ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, July 12, 2014

HII HAPA G.SENGO BONGO & NIGERIA MIXX 2014

Mara baada ya kiu na maombi ya mashabiki wengi wa burudani kutaka mixxing za Gsengo ilikuweza kusikiliza au pengine ku-download kwaajili ya kujilia burudani popote. Basi safari imeanza mdogo mdogo hebu tuanzie hapa. BOFYA PLAY KUSIKILIZA. 

LUIS SUAREZ AHAMIA BARCELONA

Liverpool imekubali kumuuza mshambulizi wake Luis Suarez kwa Barcelona kwa kima cha pauni milioni 75.
Mchezaji huyo wa Uruguay mwenye umri wa miaka , 27, ambaye amepigwa marufuku ya miezi miinne kwa kumuuma mchezaji mwenzake wa Italy, Giorgio Chiellini wakati wa mechi yao katika kombe la dunia, atasaini mkataba wa miaka mitano.
Suarez, ambaye aliingiza mabao, 31 katika ligi ya premier msimu uliopita, atasafiri kwenda Uhispania wiki ijayo kwa uchunguzi wa kimatibabu.
"Luis ana kipaji cha kipekee, na ninamshukuru kwa alivyotuwakilisha,'' alisema meneja wa Liverpool Brendan Rodgers.
Suarez anasema kuwa yeye pamoja na familia yake, daima watakuwa mashabiki wa Liverpool.
Suarez alikuwa mfungaji mabao mengi zaidi katika msimu uliopita na mshindi wa tuzo la mchezaji bora . Alitia saini mkataba na Liverpool alipotoka Ajax mwaka 2011 kwa pauni 22.7.
Alikuwa amesalia na miaka minne katika mkataba wake.
Hatua ya Suarez kuhamia Barcelona inampeleka karibu na mkewe pamoja na familia yake.
"Ni kwa majonzi mengi nimeamua kuondoka Liverpool, kwa maisha mapya nchini Uhispania na cha mno ni kwamba nimefurahishwa sana na mashabiki, '' alisema Suarez
"Ninatumai nyote mtaelewa uamuzi wangu. Klabu hii ilinifanyia kila nilichokitaka, lakini kucheza na kuishi uhispania, ilikuwa ndoto yangu kubwa. Muda huu uko sawa sana kwangu. ''
"Ninamtakia Brendan Rodgers na kikosi chake kila la heri na mustabali mwema. Klabu hiyo iko chini ya usimamizi mzuri na pia natumai watafanikiwa msimu ujao.''CHANZO BBC.

Friday, July 11, 2014

KUKU NILIYEMFUMA SENGEREMA...!!

Ni kuku asiyekuwa na manyoya amefumwa na kamera ya mtandao huu katika kijiji cha Busisi wilayani Sengerema mkoani Mwanza.
Manyoya au magoya kama wengine wanavyoyaita humsitiri kuku katika mvua, kujikinga na baridi kwa kumpa joto, hutumika kama kinga ya kuchomwa na vitu vyenye ncha kali kwani ngozi ya ndege ni laini, hivyo anapoingia kwenye purukushani hususani vichaka vyenye miiba hawezi kudhulika. Sasa anapokuwa katika hali hii ya kukosa magoya ni shida.
Ndege huyu yuko tayari tayari, ni kisu chako tu, haitaji kunyonyolewa!! Cha ajabu si mwewe wala ndege mwarabu (sijui ndiyo ndege aina ya Tai) wala wanyama wakali kama mbwa wote hawajawahi kumdhuru kuku huyu zaidi ya kumpita tu. Duh  na uroho wote walionao ..Maajabu..!

MIRADI 10 YA MAJI KUTEKELEZWA KWA SHILINGI BILIONI 29.1 WILAYANI SENGEREMA

Mbunge wa Jimbo la Sengerema William Ngeleja. 
NA PETER FABIAN, SENGEREMA.

HALMASHAURI ya Wilaya ya Sengerema kutekeleza miradi 10 ya maji kwa gharama ya shilingi bilioni 29.1kutoka katika chanzo cha maji cha ziwa Victoria.

Akihutubia kwenye mikutano ya hadhara nyakati tofauti wananchi wa Kata za Nyamatongo na Busisi wakati wa ziara yake ya kikazi, Mbunge wa Jimbo la Sengerema William Ngeleja aliwaeleza wananchi hao kwamba Halmashauri hiyo imepitisha kiasi cha fedha Shilingi bilioni 29.1 katika bajeti za fedha za mwaka 2013/2014 na 2014/2015 kutekeleza miradi hiyo.

“Baada ya kumaliza kero ya upatikanaji wa umeme kwenye maeneo mbalimbali ya vijiji sasa tunashughulika na kumaliza tatizo la upatikanaji wa maji safi na salama katika maeneo yanayokabiliwa na uhaba katika baadhi ya Kata ikiwemo Mji wetu wa Sengerema ambapo utekelezaji wake unaendelea,”alieleza.

Ngeleja aliwaeleza wananchi hao kuwa katika utekelezaji wa miradi hiyo iliyogawanywa sehemu kumi imelenga kumaliza kabisa kero hiyo ya maji ifikapo mwishoni mwa mwaka 2015 kama ilivyokusudiwa ili wanananchi katika maeneo hayo wapate maji safi na salama.

Katika kata ya Nyamatongo Mbunge alitoa kiasi cha shilingi 200,000. kwa ajili ya kununulia vipuli vipya vya Pampu ya kusukuma maji ambavyo vimeharibika na kusababisha kuwepo kero ya upatikanaji wa maji katani humo huku katika Kata ya Busisi akiahidi kufatilia.

Halmashauri ili kurejesha mashine mpya iliyokuwepo baada ya kuondolewa na kuretwa mashine mbovu na kusababisha maji kuwa tatizo.
Mbunge huyo akiwa Kata ya Busisi alitumia fursa hiyo kuwaeleza wananchi kuhusu miradi iliyokwishakuanza kutekelezwa itakayotekelezwa kupitia fedha za bajeti zilizopangwa kwa miaka miwili ambapo aliitaja maeneo ilipo na gharama itakatotumika.

Ngeleja aliwaeleza wananchi hao kuwa miradi 10 ya maji inayotekelezwa kwa kiasi cha shilingi bilioni 29.1 kutoka ziwa Victoria katika Kata za Nyasigu hadi Ngoma kwa gharama ya bilioni 1.6, Kata ya Chamabanda hadi Kasomeko kwa gharama shilingi milioni 500, Kata ya Nyatakubwa hadi Kasungamile kwa shilingi milioni 250.5.

Miradi mingine ni ilie iliyopo Kata ya Buyagu hadi Bitoto wa gharama ya bilioni 1.3, Kataya Chamabanda hadi Nyantakubwa wa gharama ya shilingi milioni 713.2, Kata ya Katunguru hadi Nyamutelela wa shilingi milioni 794.7, Kata ya Kakumulo hadi Nyampande wa shilingi milioni 408, Kata ya Chifumfu wa shilingi milioni 140.

Ngeleja alitaja mingine kuwa ni mradi wa maji wa Kata ya Kamanga hadi Nyamatongo wa shilingi milioni 405 na mradi mkubwa wa maji wa mjini Sengerema kutoka chanzo cha maji kilichopo kijiji cha Nyamazugo utakaogharimu kiasi cha bilioni 23sawa na USD milioni 14 ambapo baadhi itakamilika mwishoni mwa mwaka huu na mingine katikati ya mwaka 2015.

"Tutaendelea na utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo na kuzitafutia ufumbuzi kero na changamoto ambazo zitaonekana kukwamisha utekelezaji wa miradi hiyo ili kuwawezesha wananchi kupata huduma kwa wakati na zenye kiwango ambacho kinakubalika na hatuna muda wa kujadili baadhi ya maneno ya wapinzani wetu yanayolenga kutukatisha tamaa ili tusifikie lengo,"alisisitiza

THOMAS MASHALI KUZIPIGA NA MADA MAUGO NANE NANE KATIKA UWANJA WA TAIFA.


Rais wa TPBO Yassin Abdallah 'Ostadhi' akiwainua mikono juu mabondia Mada Maugo kushoto na Thomas Mashali baada ya kusaini mkataba wa makubaliano wa kupambana Sikukuu ya Nanenane (8/8/2014) katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam wakati wa tamasha la usiku wa matumaini lililoandaliwa na kampuni ya global publisher. 
Mabondia Mada Maugo na Thomas Mashali wakitunishiana misuli baada ya kusaini mkataba wa makubaliano ya kupambana Agost 8 katika uwanja wa taifa Dar es salaam wakati wa tamasha la matumaini siku ya Sikukuu ya Nanenane lililoandaliwa na kampuni ya global publisher.
Rais wa TPBO Yassin Abdallah 'Ostadhi' kushoto akimkabidhi sehemu ya fedha kidogo bondia Mada Maugo  kwa ajili ya maandalizi ya mpambano wake na Thomas Mashali utakaofanyika Agost 8 katika uwanja wa taifa Dar es salaam wakati wa tamasha la matumaini siku ya Sikukuu ya Nanenane lililoandaliwa na kampuni ya global publisher.
Rais wa TPBO Yassin Abdallah 'Ostadhi' kushoto akimkabidhi sehemu ya fedha kidogo bondia Thomas Mashali  kwa ajili ya maandalizi ya mpambano wake na Mada Maugo utakaofanyika Agost 8 katika uwanja wa taifa Dar es salaam wakati wa tamasha la matumaini siku ya Sikukuu ya Nanenane lililoandaliwa na kampuni ya global publisher.
Mabondia Mada Maugo na Thomas Mashali wakitunishiana misuli baada ya kusaini mkataba wa makubaliano ya kupambana Agost 8 katika uwanja wa taifa Dar es salaam wakati wa tamasha la matumaini siku ya Sikukuu ya Nanenane lililoandaliwa na kampuni ya global publisher Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

NGUVU ZA KIUME ZIKO NDANI YA KAZI ZA WANAUME = UMIA UJAE..!!

Moja ya kazi zanye kuimarisha afya ya mwanaume.
@udakuzi mtandaoni
SUALA la nguvu za kiume kwa sasa limeshakuwa ishu kubwa kwa vijana wengi wa sasa, kwa utafiti uliofanywa mwaka 2013 na shirika la Afya duniani unaonesha kuwa zaidi ya asilimia themanini ya wanawake hawatoshelezwi kimapenzi.

Moja ya sababu kubwa inayochangia kutotoshelezwa huku kwa hawa wadada ni tatizo la upungufu wa uwezo wa mwanaume kumnyuka mwanamke kisawasawa ili kumkata ny3g3 (3=e) kabisa kwa kufika kileleni.

Wanaume wengi wa sasa wamekuwa wabovu kabisa katika kusimamisha mashine zao kiasi cha kuwa hata mdada awe mkali na mwenye mvuto namna gani amejitahidi sana kumtandika basi bao tatu kisha kitu inalala kabisaaa, tena kila bao huchukua dakika mbili tayari ameutupa ...da..da..da duh!
Zifuatazo ni njia chache za asili zilizo salama kabisa za kuamsha nguvu za kiume maradufu.


*AINA ZA VYAKULA
Tusidanganyane chakula ndio kila kitu mwilini,vyakula vya nafaka zisizokobolewa ni vizuri sana kuupa uume nguvu kuliko unavyodhani. Hivyo kama ni ugali basi penda sana kula ugali wa dona na sio sembe kwani sembe huwa haina kiini cha njano chenye protini na wanga ambacho ni silaha sana katika kuutia nguvu uume na mwili kwa ujumla.

Matunda pia kama matango,karoti ni muhimu sana katika kujenga nguvu za kiume.Vyakula vingine ni kama mihogo mibichi,magimbi nk. Lazima uwe na utamaduni wa kutumia aina hii ya vyakula katika maisha yako ya kila siku, sio eti leo una mechi na mdada ndio unajifanya kufakamia mamihogo loo siku hiyo!

*MAZOEZI
Mazoezi ya viungo ni muhimu sana kwani hufanya mwili uwe fit na hivyo huimarisha hata uume na kuufanya usilale kirahisi pale unapokuwa katika show na mrembo. Kufanya kazi ngumu, Push up, Kukimbia, Kurukaruka na Mazoezi mengine mengi ni muhimu sana.

*ACHANA NA UNYWAJI WA POMBE ULIOPITA KIASI
Pombe ni hatari sana na inadhoofisha sana nguvu za kiume hivyo chunga sana unywaji wa pombe uliopitiliza kwani ipo siku utajikuta unamwangalia tu mkeo kama dada ako vile wakati yeye nyege zimempanda balaa,matokeo yake itabidi achapwe na njemba zinazojua shughuli huko nje.

*ACHANA NA DAWA ZA KUONGEZA NGUVU ZA KIUME
Hizi dawa ni hatari sana hasahasa zile za hospitali kwani maranyingi zimetengenezwa kwa kemikali ambazo huamsha vichocheo mwili kwa muda flani lakini baada ya muda  tatizo litaongezeka maradufu kwani ni tiba kwa muda mfupi tu.

NGELEJA AONYA WATUMISHI NA WATENDAJI WATAKAO CHAKACHUA FEDHA ZA MIRADI SENGEREMA.

Mbunge wa Jimbo la Sengerema William Ngeleja (kushoto) akimtaka Mhandisi wa Idara ya Maji Halmashauri ya wilaya ya Sengerema Barnabas Gishini kutoa ufafanuzi kuhusu hatma ya utatuzi wa kero ya maji inayo kikabili kijiji cha Busisi, ni katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Busisi jana.
Wananchi wakisikiliza kwa umakini uwasilishaji Kero kwenye mkutano wa mbunge wa Jimbo la Sengerema William Ngeleja katika kijiji cha Busisi jana.
Sehemu ya mkutano.
Wazee wa mji.

Viongozi na Baraza la wazee.
Wananchi wakisikiliza kwa umakini uwasilishaji Kero kwenye mkutano wa mbunge wa Jimbo la Sengerema William Ngeleja katika kijiji cha Busisi jana.
Viongozi meza kuu waliokuwa kwenye ziara ya  mbunge ya kukagua miradi ya Maendeleo jimboni humo katika kata za Busisi, Nyamatondo na nyingine jimboni humo.
Robert Mathayo akitoa Kero ya uhaba wa maji, ardhi na zahanati kwenye mkutano wa mbunge wa Jimbo la Sengerema William Ngeleja katika kijiji cha Busisi jana. 
Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Sengerema Mathew Lubongeja akifafanua jambo kwa wananchi wa kijiji cha Busisi wakati alipotakiwa kufanya hivyo na mbunge Ngeleja alipokuwa kwenye ziara ya kikazi jimboni humo.
NA PETER FABIAN, SENGEREMA.  
MBUNGE wa Jimbo la Sengerema William Ngeleja amecharukia baadhi ya watendaji wa Halmashauri Wilaya hiyo wanaokwamisha utekelezaji wa Ilani na wanaochakachua fedha za miradi ya maendeleo.

Ngeleja alitoa kauli hiyo juzi wakati akihutubia wananchi wa kijiji cha Busisi Kata ya Busisi wilayani humo wakati wa ziara yake ya kikazi kukagua miradi ya maendeleo iliyotekelezwa na Halmashauri na kusikiliza hoja za wananchi katika maeneo mbalimbali ya Kata za jimbo hilo.
Mbunge huyo alisema kwamba Halmashauri hiyo itaendelea kuwawajibisha watumishi na watendaji wanaokwamisha utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2010/2015 na wanaochakachua fedha kwa kutumia nafasi zao za kiutendaji na kusababisha kukwamisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo na hata kutokamilika kwa wakati na chini ya kiwango.

“Tutaendelea kuwachukulia hatua za kimaadili ikiwa ni pamoja na kuwawajibisha watumishi na watendaji wabadhilifu wa fedha za miradi ya maendeleo katika maeneo mbalimbali ya Halmashauri yetu ambao wanasababisha wananchi kuilalamikia Serikali ya Chama Cha Mapinduzi iliyopo madarakani kwa kukosa huduma muhimu kwenye maeneo yao,”alisema.

Akizungumzia watumishi hao alisema kwamba hadi sasa Halmashauri hiyo kupitia Baraza la Madiwani kwa kushirikiana na viongozi wa serikali na Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (TAKUKURU) na Kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya imewawabisha tatumishi wapatao 13 waliothibitika kutenda ubadhilifu wa mamilioni ya fedha za miradi ya maendeleo.

“Hapa Busisi tulizindua mradi wa maji toka ziwa Victoria tangu mwaka jana mwezi wa Februari lakini leo Pampu iliyokuwa inasukuma maji kwenda kwenye tanki iliondolewa na watendaji wa maji na kuletwa Pampu mbovu ambayo karibu mwaka hakuna hata kinachoendelea na kusababisha wananchi kupata usumbufu wa maji wakati wako jirani na ziwa na majibu hayatulidhishi,”alisisitiza.

 Hatua hiyo inafuatia majibu ya Mhandisi wa Idara ya Maji wa halmashauri hiyo Barnabas Kishina kushindwa kutoa majibu sahihi, wakati alipotakiwa na Mbunge Ngeleja kujibu kwa wananchi waliouliza swali la kero ya kutopatikana maji wakati Pampu yake mpya ilitolewa na kuletwa mbovu ya zamani jambo ambalo liliwafanya wananchi kulalamika na kudai kupata adha ya upatikanaji wa maji safi.

Ngeleja aliwabeza wapinzani wake wa kisiasa jimboni humo wanaopita kumchafuwa na kumtolea lugha ya kejeli na matusi kwa hajafanya kitu huku yeye akitaja kutekeleza miradi ya umeme katika kila kijiji jimboni humo, maji na sasa anaendelea kumalizia baadhi ya miradi ya Afya, Elimu na Miundombinu ya barabara baada ya Halmashauri kununua Greda kufanya kazi hiyo.

MARY NAGU MGENI RASMI KONGAMANO LA NNE LA KITAIFA LA MAKATIBU MUHTASI TANZANIA LEO JIJINI MWANZA.

Pichani kushoto ni Waziri wa Uweshaji na Uwekezaji Ofisi ya Waziri Mkuu,Mh.Mary Nagu ambaye ndiye mgeni rasmi wa Kongamano la nne laKitaifa la Makatibu Muhtasi Tanzania (TAPSEA),akizungumza jambo na Naibu Waziri wa Katiba na Sheria ambaye pia ni Mshauri wa Masuala ya Kisheria wa TAPSEA wakati alipokuwa akiwasili kwenye ufukwe wa hotel ya Malaika, ambako Kongamano hilo linafanyika leo jijini Mwanza.

Pichani kushoto ni Waziri wa Uweshaji na Uwekezaji Ofisi ya Waziri Mkuu,Mh.Mary Nagu akizungumza jambo na Naibu Waziri wa Katiba na Sheria ambaye pia ni Mshauri wa Masuala ya Kisheria wa TAPSEA wakati alipokuwa akiwasili kwenye ufukwe wa hotel ya Malaika,ambako Kongamano hilo linafanyika leo jijini Mwanza,pichani kati Mwenyekiti wa Makatibu Muhtasi Tanzania (TAPSEA),Bi.Pilly Mpenda wakiwa wamezungukwa na washirki wengine mbalimbali wakiwasili kwenye ufukwe wa hotel ya Malaika,ambako Kongamano hilo linafanyika leo jijini Mwanza. 
Ngoma ya asili ya wasukuma ikipigwa kuwakaribisha washiriki mbalimbali waliokuwa wakiendelea kuwasiliasubuhi hii kwenye kongamanno hilo jijini Mwanza.
Washiriki mbalimbali wakiendelea kujiandikisha kwa ajili ya ushiriki wa kongamano hilo
Mazungumzo ya utaratibu wa washiriki wa Kongamano hilo ukiendelea kuwekwa sawa na waandaaji .
Waandaji wa Kongamano hilo wakiendelea kujadiliana jambo.
Washiriki wa kongamano hilo wakiwa katika picha ya pamoja.
Washirii wa kongamano hilo wakijadiliana jambo kabla ya kuanza kwa mkutano huo.
Washiriki wa Kongamano hilo wakitabasamu mbele ya Camera ya Globu ya Jamiii.
Wadau wa TAPSEA wakiwa katika picha ya pamoja.
Washiriki wakendelea kuwasili kwenye ufukwe wa hotel ya Malaika,ambako Kongamano hilo linafanyika leo jijini Mwanza.
PICHA NA MICHUZI MEDIA GROUP-MWANZA.

AIRTEL NA MOJIFA WAANZA USHIRIKA WA KUTUNZA MAZINGIRA MIKOANI... WAANZIA ARUSHA.

Mkuu wa shule ya sekondari Sing’isi mwalimu Upendo Kanana akipanda mti katika viwanja vya shule ya sekondari Sing’isi wakati wa siku maalumu ya upandaji miti zoezi lililoendeshwa na wafanyakazi wa kampuni ya AIRTEL Arusha  huku wanafunzi wa shule hiyo nao wakishiriki tendo hilo jana
Na Mwandishi wetu.
Kampuni ya simu za mkononi Airtel kwa kushirikiana taasisi isiyo ya kiserikali inayojihusisha na shughulu za utunzaji wa mazingira ‘Sustainable Enviromental’ ya Moivaro Jitegemee Family (MOJIFA) leo wamefanya shughuli ya upandaji miti kwa shule za sekondari mkoani Arusha katika kijiji cha Sing’isi wilayani Arumeru mkoani Arusha

Airtel na taasisi hiyo binafsi na  wadau mbalimbali katika utunzaji wa mazingira wamechukua hatua stahiki za kuhifadhi mazingira ili  kupunguza wimbi la uharibifu wa vyanzo  vya maji katika  maeneo mbalimbali nchini.

tukio hilo maalumu la upandaji wa miti  lililoongozwa na  wafanyakazi wa kampuni ya simu za mkononi ya Airtel mkoa wa Arusha, katika shule ya sekondari  Sing’isi.

Meneja biashara na mauzo kanda ya kaskazini Brighton Majwala alisema “airtel imekuwa mdau mkubwa wa maendeleo ya elimu nchini na safari hii tumeamua kupanda miti hii ili  kuwahamasisha wanafunzi kutambua umuhimu wa kutunza mazingira  ambayo yana mchango wa moja kwa moja katika kujifunza kwao”
Nae  mkuu wa shule ya sekondari Sing’isi  upendo Kakana ameishukuru kampuni ya airtel kwa kuendesha zoezi hilo  katika shule hiyo na kuongeza kuwa kijografia shule hiyo ipo katika eneo lenye upepo mkali wa mara kwa mara na kwa maana hiyo kuwepo kwa miti ya kutosha  katika eneo la shule kutasaidia kuzuia athari zinazoweza kujitokeza kutokana na upepo.

DIWANI wa Sing’isi mh, Peter kiyungai alitoa rai kwa wananchi wote kuendelea na zoezi la kupanda miti kama walivyofaya Airtel na kutunza mazingira hasa maeneo ambayo ni vyanzo vya maji kwani kwa kutofanya hivyo ni dhahiri tunahatarisha maisha yetu wenyewe kwa kuwa hatar ya kukosekana kwa maji hayo kutokana na uharibifu wa mazingira huenda ikapelekea hata kupotea kwa Amani ya maeneo husika 
Mgeni Rasmi wa tukio hilo maalum Bi Recho Ngowi ambae ni Afisa mtendaji wa kata ya Sing’isi aliipongeza Airtel na taasisi hiyo binafsi ya MOJIFA pamoja na  wadau mbalimbali wa maendeleo  waliohudhuria katika upandaji miti na utunzaji wa mazingira katika kijiji cha Singisi

“Naahidi kuwa jitihada hizi zitaendelezwa na serikali ili kuhakikisha nchi haiingii katika changamoto ya kukosa uhai kwa janga la uharibifu wa mazingira yetu” alisema Bi Recho

Kampuni ya simu za mkononi tawi la Arusha kwa kushirikiana na taasisi ya MOJIFA wamepanda jumla ya miti 200 na kuahidi  zoezi hilo kuwa endelevu katika maeneo mengine yenye uhitaji wa miti.

STEVE NYERERE AWAANDALIA CHAKULA CHA JIONI WASANII WA FILAMU NA WADAU

Rais wa Bongo Movie, Steve Nyerere akizungumza machache wakati wa hafla aliyowakaribisha chakula cha jioni wasanii wa Filamu na wadau mbalimbali wa filamu Bongo ikiwa ni kuungana na wenzao waliokatika mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan. Hafla hiyo ilifanyika ndani ya Great Wall Restaurant iliyopo Osterbay jijini Dar esa Salaam.

Wageni waalikwa wakisikiliza kwa makini maneno yaliyokuwa yakitolewa na Rais wa Bongo Movie, Steve Nyerere.
Wasanii wakipata maakuli...
Wolper na Kajala wakila chakula wakati wa hafla hiyo.…
Talks n' talk...za hapa na pale.
Mazungumzo ya hapa na pale hayakukosa...
Kila mmoja aliona ni wakati mwafaka kuongea na mwenzake aliyepotezana nae miaka kadhaa.
Ilikuwa ni furaha maana wasanii wengine kuonana huwa ni mara chache chache.
Jini Kabula, Mariam Mndeme na Isabela Mpanda wakijumuika katika hafla hiyo.
 Meza ya waheshimiwa...
Ester akiwa na rafiki yake Zilpa.
Jose Mara nae hakuwa nyuma...
Samaki aina ya Kaa.
Chaz Baba akipakua chakula.
 Zungu wa GPL akiwa na Mkurugenzi wa Kajunason blog, Cathbert Angelo pamoja na msanii Rich.
Msanii Nguri wa Muziki wa Bongo Fleva, Profesa J akipata chakula....
Msanii Haji akimsurubisha samaki aina ya Kaa.
Mshereheshaji wa hafla hiyo akieleza machache. 
Msanii JB akiwasisitiza wenzake suala la upendo miongoni mwao.
Rais wa Bongo Movie, Steve Nyerere akizungumza machache wakati wa hafla aliyowakaribisha chakula cha jioni wasanii wa Filamu na wadau mbalimbali wa filamu Bongo ikiwa ni kuungana na wenzao waliokatika mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan. Hafla hiyo ilifanyika ndani ya Great Wall Restaurant iliyopo Osterbay jijini Dar esa Salaam.
Malkia wa Mipasho, Bi. Khadija Kopa akilto nasaha kwa wasanii wenzake pamoja na wadau waliojumuika katika hafla hiyo.
Msanii Nguri wa Muziki wa Bongo Fleva, Profesa J akitoa machache. 
Wasanii wakipongeza Msanii Nguri wa Muziki wa Bongo Fleva, Profesa J mara baada ya kutoa neno zito.
Mwandishi Sauda Mwilima nae alikuwa ni miongoni mwa wadau walialikwa. 
Chaz Baba nae hakuwa nyuma kutoa shukrani zake za pekee.
Mwalimu Julio alikuwa ni miongoni mwa wageni waliofika na kutoa maneno/wosia mzito kwa wasanii.
Mboni Masimba akieleza machache na kutoa shukrani zake kwa Rais wa Bongo Movie Steve kumutambua kuwa yeye mdau muhimu katika tasnia hiyo.
Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Mbeya, Amani Kajuna alikuwa ni miongoni mwa wageni waalikwa waliohudhuria katika hafla hiyo na kuwakaribisha wasanii hao mkoani kwake ili waweze kufungua milango ya uwekezaji.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) Sixtus Mapunda akiwasisitiza vijana namna ya kufanya sanaa yao ikawaletea matunda mema.
Zamaradi akizungumza machache na wasanii.
Mboni akipata ukodak na Zungu wa GPL.
Furaha za hapa na pale nazo zilitanda. 
PICHA ZOTE NA CATHBERT KAJUNA WA KAJUNASON BLOG.