ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, September 7, 2018

VIDEO:- RAIS MAGUFULI ATUMA SALAMU ZA POLE KWA WAANDISHI WA HABARI WALIOPATA AJALI



GSENGOtV
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli ametuma salamu za pole kwa Waandishi wa Habari waliopata ajali katika Msafara wake wa Ziara ya fupi mkoani Mwanza.

Akiwasilisha salamu hizo za pole, mapema asubuhi ya leo  kwa Wanahabari Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella amesema kuwa Rais anatambua mchango wa Waandishi kwa maendeleo ya taifa, upashaji wa habari na uelimishaji na toka alipofika jijini hapa 3, Septemba 2018 na kuzindua miradi mbalimbali ikiwemo utiaji saini mkataba wa Kandarasi ya  ujenzi wa meli kubwa ya kisasa wamekuwa wakitoa ushirikiano bila kuchoka kwa maslahi ya umma.

"Waandishi wa Habari wamefanya kazi kubwa mimi mwaka wa tatu nipo jijini hapa  mnatueleza changamoto ziko wapi naomba tuendelee hivyo kuchangia maendeleo ya nchi yetu," alisema Mongella.

Wakizungumzia ajali hiyo iliyotokea kwenye msafara wa Ziara ya fupi ya Rais, wilayani  Bunda kuelekea Kisorya ilisababishwa na mwendo kasi, vumbi kuwa jingi, madereva kushindwa kuona mbele hata 9dkupelekea magari kugongana na jingine kupinduka Waandishi hao walikuwa na haya ya kusema.

Aidha mmoja kati ya Wanahabari waliopata ajali hiyo Emmanuel Meshack aliyeumia sehemu ya bega na goti la mguu, ameshukuru Serikali ya Mkoa kutambua umuhimu wao na kuomba wasisite kutoa ushirikiano kwa waandishi kwa maendeleo ya Taifa.

KANUNI 10 ZAPITISHWA KUMLINDA MTOTO.

 Kamati ya maendeleo ya kata ya Igogo Nyamagana,  Mwanza  kwa kushirikiana na Shirika la wotesawa sept 6, 2018 walipitisha kanuni kumi(10) za kumlinda mtoto mfanyakazi wa nyumbani kwa lengo la kuondoa migogoro na migongano iliyopo kwenye mitaa yao kwa ajili ya wafanyakazi wa majumbani.

Mwenyekiti wa mtaa wa Mwenge kata ya Igogo wilayani Nyamagana Ramadhan Salum Mahira ambaye ni mwenyekiti wa kikao kazi hicho alisema wamefikia maamuzi hayo kutokana na vitendo mbalimbali vya ukatili dhidi ya watoto wafanyakazi vinavyoendelea kufanyika katika kata hiyo.

“Kata ya Igogo ni moja kati ya kata zenye migogoro mingi baina ya waajiri na watoto wafanyakazi za nyumbani hivyo wenzetu wote sawa walipokuja tukaona kuna haja ya kuandaa hizi kanuni kwa lengo la kuondoa hiyo migogoro na migongano na kweli tumefanikiwa na leo hii ndiyo tunazipitisha ili ziende kutumika ambazo tunaamini zitaleta usawa”alisema Menyekiti Ramadhan 

Aidha amesema kanuni hizo zitaleta muelekeo pamoja na kupunguza migongano na migogoro kwa jamii na  wengine watajifunza kutoka katika kata hiyo kwa sababu kila mtu atajua haki na wajibu wake kwa mwingine.

Nao wenyeviti wa mitaa mbalimbali iliyopo kwenye kata hiyo walielezea kufurahishwa na kanuni hizo wakisema kutokuwepo kwake ni chanzo cha matatizo kwenye mitaa wanayoiongoza huku wakikiri kuwa hawakuwahi kuwa na kanuni hizo.

Wamezitaja faida mbalimbali watakazonufaika nazo watoto wafanyakazi za nyumbani kuwa ni jamii kutambua haki zao zikiwemo haki ya kupata likizo, kulipwa mshahara wake kwa wakati, haki ya kupatiwa huduma za matibabu pamoja na  kiwango cha mshahara.

“tulikuwa hatuna hizi kanuni kwahiyo zitatusaidia sana katika kusaidia wafanyakazi kwenye majumba wafanyakazi watakuwa wamepata faida kubwa kwani wengi wao pia walikuwa hawazijui wala kuzitambua  kwahiyo zitawasaida sana”

“kwa upande wetu wenyeviti  ilikuwa yakitokea matatizo hatujui wapi tuanzie ila kupitia kanuni hizi tumepata utaratibu wa kuanzia”alisema Anthony Kimazi M/kiti wa mtaa wa Kambarage

Kwa upande wake muwakilishi wa shirika la wote sawa ambalo ndilo muandaaji wa kikao kazi hicho Elisha David amesema shirika lipo katika utekelezaji wa mradi wa ushirikishwaji wa wafanyakazi za majumbani ambao umefanyika katika kata 6 zilizopo Nyamagana.

Amesema kanuni hizo ni matokeo ya vikao baina yao na kamati za maendeleo ya kata WODC ambapo kupitia vikao hivyo waliamua kuandaa kanuni ambazo lengo lake ni kuleta ushirikiano kati ya pande hizo na zitaondoa migogoro mingi pamoja na changamoto zinazojitokeza.

“lengo ni kuboresha uhusiano tukiamini kuwa mfanyakazi ana thamani kubwa kwenye familia, kwani mwajiri akiondoka kazini anamwachia binti nyumba yenye thamani kubwa na vitu vingi ndani yake, kama hakuna mahusiano mazuri wanaweza kufanya vitu vibaya sana”Alisema Elisha

Miongoni mwa kanuni hizo kumi(10) zilizoandaliwa ambazo zitatumika kwenye mitaa yao ni pamoja na kila muajiri anatakiwa kumsajili mfanyakazi wa nyumbani katika uongozi wa serikali ya mtaa, kila mtaa uandae orodha ya wafanyakazi wa nyumbani, mwajiri atoe mkataba na mwajiri kutoruhusiwa kuajili mtoto chini ya miaka 13, Mwajiri kutomuajiri mtoto mwenye umri chini ya miaka 14  na nyingine inasema mfanyakazi wa nyumbani atamtii na kumuheshimu mwajiri wake.




RC HAPI : KUTEMBELEA JUMLA YA MIRADI 55 YENYE THAMANI YA SH. 78,138,549,216 KATIKA ZIARA YA TARAFA KWA TARAFA

Mkuu wa mkoa wa Iringa Ally Hapi akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake juu ya ziara ya tarafa kwa tarafa ambayo anatarajia kuianza siku ya kesho katika wilaya ya Mufindi kwa lengo la kuijenga Iringa mpya yenye maendeleo 

NA FREDY MGUNDA,IRINGA

Mkuu wa mkoa wa Iringa Ally Hapi anatarajia kuanza ziara ya kikazi kwa kuzitembelea tarafa zote 15 za wilaya zote 3 za mkoa wa Iringa lengo likiwa ni kufanya jumla ya mikutano 37 na kutembelea jumla ya miradi 55 yenye thamani ya shilingi 78,138,549,216 ambayo itausisha ukaguzi,uzinduzi na uwekaji wa mawe ya msingi.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mh: Hapi alisema kuwa anatarajia kutembea jumla ya kilometa 2,611 wakati wa ziara hiyo ya kikazi kwenye mkoa wote wa Iringa.

“Nitatembea tarafa tano za wilaya ya Mufindi ambazo ni Ifwagi,Malangali,Kibengu,Sadani na Kasanga,wilaya ya kilolo nitatembelea tarafa tatu ambazo ni Mazombe,Kilolo na Mahenge na kumalizia wilaya ya Iringa yenye tarafa saba ambazo ni Kalenga,Ismani,Pawaga,Idodi,Mlolo,Kiponzelo na Iringa mjini hapo ndio nitakuwa nimemaliza ziara yangu ya tarafa kwa tarafa” alisema Hapi

Hapi alisema kuwa lengo la ziara hiyo ni kuijenga Iringa mpya katika dhana ya kuboresha utendaji wa serikali,kuimarisha sekta za kilimo,ujenzi wa viwanda,utalii,miundombinu,biashara,huduma za afya,maji,elimu,utatuziwa kero za wananchi na kutengeneza fursa zilizopo katika mkoa wa Iringa.

Aidha Hapi alisema kuwa atafanya mikutano mikubwa kumi na saba na midogo 20 ambapo mikutano kumi na tano itafanyika katika tarafa kumi na tano kwa kuambatana na wataalam mbalimbali kutoka idara zote za serikali na taasisi za UMMA.

“ Katika ziara yangu zitatoa sana fursa kwa wananchi kuuliza maswali na kutoa kero zao kwa lengo la kutatua matatizo ambayo yanawakumba wananchi  na nitawaeleza muelekeo wa kujenga Iringa mpya” alisema Hapi

Hapi aliwataka viongozi wote wa mkoa kuanzia wakuu wa wilaya haviongozi wa chini kuiga mfano wake wa kwenda kutatua kero za wananchi na wasipofanya hivyo hatakuwa na msamaa kwa viongozi wote wazembe na ambao hawatatui kero za wananchi.


Naomba kumalizia kwa kuwaomba wananchi kujitokeza kwa wingi kwenye mikutano yangu na kuhumiza viongozi wanatakiwa kuwepo kwenye ziara yangu bila kukosa.


Believe in thomthinEven if it meanth thacrifithing everythin

VIDEO:- MAAMUZI YA MUSUKUMA BAADA YA HABARI ZA MALI ZAKE KUPIGWA MNADA NA NBC



GSENGOtV
Mbunge wa Geita Vijijini Joseph Kasheku maarufu kama Musukuma amesema kuwa  waandishi wote waliomuandika kwa taarifa za uongo waombee tarehe 22 mwezi huu nyumba zake zipigwe mnada kwani isipofanyika hivyo ameapa kushughulika na mmoja baada ya mwingine.

Musukuma amesema hayo hii leo wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Mwanza akibu taarifa anazozitaja kuwa ni za uzushi, zilizoandikwa na moja kati ya magazeti hapa nchini, kwamba Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) kupitia kampuni ya udalali ya LJ International Ltd imetangaza kuzipiga mnada mali za Mbunge wa Geita Vijijini, Joseph Kasheku maarufu kama Musukuma.

Pia sakata hilo Mbunge Musukuma amemjumuisha Afisa wa Benki ya NBC William Kalage anayenukuliwa na gazeti hilo akithibitisha hatua za mnada huo, akimtaka amsafishe ndani ya siku 7 kabla hajachukuwa hatua za kisheria.

Mali zilizotajwa kupigwa mnada ni pamoja na kiwanja Na.275 Block kilichopo Mbezi Dar es Salaam na kiwanja Na.’2’ block ‘A’kilichopo Korogwe mjini.

Mali nyingine ni shamba Na.201 liliolopo kijiji cha Igate Mkoani Geita, kiwanja Na. 116 block A Buswelu Kaskazini na kiwanja Na. 48 block T katikati ya jiji la Mwanza.

"Hakuna nyumba yangu hata moja itakayopigwa mnada haya ni maneno ya uchonganishi, kiukweli hawatoniweza kwani siasa zangu ni za ukweli" na kisha akaongeza "Aliyeniandika ajisalimishe kabla ya tarehe aliyoitaja, kabla sijaanza kushughulika na mmoja mmoja, si mnanijua mimi ni nani........... " alimaliza Musukuma.


Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Benki ya NBC, William Kalage amesema ni kweli mali hizo zinapigwa mnada.
“Ni kweli tumetoa tangazo na sisi ndiyo tumeipa kazi hiyo kampuni ya udalali kupiga mnada mali hizo,” amesema
Mbali na Musukuma, kampuni ya LJ International Ltd pia imetangaza watu 19 wanaodaiwa na benki hiyo ambao mali zao zitanadiwa.

AJIBU ASEMA HAYA KUHUSU YANGA.


BAADA ya kocha wake Mwinyi Zahera kumsifia kuwa ana dhahabu miguuni mwake ingawa hajui kuzitumia, mshambuliaji wa Yanga, Ibrahim Ajibu amefunguka kuwa kwa sasa yuko vizuri na yupo tayari kupambana.
Ajibu amefanya vizuri kwenye michezo ya hivi karibuni hadi kufikia hatua ya kusifiwa na kocha wake huyo raia wa DR Congo.

Msimu uliopita, Ajibu alifanikiwa kufunga mabao saba huku mechi za mwishoni mwa ligi hiyo nyingi akikosa kutokana na sababu mbalimbali.

Akizungumza na Championi Ijumaa, mshambuliaji huyo alisema kuwa anaendelea kujifua kuhakikisha anakuwa fiti kuweza kuipambania Yanga.

“Nashukuru Mungu binafsi naendelea vizuri na sasa nafanya mazoezi kwa ajili ya kupambana zaidi kwa sababu ndiyo kwanza msimu umeanza, hivyo ni vyema kuanza vizuri tangu mwanzo,” alisema Ajibu.

Thursday, September 6, 2018

KIVULINI YAZIDI KUIMARISHA MKAKATI WA KUTOKOMEZA ZERO NA MIMBA BWIRU GIRLS



GSENGOtV
Shule kongwe ya sekondari ya wasichana ya Bwiru,Jijini Mwanza imeanzisha mkakati maalumu wa kukuza kiwango cha taaluma na ufaulu na kupambana na matukio ya mimba na division ziro  kwa wanafunzi. 

Licha ya kuwaasa na kuwapa mbinu nini chakufanya wakiwa shuleni na wawapo nje ya shule, Mkurugenzi wa Shirika la Kutetea haki za wanawake na watoto la KIVULINI, Yasin Ally amefunguka siri ya matoke chanya yaliyojiri kwa matokeo kidato cha sita mtihani wa 2017-2018.

RAIS MAUFULI AAGIZA SHULE ALIYOSOMA NYERERE KUKARABATIWA NA KUZUNGUSHIWA UZIO.

 RAIS John Pombe Magufuli ameonyesha kusikitishwa na majengo yasoyokuwa na ubora ya shule ya msingi Mwisenge ya mjini Musoma mkoani Mara ambayo alisoma Mwalimu Julius Kambarage Nyarara ambaye ni Baba wa Taifa.

Kufuatia kitendo hicho Rais Magufuli jana alipotembelea shule hiyo ameendelea kusisitiza kuwa viongozi waliopo serikalini aliowachagua na wale wa kuchaguliwa wachukue  hatua ya kushirikiana ili kuhakikisha shule hiyo inakarabatiwa majengo yake pamoja na kujengwa uzio ili majengo ya shule hiyo kuonekena kuwa yanaubora.

"Shule aliyosoma Marehemu Mwalimu Juliujs Kambarage Nyarere mwanzilishi wa Taifa letu miaka ya 1930 inakuwa hivyo na viongozi tupo tunatakiwa kumuenzi Nyerere kwa vitendo na sio kwa maneno vawaagiza viongozi walipo serikalini kuhakikisha mnasimamia ukarabati wa shule ya Mwisenge pamoja na kujengwa uzio"alisema Magufuli.

Kauli hiyo aliitoa jana na leo kuirudia wakati alipokuwa ametembelea Mwitongo alipozaliwa Nyerere wakati akihutubia wananchi wa halmashauri ya Butiama ambapo amesema kuwa kunahaja Waziri wa Elimu kutafuta fedha mahali popote na kuhakikisha shule hiyo inakarabatiwa na kujengwa uzio na kuwa na hadhi.

"Natoa milionim20 zifanye ukarabati na wahakikishieni kuwa fedha hizo zitakuja kabla ya wiki mbili zijazo, hakikisheni haziliwi na zikafanye kazi iliyokusudiwa" 


Pia Magufuli ameendelea kusema kuwa Taifa la Tanzania lazoma limuenzi Marehemu Nyerere kwasababu amehangaikia Uhuru wa Tanzania kwa kutumia juhudi zake ili kuhakikisha Tanzania inakuwa uhuru na watu wake.

Magufuli amewataka viongozi aliowachagua kuwatumikia wananchi wanyonge kwasbabu bila wananchi hao hao viongozi wasingeteuliwa kwa hali hiyo watatue matataizo ya wananchi.

Rais Magufuli baada ya kumaliza hotuba yake halmashauri ya Butiam,a alianza ziara ya kuelekea Wilaya Serengeti na kesho anatarajiwa kuingia Hlamashauri ya Tarime Vijijini na halmashauri ya Mjini wa Tarime mkoani Mara ili kusikiliza shida za wananchi.

KATIBU MKUU UVCCM AWATAMBULISHA WAKUU WA IDARA WAPYA KWA WATUMISHI WA MAKAO MAKUU UVCCM LEO.

 Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi Mwl Raymond Mwangwala (MNEC) pamoja na wakuu wa Idara wapya wa Umoja wa Vijana walipowalisi katika Ukumbi wa Mikutano Ofisi ndogo ya Makao Makuu UVCCM Upanga Dar Es Salaam

 Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi Mwl.Raymond Mwangwala (MNEC) akizungumza na watumishi wa Makao makuu wakati akiwatambulisha wakuu wa Idara wapya wa Umoja wa Vijana walioteuliwa na Kuthibitishwa na baraza kuu la UVCCM Taifa lililoketi jijini Dodoma wiki iliyopita
 Wakuu wa Idara za Makao makuu UVCCM wakifuatilia mazungumzo ya Katibu Mkuu UVCCM Mwl Raymond Mwangwala (MNEC) alipokuwa akiwatambulisha kwa watumishi wa UVCCM makao makuu.
 watumishi wa UVCCM makao makuu wakifuatilia kwa makini mazungumzo ya Katibu Mkuu wa UVCCM Mwl Raymond Mwangwala (MNEC) alipokuwa akiwatambulisha wakuu wa idara za UVCCM  makao makuu kwao
 Mkuu wa Idara ya Oganaizesheni na Siasa Ndg Peter Kasela akizungumza na watumishi wa Ofisi ndogo ya Makao Makuu ya UVCCM leo wakati wa kutambulishwa Kwa watumishi wa Makao makuu ya UVCCM
Katibu wa Idara ya Uhamasishaji na Chipukizi Ndg.Hassan Bomboko  akizungumza na watumishi wa Ofisi ndogo ya Makao Makuu ya UVCCM leo wakati wa kutambulishwa Kwa watumishi wa Makao makuu ya UVCCM
Katibu wa Idara ya Vyuo na Vyuo Vikuu Ndg Kamana Juma Simba  akizungumza na watumishi wa Ofisi ndogo ya Makao Makuu ya UVCCM leo wakati wa kutambulishwa Kwa watumishi wa Makao makuu ya UVCCM
Katibu wa Idara ya Uchumi na Uwezeshaji Ndg.Nelson Lusekelo akizungumza na watumishi wa Ofisi ndogo ya Makao Makuu ya UVCCM leo wakati wa kutambulishwa Kwa watumishi wa Makao makuu ya UVCCM
 Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi Mwl Raymond Mwangwala (MNEC) akiwakabidhi Mpangokazi wa Utekelezaji wa UVCCM Mwaka 2018/2019
 Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi Mwl Raymond Mwangwala (MNEC) akiwaongoza wakuu wa Idara za Makao makuu ya Umoja wa Vijana wakati akiwatembeza maeneo mbali mbali ya Ofisi ndogo ya Makao makuu ya UVCCM Upanga Dar es Salaam(Picha na FahadiSiraji wa UVCCM)

RC HAPI: MARUFUKU KUWANYANYASA MACHINGA KATIKA MAENEO WANAYOFANYIA KAZI ZAO


Mkuu wa mkoa wa Iringa Ally Hapi akiongea na wafanyabiashara wadogo wadogo maarufu kama machinga wa manispaa ya Iringa kwa lengo la kusikiliza kero na changamoto ambazo wanakabiliana katika kuleta maendeleo ya mkoa wa Iringa na kuhakikisha wanaijenga Iringa mpya ambayo inatakiwa na wanairinga 
Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela akiongea wakati wa kikao cha wafanyabiashara wadogo wadogo maarufu kama machinga na mkuu wa mkoa wa Iringa
Baadhi ya wafanyabiashara wadogo wadogo maarufu kama machinga walijitokeza kumsikiliza mkuu wa mkoa wa Iringa Ally Hapi na kama ambavyo unawaona walivyokuwa makini kumsikiliza hapo

 NA FREDY MGUNDA,IRINGA.

Mkuu wa mkoa wa Iringa amepiga marufuku wafanyabiashara wadogo wadogo kunyanyaswa katika mahali ambazo wanafanyia biashara kwa kuwa wanatoa kodi ambayo inachochea kuleta maendeleo ya watanzania hususani mkoani iringa tukielekea kuijenga Iringa mpya.

Akizungumza kwenye mkutano na wafanyabiasha wadogodogo wa manispaa ya Iringa mkuu wa mkoa Ally Hapi alisema kuwa wafanyabiasha wadogo wadogo maarufu kama machinga wanatakiwa kufanya biashara zao kwa kufuta taratibu na sheria za nchi huku viongozi wakiancha kuwanyanyasa kwa kuwa nao ni wafanyabiashara.

“Toka nikiwa mkuu wa wilaya najua umuhimu wafanyabiasha wadogo wadogo kwa kuchangia katika kukuza uchumi wa eneo husika hivyo natangaza rasmi ni marufuku kuwanyanyasa wafanyabiasha wadogo wadogo wa mkoa wa Iringa” alisema Hapi

Hapi aliwataka polisi wanasimamia eneo lastand kuu kuacha mara moja kunyanyasa wafanyabiasha wadogo wadogo wanaofanyia biashara katika eneo hilo.

Kauli hiyo imekuja mara baada ya katibu na mwenyekiti wa chama cha wafanyabiasha wadogo wadogo (machinga) kutoa kilio hicho mbele ya mkuu ya mkoa kwa kusema wamekuwa wakinyanyaswa na askari ambao wanafanya kazi katika stand kuu.

Katibu wa wafanyabiasha wadogo wadogo manispaa ya Iringa Joseph Kilyenyi alisema kuwa baadhi ya viongozi wa halimashauri ya manispaa ya Iringa pamoja na baadhi ya polisi wamekuwa kikwazo cha kufanya biasha kwa uhuru na kuongeza pato la manispaa ya Iringa.

“wafanyabiasha wadogo wadogo tupo zaidi ya elfu moja tukiwekewa mfumo sahihi kwa wakati sahihi tunaweza kutoa kodi zaidi ya shilingi milioni tisa  ambapo hapo tunatoa shilingi mia tatu  na ikiwa shilingi mia tano halmashauri itaingiza mapato mengi ambayo yatachangia maendeeleo ya manispaa” alisema Kilyenyi

Kilyenyi alisema kuwa wafanyabiasha wadogo wadogo wa manispaa ya Iringa wapo tayari kulipa kodi kama ambavyo Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuleta maendeleo na kuwapa nafasi wafanyabiasha wadogo wadogo kufanya kazi kwa uhuru na kuchochoe maendeleo.

“Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania DR John Pombe Magufuli amekuwa akitupelea na kuthamini hivyo hata sisi tunawajibu wa kuhakikisha tunalipa ushuru na kodi pale inapotakiwa ili kukuza juhudi za kuleta maendeleo ya nchi yetu” alisema Kilyenyi

Kilyenyi alimpongeza mkuu wa wilaya ya Iringa Richard kasesela pamoja na MNEC wa mkoa wa Iringa Salim Asas kwa kuwasaidia kutatua migogoro mbalimbali ambayo imekuwa ikiwakabili wafanyabiasha wadogo wadogo

“Baada ya kupokea kero za wafanyabiasha wadogo wadogo mkuu wa mkoa wa Iringa Hapi alimtaka Mkurugenzi wa halmashauri ya Iringa ndani ya mwezi mmoja kuhakikisha wanatengeza mfumo rafiki ambao utakuwa utasidia kukusanya kodi kwa wafanyabiasha hao.

Nimetoa siku thelathini kwa viongozi wa halmashauri kuhakikisha wanatengeza mfumo rafiki ambao hausababisha wafanyabiasha wadogo wadogo kulipa kodi katika maeneo wanayofanyia kazi ili kuwaondolea usumbufu wa kuwafuta mliko” alisema Hapi

Aidha hapi alisema kuwa hatawavumia viongozi wowote wale ambao watakwamisha kuijenga Iringa mya ambayo inatakiwa kuwa kama kituvu cha utalii nyanda za juu kusini

Naye afisa biashara wa manispaa ya Iringa kassim majariwa alisema kuwa ameyapogea maagizo yote ambayo mkuu wa mkoa ameagiza kuhakikisha kunakuwa na ongezeko la ukusanyaji wa kodi katika halmashauri ya Iringa.

NHIF TANGA YAPIGA KAMBI WILAYANI KILINDI KUHAMASISHA MPANGO WA TOTO AFYA KADI


 MENEJA wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga(NHIF) Ally Mwakababu kulia akitoa elimu juu ya umuhimu wa wananchi kuwaingiza watoto wao kwenye Mpango wa Toto Afya Kadi ili waweze kupaa huduma za matibabu wanapougua kwenye kijiji cha Gitu wilayani Kilindi mkoani Tanga
 Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) Ally Mwakababu kulia akitoa elimu kwa muuza nguo kwenye soko la Gitu wilayani Kilindi mkoani Tanga juu ya umuhimu wa kuwaingiza watoto wao kwenye mpango wa Toto Afya kadi wakati wa uhamasishaji wa mpango huo
Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga{NHIF) Ally Mwakababu akitoa elimu kwa wakazi wa Kijiji cha Gitu wilayani kilindi kuhusu umuhimu wa Toto Afya kadi kwa ajili ya watoto wao ili waweze kunufaika na matibabu wanapougua
 Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga{NHIF) Ally Mwakababu katikati akitoa elimu kwa wakazi wa Kijiji cha Gitu
 Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga{NHIF) Ally Mwakababu akitoa elimu juu ya umuhimu wa Mpango wa Toto Afya Kadi kwa mkazi wa Kijiji cha Gitu wilayani kilindi juu umuhimu wa watoto wao wakati wanapougua wakati wa uhamasishaji huo

 Afisa matekelezo wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) mkoani Tanga Macrina Clemens kushoto akihamasisha mpango wa Toto Afya Kadi kwa wananchi wa Kijiji cha Gitu
 Afisa matekelezo wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) mkoani Tanga Macrina Clemens akigawa vipeperusi kwa watoto vinavyoelezea mpango wa Toto Afya Kadi wakati wa uhamasishaji wa mpango huo
 MUUGUZI wa Afya akimpima mkazi wa Kijiji cha Gitu wilayani Kilindi
Mratibu wa NHIF wilaya ya Kilindi katika akimsikiliza mkazi wa Kijiji cha Gitu kushoto ni Mhasibu wa NHIF mkoani Tanga Hellena Manyanda
Afisa matekelezo wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) mkoani Tanga Macrina Clemens kulia akichukua maelezo ya mkazi wa Kijiji cha Gitu ambao walijitoikeza kwa ajili ya upimaji wakati wa uhamasishaji wa mpango wa Toto Afya Kadi wilayani Kilindi
 Mmmoja wa wahudumu wa Afya akimpima mmoja wa wakazi wa kijiji cha Gitu wilayani kKilindi
Sehemu ya wananchi wakisubiri huduma ya Upimaji wakati wa uhamasishaji wa Mpango wa Toto Afya Kadi katika Kijiji cha Gitu wilayani Kilindi Mkoani Tanga uliofanywa na NHIF mkoani Tanga





NA MWANDISHI WETU,KILINDI.

MFUKO wa Taifa wa Bima ya Afya mkoani Tanga(NHIF) umepiga kambi Kijiji cha Gitu wilayani Kilindi mkoani humo kuhamasisha umuhimu wa mpango wa Toto Afya kadi kwa wananchi ili kuwawezesha watoto wao kupata matibabu wanapougua.

Uhamasishaji huo ulifanywa na Meneja wa Mfuko huo mkoani Tanga Ally Mwakababu akiwa ameambatana na watumishi wengine wa mfuko huo ambao walitembelea maeneo mbalimbali wilayani humo.

Akizungumza wakati akitoa elimu kuhusu umuhimu wa wananchi kujiunga na mpango huo wakiwemo watoto wao ambao utawasaidia kuweza kupata huduma za matibabu wakati wanapougua 

Meneja Mwakababu alisema suala hilo ni muhimu kwa watoto wao hususani wakati wa ukuaji wao kutokana na kukabiliwa na magonjwa mbalimbali hivyo mpango huo utawasaidia wazazi kuondokana na gharama za matibabu

“Kama unavyojua huu mpango wa Toto Afya Kadi ni mzuri na unampa uhakika mtoto wako kuweza kupata huduma za matibabu pindi wanapougua kwani sio nyakati zote wanaweza kumudu gharama za matibabu kutokana na kupanda kila wakati”Alisema.

Hata hivyo aliwataka pia wananchi wa Kijiji hicho kuona namna bora ya kujiunga kwenye mfuko huo ili waweze kunufaika na huduma za matibabu wakati wanapokumbana na magonjwa mbalimbali.


Uhamasishaji huo unafanyika umefanywa na mfuko huo kwenye maeneo mbalimbali mkoani Tanga ili kuwawezesha wananchi kuchangamkia fursa hiyo wa kujiunga na mpango wa Bima ya Afya wao na Watoto wao

RAIS MAGUFULI ATENGUA NA KUTEUA MKURUGENZI TAKUKURU

 Rais John Magufuli amemteua Kamishna wa Polisi, Diwani Athumani kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(TAKUKURU) kuchukua nafasi ya Kamishna wa Polisi Valentino Mlowola ambaye ameteuliwa kuwa Balozi.