yangu nikioona nitaitambua kwa logo ya taasisi yetu, Jeshi la Polisi, majina yangu, saini yangu, mhuri wa Jeshi la Polisi


Shahidi: Simu niiyoipa alama E niliona nitaitambu kutokana na IME za kiuchunguzi lakini ni naomba mahakama inielewe namba za IMEI ni 14 hadi 15 15 kwahiyo nichofanya ni kushika baadhi ya namba za mwanzo na mwisho 35 na namba za mwisho 45


Shahidi: Kigezo cha pili cha kutambua ni taarifa zilizoko kwenye report kwanza itakuwa na mhuri wa Polisi, sahihi yangu laboratory namba.


Shahidi: Kigezo kingine kitakuwa kuna majina yangu pia kwa maana ya mchunguzi.


Shahidi: Kigezo kingine ambapo ripoti zinatokana na cerebrate (mashine ya Uchunguzi) pia Kuna kuwa na neno cerebrate


Shahidi: Extracted report ya simu H nitaitambua kwa IMEI yake namba za mwanzo ni 35, saini yangu, mhuri wa Police Forensic Bureau Dar es Salaam, Lab number FB/Cyber/ 2020/476,  majina yangu na neno Cerebrate.


Shahidi: Taarifa kwenye ripoti hizo ni kama vile zilivyokwenye vifaa husika kwa sababu wakati wa extracted na analysis mifumo hii ina teknolojia ambayo hairuhusu kufanya manipulation yoyote, hivyo tekonolojia hiyo inasaidia standard na hivyo ushahidi huo unakuwa uko intact.


Wakili Hilla: Mheshimiwa Jaji kwa kuwa shahidi amesema anao uwezo wa kutambua nyaraka hizo kumuonesha ili aweze kuzitambua


Wakili Hilla: Shahidi naomba utazame nyaraka hizi.


Shahidi anapekuapekua baadhi ya nyaraka alizopewa.


Wakili Hilla: Ieleze mahakama nyaraka hizo ni kitu gani?


Shahidi: Nyaraka hizi Mheshimiwa ni nyaraka ambazo nimeziandaa mwenyewe na nazitambua kuwa ni ripoti ya uchunguzi nilioufanya.


Wakili: Katika ripoti hiyo Kuna nyaraka zipi?


Shahidi: Kuna covering letter, Kuna taarifa niliyoiandaa.


Wakili: Jana shahidi ulieleze annexures kwenye ripoti yako ni zipi hizo?


Shahidi: Taarifa kutoka Airtel na Tigo.


Wakili: Jana uliongelea annexures hizo ziko wapi?


Shahidi: Zilitolewa hapa mahakama


Wakili: Hebu ieleze Mahakama covering letter umeitambua vipi?


Shahidi: Kuna mhuri wa Kamisha wa Uchunguzi, jina la jalada


Wakili: Taarifa yako ina vigezo gani?


Shahidi: Kuna Lab number F? Cyber/2020/.. 479 pamoja na case no., Majina yangu, saini yangu na mhuri wa Police Forensic Bureau


Wakili Hilla: Itazame extracted report ya simu ya alama E, na ieleze mahakama umeitambua?


Shahidi: Ni hii hapa na IMEI kama nilivyozitaja, mhuri wa Police Bureau Dar, saini yangu majina yangu na Lab no.,  fB/Chber/202/Lab/479 pamoja na neno cerebrate


Wakili Hilla: Sasa twende extracted report ya simu namba H unaitambuaje?


Shahidi: IMEI ni, mhuri wa Police Bureau Dar, majina yangu, saini, Lab number na neno cerebrate.


Wakili Hilla: Sasa twende extracted report ya simu namba E unaitabuaje?


Shahidi: kwa IMEI number yake, mhuri wa Tanzania Police Forensic Bureau, majina yangu na Lab number


Wakili Kibatala anasimama na kusema Mheshimiwa nimeshamnong'oneza Wakili Hilla lakini naona bado mambo ni yale yale tu, shahidi anasoma content


Wakili Kidando: Shahidi yuko katka utambuzi na taarifa hizi alishazitaja.


Kibatala: Ndio anasoma na Lab number?


Kidando: Mheshimiwa hizo tayari shahidi alishazitaja.


Jaji nakumbuka wakati akieleze kuwa anazitambuaje nyaraka hizo alisema kwa IMWI numbe na Lab number.


Wakili Hilla: Kwa maana ya utambulisho wa ripoti alizoziandaa anataja alama au vigezo vilivyopo Kama alivyovitaja, kwa hivyo kwa kutaja IMEI number ya kwanza na ya mwisho sidhani kama ana- violate admissibility ya exhibits


Jaji: Napata changamoto kwa sababu anachokisema shahidi ni reference ya kile alichokuwa amekitaja.


Kibatala: Kwa ruhusa yako acha tuendelee maana si kitu kikubwa saana.


Jaji: Na naona alikuwa anaelekea kwenywe kielelezo cha mwisho.


Kibatala: Sawa Mheshimiwa, acha tuendelee.


Jaji anakumbusha shahidi alikokuwa amefikia kisha Wakili Hilla anaendelea kumuongoza shahidi.


Wakili Hilla: Shahidi, Sasa unaiomba nini mahakama, kuhusu nyaraka hizo?


Jaji Tiganga: Hebu ngoja kwanza, ziko ngapi hizo nyaraka? Maana kuna nyaraka ya mwisho ya extracted report H ndio alikuwa anaimalizia.


Kwa mwongozo huo wakili Hilla anamuongoza shahidi kutaja vigezo vya kuitambua ripoti hiyo naye shahidi anavitaja kama alivyokuwa ameshavitaja awali


Wakili Hilla: Shahidi sasa baada ya utambuzi huu sasa unaiomba mahakama ifanye nini


Shahidi: Mheshimiwa naomba nyaraka hizi zipokewe kama ushahidi wangu.


Wakili: Hilla, Mheshimiwa Jaji Shahidi anaomba nyaraka hizi ambazo ameshazitambua zipokewe.


Mawakili wa utetezi wanazipitia nyaraka hizo, ili watoe maoni au msimamo wao kabla ya mahakama kuzipokea.


Wakili Nashoni Nkungu: Mheshimiwa Jaji kwa niaba ya mshtakiwa wa kwanza (Halfan Bwire Hassan) sina pingamizi


John Mallya kwa niaba ya mshtakiwa wa pili (Adamu Hassan Kasekwa) hatuna pingamizi


Wakili Fredrick Kihwelo: Mheshimiwa kwa niaba ya mshtakiwa wa tatu( Mohamed Ling'wenya) hatuna pingamizi


Peter Kibatala: Kwa niaba ya mshtakiwa wa nne (Freeman Mbowe) Mheshimiwa Jaji hatuna pingamizi


Jaji Tiganga: kielelezo chenye covering letter ya Police Forensic Bureau


Repoti ya uchunguzi, Extracted report ya simu nne vyote vipokelewa kuwa 22 mpaka 27.


Baada ya vielelezo hivyo kupokewa sasa shahidi anaanza kusoma yaliyomo ndani ya ripoti hizo.


Taarifa ya Uchunguzi:


Shahidi: 13/8/2020 Maabara ya uchunguzi wa Kisayansi ikipokea barua na vielelezo simu nane pamoja na simu card zake kwa ajili ya uchunguzi kubaini Mawasiliano kupitia mitandao ya kijamii Kama vule Whatsapp, Telegram, unumbe mfupi na kupiga nakupigiwa katika namba za simu zilizotangulia, usajili wa namba hizo na Mawasiliano mengine


Kisha shahidi anasoma matokeo ya uchunguzi wake.


Shahidi: Katika uchunguzi huo shahidi anabainisha jinsi namba za simu hizo ambazo amebainisha usajili wake kuwa ni za baadhi ya washtakiwa, hususan Mbowe pamoja na shahidi mtarajiwa wa Jamhuri, Luten Denis Urio, wakijadiliana kuhusu kuwapata vijana ambao wengine  wametajwa miongoni mwa washtakiwa.


Shahidi: Ripoti ya uchunguzi huo inabainisha muda wa mawasiliano hayo kupitia mitandao ya kijamii, zote ujumbe mfupi wa maneno, kupiga na kupokea simu na miamala ya fedha huku mmoja akimtahadharisha mwingine kuwa asiwe anatumia namba yake binafsi kwa masuala ya pesa


Wakati Shahidi anaendelea kusoma taarifa hizo, Jaji anahoji kama kuna kusoma taarifa zote hizo na hasa viambatanisho. Anashauri isomwe ripoti ya uchunguzi na wakili Hilla anamuongoza kwenye maneo muhimu ya uchunguzi.


Shahidi anabainisha mawasiliano Kati ya Mbowe na Denis Urio kuanzia Januari 2020 jinsi walivyotafutana kwa njia ya ujumbe wa mitandao na ujumbe na call kupitia telegram na ujumbe wa maneno


Shahidi: 20/7/2020 saa 1:59 asubuhi kupitia telegram Mbowe anasema kaka wale mtu tatu au nne ni muhimu sana siku zimekwisha.


Shahidi: Baadaye alipiga simu kwa telegram


Shahidi: Saa 1:45 asubuhi Denis alimpigia Mbowe


Shahidi: Saa 1:47'46 Mbowe alimpigia Denis


Shahidi: 20/7/2020 saa 2;20 Denis amtumia Mbowe ujumbe, bro kuna memba wawili mmoja yuko Tunduma anashughulika na mabasi ya safari za nje na mwingine yuko Dodoma


Shahidi:Mboye baadaye simu siyo salama


Shahidi: Baadaye Mbowe atuma ujumbe hao wawili kuanzia siyombaya na hawawezi kutelekezwa wameshakwanbia mahitaki yao


Shahidi: Denis anamtumia Mbowe ujumbe mmoja kazaliwa 1980


Shahidi: Baadaye Denis ujumbe kwa Mbowe nitumie nauli ya kwenda nao Moro


Shahidi: Mbowe anajibu hakuna tatizo, kiasi gani


Shahidi: Denis anajibu laki 5


Shahidi: Saa 2:21:48, Mbowe anajibu sawa kaka


Shahidi: 2:22:29 Denis kwa Mbowe Nashukuru nitakujibu jioni


Shahidi: Denis usiwe unatumia namba yako binafsi kutuma pesa tumia wakala au mtu mwingine


Shahidi: Mbowe Ok


Shahidi: 27/7/2020. Denis yule jamaa anayefanya kazi Yard ameshafika


Shahidi: Yule mtu wa Tunduma anakaribia Moro


Shahidi: Denis Ila Kuna maswali wanauliza kuhusu malazi na mishahara yao.


Shahidi: Baadaye Denis ampigia Mbowe


Shahidi: 22/7/2020 : 6:26  Denis ampigia Mbowe


Shahidi: 2/7/2020 saa 6: Denis Shikamoo mkuu wale vijana tayari niko nao nimekutana nao na wako tayari kwa kazi


Shahidi: Denis naomba unipe utaratibu wao


Shahidi: Mbowe 7:38 Denis amtumia Mbowe kuwa wamekuja Dar anaomba nauli na mahali pa kukutana


Shahidi: 22/7/2020 saa7:51 Denis kwa nauli na chakula kwa wote ni Sh200.000


Shahidi: Mbowe natuma namba gani


Shahidi: Denis 0787555200


Shahidi: Mbowe ni namba ya nani?


Denis: Namba yangu


Shahidi: Denis uliyotumia juzi


Shahidi: Denis Lakini wewe usitumie namba yako


Shahidi: Mbowe: Ok


Shahidi: Mbowe wakiwa around Mlandizi watume sms wanafika muda gani nitatuma gari kuwapokea Ubungo


Shahidi: Denis: niwape namba gani muweze kuwasiliana?


Shahidi: Siku hiyo 3 Mbowe namba ninayotumia unumbe ni ya dereva wangu wamtafute yeye


Shahidi: Denis sawa, nitumie hiyo namba baadaye Denis


Shahidi: Tayari nimeipata


Shahidi: Denis: Nashukuru nimeelewa nitawapa hiyo namba.


Shahidi: Saa 12:20 jioni Denis: Tayari wameshaondoka wanakaribia Ruvu


Shahidi: Denis wale vijana wengine nimewapata Mwanza, Mtwara na Dodoma


Shahidi: Denis: Naomba kushauri uwe unanitumia fedha za kutosha kwa ajili ya ku-mobilize


Shahidi: Mbowe: kaka bado niko kamati kuu tuma ujumbe please.


Shahidi: Denis: Kuna MSG nilizokutumia kuhusu wale vijana wengine ambao wako tayari.


Shahidi: 13/7/2020 Denis: Naomba rejea msg zangu za jana usiku


Shahidi: 23/7/2020 saa 1:03 jioni Urio anapokea ujumbe  wenye jina la Mohamed Abdillahi Ling'wenya


Shahidi: Urio: Mbona hujatuma majina na picha ya Adamoo ( Adamu Hassan Kasekwa, mshtakiwa wa pili?


Shahidi: Baadaye Urio apokea picha nyingine Kisha ujumbe usemao Adamu Hassan Kasekwa


Baada ya shahidi kumaliza kusoma ripoti hizo wakili Hilla anaomba ahirisho.


Jaji Tiganga anaahirisha kesi hiyo hadi saa 7:55 mchana huu ili upande wa mashtaka uendelee kumuongoza shahidi wake kutoa ushahidi wake.


Mahakama imerejea kwaajili Shahdi kuendelea kuhojiwa na wakili wwa serikali Piusi Hilla.


Shahidi: Baada ya kumaliza kufanya uchunguzi vielelezo hivi nilivifunga na kufihifadhi sikuviona tena hadi jana Ijumaa Januari 17.


Shahidi: Ijumaa iliyopita nilipigiwa simu na Inspekta Swilla kutakiwa kuja kutoa ushahidi kuhusiana na uchunguzi niliofanya.


Shahidi: Nilienda kuangalia kwenye register ya maabara ili kufahamu na Jumatatu tuliwasiliana aliniletea vielelezo.


Shahidi: Vielelezo hivyo ni simu nane na kwakuwa nilizifanyia kazi kwa kuangalia stika zilizokuwa kwenye simu zile…..


Shahidi: Hali ya vielelezo hivyo niliona jina langu na juu ya bahasha ilikuwa imeandikwa kwa makapeni.


Shahidi: Nilivihifadhi kwenye begi langu kwaajili ya usalama na kuja navyo mahakamani kwa ajili ya kuvitolea ushahidi.


Shahidi: Lakini jana kutokana na changamoto ya kiafya, nilirudi navyo na kwenda kuvihifadhi ofisini Kitengo cha uchunguzi wa kisayansi katika makao Makuu ya Polisi ya zamani na leo kuvichukua kuja navyo mahakamani.


Shahidi: Vielelezo hivyo vitakuwa na alama A, B, C, D, E, F, G na H ambapo kuna tekno nne Itel na Samsung ambazo zimeandikwa stika ya kijani.


Shahidi: Hivi ni vile vielelezo nilivyovifanyia kazi ni simu, kwenye hicho kimfuko kuna majina yangu, tarehe 9/7, 2020 lakini pia kuna kumbukumbu za maabara zimeandikwa kwa mkono.


 Shahidi: Mheshimiwa taarifa niliyowasiliaha awali ndio nilipoifanyia kazi naomba Mahaka yako izipokee kama kielelezo


Wakili wa utetezi baada ya kupitia vielelezo hivyo hawana pingamizi hivyo mahakama imepokea vielezo hivyo ambavyo ni simu nane kama kielelezo namba 28 hadi 35.


Wakili wa Serikali Piusi Hilla Mheshimiwa Jaji sina tena swali kwa shahidi.


Wakili wa utetezi Nashon Nkungu.


Wakili: Sahihi nisikia una miaka 37


Shahidi: Sahihi


Wakili: Kwani jeshi la Polisi unastaafu ukiwa na miaka mingapi


Shahidi: Sifahamu


Wakili: Ijumaa tarehe 14 tuliambiwa kuna Shahidi ni mstaafu anamuunguza baba yake


Shahidi: Sio sahihi


Wakili: Inawezekana wewee ndio ulityetoa hizi taarifa


Sahahid: Sio sahihi


Wakili: Ni sahihi ni kusema sio hacker anaweza kuingilia taarifa za mtu mwingine?


Shahidi: Sio kweli


Wakili: Hacker hawezi kuingilia na kudukua taarifa kwenye software


Shahidi: Sio sahihi


Wakili: Inawezekana kifaa kinachorun software kuingiliwa?


Shahidi: Haliwezekani


Wakili: Mwambie Jaji ulitumia muda gani kuchunguza vifaa vyako


Shahidi: Siku kadhaa


Wakili: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji ukikaa na hizo data zako kwenye kompyuta kwa muda gani


Shahidi: Sikumwambia


Wakili: Ulimwambia ni watu wangapi wana access na hicho chumba


Shahidi: Nilimwambia


Wakili: Pamoja na access mtu anaweza kuingilia


Shahidi: Ndio


Wakili: Baada ya kupokea majibu Julai,2, 2021 ndio ukaanza kufanyia uchunguzi


Shahidi: Hapana sikusema hivyo


Wakili: Ni sahihi toka tarehe 13,8,2020 ukaviweka na kuifanyia kazi tarehe 1/7/2021


Shahidi: So kweli


Wakili: Kutokana na ushahidi wako hakuna ukichokifanya hapao katikati


Shahaidi: Nilianza kuomba taarifa