Shirikisho la soka duniani, Fifa, limetangaza Urusi kuandaa Kombe la Dunia mwaka 2018, baada ya kuzishinda nchi za England, Ureno na Uhispania, na Uholanzi na Ubelgiji.
Aidha Qatar nayo imechaguliwa kuandaa michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2022. Nchi nyingine zilizokuwa zikiwania nafasi hiyo ni Australia, Marekani, Japan na Korea Kusini. Kwa mara ya kwanza katika historia, mashindano hayo ya kombe la dunia yanakwenda kufanyika nchini Urusi, Captain wa timu ya taifa hilo Andrey Arshavin ambaye pia hukiputa katika timu ya Arsenal, huku akishangilia, aliruka kwa furaha toka katika kiti alichokuwa amekaa akimpa mkono kila aliyekutana naye kuonyesha furaha yake ambayo ilikuja kama zali la mentali.
"Nina furaha kubwa, kwasababu hili ni tukio kubwa kwetu. Hakuna anayeelewa tukio hili lina maana gani kwa nchi yangu. Lakini ninaamini mara baada ya 2018 watu watatuelewa nini tunamaanisha." Kauli yake Arshavin.
Je, Upweke una athari gani kiafya?
-
Wataalamu wengi wanakubali kwamba upweke hutokea unapohisi ubora wa
mahusiano yako binafsi na watu wengine yako chini kuliko vile unavyotamani
yawe.
RAIS SAMIA AFTURISHA WATOTO KIKOMBO DODOMA
-
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe.
Mwanaidi Ali Khamis akigawa iftar kwa mmoja ya mtoto anayelelewa katka
Makao ...
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.