KLABU ya Yanga imempa mkono wa kwaheri Kocha wake Maaidizi, Filipe Duarte da Silva Pedro baada ya miezi miwili na ushei tangu awasili na nafasi yake inachukuliwa na Mreno mwingine, Marques Pereira Da Silva.

Kumekuwa na mjadala baada ya ziara ya YouTuber maarufu IShowSpeed nchi jirani, kuwa ziara hiyo ilikuwa ya kulazimisha ili kupandisha sifa za utalii wa majirani.
Pamoja na kelele zao za mtandaoni takwimu za Tanzania zinaonesha kutomhitaji IshowSpeed katika kutangaza utalii wake.
"Hatuogopi mbinu za kutafuta umaarufu, kwani ukweli wa mazingira yetu, kutoka Zanzibar hadi Serengeti, hauwezi kununuliwa kwa helikopta ya kukodi," alimalizia mchambuzi mmoja wa masuala ya utalii.
Hata hivyo, Rais Samia Suluhu Hassan, katika hotuba yake ya Sherry Party, ametoa jibu la kishindo kupitia takwimu.
"Tanzania haihitaji kutengeneza hadithi za kufikirika," alisema Rais Samia huku akionyesha kuwa mapato ya utalii yamefikia Dola bilioni 4 mwaka 2025. Huku majirani wakihaha kutafuta umaarufu kupitia TikTok na YouTube, Tanzania imejikita katika kuboresha miundombinu kama SGR na viwanja vya ndege ili kumfanya mtalii wa kawaida awe balozi wa nchi.
Kilimanjaro ni Moja, na Ipo Tanzania
Ni kama akijibu hoja za baadhi ya nchi jirani kujaribu kujimilikisha alama za Tanzania kama Mlima Kilimanjaro na utamaduni wa Kimaasai, Rais amesisitiza kuwa Dira ya 2050 italinda rasilimali hizo kama mali ya taifa. "Tunajiuza kwa kile tulichonacho. Utulivu wetu na asili yetu ndiyo sumaku kubwa zaidi duniani," aliongeza.
Mkakati wa 'Royal Tour' Unadunda
Wakati ziara za mastaa wa mtandaoni kama IShowSpeed zikiwa na maisha mafupi (viral for a day), mkakati wa Tanzania kupitia The Royal Tour unaendelea kuleta watalii wa kudumu na wawekezaji wakubwa.
Uchaguzi Uganda 2026: Museveni achukua uongozi wa mapema wa kura zilizohesabiwa kufikia sasa
Jaji Simon Byabakama, mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Uganda amesema matokeo hayo yanazingatia vituo 133 vya kupiga kura na yanawakilisha asilimia 0.26 ya jumla ya kura zilizopigwa.
Wakati huo huo Rais Museveni amewaonya raia wanaopanga kuandamana siku ya Jumanne akisema kwamba 'wanacheza na moto'.
Mgongano unaokuja baada ya wimbi la maandamano ya kupingana na serikali yaliyoigonga nchi ya jirani ya Kenya, ambapo watu wasiopunguwa 50 walipoteza maisha katika mapambano na vyombo vya usalama, kulingana na takwimu zilizo chapishwa na Tume ya Kitaifa ya Haki za Binadamu.
Rais Yoweri Museveni, 79, aliyekuwa akitawala taifa la Uganda kwa karibu miongo minne kwa mkono wa chuma, alisema katika hotuba iliyorushwa hewani Jumamosi kuwa maandamano ya kupambana na ufisadi hayataruhusiwa.
“Ana haki gani… unao nayo wa kuleta tabia ya maangamizi? … Tunaanza kuzalisha chakula cha bei rahisi, watu wengine katika sehemu nyingine za dunia wanaachu (kuwa na njaa)… wewe unataka kutulazimisha kuvuruga. Unacheza na moto kwa sababu hatuwezi kukuruhusu kutuvuruga,” Museveni aliweka maneno yake katika hotuba iliyotumia saa tatu.
Wengi wa vijana wa Uganda wanasema kupitia mitandao ya kijamii kuwa wanapanga kuendelea na maandamano hadi ofisi za bunge la taifa, licha ya jeshi la polisi kukataa kutoa vibali vya maandamano.
Jeshi la Polisi wa Uganda liliutanabaisha umma kwa maandamano yaliyopangwa kuwa “yanayoweza kusababisha vurugu” katika taarifa ya Jumatatu, likionya kwamba “hawatahimili tabia ya utulivu mbovu.”
Baadhi ya waandamanaji vijana waliodhamiria kujiunga na maandamano hayo ya Jumanne wameanza kutupia picha zao kwenye mitandao ya kijamii, wakihanikiza raia wenzao nao wafanye vivyo hivyo ili wapate kuwataja wakirudi salama nyumbani.
Na hata ikitokea wakapotea basi ijulikane ni kipi kiliwapoteza.
Penalty imeamua matokea Azam Fc 4 - 5 Yanga Sc
Okelo Mechi 0 Kombe 1
TIMU ya Yanga SC imefanikiwa kutwaa Kombe la Mapinduzi baada ya ushindi wa penalti 5-4 dhidi ya Azam FC kufuatia sare ya bila kufungana ndani ya dakika 120 jioni ya leo Uwanja wa Gombani, Pemba.
Shujaa wa Yanga SC leo ni mlindamlango, Abdultwalib Mshery aliyeokoa penalti ya beki wa kati raia wa Ivory Coast, Ahoutou Angenor Landry Zouzou.
Waliofunga penalti za Yanga ni washambuliaji Emmanuel Mwanengo, Mzimbabwe Prince Dube, viungo Pacome Zouzoua, Mudathir Yahya na beki na Nahodha, Bakari Nondo Mwamnyeto.
Waliofunga penalti za Azam FC ni kiungo, Yahya Zayd, beki Twalib Nuru, kiungo raia wa Mali, Sadio Kanoute na mshambuliaji Ngita Kamanya.
Yanga ingeweza kuondoka na ushindi mapema tu kama kiungo wake Muivory Coast, Peodoh Pacome Zouzoua amgefunga penalti dakika ya 115, lakini ikaokolewa na kipa Aishi Salum Manula.
Aidha, Yanga SC pia ilishindwa kutumia mwanya wa Azam FC kucheza pungufu tangu dakika ya 55 baada ya winga wa Kimataifa wa Mali, Cheickna Diakité kutolewa kwa kadi nyekundu kufuatia kuonyeshwa kadi ya pili ya njano.
Katika kuadhimisha Siku ya Mapinduzi ya Zanzibar, jiji la Mwanza linawaletea burudani ya kipekee, mechi ya kirafiki ya kihistoria… Mashabiki wa Simba vs Pamba Jiji!
Watachuana mastaa wa zamani waliowahi kung’ara kwenye timu hizi mbili maarufu nchini – ni kumbukumbu, ni burudani, ni hadithi za mpira zinazofufuka tena!
Na si mpira tu! Kutakuwa na michezo ya kina dada, kina mama, zawadi kibao na burudani ya nguvu kwa familia nzima!
Jumatatu ya tarehe 12 Januari 2026, kuanzia saa nane mchana, pale Uwanja wa Nyamagana – usikose kushuhudia historia ikiandikwa upya!
MAPINDUZI DAY – Mwanza inasherehekea kwa mshikamano, amani na burudani ya kufungia mwaka!
Mgeni rasmi: Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mh. Said Mtanda
Kampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imeendelea kuthibitisha dhamira yake ya uwajibikajo kwa jamii kwa kutoa msaada wa hundi ya shilingi milioni 50 kwa kituo cha kulelea watoto yatima cha Moyo wa Huruma wakati wa sherehe za kuukaribisha mwaka mpya 2026 zilizofanyika kituoni hapo, mkoani Geita mwishoni mwa wiki.
Akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi mfano wa hundi hiyo kwa uongozi wa kituo hicho, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa GGML, Bw. Duan Campbell, amesema uwepo wa GGML katika moa wa Geita haujikiti tu katika uchimbaji wa dhahabu bali pia katika kuigusa jamii kwa kujenga jamii yenye afya, matumaini na fursa hasa kwa Watoto walioko katika mazingira magumu.
“Kujenga jamii yenye afya na yenye matumaini ni sehemu ya jukumu letu kama kampuni inayojishughulisha na uchimbaji wa madini. Uwekezaji wetu katika maendeleo ya kijamii unaendelea kuwa kichocheo cha ukuaji wa ndani, kikanda na kitaifa. Tunajivunia kushirikiana na Moyo wa Huruma na kuona jinsi maisha ya Watoto yanavyobadilika kwa misaada na fursa wanazopata.
“Tunajisikia fahari kuona watoto wanaolelewa katika kituo hiki wanapata mafanikio, ikiwemo wale wanaohitimu katika vyuo vikuu,”
“Hivyo, kama wadau wa maendeleo ya jamii, GGML tutaendelea kuhakikisha kuwa kituo hiki kinapata mafanikio zaidi na kushirikiana na Serikali katika kutokomeza watoto wa mitaani,” amesema Bw. Campbell.
Kituo cha Moyo wa Huruma kilianzishwa mwaka 2006 kupitia ushirikiano kati ya GGML, Jimbo Katoliki la Geita na Halmashauri za Serikali ya mkoa wa Geita, kama sehemu ya mkakati wa muda mrefu wa kukabiliana na changamoto za watoto yatima na wanaoishi katika mazingira magumu—ikiwemo watoto waliopoteza wazazi kutokana na VVU/UKIMWI.
Kupitia mfuko wa GGML Kili Challenge Against HIV & AIDS, GGML imekuwa ikishirkiana na wadau mbalimbali ikiwemo Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS) kukusanya rasilimali kwa kupanda Mlima Kilimanjaro kwa lengo la kusaidia watu wanaoishi na VVU pamoja na taasisi zinazohudumia makundi yaliyo katika hatari, ikiwemo Kituo cha Moyo wa Huruma. Juhudi hizi zimewezesha kujengwa kwa kituo hicho ambacho kimeweza kukua kutoka kulea watoto 12 mwaka 2006 hadi kuwahudumia zaidi ya watoto 100 kwa sasa, wakiwemo wahitimu wa vyuo vikuu na watumishi wa umma.
Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mh. Martine Shigela ambaye alikuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo, ameipongeza GGML kwa kuendelea kusaidia makundi mbalimbali katika jamii.
“Napenda kuwapongeza GGML kwa ibada hii ya kulea kituo hiki chenye watoto wakiwemo watoto wadogo na wakubwa ambao baadhi yao ni wahitimu wa vyuo vikuu mbalimbali wanaosomea masomo ya Sayansi na wale walioajiriwa Serikalini ambao wamepitia katika kituo hiki,” amesema RC Shigela
Akizungumza katika hafla hiyo, Askofu wa Jimbo Katoliki la Geita, Askofu Flavian Kasala amesisitiza umuhimu wa jamii kuendelea kushirikiana katika kujiepusha na kuzuia vyanzo vinavyopelekea ongezeko la watoto wanaoishi katika mazingira magumu ambao hukosa msaada na hatimaye kutapakaa mitaani.
“Matatizo mbalimbali katika jamii ikiwemo changamoto zinazotokana na uzazi katika umri mdogo, maambukizi ya Virusi vya UKIMWI na ugumu wa maisha yamepeleka uwepo wa watoto wa mitaani wenye uhitaji kutoka katika jamii”
“Hivyo, kituo kama hiki, kinatupa somo la kuwapa faraja watoto wenye uhitaji na kuweka jitihada za makusudi za kuzuia ongezeko la watoto hao wanaoishi katika mazingira magumu,” amesema Askofu Kasala.
Akizungumza mara baada ya hafla ya kukabidhi hundi, Mwakilishi wa GGML kutoka idara mahusiano Mussa Shunashu ameeleza majukumu ya GGML katika kituo hicho kilichoanzishwa kwa ushirikiano kati ya GGML, Jimbo Katoliki la Geita na Halmashauri za Mkoa wa Geita.
“GGML katika kuanzisha na kuendeleza kituo hiki, ilikuwa na wajibu wa kutoa fedha na halmashauri wakati huo ilikuwa na wajibu wa kutoa eneo na Jimbo Katoliki la Geita lilikuwa na wajibu wa kusimamia malezi bora na tunashukuru mpaka leo hii kituo hiki kinaendelea kutoa huduma,”
“Kama ilivyo katika mikoa mingine, mkoa wa Geita pia una watoto yatima, ambao walipoteza wazazi/ walezi kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo ugonjwa wa UKIMWI, hivyo, tuliamua kuwa na kituo hiki kwa msaada wa malezi na elimu kwa watoto wenye uhitaji,” amesema.
Katika hafla hiyo ya kuadhimisha Mwaka Mpya 2026, GGML pia ilitoa zawadi mbalimbali, kuandaa burudani, michezo na chakula kwa watoto na walezi wao, pamoja na mazungumzo ya faraja yaliyoimarisha dhana ya malezi ya pamoja na mshikamano wa kijamii.
Mmoja wa watoto wanaolelewa katika kituo hicho (jina limehifadhiwa) amesema msaada unaotolewa na GGML na wadau wengine umewapa nguvu ya kuota ndoto kubwa.
“Tunajisikia kama tupo nyumbani. Tunathamini sana kuona kuna watu wanaojali maisha yetu na mustakabali wetu,” amesema mtoto huyo.
Hatua hii inaendelea kuonesha utekelezaji wa sera ya Uwajibikaji kwa Jamii (CSR) ya GGML, inayolenga kuimarisha afya, elimu na ustawi wa watoto na familia katika mkoa wa Geita na Tanzania kwa ujumla, kwa kutambua kuwa maendeleo endelevu huanza na uwekezaji kwa watu.
Daktari mmoja alisema hospitali ya macho ya Tehran ilikuwa iko katika hali ngumu, huku BBC pia ikipokea ujumbe kutoka kwa daktari katika hospitali nyingine ikisema haikuwa na madaktari bingwa wa kutosha kukabiliana na ongezeko la wagonjwa.
Siku ya Ijumaa, Rais wa Marekani Donald Trump alisema Iran ilikuwa katika "matatizo makubwa" na akaonya "ni vyema isianze kufyatua risasi kwa sababu sisi pia tutaanza kufyatua risasi".
Katika barua kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, Iran iliilaumu Marekani kwa kuyageuza maandamano hayo kuwa kile ilichokiita "vitendo vya uasi na uharibifu mkubwa".
CHANZO BBC SWAHILI

