Saturday, December 4, 2010
MASHINDANO YA MITUMBWI YA BALIMI YAFANA.
Friday, December 3, 2010
"MENU YA STONE CLUB WIKI NI NOUMAa!!!"

IJUMAA NA JUMAMOSI KANBAAAaa!
ONCE AGAIN THA SAGA CONTINUE TONIGHT PALE CHIMBO LA KATI NAZUNGUMZIA 'STONE CLUB'
ITALETA MAANA ZAIDI UKIJUMUIKA NASI!!!!!!
GATE PASS NI 5,000tsh.
URUSI KUANDAA KOMBE LA DUNIA 2018

Aidha Qatar nayo imechaguliwa kuandaa michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2022. Nchi nyingine zilizokuwa zikiwania nafasi hiyo ni Australia, Marekani, Japan na Korea Kusini.

"Nina furaha kubwa, kwasababu hili ni tukio kubwa kwetu. Hakuna anayeelewa tukio hili lina maana gani kwa nchi yangu. Lakini ninaamini mara baada ya 2018 watu watatuelewa nini tunamaanisha." Kauli yake Arshavin.
CECAFA TUSKER CHALLANGE CUP ETHIOPIA YAINYUKA KENYA 2-1.


HABARI KAMILI TEMBELEA MICHUZI JR.
Thursday, December 2, 2010
TAFAKARI YA LEO, NAMALIZIA HIVI.......
'AFRIKA YAWEZA KUJILISHA'
AFRIKA INA UWEZO WA KUJILISHA YENYEWE NA PIA IKAZALISHA CHAKULA CHA KUTOSHA KUUZA NJE.
KILIMO.
Hayo ni kwa mujibu wa kitabu kipya kilichozinduliwa hii leo na professa wa chuo kikuu cha Havard Calestous Juma. Kitabu hicho 'The New Harvest' kinatoa wito kwa viongozi wa Afrika kutilia mkazo upanuzi wa kilimo kupitia sera na mikakati yao ya kitaifa.
Kuafikia hilo, viongozi wa Afrika watahitaji kuboresha miundo mbinu, kutumia teknologia ya kisasa pamoja na kuhimiza kilimo cha mazao ya kufyatua kisayansi, yaani GM.
Ripoti hiyo itawasilishwa kwa viongozi wa Afrika siku ya Ijumaa mjini Arusha katika mkutano unaofanyika ndani ya hoteli ya Ngurdoto Mountain Lodge nchini Tanzania, ambapo Marais wa Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi wanafanya kikao kuzungumzia usalama wa chakula pamoja na suala la mabadiliko ya hali ya anga.
Professa Juma alisema viongozi wa Afrika hawana budi kutambua uhusiano wa kilimo na uchumi wa Afrika. ''Ni jukumu la viongozi wa Afrika kuuboresha uchumi wao na hiyo inamaanisha kuanza kutumia teknonologia ya kisasa katika kilimo''.
Kwa mujibu wa Professa Juma, uzalishaji wa chakula duniani unaendelea kuongezeka lakini katika maeneo mengi ya Afrika hali ni tete licha ya kuwepo na ardhi ya kutosha ya kilimo.

Hayo ni kwa mujibu wa kitabu kipya kilichozinduliwa hii leo na professa wa chuo kikuu cha Havard Calestous Juma. Kitabu hicho 'The New Harvest' kinatoa wito kwa viongozi wa Afrika kutilia mkazo upanuzi wa kilimo kupitia sera na mikakati yao ya kitaifa.
Ripoti hiyo itawasilishwa kwa viongozi wa Afrika siku ya Ijumaa mjini Arusha katika mkutano unaofanyika ndani ya hoteli ya Ngurdoto Mountain Lodge nchini Tanzania, ambapo Marais wa Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi wanafanya kikao kuzungumzia usalama wa chakula pamoja na suala la mabadiliko ya hali ya anga.
Kwa mujibu wa Professa Juma, uzalishaji wa chakula duniani unaendelea kuongezeka lakini katika maeneo mengi ya Afrika hali ni tete licha ya kuwepo na ardhi ya kutosha ya kilimo.
PIGA KURA SASA FILAMUCENTRAL BORA ZA 2010.

MAKUNDI YA FILAMUCENTRAL BORA ZA 2010.
Msanii chipukizi wa mwaka
Muigizaji bora wa kike
Muigizaji bora wa kiume
Mwandishi bora wa Mswaada
Mchekeshaji Bora
Filamu Yenye Kava bora
Mtayarishaji bora wa filamu
Kampuni bora ya utengenezaji filamu
Msambazaji Bora
Muongozaji Bora
ILI UWEZE KUCHAGUA TEMBELEA
http://www.filamucentral.co.tz/bora-za-2010/
WE-WE-CHINI YA ULINZI......!!!
MEMORIAL TREE.
Used by Germany colonial rulers to hang criminals during the period of 1890 - 1918.
Wednesday, December 1, 2010
GADNA AJIENGUA CLOUDS FM!!
MTANGAZAJI MAHIRI WA KIPINDI CHA JAHAZI KINACHO RUSHWA KILA SIKU JIONI SAA YA 10 HADI 12 KAMILI KUPITIA REDIO YA WATU CLOUDS FM AMEAMUA KUJIENGUA KWA SABABU AMBAZO AMESEMA NI ZA KUTAKA KUJARIBU UJASIRIAMALI BINAFSI.
Uongozi wa CLOUDS FM umethibitisha habari hizo na kwamba kesho tarehe 2DEC.2010 utatoa tamko rasmi siyo tu kwa kuondoka GADNA ambaye alijulikana kama KEPTEEEEEIN!!na kumechi vilivyo na mtangazaji mwenzie KIBONDE katika kipindi pendwa cha jioni ambacho huwapa kampani sana watanzania kote inapofika redio hiyo.
Awali kabla ya hatua hiyo ya Gadna mtangazaji wa kike SOPHIA KESSY nae alitangaza kuvunja ndoa baina yake na kipindi cha Afrika Bambataa na kusema kuwa ameamua kujitosa kwenye majukumu mengine bila kufafanua kama ilivyo kwa Gadna ambaye pia hajafafanua juu ya ujasiliamali anaokwenda kudil nao.
"Habari za Gadna ni za kweli, ameondoka, hayo mengine tutayaweka bayana kesho tutakapotoa tamko rasmi wa jinsi tunavyo jiandaa na mambo mapya ya mabadiliko". Alisema mmoja wa wakurugenzi wa CLOUDS MEDIA, bwana RUGE MUTAHABA.
DUH NOVEMBER NI NOMA!!!
Awali kabla ya hatua hiyo ya Gadna mtangazaji wa kike SOPHIA KESSY nae alitangaza kuvunja ndoa baina yake na kipindi cha Afrika Bambataa na kusema kuwa ameamua kujitosa kwenye majukumu mengine bila kufafanua kama ilivyo kwa Gadna ambaye pia hajafafanua juu ya ujasiliamali anaokwenda kudil nao.
"Habari za Gadna ni za kweli, ameondoka, hayo mengine tutayaweka bayana kesho tutakapotoa tamko rasmi wa jinsi tunavyo jiandaa na mambo mapya ya mabadiliko". Alisema mmoja wa wakurugenzi wa CLOUDS MEDIA, bwana RUGE MUTAHABA.
DUH NOVEMBER NI NOMA!!!
MAAFALI YA MADAKTARI WETU YAJA.......!!!!
Chuo kikuu kishiriki cha sayansi za afya Weill Bugando cha chuo kikuu cha mtakatifu Agustino Tanzania jumamosi ya tarehe 4Desemba2010 kinataraji kufanya maafali yake ya tatu kutunukisha stashahada na shahada.
Maafali hayo yatatanguliwa na kongamano la wafanyakazi na wanafunzi wote linalofanyika leo trh 1 Nyumbani hotel ambapo mada mbalimbali zitatolewa. Na tarehe 3 pambano la soka baina ya Wafanyakazi na Wanafunzi.
Tatizo la uhaba wa madaktari NCHINI limekuwa sugu kwa muda mrefu kutokana na wazazi wengi kutokuwa na uwezo wa kumudu gharama kubwa kuwasomesha vijana wao masomo hayo amabyo yanakadiriwa kufikia kiasi cha SHILLINGI MILLIONI 25 HADI 50 ILI KUWA DAKTARI KAMILI.
BAADA YA REAL MADRID KULIZWA RUNGU 5 NA BARCELONA, MOURINHO AKATAA TIMU YAKE KUFEDHEHESHWA.

Meneja wa Real Madrid Jose Mourinho amekanusha kwamba timu yake ilifedheheshwa na Barcelona baada ya kushindiliwa mabao 5-0 katika uwanja wa Camp Nou. Mabingwa wa Hispania Barca walicheza katika kiwango cha juu walipoisambaratisha Madrid katika mchezo wa kwanza wa El Clasico kwa Mourinho tangu aanze kuifundisha Madrid.

Alisema:"Timu moja ilicheza katika kiwango chake na nyingine haikucheza vizuri. "Kupoteza sawa tumepoteza, lakini kufedheheshwa hapana. Ilikuwa sahihi kupoteza mchezo ule, kwa sababu hatukucheza vizuri. "Nimezungumza na wachezaji wangu na nimewaambia msimu haujamalizika. Aliuliza: "Nani ajuaye kitakachotokea mwaka huu?"


Kwa upande wa Pep Guardiola, ambaye ameshinda kwa mara ya tano El Clasico tangu awe meneja wa Barcelona, amesema amefurahishwa sana kuona namna timu yake ilivyocheza katika kiwango cha juu na kuangaliwa na mamilioni ya wapenda soka duniani kupitia televisheni zao wanaokisiwa kufikia milioni 400. Alijigamba: "Ningependa kuzoa pointi nyingi zaidi dhidi ya Madrid lakini hilo haliwezekani.
Tuesday, November 30, 2010
MAMA HASHEEM THABEET AKABIDHI MSAADA KWA TIMU ZA BASKETBALL MWANZA.
Mama Hasheem Thabeet (Rukia Thabeet) leo amefanya ziara yake jijini Mwanza kwania ya kutoa msaada wa jezi kwa timu tatu za mpira wa kikapu jijini Mwanza nia na lengo ikiwa ni kuuendeleza mchezo huo nchini.
BEI MPYA YA SODA ZA COCA COLA KANDA YA ZIWA YATAMBULISHWA SAMBAMBA NA MOTISHA.

Subscribe to:
Posts (Atom)