Huku maandamano nchini Iran yakiendelea na mamlaka ya Iran ikitoa maonyo yaliyoratibiwa kwa waandamanaji, daktari na muuguzi katika hospitali mbili waliiambia BBC kwamba vituo vyao vya matibabu vilikuwa vimejaa watu waliojeruhiwa.
Daktari mmoja alisema hospitali ya macho ya Tehran ilikuwa iko katika hali ngumu, huku BBC pia ikipokea ujumbe kutoka kwa daktari katika hospitali nyingine ikisema haikuwa na madaktari bingwa wa kutosha kukabiliana na ongezeko la wagonjwa.
Siku ya Ijumaa, Rais wa Marekani Donald Trump alisema Iran ilikuwa katika "matatizo makubwa" na akaonya "ni vyema isianze kufyatua risasi kwa sababu sisi pia tutaanza kufyatua risasi".
Katika barua kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, Iran iliilaumu Marekani kwa kuyageuza maandamano hayo kuwa kile ilichokiita "vitendo vya uasi na uharibifu mkubwa".
CHANZO BBC SWAHILI
Tupe maoni yako

0 comments:
Post a Comment