ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, September 14, 2023

TRA PWANI YAWAHIMIZA WAFANYABIASHARA KUTUMIA MASHINE ZA EFD

 NA. VICTOR MASANGU,PWANI


Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Pwani katika kupambana na kudhibiti mianya ya ulipaji wa kodi imezindua kampeni maalumu yenye lengo la kutoa elimu kwa wafanyabiashara juu kutumia mashine za kielekroniki (EFD) pindi wanapouza bidhaa zao. Hayo yamebainishwa na Meneja wa TRA Mkoa wa Pwani, Masawa Masatu wakati akizungumza na waandishi kuhusiana na kampeni hiyo ambayo pia itaenda sambamba na kuwahimiza wananchi kuhakikisha wanasai risiti pindi wanapofanya manunuzi kwani ni haki yao. Nao baadhi ya wafanyabiashara wa Mkoani Pwani hawakusita kuzungumzia juu ya umuhimu wa kutumia mashine hizo za EFD huku wameipongeza TRA kwa hatua ya kwenda kuwatembea na kuwapa elimu ya umuhimu wa kulipa kodi kwa maslahi ya maendeleo ya Taifa. Jisena Simon na Ramadhani Kassim Wafanyabiashara Mkoa wa Pwani. Kampeni hiyo maalumu ambayo imepewa jina la Tuwajibike itafanyika kwa kipindi cha wiki moja katika Wilaya mbalu mbali za Mkoa wa Pwani ambapo italenha zaidi kutoa elimu kwa wananchi na wafanyabiashara juu ya kutoa risiti halali pamoja na kudai risiti.

Wednesday, September 13, 2023

Rais Mwinyi aipongeza Benki ya CRDB kwa huduma za kibenki zinazozingatia msingi ya Kiislamu

 


Unguja. Tarehe 10 Septemba 2023: Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mheshimiwa Dkt Hussein Ali Mwinyi ameipongeza Benki ya CRDB kwa kuanzisha huduma za kibenki zinazofuata misingi ya sharia hivyo kuwahamasisha Waislamu wengi kutumia huduma zake jambo linalochochea ujumuishi wa kifedha.

Rais Mwinyi ambaye alikuwa mteja wa kwanza kufungua akaunti ya Al Barakah mwishoni mwa mwaka 2021 huduma hiyo ilipozinduliwa, ametoa pongezi hizo alipokabidhiwa kadi ya akaunti hiyo mwishoni mwa wiki alipotembelewa na ujumbe wa Benki ya CRDB ikulu mjini Zanzibar.
“Tulijua Al Barakah itakuwa na mafanikio lakini hatukutarajia kuwa yangepatikana ndani ya muda mfupi namna hii. Nawapongeza kwa mafanikio mliyoyapata na niwaahidi kwamba Serikali ya Mapinduzi Zanzibar itaendeleza ushirikiano na benki yenu kuhakikisha huduma hizi zinawafikia Waislamu wengi walipo visiwani humu ili kwa Pamoja tushiriki kulijenga Taifa letu huku tukimwabudu Mwenyezi Mungu bila kukiuka maagizo yake,” amesema Dkt Mwinyi.

Rais Mwinyi pia ameishukuru Benki ya CRDB kwa heshima iliyompa ya kuwa mteja wa kwanza kukabidhiwa kadi ya Akaunti ya Al Barakah na akasema jambo hilo limemhamasisha zaidi hivyo ataangalia namna ya kuongeza amana kwenye akaunti yake ili kufurahia huduma hizo zinazokidhi mahitaji yake ya kifedha na imani ya kiroho.
Akimkabidhi kadi ya Al Barakah, Meneja wa Kanda ya Mashariki wa Benki ya CRDB inayojumuisha Zanzibar na mikoa ya Dar es Salaam na Pwani, Badru Idd amesema Rais Mwinyi sio tu alihamasisha kuanzishwa kwa huduma hizo bali alionyesha mfano kwa kuwa wa kwanza kufungua akaunti hiyo mwaka 2021 ambayo mpaka sasa ina wateja zaidi ya 70,000 nchini kote.

“Mpaka sasa hivi, tumekopesha zaidi ya shilingi bilioni 90 kwa misingi ya sharia na tumepokea amana za wateja zaidi ya shilingi 85 bilioni ndani ya miaka miwili ya kutoa huduma hizi. Huduma za CRDB Al Barakah Banking zinaendelea kutoa mchango mkubwa sana katika serikali yako ya Zanzibar na wananchi wake kwani tumekopesha zaidi ya shilingi 18 bilioni kwenye uchumi wa buluu na wafanyabiashara wamepata Zaidi ya shilingi bilioni 33,” amesema Idd.

Ili kusogeza huduma kwa wananchi visiwani humu, Benki ya CRDB ilifungua tawi mjini Wete lililozinduliwa na Rais Mwinyi mwaka 2021 alikoiomba benki kuanzisha huduma zenye misingi ya sharia na mpaka sasa, kwenye matawi manne ya Benki ya CRDB yaliyomo Zanzibar, wananchi wameweka amana za zaidi ya shilingi bilioni 28.
Kuhusu kadi za Akaunti ya Al Barakah, Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Benki Zinazofuata Sharia (Islamic Bankink) wa Benki ya CRDB, Rashid Rashid amesema zipo za aina nne na zote zinaweza kutumika katika majukwaa yote ikiwamo kwa mawakala zaidi ya 200 waliopo Zanzibar kama ilivyo kwa kadi zinazotumiwa na wateja wengine wote wa Benki ya CRDB.

“Pamoja na mafanikio haya makubwa, CRDB Al Barakah Banking tunaendelea kuboresha huduma zetu ili kuwafikia wateja wetu na kuwapa amani wanayoitegemea kwa kuweka pesa zao katika akaunti za Al Barakah zinazofuatisha misingi ya sharia. Kila mteja mwenye akaunti hii, ana amani kwa kujua kwamba pesa zake ziko mahala salama na zina uangalizi maalum unaoendana na imani na maadili yake,” amesema Rashid.
Akizungumzia umuhimu wa huduma za fedha kwa maendeleo ya Taifa, Mwenyekiti wa Bodi ya Huduma za Fedha Zinazofuata Misingi ya Sharia ya Benki ya CRDB, Abdul van Mohammed amesema kuna fursa nyingi ambazo Zanzibar inaweza kunufaika nazo iwapo itafungua milango.

“Zanzibar ndio yenye matumizi makubwa ya Islamic Banking Afrika Mashariki. Naomba Serikali iangalie uwezekano wa kuifanya kuwa ya kwanza kuuza hatifungani ya Kiislam ili kupata fedha zitakazochangia maendeleo ya watu wetu,” amesema Mohammed.




TPA YAUNGA MKONO JUHUDI ZA RAIS DKT SAMIA KWA KUTOA MSAADA WA VIFAA TIBA HOSPITALI YA WILAYA YA KOROGWE

 

MKUU wa wilaya ya Korogwe Jokate Mwegelo kushoto akipokea msaada wa vifaa tiba wenye thamani ya Milioni 10 kutoka kwa Meneja wa Bandari ya Tanga Masoud Mrisha kwa ajili ya Hospitali ya wilaya ya Korogwe ikiwa leo ni siku yao ya kusheherekea kuanzishwa kwa Mamlaka ya Bandari nchini.
MKUU wa wilaya ya Korogwe Jokate Mwegelo kushoto akipokea msaada wa vifaa tiba wenye thamani ya Milioni 10 kutoka kwa Meneja wa Bandari ya Tanga Masoud Mrisha kwa ajili ya Hospitali ya wilaya ya Korogwe ikiwa leo ni siku yao ya kusheherekea kuanzishwa kwa Mamlaka ya Bandari nchini.
MKUU wa wilaya ya Korogwe  Jokate Mwegelo  kushoto akipokea msaada wa vifaa tiba wenye thamani ya Milioni 10 kutoka kwa Meneja wa Bandari ya Tanga Masoud Mrisha kwa ajili ya Hospitali ya wilaya ya Korogwe ikiwa leo ni siku yao ya kusheherekea kuanzishwa kwa Mamlaka ya Bandari nchini.
MKUU wa wilaya ya Korogwe Jokate Mwegelo kushoto akipokea msaada wa vifaa tiba wenye thamani ya Milioni 10 kutoka kwa Meneja wa Bandari ya Tanga Masoud Mrisha kwa ajili ya Hospitali ya wilaya ya Korogwe ikiwa leo ni siku yao ya kusheherekea kuanzishwa kwa Mamlaka ya Bandari nchini.
MKUU wa wilaya ya Korogwe Jokate Mwegelo  kushoto katikati akimkabidhi  msaada wa vifaa tiba wenye thamani ya Milioni 10 Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Korogwe Miriam Cheche mara baada ya kuvipokea kutoka kwa Meneja wa Bandari ya Tanga Masoud Mrisha kulia  kwa ajili ya Hospitali ya wilaya ya Korogwe ikiwa leo ni siku yao ya kusheherekea kuanzishwa kwa Mamlaka ya Bandari nchini.
MKUU wa wilaya ya Korogwe     Jokate Mwegelo  kushoto akiwa na Meneja wa Bandari ya Tanga Mrisha Masoud wakiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya kukabidhiwa vifaa hivyo
MKUU wa wilaya ya Korogwe   Jokate Mwegelo    kushoto akiwa na Meneja wa Bandari ya Tanga Mrisha Masoud wakiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya kukabidhiwa vifaa hivyo



Sehemu ya vifaa hivyo





Na Oscar Assenga,KOROGWE

MAMLAKA ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) wamekabidhi msaada wa vifaa tiba vyenye thamani ya Milioni 10 katika Hospitali ya wilaya ya Korogwe  ikiwa kuunga mkono juhudi za Rais Dkt Samia Suluhu za kuondoa changamoto kwenye sekta ya afya, elimu na mambo mengine kwenye jamii.


Vifaa vilivyotolewa ni viti mwendo 10 vyenye thamani ya milioni 4 na ya mashine ya ECG kwa ajili ya matibabu ya moyo ambavyo vitakwenda kuwasaidia wananchi wanapata huduma kwenye Hospitali hiyo kutoka maeneo vijiji mbalimbali wilayani humo ikiwa  ni kurudisha kwa jamii

Akizungumza mara baada ya kukabidhi vifaa hivyo kwa Mkuu wa wilaya ya Korogwe  Jokate Mwegelo , Meneja wa Bandari ya Tanga Masoud Mrisha alisema kwamba wameamua kutoa msaada huo ikiwa leo ni siku yao ya kusheherekea kuanzishwa kwa Mamlaka ya Bandari nchini.

Alisema wao wametoa kwa jamii walichokipata mwaka huu na wameamua kupeleka msaada huo kwenye Hospitali hiyo ili kuweza kuwasaidia kuwapunguzia baadhi ya changamoto zilizokuwa zikiwakabili kwenye Hospitali ya Korogwe.

“Licha ya kutoa msaada huu hapa lakini tutaendelea kusaidia kitakachpatikana ili kuweza kutatua changamoto kwenye hospitali ili kuhakikisha wananchi wanaondokana na vikwazo mbalimbali katika kupata huduma za matibabu”Alisema

Awali akizungumza mara baada ya kupokea msaada huo Mkuu wa wilaya ya Korogwe  Jokate Mwegelo   aliishukuru Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) kwa msaada huo mkubwa ambao wamewapatia kwa ajili ya hospitali ya wilaya ya Korogwe ambao ni vitindi mwendo ambavyo uhitaji wake ulikuwepo.

Alisema pia msaada huo mashine ya  ECG   kwa ajili ya matibabu ya moyo utawasaidia wananchi katika wilaya hiyo kutokana na idadi ya watu wenye matatizo ya moyo inaongezeka vijijini kutokana na matumizi ya chumvi kuongezeka.

Alisema pia matumizi ya mafuta vinachangia pia na mtindo wa maisha huku akieleza kifaa hicho kitakwenda kuwatibu wananchi na hivyo kuwasaidia kuwa na afya bora kutokana na kwamba Taifa lenye nguvu lazima wananchi wake wawe na afya bila afya hawaweze kufanya kazi na kuweza kushiriki shughuli za kijamii ili kuweza kukuza uchumi.

Naye kwa upande wake Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Korogwe Miriam Cheche aliishukuru TPA kwa kugawawia msaada wa vifaa hivyo ikiwemo kifaa cha kisasa ambacho kinagundua matatizo ya moyo kwa mtu anayeugua kabla ya kupelekwa kwenye Hospitali za Rufaa.

“Kwa kweli tunawashukuru sana TPA kwa msaada huu kwa sababu wananchi watafaidika na mashine hii lakini tunamshukuru DC kwa hamasa zake na hivyo kupelekea wadau mbalimbali kujitokeza kusaidia pia Rais Dkt Samia Suluhu kuendelea kutupatia fedha kuendeleza hospitali yetu ya wilaya hapa Makuyuni”Alisema

MBUNGE KOKA AFANYA KWELI ATEKELEZA AHADI ZAKE SOKO LA MNARANI.


 Na Victor Masangu,Kibaha


Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini Silvestry Koka ametekeleza ahadi yake kwa vitendo kwa wafanyabiashara wa soko la mnalani kwa kuwakabidhi matenki makubwa matatu kwa ajili ya kuhifadhia maji.

Koka amekabidhi matanki hayo wakati wa ziara yake ya kikazi yenye lengo la kuweza kuwatembelea na kuzungumza na wafanyabiashara wa bidhaa  mbali mbali ikiwa sambamba na kutekeleza ahadi zake ambazo aliziahidi kipindi cha nyuma.

Aidha katika ziara hiyo Mbunge Koka ambaye aliambatana na viongozi mbali mbali wa chama pamoja na viongozi wa serikali akiwemo Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nikson Saimon pamoja na Mwenyekiti wa Halmashauri ya mji wa Kibaha Mussa Ndomba.

Mbunge huyo alisema kwamba ana imani kwamba matanki hayo ya maji yataweza kuwasaidia  kwa kiasi kikubwa kupunguza kero na adha ambayo ilikuwa ikiwakabili wafanyabiashara hao kwa kipindi cha muda mrefu.

Sambamba na hilo Koka amekabidhi televisheni (TV) mbili za kisasa  zenye ukunbwa wa nchi 45 kwa lengo la kuwapa guess ya wafanyabiashara hao kutazama na  kupata  matukio na taarifa  mbali mbali kutoka   ndani na nje ya nchi.

"Kipindi cha nyuma nilipita katika soko hili na niliahidi matanki ya maji makubwa matatu.,Televisheni mbili sambamba na vifaa vya michezo ikiwemo mipira pamoja na jezi na leo hii nimekuja rasmi kwa ajili ya kuvikabidhi,alisema Koka.

Aidha Mbunge huyo aliongeza kwamba lengo lake kubwa ni kuwawekea mazingira mazuri wafanyabiashara hao ili soko liweze kuwa la kisasa zaidi na waweze kufanya biashara zao katika mazingira ambayo ni rafiki.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nikson Saimon alimshukuru kwa dhati Mbunge huyo kwa kuweza kuona umuhimu wa kuwasaidia wafanyabiashara hao na kwamba serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya kuendelea kuboresha miundombinu ya soko hilo.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya mji Kibaha Mussa Ndomba alibainisha kuwa kwa sasa wameshatenga zaidi ya milioni 200 kwa ajili ya kuezeka paaa katika soko hilo ili kuondokana na changamoto hasa katika kipindi cha mvua kwani bidhaa zimekuwa zikilowa.


Nao baadhi ya wafanyabiashara katika soko hilo wamempongeza Mbunge huyo kwa kuweza kutekeleza ahadi yake kwa vitendo na kwamba matanki ya maji waliyopatiwa yatakuwa ni mkombozi mkubwa wa upande wao katika kuhifadhi maji.

TRA PWANI YAZINDUA KAMPENI YA KUWANOA WAFANYABISHARA JUU YA UMUHIMU WA KODI

 


Na Victor Masangu,Pwani 


Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Pwani katika kupambana na kudhibiti mianya ya ulipaji wa kodi imezindua  kampeni maalumu yenye lengo la kutoa elimu kwa wafanyabiashara juu kutumia mashine za kielekroniki (EFD) pindi wanapouza bidhaa zao.

Hayo yamebainishwa na Meneja wa TRA Mkoa wa Pwani Masawa Masatu  wakati akizungumza na waandishi kuhusiana na  kampeni hiyo ambayo pia itaenda sambamba na kuwahimiza wananchi kuhakikisha wanasai risiti pindi wanapofanya manunuzi kwani ni haki yao ya msingi.

Meneja Masawa alisema kwamba kampeni hiyo itaweza kuwasaidia kwa kiasi kikubwa wafanyabiashara waweze kutimiza wajibu wao katika suala zima la ulipaji wa kodi kwa hiari bila ya kukwepa lengo ikiwa ni kuisaidia serikali kukusanya mapato yake.
"Kikubwa nimewaita kwa ajili ya kampeni hii maalumu ambayo itajulikana kwa jina la Tuwajibike,'kodi yetu maendeleo yetu' na kikubwa ni kutoa elimu katika Wilaya mbali mbali za Mkoa wa Pwani na kikubwa ni wafanyabiashara kulipa kodi ili kuisaidia serikali,"alisema Masawa.

Alifafanua kuwa wananchi wanapaswa kuhakikisha wanasai risiti zao halali pindi wanaponunua bidhaa zao na pia wafanyabiashara watoe risiti za kielectoniki pindi wanapouza bidhaa zao kwani kufanya hivyo kunasaidia serikali kupata mapato yake kihalali.


Aidha Meneja huyo alibainisha kuwa lengo kubwa ni kuweka mikakati madhubuti katika ukusanyaji wa kodi ambayo itaweza kusaidia katika mambo mbali mbali ikiwemo kutekeleza miradi ya maendeleo  kama vile ya elimu,afya,umeme,pamoja maeneo mengine.



Nao baadhi ya wafanyabiashara wa Mkoani Pwani hawakusita kuzungumzia juu ya umuhimu wa kutumia mashine hizo za EFD huku wameipongeza TRA kwa hatua ya kwenda kuwatembea na kuwapa elimu ya umuhimu wa kulipa kodi kwa maslahi ya maendeleo ya Taifa.

Mmoja wa wafanyabiashara wa eneo la Loliondo alibainisha kuwa kutokana na elimu ambayo wamekuwa wakiipata kutoka kaa TRA Mkoa wa Pwani kumewasaidia wateja wao kusai risiti zao baada ya kumaliza kufanya manunuzi ya bidhaa zao.

Kampeni hiyo maalumu ambayo imepewa jina la Tuwajibike itafanyika kwa kipindi cha wiki moja katika Wilaya mbalu mbali za Mkoa wa Pwani ambapo italenha zaidi kutoa elimu kwa wananchi na wafanyabiashara juu ya kutoa risiti halali pamoja na kudai risiti.

WATATU KUPAMBANA LEO HATUA YA ROBO FAINALI

 


MABONDIA WATATU WA TANZANIA LEO WATINGA ROBO FAINALI YA MASHINDANO KUFUZU KUSHIRIKI OLIMPIKI. 

 Watanzania watatu leo kuanzia saa kumi na moja jioni kwa saa za Senegal, watapanda ulingoni kutafuta tiketi ya kuingia nusu fainali katika mashindano ya kufuzu kushiriki mashindano ya Olimpiki 2024 Paris Ufaransa yanayoendelea Dakar Senegal. Mabondia hao ni, katika uzito wa 66Kg. wanawake Grace Mwakamele (Tanzania) atapambana na Khelif Imane (Algeria), katika uzito wa 51Kg. 

Abdallah Mohamed (Tanzania) atacheza na Mortaji Said (MOROCCO) na katika uzito wa 80Kg. Yusuf Changalawe atacheza na Seydna Konate (Senegal)  

Mabondia waliofuzu kufika hatua hiyo jumla yao ni 104 kutoka katika mataifa 26 ya AFRIKA.  

Jumla ya mabondia walioshiriki mashindano hayo ni 235 kutoka katika mataifa 41 ya Afrika.  

Mabondia wengine wa Tanzania walishindwa katika hatua za awali ni 50Kg. Zulfa Macho, 57Kg. Mwalami Salum na 92 Kg. Mussa Maregesi. 

Viongozi waliombatana na timu ni Lukello Wililo (Raisi na Mkuu wa Msafara),Makore Mashaga (katibu na kocha msaidizi), Samwel Batman (Kocha mkuu) na Aisha George (Matron) Fainali za mashindano hayo zitafanyika ijumaa ya tarehe 15.09.2023. 

Timu itarejea nyumbani Jumapili ya tarehe 17.09.23 saa tisa Alfajiri. 

Naambatanisha na ratiba ya leo.