ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, September 13, 2023

TPA YAUNGA MKONO JUHUDI ZA RAIS DKT SAMIA KWA KUTOA MSAADA WA VIFAA TIBA HOSPITALI YA WILAYA YA KOROGWE

 

MKUU wa wilaya ya Korogwe Jokate Mwegelo kushoto akipokea msaada wa vifaa tiba wenye thamani ya Milioni 10 kutoka kwa Meneja wa Bandari ya Tanga Masoud Mrisha kwa ajili ya Hospitali ya wilaya ya Korogwe ikiwa leo ni siku yao ya kusheherekea kuanzishwa kwa Mamlaka ya Bandari nchini.
MKUU wa wilaya ya Korogwe Jokate Mwegelo kushoto akipokea msaada wa vifaa tiba wenye thamani ya Milioni 10 kutoka kwa Meneja wa Bandari ya Tanga Masoud Mrisha kwa ajili ya Hospitali ya wilaya ya Korogwe ikiwa leo ni siku yao ya kusheherekea kuanzishwa kwa Mamlaka ya Bandari nchini.
MKUU wa wilaya ya Korogwe  Jokate Mwegelo  kushoto akipokea msaada wa vifaa tiba wenye thamani ya Milioni 10 kutoka kwa Meneja wa Bandari ya Tanga Masoud Mrisha kwa ajili ya Hospitali ya wilaya ya Korogwe ikiwa leo ni siku yao ya kusheherekea kuanzishwa kwa Mamlaka ya Bandari nchini.
MKUU wa wilaya ya Korogwe Jokate Mwegelo kushoto akipokea msaada wa vifaa tiba wenye thamani ya Milioni 10 kutoka kwa Meneja wa Bandari ya Tanga Masoud Mrisha kwa ajili ya Hospitali ya wilaya ya Korogwe ikiwa leo ni siku yao ya kusheherekea kuanzishwa kwa Mamlaka ya Bandari nchini.
MKUU wa wilaya ya Korogwe Jokate Mwegelo  kushoto katikati akimkabidhi  msaada wa vifaa tiba wenye thamani ya Milioni 10 Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Korogwe Miriam Cheche mara baada ya kuvipokea kutoka kwa Meneja wa Bandari ya Tanga Masoud Mrisha kulia  kwa ajili ya Hospitali ya wilaya ya Korogwe ikiwa leo ni siku yao ya kusheherekea kuanzishwa kwa Mamlaka ya Bandari nchini.
MKUU wa wilaya ya Korogwe     Jokate Mwegelo  kushoto akiwa na Meneja wa Bandari ya Tanga Mrisha Masoud wakiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya kukabidhiwa vifaa hivyo
MKUU wa wilaya ya Korogwe   Jokate Mwegelo    kushoto akiwa na Meneja wa Bandari ya Tanga Mrisha Masoud wakiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya kukabidhiwa vifaa hivyo



Sehemu ya vifaa hivyo





Na Oscar Assenga,KOROGWE

MAMLAKA ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) wamekabidhi msaada wa vifaa tiba vyenye thamani ya Milioni 10 katika Hospitali ya wilaya ya Korogwe  ikiwa kuunga mkono juhudi za Rais Dkt Samia Suluhu za kuondoa changamoto kwenye sekta ya afya, elimu na mambo mengine kwenye jamii.


Vifaa vilivyotolewa ni viti mwendo 10 vyenye thamani ya milioni 4 na ya mashine ya ECG kwa ajili ya matibabu ya moyo ambavyo vitakwenda kuwasaidia wananchi wanapata huduma kwenye Hospitali hiyo kutoka maeneo vijiji mbalimbali wilayani humo ikiwa  ni kurudisha kwa jamii

Akizungumza mara baada ya kukabidhi vifaa hivyo kwa Mkuu wa wilaya ya Korogwe  Jokate Mwegelo , Meneja wa Bandari ya Tanga Masoud Mrisha alisema kwamba wameamua kutoa msaada huo ikiwa leo ni siku yao ya kusheherekea kuanzishwa kwa Mamlaka ya Bandari nchini.

Alisema wao wametoa kwa jamii walichokipata mwaka huu na wameamua kupeleka msaada huo kwenye Hospitali hiyo ili kuweza kuwasaidia kuwapunguzia baadhi ya changamoto zilizokuwa zikiwakabili kwenye Hospitali ya Korogwe.

“Licha ya kutoa msaada huu hapa lakini tutaendelea kusaidia kitakachpatikana ili kuweza kutatua changamoto kwenye hospitali ili kuhakikisha wananchi wanaondokana na vikwazo mbalimbali katika kupata huduma za matibabu”Alisema

Awali akizungumza mara baada ya kupokea msaada huo Mkuu wa wilaya ya Korogwe  Jokate Mwegelo   aliishukuru Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) kwa msaada huo mkubwa ambao wamewapatia kwa ajili ya hospitali ya wilaya ya Korogwe ambao ni vitindi mwendo ambavyo uhitaji wake ulikuwepo.

Alisema pia msaada huo mashine ya  ECG   kwa ajili ya matibabu ya moyo utawasaidia wananchi katika wilaya hiyo kutokana na idadi ya watu wenye matatizo ya moyo inaongezeka vijijini kutokana na matumizi ya chumvi kuongezeka.

Alisema pia matumizi ya mafuta vinachangia pia na mtindo wa maisha huku akieleza kifaa hicho kitakwenda kuwatibu wananchi na hivyo kuwasaidia kuwa na afya bora kutokana na kwamba Taifa lenye nguvu lazima wananchi wake wawe na afya bila afya hawaweze kufanya kazi na kuweza kushiriki shughuli za kijamii ili kuweza kukuza uchumi.

Naye kwa upande wake Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Korogwe Miriam Cheche aliishukuru TPA kwa kugawawia msaada wa vifaa hivyo ikiwemo kifaa cha kisasa ambacho kinagundua matatizo ya moyo kwa mtu anayeugua kabla ya kupelekwa kwenye Hospitali za Rufaa.

“Kwa kweli tunawashukuru sana TPA kwa msaada huu kwa sababu wananchi watafaidika na mashine hii lakini tunamshukuru DC kwa hamasa zake na hivyo kupelekea wadau mbalimbali kujitokeza kusaidia pia Rais Dkt Samia Suluhu kuendelea kutupatia fedha kuendeleza hospitali yetu ya wilaya hapa Makuyuni”Alisema

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.