ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, November 27, 2019

WATUHUMIWA WAWILI WA UJAMBAZI WAUAWA KWENYE MAJIBIZANO YA RISASI NA POLISI MWANZA.


Jeshi la Polisi mkoa wa Mwanza  limefanikiwa kuipata silaha moja aina ya bastola ikiwa na risasi tatu  zinatumiwa na wahalifu (majambazi) kwenye matukio mbalimbali kanda ya ziwa  baada ya watuhumiwa wawili wa ujambazi wanaume  ambao bado hawajafamika  majina wala makazi yao wanaokadiriwa kuwa na umri kati ya  miaka 25 hadi 30,  watuhumiwa hao walifariki wakati wakipelekwa hospitali baada ya majibizano ya kurushiana risasi na askari polisi baada ya kumtishia kumuua  kwa bunduki na baadae kupora pikipiki ya ” mwendesha bodaboda “.

Tukio hilo limetokea tarehe 26.11.2019 majira ya  23:40hrs huko maeneo ya Sweya – Fisheries wilayani Nyamagana, hii ni baada ya mwendesha pikipiki samwel masanja (bodaboda)   kuporwa pikipiki yake maeneo ya maina na watu hao  na baadae wananchi kutoa taarifa polisi.

Baada ya kupatikana kwa taarifa hizo askari  Polisi (makachero) walifanya ufuatiliaji wa haraka na baadae wakakutana na wahalifu  hao uso kwa uso maeneo ya Sweya, walipobaini kufuatiliwa walianza kuwarushia  risasi askari  na  askari walijihami na kufanikiwa  kuwajeruhi kwa  risasi  wahalifu hao ambao baadae  walifariki dunia  wakati wakipatiwa matibabu hospitali ya Bugando.

Katika eneo la tukio kumepatikana bastola moja aina ya Starbird yenye namba za usajili US Patten 2563720 pamoja na risasi tatu ndani ya magazine na pikipiki aina ya San LG nyekundu yenye namba za usajili MC 617 ABX ambayo ilikua imeporwa. 
Imepatikana  miili ya marehemu wote wawili imehifadhiwa Hospitali ya Rufaa ya Bugando kusubiri utambuzi na uchunguzi wa daktari.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.