ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, November 29, 2019

KWAHERI BI. CHEKA


Msanii mkongwe wa kike wa muziki wa Bongo Fleva, Cheka Hija Mzee, maarufu kwa jina la ‘Bi Cheka’ amefariki dunia mchana wa Alhamisi ya Novemba 28, 2019 katika Hospitali ya Mloganzila, Dar es Salaam.

Kifo cha msanii huyo mkongwe kimethibitishwa na mtoto wake wa kiume, Adam Juma, ambaye amesema kuwa mama yake alikuwa akisumbuliwa na tatizo la moyo.

Bi Cheka atakumbukwa kwa umahiri wake wa ku-rap ambapo aliwahi kufanya kazi nyingi za muziki hasa akiwa na Kundi la TMK. Baadhi ya wasanii aliowahi kufanya nao ngoma ni Mheshimiwa Temba na marehemu Godzilla.


Jembe Fm inaungana na wale wote wailioguswa na msiba huu.

RIP Bi. Cheka.

RAIS WA ZAMANI WA VISIWA VYA MALDIVES AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MIAKA MITANO JELA.


Rais wa zamani wa visiwa vya Maldives Abdulla Yameen amehukumiwa kifungo cha miaka 5 jela baada ya kukutwa na hatia ya utakatishaji wa fedha.

Hukumu hiyo imetolewa baada ya uchunguzi ktika utawala wa kiimla wa kiongozi huyo, katika visiwa hivyo vinavyopendwa na watalii.

Yameen aliitawala Maldives kwa mkono wa chuma hadi mwaka 2018 aliposhindwa uchaguzi kwa hali ya kushtukiza.

Anashutumiwa kuhamisha kinyume cha sheria dola milioni moja kutoka akaunti yake ya benki, wakati uchunguzi dhidi yake ukiendelea.

Abdalla Yameen mwenye umri wa miaka 60 alikamatwa mwezi Februari, na kufunguiwa mashitaka ya kuwahonga mashahidi wakati kesi dhidi yake ikiendelea.

Mwishoni mwa mwaka jana serikali ya visiwa hivyo vya bahari ya Hindi iliishikilia akaunti yake yenye kiasi cha dola milioni 6.5, ikimtuhumu kupokea malipo yasio halali.

Waendeshamashtaka wanaamini kuwa kiongozi huyo wa zamani ameficha mamilioni mengine ya dola nje ya nchi.

Thursday, November 28, 2019

TB KUWAKUTANISHA WABUNGE, VIONGOZI WA DINI MWANZA



 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongela (katikati) akizungumza na waandishi wa habari jana (hawapo pichani) jana kuhusu mkutano wa wadau ili kuweka mikakati ya kukabiliana na ugonjwa wa Kifua kikuu (TB),utakaofanyika Ijumaa jijini humu.
 Mwenyekiti wa Kamati ya Wabunge walio kwenye mapambano ya ugonjwa wa Kifua kikuu (TB) Oscar Mukasa, akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) jana, kuhusu mkutano  wao na viongozi wa dini ambapo mgeni rasmi atakuwa Spika wa Bunge Job Ndugai.
 Mwenyekiti wa Kamati ya Wabunge walio kwenye mapambano ya ugonjwa wa Kifua kikuu (TB) Oscar Mukasa, akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) jana.
Mjumbe wa kamati ya wabunge walio kwenye mapambano ya ugonjwa wa kifua kikuu (TB) na na Ukimwi akielezea mikakati ya kamati hiyo ili katika juhudi za kudhibiti ugonjwa huo nchini ambapo Ijumaa wiki watakuna na viongozi wa dini zote nchini na  Spika wa Bunge Job Ndugai atakuwa mgeni rasmi wa mkutano huo. 

TB KUWAKUTANISHA WABUNGE, VIONGOZI  WA DINI MWANZA
NA BALTAZAR MASHAKA, MWANZA

KAMATI ya Wabunge wanaojihusisha na mapambano dhidi ya ugonjwa wa Kifua Kikuu (TB) na Ukimwi imesema changamoto ya inayowakabili watu wanaougua ugonjwa huo lakini hawafikiwi na huduma za tiba imeishawishi kukutana na viongozi wa dini zote nchini.
Mwenyekiti wa Kamati hiyo wabunge walio kwenye mapambano ya TB Oscar Mukasa ameyasema hayo jijini Mwanza alipozungumza na waandishi wa habari kuhusiana na mkutano utakaowakutanisha viongozi wa dini mbalimbali nchini ili kusaidia kusambaza elimu kwenye jamii.

Mkutano huo utakaofanyika Ijumaa jijini Mwanza, mgeni rasmi atakuwa Spika wa Bunge, Job Ndugai, ambapo Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenister Mhagama na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI),Seleman Jafo watashiriki.

Alisema idadi ya watu nchini, wanaougua ugonjwa wa TB  nchini ni kubwa huku changamoto yao kubwa ikiwa ni kutofikiwa na huduma za tiba.

“Ugonjwa wa TB ni tatizo kubwa la kiafya duniani,na hapa nchini watu zaidi ya 60,000 wanaougua hawafikiwi na huduma za tiba, hivyo kama hawapati matibabu jambo ambalo ni hatari  kwa kuwa mtu mmoja anaweza kuambukiza watu 20,”alisema
Mukasa  alisema wameamua kushirikisha viongozi wa dini kueneza elimu kuoitia nyumba za na endapo zitatumika vizuri zitasaidia kufikisha ujumbe na kuleta ufahamu kwa jamii juu ya tatizo na watakuwa wameunganisha  nguvu pamoja na serikali yao.

“Kazi ya Bunge ni kuleta ushawishi, kuleta ustashi wa kisiasa na  kuisimamia serikali na hivyo kutumia nyumba za ibada ni mkakati wa kuongeza elimu kwa jamii katika vita ya  kupambana na TB  kuhakikisha jamii haiathiriwi ,kwa sababu kabla ya kutumia dawa watajua unavyoambukiza,unatibiwaje  lakini bila elimu itakuwa kazi bure,”alisema Mukasa.
 Alieleza kuwa ushawishi huo wa viongozi wa dini utaifanya serikali  kuendelea kuongeza nguvu  kwenye vita hiyo  kwa kuwa hayatengenishwi na mifumo ya dini na wakiamua wanaweza kufikia maeneo mengi.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongela alisema maambukizi ya TB yako juu kwani takwimu za 2018 zinaonyesha wagonjwa wa TB 4,640 sawa na asilimia 6 wanatoka mkoani humu.

“Jambo hili ni kubwa lakini linazungumzwa juu juu, hivyo wataalamu wabobezi watatusaidia kupata elimu na taarifa sahihi kwenye mkutano huo wa wadau ili kupambana na tatizo hilo kwa umahiri na ufanisi mkubwa,”alisema Mongela. 

Wednesday, November 27, 2019

WAZIRI ANYESHEWA MVUA AKIZINADI SERA ZA MAGUFULI


WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi ameendelea na mikutano yake katika Jimbo la Kisesa Wilaya ya Meatu Mkoa wa Simiyu licha ya mvua kubwa kunyesha na kuonesha kutokata tamaa ili lengo la kuwasikiliza na kuwaeleza wananchi juhudi zinazofanywa na Serikali katika kuwahudumia wafugaji.

Akizungumza na wananchi wa Mwakaluba, Wilaya ya Meatu Mkoa wa Simiyu, Waziri Mpina alisisitiza msimamo wa Serikali katika kutoa huduma bora kwa mifugo ikiwemo kupunguza gharama za uogeshaji mifugo kutoka shilingi 500 kwa kichwa cha ng'ombe hadi kufikia sh 50.

Pia Mbuzi na Kondoo kutoka shilingi 100 hadi shilingi 10 kwa kichwa cha mbuzi au kondoo hali ambayo haijawahi kutokea isipokuwa ni Serikali ya awamu ya tano pekee inayoongozwa na Rais Dk John Pombe Magufuli

WATUHUMIWA WAWILI WA UJAMBAZI WAUAWA KWENYE MAJIBIZANO YA RISASI NA POLISI MWANZA.


Jeshi la Polisi mkoa wa Mwanza  limefanikiwa kuipata silaha moja aina ya bastola ikiwa na risasi tatu  zinatumiwa na wahalifu (majambazi) kwenye matukio mbalimbali kanda ya ziwa  baada ya watuhumiwa wawili wa ujambazi wanaume  ambao bado hawajafamika  majina wala makazi yao wanaokadiriwa kuwa na umri kati ya  miaka 25 hadi 30,  watuhumiwa hao walifariki wakati wakipelekwa hospitali baada ya majibizano ya kurushiana risasi na askari polisi baada ya kumtishia kumuua  kwa bunduki na baadae kupora pikipiki ya ” mwendesha bodaboda “.

Tukio hilo limetokea tarehe 26.11.2019 majira ya  23:40hrs huko maeneo ya Sweya – Fisheries wilayani Nyamagana, hii ni baada ya mwendesha pikipiki samwel masanja (bodaboda)   kuporwa pikipiki yake maeneo ya maina na watu hao  na baadae wananchi kutoa taarifa polisi.

Baada ya kupatikana kwa taarifa hizo askari  Polisi (makachero) walifanya ufuatiliaji wa haraka na baadae wakakutana na wahalifu  hao uso kwa uso maeneo ya Sweya, walipobaini kufuatiliwa walianza kuwarushia  risasi askari  na  askari walijihami na kufanikiwa  kuwajeruhi kwa  risasi  wahalifu hao ambao baadae  walifariki dunia  wakati wakipatiwa matibabu hospitali ya Bugando.

Katika eneo la tukio kumepatikana bastola moja aina ya Starbird yenye namba za usajili US Patten 2563720 pamoja na risasi tatu ndani ya magazine na pikipiki aina ya San LG nyekundu yenye namba za usajili MC 617 ABX ambayo ilikua imeporwa. 
Imepatikana  miili ya marehemu wote wawili imehifadhiwa Hospitali ya Rufaa ya Bugando kusubiri utambuzi na uchunguzi wa daktari.

RAIS MAGUFULI MGENI RASMI MAADHIMISHO YA 58 YA UHURU WA TANGANYIKA


RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt John Joseph Pombe Magufuli anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye maadhimisho ya sherehe za miaka 58 ya Uhuru na Miaka 57 ya jamhuri zitakazofanyika Kitaifa Mkoani Mwanza tarehe 9 Disemba 2019 katika viwanja vya CCM Kirumba.

Akiwasilisha taarifa hiyo mbele ya wanahabari Mkuu wa Mkoa wa Mwanza  John Mongella amesema kuwa sherehe hizo zinazofanyika kitaifa kwa mara ya kwanza katika Kanda ya Ziwa mkoa wa Mwanza ni za kihistoria na zitahusisha matukio mbalimbali yakiwemo Gwaride litakaloundwa na askari wa majeshi mbalimbali ya Ulinzi na Usalama nchini.

Aidha Mongella amewataka wananchi wa Mkoa wake na Kanda ya Ziwa kwa ujumla kuzichangamkia fursa mbalimbali zitakazojitokeza sanjari na kutumia maadhimisho hayo kama jukwaa la kutambulisha ustaarabu wa amani na utulivu walionao utakaotoa mwanya kuhamasisha wageni kufanya uwekezaji jijini humo.

CCM WAMPA ONYO BERNAD MEMBE.




Chama cha Mapinduzi (CCM) kimemuonya Benard Membe, kutokuwa juu ya katiba ya chama hicho.

Onyo hilo limetolewa leo  na Dk. Bashiru Ally, Katibu Mkuu wa CCM, wakati akizungumza katika mahojiano na kipindi cha Konani kinachorushwa na Kituo cha ITV  kupitia mitandao yao ya kijamii.

Dk. Bashiru ameeleza kuwa, kama Membe ataendelea kutofuata utaratibu, uongozi wa chama hicho utamlazimisha kufuata utaratibu.

“Membe ni mwanachama mwenye haki ya kikatiba lakini ana wajibu. Kwa hiyo kama anataka kuwa mwanachama wa CCM kama walivyo wengine, lakini wametupa ushindi tunaojivunia afutae utaratibu. Asipofuata utaratibu, atalazimishwa kufuata utaratibu,” ameeleza Dk. Bashiru.

Hata hivyo, Dk. Bashiru amesema Membe hakuwahi kujadiliwa katika vikao vya chama, licha ya kwamba hakuitikia wito wake, alipomtaka kuonana nae akiwa mkoani Geita.

“Hatukuwahi kumjadili na kwenye vikao hakuwahi kufika, kosa halifi kama jinai, kosa halifi unaweza ukadhani limekufa kumbe ni utaratibu wa wakati. Kupitia kwako, naomba kueleza wana CCM tuko makini kulinda utamaduni wa chama, na wanachama kutii viapo vyao,” amesema Dk. Bashiru.

RAIS DKT. MAGUFULI AKIWA NJIANI KUELEKEA KAHAMA - SHINYANGA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Wananchi mbalimbali waliomsubiri njiani akilekea Mkoani Shinyanga

Monday, November 25, 2019

VIJANA WANAOGOPA ZAIDI MIMBA KULIKO UKIMWI


NA ALBERT SENGO / GSENGOTv

Maambukizi mapya ya VVU bado yanatokea nchini. Takwimu zinaonyesha kuwa watu takribani 72,000 hupata maambukizi mapya nchini; hii ni sawa na wastani wa watu 6,000 kwa mwezi ama watu 200 kwa siku au watu 8 kwa saa. 
 Akimwakilisha Waziri wa Afya Dr. Ummy Mwalimu, mgeni rasmi wa Uzinduzi wa Wiki ya Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI duniani ambapo kilele chake kitakuwa Tarehe mosi Disemba, Mkuu wa mkoa wa Mwanza John Mongella amesema kutokana na  asili ya shughuli zinazofanyika, biashara na muingiliano wa idadi kubwa wa watu wanaoingia na kutoka, maeneo ya visiwa vya mkoa wa Mwanza yanatajwa kuwa sehemu hatarishi.

Aidha Unyanyapaa unatajwa kuwa tishio kubwa kuliko VVU na UKIMWI. Kama inavyojulikana mapambano ya Virusi vya Ukimwi huanzia pale mtu anapoitambua afya yake, Bi. Leticia Moris ni mwenyekiti wa baraza la watu wanaoishi na vurusi vya UKIMWI anasema Pamoja na watu kujitokeza kwa wingi katika mazoezi mbalimbali ya upimaji VVU, idadi kubwa ya watu wanashindwa kufuata dozi au kuendelea na dozi kwa kuhofia kuonwa na watu na kunyooshewa vidole, hivyo wamekuwa watoro wa dawa.

 "Kauli Mbiu ya Maadhimisho ya mwaka huu wa 2019 ni “JAMII NI CHACHU YA MABADILIKO; TUUNGANE KUPUNGUZA MAAMBUKIZI MAPYA YA VVU” Hivyo, msisitizo mkubwa katika Kauli Mbiu ya mwaka huu ni ushiriki wa jamii kwenye  kupunguza maambukizi mapya ya VVU kuanzia kwenye kuibua changamoto, kupanga mipango utekelezaji wa mipango na tathmini ya mipango hiyo.
Imefahamika kuwa ushirikishwaji wa jamii una tija kubwa unapofanywa kwa kuzingatia vipaumbele na mahitaji ya mahali husika. Jamii ndio yenye uwezo mkubwa wa ushawishi kwa mtu mmoja mmoja, familia na hata kwa viongozi wanaowawakilisha. 
Aidha, kauli mbiu hii inatilia mkazo kwenye kuunganisha nguvu katika kupunguza maambukizi mapya ya VVU na hasa kwenye kundi la vijana. 
Takwimu zinaonyesha kuwa kundi la vijana wa umri wa miaka 15 hadi 24 linachangia maambukizi mapya ya VVU kwa asilimia 40 na hivyo kulifanya kundi hili kuwa kwenye hatari kubwa zaidi ya kupata maambukizi ya VVU kuliko kundi lingine.
 "Vijana wa umri huu hofu yao kubwa siyo UKIMWI, siyo Magonjwa ya zinaa bali wanaogopa MIMBA" Amesema Bw. Yassin Ally ambaye ni Mkurugenzi wa Shirika la kupambana na Ukatili wa Jinsia, Utetezi wa Wanawake na Watoto (KIVULINI) na kisha kuongeza.
"Kwa hiyo utaona msisitizo mkubwa wengi wanadiriki mpaka kujifungia njiti mashuleni au nje ya shule wakikwepa mimba, ni lazma tutafakari tunabadilishaje mbinu ili kuokoa kizazi chetu" 

Hivyo Kauli mbiu hii inalenga kuhamasisha Wananchi, Makampuni na makundi mbalimbali ya jamii kushiriki kikamilifu kwenye shughuli za kudhibiti VVU/UKIMWI nchini ili kwa pamoja tuweze kuendana na mtazamo wa kimataifa wa kumaliza maambukizi mapya ya VVU ifikapo mwaka 2030.







 









WATOTO HAWA NI BALAA WAISHANGAZA MWANZA.



UKATILI haukubaliki.

VIDEO YA WIMBO WA HARMONIZE 'Uno' YAREJEA YouTube KWA KISHINDO.


Wimbo wa Msanii Harmonize, Uno tayari umerejeshwa kwenye mtandao wa YouTube tangu utoweke Novemba 20 mwaka huu.

Ikumbukwe video hiyo iliondolewa baada ya Producer Magix kudai kwamba biti ya wimbo huo ni sampo ya biti yake aliyotumia kwenye wimbo wa Dundaing wa King Kaka.

Video ya wimbo huu imereja saa chache mara baaada ya  Magix Enga kutangaza kumsamehe Harmonize.

“Kila mtu aseme Uno, sasa unapatikana youtube katika audio na video.” aliandika Enga  kwenye ukurasa wake wa Instagram. 


KWA UTHIBITISHO CHUNGULIA KICHUPA HICHO SASA HAPA CHINI.....

Sunday, November 24, 2019

9 WAPOTEZA MAISHA KATIKA MAFURIKO SENGEREMA


Watu 9 wamefariki dunia  kufuatia mvua kubwa iliyonyesha wilayani Sengerema mkoani Mwanza.

Mvua hiyo iliyoanza kunyesha majira ya saa 12 asubuhi hadi saa 7 mchana Jumamosi ya tarehe 23 Nov 2019, licha ya vifo hivyo pia imesababisha maafa ya mafuriko yaliyo ziacha kaya kadhaa zikiwa hazina makazi, upotevu wa mali na vyakula kuharibiwa na maji.
 John Mongella ni Mkuu wa Mkoa wa Mwanza ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa huo, ametia mkazo kwa kuwataka wananchi wote wanaoshi nyumba zilizo ndani au pembezoni mwa mkondo wa maji na maeneo mengine hatarishi kuhama mara moja katika kipindi hiki ambapo Mamlaka ya Hali ya Hewa Nchini imetoa angalizo kuwa KUTAKUWA NA VIPINDI VIFUPI VYA MVUA KUBWA VINATARAJIWA KATIKA BAADHI YA MAENEO YA MIKOA YA GEITA, MARA, SINGIDA,
SHINYANGA, TABORA, SIMIYU NA MWANZA.

Akitoa taarifa ya tukio hilo kwa mkuu wa mkoa wa Mwanza  John Mongella, mkuu wa wilaya ya Sengerema  Emmanuel Kipole, amesema miongoni mwa waliofariki wamo watoto watano wa kike wawili, wakiume watatu. 

Wengine wanne waliosalia watu wazima wote ni wanawake. 

  Athari na uharibifu mkubwa katika miundo mbinu ya barabara imejitokeza ikiwa ni pamoja na kukatika na kusombwa maji kwa daraja la Nyatukara lililopo katikati ya mji wa Sengerema kata ya Nyatukara mtaa wa Nyatukara.