ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, August 3, 2023

MBUNGE MAIMUNA PATHANI KUANDAA MPANGO KABAMBE KUWAKOMBOA WANAWAKE WA LINDI

 

Mbunge wa viti maalum mkoa wa Lindi kupitia chama cha mapinduzi CCM Maimuna Pathan akiongea na waandishi wa habari baada ya kutelea mabanda kadhaa katika maonyesho ya nanenane mkoani Lindi
Mbunge wa viti maalum mkoa wa Lindi kupitia chama cha mapinduzi CCM Maimuna Pathan akiangalia bidhaa zinazozalishwa na wanawake wa Mkoa wa Lindi wilaya ya Nachingwea


MBUNGE wa viti maalum mkoa wa Lindi kupitia chama cha mapinduzi CCM Maimuna Pathan amesema amejipanga kuandaa mpango kabambe wa kuwakomboa wanawake wa huo kiuchumi.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wiki ya nane nane Mikoa ya nyanda za kusini, mbunge huyo alisema kuwa amewaona wanawake wengi wakishughulisha na shughuli mbalimbali za kujikomboa kiuchumi  alipotembelea mabanda ya moenyesho hayo.


Mbunge Pathan alisema kuwa amefarijika kuona wanawake wengi wamejikita kwenye shughuli za kukuza uchumi hivyo ameamua kuandaa mpango kabambe wa kuwaongezea ujuzi wanawake wa Mkoa wa Lindi.

Alisema kuwa mkoa wa Lindi unafursa nyingi za kiuchumi hivyo ni lazima kuwapatia elimu ya uchumi na ujasiliamali wanawake wa Mkoa huo.


Alimazia kwa kuwataka wanawake kuendelea kujikita kufanya shughuli za kimaendeleo bila uoga wowote ule.

BUGANDO WANAUMIZA VICHWA KUBAIN CHANZO KANDA YA ZIWA KUWA NA IDADI KUBWA YA WATOTO WENYE UTUMBO NJE

 NA ALBERT G. SENGO/MWANZA

HOSPITALI ya Rufaa ya Kanda Bugando inapokea watoto si chini ya 290 kwa mwaka wanazaliwa wakiwa na utumbo nje na wengi wao huko nyuma walikuwa wanapoteza maisha. Akizungumza katika Maadhimisho ya Siku ya Watoto Wanaozaliwa na Utumbo Nje Duniani, Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Bugando Dk. Fabian Massaga amesema kwa dunia takwimu zimeeleza kati ya watoto 4000 wanaozaliwa mmoja anakuwa na changamoto hiyo.

"Hapa Bugando kama hospitali ya kanda kwa mwaka mzima tunapokea wastani wa watoto 290 wenye changamoto ya utumbo nje" "Kwa mwezi siyo chini hya watoto 10, kwa wili watoto wa 3 hadi wa 5, sasa unaweza kuona jinsigani tatizo ni kubwa" amesema Dkt Massaga. Daktari Mkuu kitengo cha Upasuaji wa Watoto Dkt Langa Michael ametoa ushauri kwa akina mama wanapokuwa wajawazito kufanya kipimo cha Ulta Sound ili kugundua tatizo hilo mapema kwa watoto wao kabla ya kujifungua. Dkt. Neema Neema Kayanga ni Mkuu wa Idara ya watoto "Tusiishie tu kupunguza madhara tata kwa kuwaasa akinamama wajawazito kuchukuwa vipimo mapema kabla ya kujifungua, bali pia kama madaktari kupitia takwimu tulizonazo tunalo jukumu na wajibu la kujikita katika kufanya tafiti ili kubaini kwa nini idadi kubwa ya watoto wanaozaliwa na tatizo la utumbo nje nchini wanatokea Kanda ya Ziwa!?" "Tufanyeje, mbona Kanda nyingine tatizo hili ni dogo?"


Wednesday, August 2, 2023

NANE NANE MWANZA SIKU YA KWANZA TU TAYARI PAMENOGA

 NA ALBERT G. SENGO/MWANZA

Kutoka katika viwanja vya Nyamhongolo wilayani Ilemela jijini Mwanza hiki ndicho kinachoendelea. ........................................................................................................ MWENYEKITI WA KAMATI YA MAANDALIZI YA NANENANE KANDA YA ZIWA MAGHARIBI, MKUU WA MKOA WA MWANZA MHE. Mhe. CPA Amos Makalla ANAYO FURAHA KUUJULISHA UMMA KUWA, MAONESHO YA NANENANE MWAKA 2023 YANAFANYIKA KATIKA UWANJA WA NYAMHONGOLO ULIOPO MANISPAA YA ILEMELA KUANZIA TAREHE 01 HADI SIKU YA KILELE TAREHE 08/8/2023 WADAU, TAASISI, ASASI, MASHIRIKA NA MAKAMPUNI YOTE MNAKARIBISHWA KUSHIRIKI/KUONYESHA NA KUTANGAZA BIDHAA NA HUDUMA ZENU. KWA MAELEZO ZAIDI FIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA MWANZA IDARA YA KILIMO