ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, December 3, 2010

URUSI KUANDAA KOMBE LA DUNIA 2018

Shirikisho la soka duniani, Fifa, limetangaza Urusi kuandaa Kombe la Dunia mwaka 2018, baada ya kuzishinda nchi za England, Ureno na Uhispania, na Uholanzi na Ubelgiji.

Aidha Qatar nayo imechaguliwa kuandaa michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2022. Nchi nyingine zilizokuwa zikiwania nafasi hiyo ni Australia, Marekani, Japan na Korea Kusini.

Kwa mara ya kwanza katika historia, mashindano hayo ya kombe la dunia yanakwenda kufanyika nchini Urusi, Captain wa timu ya taifa hilo Andrey Arshavin ambaye pia hukiputa katika timu ya Arsenal, huku akishangilia, aliruka kwa furaha toka katika kiti alichokuwa amekaa akimpa mkono kila aliyekutana naye kuonyesha furaha yake ambayo ilikuja kama zali la mentali.

"Nina furaha kubwa, kwasababu hili ni tukio kubwa kwetu. Hakuna anayeelewa tukio hili lina maana gani kwa nchi yangu. Lakini ninaamini mara baada ya 2018 watu watatuelewa nini tunamaanisha." Kauli yake Arshavin.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.