ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, July 1, 2017

MADHARA YA KUANGALIA VIDEO ZA NGONO NA JINSI YA KUACHA.

Kuangalia video za ngono sio jambo jipya kwa jamii yetu, kimsingi ni watu wachache sana wanaweza kujizuia kujichua au kupiga punyeto baada ya kuangalia video za ngono.

Bahati mbaya tabia ya kuangalia video hizi watu wengi huipata wakiwa wadogo sana na usipokua makini tabia hii itakufanya vibaya sana kisaikolojia.

Tabia ya kujichua sasa iko wazi kwa jinsia zote yaani wanawake na wanaume japokua imekua ikiathiri zaidi wanaume sababu ya maumbile yao.

Japo wengi hufanya kwa siri na kuficha ili wasijulikane na wengine. Vijana wengi wamekuwa wakiangalia video hizo wakiwa wamejificha wenyewe chumbani, na hasa nyakati za usiku.

Kuangalia video za ngono kuna madhara mbalimbali ya kiafya na kisaikolojia. Haya hapa ni baadhi ya madhara unayoweza kuyapata kama utaangalia sana video za ngono.
Kuishiwa hamu ya tendo la ndoa na nguvu za kiume

Kuangalia sana video za ngono hukufanya ushindwe kusisimuliwa na mwanamke au mwanaume wa kawaida, video za ngono zina wanawake na wanaume wazuri sana ambao wako vile sababu ya kufanyiwa upasuaji mbalimbali wa kuongeza makalio na matiti, hata wanaume hufanyiwa upasuaji wa kuongeza uume hivyo mwanamke anayeangalia atatamani uume mkubwa kama ule au mwanaume anayeangalia atatamani mwanamke kama yule ambaye katika mazingira ya kawaida hayupo.

Sasa wanaume wanao angalia video za ngono hawawezi kusisimka au kuamsha uume hata mwanamke wa kawaida akipita uchi na hii huweza kuathiri sana mahusiano yao na kuonekana hawana nguvu za kiume kwani wao hutegemea video hizo kuamsha uume.

Kujichua au kupiga punyeto sana
Video za ngono zina wanawake na wanaume tofauti, kila video nzuri unayoangalia utaenda kujichua huku ukimuwaza wanaume au mwanamke husika. Hii itakufanya ujichue hata mara kumi kwa siku kama unaziangalia mara kwa mara. Kuishiwa nguvu za kiume, kusahau sana, kushindwa kumpa mwanamke mimba, kuchoka sana na kufika kileleni haraka wakati wa tendo la ndoa ni moja ya madhara makuu ya punyeto.

Kushindwa kudumu kwenye mahusiano
Kuangalia video za ngono hukufanya uwaze kujiridhisha mwenyewe tu na hata mwenza wako akitaka kulala na wewe unakua hutaki tena. Lakini hata kwa vijana ambao hawako kwenye mahusiano hujikuta wanakua waoga sana kuwafuata wanawake au wasione sababu ya kua kwenye mahusiano. Vile vile wanaume hushindwa kuwaridhisha wenza wao na wanawake kusingizia kuchoka kila siku.

Kuanza kufanya ngono ambazo sio za kawaida
Hivi karibuni idadi kubwa ya wanawake wamekua wakijihusisha sana na mapenzi ya kinyume na maumbile. Hii imesababishwa sana na kuangalia video za ngono na kuona ni kitu cha kawaida wakati kina madhara mengi. Wanawake waliozoea kuingiliwa nyuma hata wakiolewa huendelea kufanywa na wanaume wa nje hasa kama waume waliowaoa hawajawahi kujihusisha na tabia hiyo. Aina zingine za ngono ambazo zinababishwa na tabia ya kuangalia video hizi ni ushoga, usagaji, au mwanamke kulala na wanaume zaidi ya mmoja au mwanaume kulala na wanawake zaidi ya mmoja kwa wakati mmoja.

Inawezekana wewe unayesoma hapa tayari hii tabia inakuumiza sana kwa sasa na umeshindwa kuiacha, kuna mambo ya msingi unaweza kufanya ili uweze kuacha kuangalia video hizi..

Ondoa zana zote za kuangalia video hizi
Kama una tarakilishi (computer) au simu futa video zote, futa tovuti (website) zote za video ambazo unazitumia kuangalia. Kuna watu wamo kwenye makundi ya WhatsApp ya kutumiana video za ngono, ondoka kabisa huko kwani unajiharibu.

Anza kufanya mazoezi
Ni mazoezi pekee yanayoweza kumfanya mtu aweze kuachana na tabia zote ambazo sio za kawaida ambazo alikua anazifanya kipindi cha nyuma. Unapofanya mazoezi utatumia nguvu nyingi na mwili wako utachoka na kupata usingizi. Vilevile ufanyaji wa mazoezi hukuepusha na kukaa bila shughuli yoyote.

Jijengee tabia ya kukaa na marafiki zako muda mrefu au kufanya shughuli nyingine zitakazokuweka ‘busy’

Kama una tabia ya kuangalia video hizi basi, fanya mpango uwe unafanya mambo mengine muda ambao umekua ukiangalia hizi video, ikiwemo kusoma vitabu au kuongea na watu. Hii itakusaidia kusahau video hizo na kuacha kabisa.

Pata ushauri wa kitaalamu na matibabu
Unaweza kumuona mtaalamu wa ushauri wa kisaikolojia ili kukusaidia ushauri wa namna ya kufanya ili kuepukana na tabia hiyo. Kama umeshapata madhara kiafya, basi waone wataalamu wa afya hasa masuala ya uzazi ili wakushauri namna ya kulitibu tatizo lako.

Jenga mahusiano ya karibu na mpenzi wako
Hii itakusaidia kumuwaza yeye zaidi ya video za ngono na pia pale unapopata hamu ya kufanya mapenzi basi hutoogopa kumwambia ili mfanye. Kuwa karibu na mpenzi wako kutakujengea ujasiri na kuyakuza mahusiano yenu.

TAREHE / SIKU NZURI KWA MIMBA KUWEZA KUTUNGWA.

Leo napenda nizungumzie jambo moja tu ambalo ni juu ya  jambo moja tu, nalo ni namna wanavyoweza kui-pin point siku ile ya kilele (i.e fruitful/productive/fertile day), hapa nina maana ya siku ile ambayo wao wanaiita siku ya 14. 

Ikumbukwe kuwa wanawake wanatofautiana katika suala zima la urefu wa MENSTRAL CYCLE, yaani idadi ya siku kati ya period ya kwanza hadi ile ya pili inayofuatia. Kundi kubwa la wanawake wana fall kwenye range ya siku 22-35. Japo walio-normal wana siku 28. Vile vile kuna wengine huwa na menstral cycle mbili, yaani fupi na ndefu. Hivyo walio na menstral cycle fupi, mathalani wale wenye siku 22, huwa vilevile wana kipindi kifupi sana cha kutokwa na damu (period), yaani damu inaweza kukatika ndani ya siku 2 tu! Na wale wenye siku 35 au zaidi huwa wana kipindi kirefu sana cha kutokwa na damu (period) ambapo wengine huwachukua hata siku kati ya 5 hadi 8. 

Hivo basi, kama wewe ni mwanaume inakubidi umwelewe vizuri mwenzi wako juu ya hayo niliyoyasema hapo juu ili ikusaidie kui-pin point ile fertile day (yaani siku ya mimba). 

Swali: Je siku ya mimba ni ipi? 
Jibu lisilosahihi: Watu wengi na hata baadhi ya wanasayansi wanafikiri siku ya mimba ni ile ya 14 baada  ya dalili za kwanza za damu ya hedhi! Wao huhesabu kuanzia siku ile damu ilipoanza kutoka hadi siku ya 14! Utaratibu huu ume-prove failure! Hii ni kwa sababu wanawake wana menstral cycle zinazotofautiana kwa urefu. Hivo basi jibu sahihi ni hili hapa chini:

Jibu sahihi:  
1. Kwanza inabidi ujue kama mwenzi wako ana menstral cycle ipi? Fupi au ndefu, ama zote mbili?

2. Baada ya kujua urefu wa menstral cycle ya mwenzi wako then pin point siku ile ya mwisho halafu uhesabu backwards siku 15 kuanzia siku ile ya mwisho. Siku hii ya 15 kuanzia mwisho ndiyo siku ya  mimba kwa mwanamke yeyote! 

Once you know the '15th day' from the last one, then you can manoeuvre whatever you want to get her pregnant or to avoid pregnancy! 

With this new approach of pin pointing the fertile day you will find that all women (menstral cycles) are covered, whereas the old way of counting fits only to women whose menstral cycles are 28 days!


Naomba nitoe mifano hai kwa faida ya dada zetu na wengine: 
1. Kama mwanamke ana menstration cycle ya siku 22 inabidi afanye kama ifuatavo: Kwanza itabidi atengeneze kalenda yake mwenyewe ya siku zake zote za menstration cycle kama hapa chini:

1st, 2nd, 3rd, 4th, 5th, 6th, 7th, 8th, 9th, 10th, 11th, 12th, 13th, 14th, 15th, 16th, 17th, 18th, 19th, 20th, 21st, 22nd.

Kisha ahesabu kuanzia ile 22nd day kurudi nyuma mpaka afikishe siku 15. Ataona kuwa siku ya kumi na tano inaangukia kwenye 8th day ya kalenda yake. Hivo 8th day ndiyo siku ya mimba kwa mwanamke yeyote ambaye ana menstration cycle ya siku 22. Akumbuke kwamba 1st day ndiyo siku anayoanza ku-bleed!


2. Kama mwanamke ana menstration cycle ya siku 28 inabidi afanye kama ifuatavo: Kwanza itabidi atengeneze kalenda yake mwenyewe ya siku zake zote za menstration cycle kama hapa chini: 

1st, 2nd, 3rd, 4th, 5th, 6th, 7th, 8th, 9th, 10th, 11th, 12th, 13th, 14th, 15th, 16th, 17th, 18th, 19th, 20th, 21st, 22nd, 23rd, 24th, 25th, 26th, 27th, 28th.

Kisha ahesabu kuanzia ile 28th day kurudi nyuma mpaka afikishe siku 15. Ataona kuwa siku ya kumi na tano inaangukia kwenye 14th day. Inamaana kwamba 14th day ndiyo siku ya mimba kwa mwanamke yeyote ambaye ana menstration cycle ya siku 28. Akumbuke kwamba 1st day ndiyo siku anayoanza ku-bleed!


3. Kama mwanamke ana menstration cycle ya siku 35 inabidi afanye kama ifuatavo:  Kwanza itabidi atengeneze kalenda yake mwenyewe ya siku zake zote za menstration cycle kama hapa chini: 

1st, 2nd, 3rd, 4th, 5th, 6th, 7th, 8th, 9th, 10th, 11th, 12th, 13th, 14th, 15th, 16th, 17th, 18th, 19th, 20th, 21st, 22nd, 23rd, 24th, 25th, 26th, 27th, 28th, 29th, 30th, 31st, 32nd, 33rd, 34th, 35th.

Kisha ahesabu kuanzia ile 28th day kurudi nyuma mpaka afikishe siku 15. Ataona kuwa siku ya kumi na tano inaangukia kwenye 21st day. Inamaana kwamba 21st day ndiyo siku ya mimba kwa mwanamke yeyote ambaye ana menstration cycle ya siku 35. Akumbuke kwamba 1st day ndiyo siku anayoanza ku-bleed!


4. Kama mwanamke ana abnormal menstration cycle ya siku 15 , BASI KUNA UWEZEKANO WA KUTOPATA MIMBA KABISA KAMA INAVYOONEKANA HAPA CHINI: 

Kwanza itabidi atengeneze kalenda yake mwenyewe ya siku zake zote za menstration cycle kama kawaida: 

1st, 2nd, 3rd, 4th, 5th, 6th, 7th, 8th, 9th, 10th, 11th, 12th, 13th, 14th, 15th.

Kisha ahesabu kuanzia ile 15th day kurudi nyuma mpaka afikishe siku 15. Ataona kuwa siku ya kumi na tano inaangukia kwenye 1st day. Inamaana kwamba, the 1st day of her bleedind ndiyo siku ya mimba kwa mwanamke yeyote ambaye ana menstration cycle ya siku 15. Akumbuke kwamba 1st day ndiyo siku anayoanza ku-bleed, na ndiyo hiyo hiyo siku ambayo mwanamke wa kundi hili anaweza kupata mimba!

Hii inamaana kwamba, siku ambayo linaharibika lile yai la upande mmoja ndiyo siku hiyo hiyo ambayo yai la upande wa pili linapevuka tayari kwa kurutubishwa. Mwanamke wa aina hii anaweza kupata mimba tu kama atakutana na mwanaume siku ile anayoanza kubleed, kwani siku ambayo yai moja linaanza kuharibika ndio siku hiyo hiyo ambayo yai la upande wa pili linakuwa tayari kurutubishwa!

Na wanawake wa kundi hili la nne ukiwauliza vizuri watakiri kwamba hawajawahi kuona au ku-feel ule ute mweupe ambao wenzao huwa wanaupata siku ile yai linapokuwa tayari kwa
kurutubishwa, kwani ute wa wanawake wa kundi hili la nne huwa unachanganyikana na damu kwa vile unatoka siku ile ile wanapoanza ku-bleed. 


Pia wanawake wa kundi hili huwa wanatokwa na kiasi kidogo sana cha damu; na bleed hukatika ndani ya siku moja au mbili tu! 

Jambo la kushangaza ni kwamba, wanawake wengi hawana knowledge ya kutosha juu ya hili suala la siku ya mimba; hasa wale ambao wana menstration cycle inayobadilikabadilika! Wao husitukia tu wameanza ku-bleed. Ndo maana hawawezi hata ku-plan kutopata mimba! Hawana ujanja kabisa ndio sababu wengi wanatumia sindano na njia zingine nyingi za artificial ambazo mwisho wa siku huwaletea matatizo ya uzazi, kwani nyingi hu-block njia ya uzazi! 


Nimeona wengi wenye matatizo ya uzazi unaosababishwa na hizi artificial family planning. Wengine hulazimika kwenda hospital kuzibuliwa ili wapate mimba jambo ambalo ni hatari kwa afya zao! Full maelezo ya kujitosheleza, ukikosa kudaka au kudakisha mimba basi kuna walakini

JPM ATOA UHAKIKA KWA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI NCHINI.


Rais John Magufuli leo katika Ufunguzi wa Maonyesho ya Kimataifa ya Sabasaba amewaondoa Hufo wafanya bisahara nchini na kuwahakikishia atawawekea Mazingira mazuri.


MOBISOL YAZINDUA TV YA SOLA YENYE UWEZO WA KUENDESHA VIFAA VINGINE.

Mkuu wa Masoko na Uhusiano wa kampuni ya Mobisol, Leslie Katharina Otto, (kushoto)akitoa maelezo kwa mmoja wa wateja waliotembelea kwenye banda la Mobisol kwenye maonyesho ya kimataifa ya biashara yanayoendelea jijini Dar es salaam.
Kaimu Balozi wa Ujereumani hapa nchini John Reyels (kushoto) akimsikiliza kwa makini Afisa Mtendaji Mkuu wa Mobisol Afrika Mashariki, Henrik Axelsson Lilja , wakati wa uzinduzi wa kutoa huduma za Mobisol jijini Dar es Salaam, kwenye banda la Ujerumani lililopo kwenye Maonyesho ya 41 ya Biashara ya Kimataifa maarufu Sabasaba jijini Dar es Salaam .
Ofisa Mkuu wa Kampuni ya Mobisol Afrika Mshariki, Henrik Axelsson Lilja, akionyesha waandishi wa habari (hawapo pichani) moja ya TV ya Sola
Mwakilishi wa Mobisol kanda ya Dar es Salaam, Allan Rwechungura akiongea na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa kampuni Mobisol mkoani Dar e salaam na Sola Tv kwenye banda la maonyesho la kampuni hiyo lililopo uwanja wa SabaSaba ---Kampuni ya Mobisol kutoka nchini Ujerumani ambayo inafunga na kuuza vifaa bora vya nishati ya umeme imezindua bidhaa mpya ya kipekee kwenye soko la Tanzania, ambayo ni TV ya sola inayojitegemea kabisa.

Akiongea jijini Dar es Salaam wakati wa Uzinduzi wake, kwenye banda la Ujerumani, katika viwanja vya sabasaba, Meneja Mkuu wa Mobisol Afrika Mashariki, Henrik Axelsson akiwa na mwakilishi wa Mobisol, kanda ya Dar es salaam, Allan Rwechungura, amesema TV hii mpya ya kioo bapa yenye ubora wa hali ya juu ya sola inajitegemea na inauwezo wa kuwasha taa na kuchaji simu hivyo ni ya kipekee na inajitegemea kwa upande wa nishati.

TV hii kisasa ya kioo bapa yenye ubora wa hali ya juu, ina betri inayofanya kazi hadi masaa 10, ina uwezo wa kuwasha taa, una waranti ya miaka 3 na huduma (service) baadaa ya mauzo.

Alisema katika msimu huu wa Sabasaba kampuni ya Mobisol imetoa punguzo maalumu kwa ajili ya kuwawezesha watanzania wengi kuunganishwa na umeme wa sola wa uhakika ikiwemo kujipatia vifaa imara na vya kisasa vilivyotengenezwa kwa teknolojia ya Kijerumani kwa gharama nafuu na kuweza kulipia kwa awamu mpaka kufikia kipindi cha miaka mitatu.
”Ofa hii inawezesha wateja wetu watakaolipa fedha taslimu kuunganishwa na mtandao wa Mobisol kupata punguzo hadi asilimia 25% na watakaolipia kwa awamu gharama ya kuanzia ni shilingi 59,000/- ambapo makato ya kila mwezi itakuwa shilingi 33,500/- ambapo kwa miaka 3 itakuwa kiasi cha shilingi 1,266,000/-”. Alisema Rwechungura.

Hii ni fursa ya kuwapatia zawadi ya maendeleo familia yako na wale uwapendao kijijini! Aliongeza kuwa kampuni ya Mobisol ambayo sasa imeanza kutoa huduma zake hapa jijini Dar es Salaam, ina mitambo ya nguvu ya kwa ajili ya matumizi mbalimbali ya nyumbani ya wati 80, 120, na 200 mbayo inakuja pamoja na betri, taa, TV, redio, tochi na waya ya kuchaji simu. Hivyo kumwezesha mtu anayeishi eneo ambalo umeme haujafika kutokuwa na tofauti na mtu aishiye mjini.

Akibainisha zaidi uwezo wa kufanya kazi wa TV hii ya sola inayojitegemea ikitumika kwa TV, kuwasha taa 3 (za Wati 1) kwa muda wa masaa 6 na kuchaji simu 2 unaweza kufanya kazi kati ya masaa 6 hadi 9. Matumizi ya King’amuzi na kuwasha taa 3 kwa masaa 6 ya kuchaji simu 2 unaweza kufanya kazi kati ya masaa 5 na 7.

Rwechungura aliendelea kufafanua kuwa iwapo mteja atawasha TV kwa masaa 4 na kuchaji simu 2 ataweza kutumia taa kwa masaa 10 hadi 15.

“Mtambo huu wa Tv ya sola unaowezesha matumizi ya aina mbalimbali unapatikana kwa gharama ya shilingi 950,000 na vifaa vya umeme ambayo mteja ataweza kununua na kutumia kwenye mtambo huu ni seti ya taa ya umeme yenye 1W au 2W, kifurushi cha King’amuzi cha Zuku chenye chaneli za kulipia, Redio ndogo na seti ya kuchaji simu. Hii ni fursa nyingine ya pekee kwa wateja kujiunga na familia ya Mobisol na kufurahia maisha ya kisasa kwa kutumia vifaa vya teknolojia bora kutoka Ujerumani” Alisema.

Mobisol ni kampuni pekee katika kanda ya Afrika yenye mitambo ya kuzalisha umeme wa nishati ya jua wenye nguvu na inauza vifaa bora vya majumbani vya matumizi ya nishati ya umeme wa jua ambapo pia imekuwa inatekeleza mpango wa kusambaza nishati ya umeme wa jua kwa kulipia kwa awamu. Kufikia sasa inao mtandao wa wateja zaidi ya 62,000 nchini Tanzania na zaidi ya wateja 85,000 katika kanda ya nchi za Afrika Mashariki.

Mobisol sasa ipo katika mikoa 23 nchini Tanzania na inaendelea kusogeza huduma karibu na wahitaji.

SPIKA AWALIPUA WABUNGE WA UPINZANI, KABUDI ANENA MAMBO MAZITO, HANS POPPE ALETA STRAIKA MZAMBIA, YANGA NAYO YASHUSHA KIFAA KIPYA.

Spika awalipua wabunge wa upinzani, Kabudi anena mambo mazito, Hans Poppe aleta straika Mzambia.
 
Miswada ya ncha kali yawasha moto, Mkoa wa kipolisi Rufiji waanzishwa, Yanga yashusha kifaa kipya. Pata kwa undani yaliyojiri katika magazeti ya leo hapa.

Friday, June 30, 2017

NI MARUFUKU MATANGAZO KWENYE MIITO YA SIMU - TCRA

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), imepiga marufuku matangazo ya biashara yanayowekwa mtumiaji anapopiga simu ili kutoa fursa kwa watumiaji kupata mawasiliano bila usumbufu.

Mkurugenzi wa TCRA, Mhandisi James Kilaba amesema leo (Ijumaa) kuwa mamlaka hiyo imepokea malalamiko mengi kutoka kwa watumiaji wa simu wakilalamikia matangazo hayo yanayotolewa na kampuni za simu.

Amesema tayari TCRA imeshaziandikia barua kampuni zote za simu kusitisha matangazo hayo na itakutana nazo kwa majadiliano ya kina Julai 6.

Amesema mamlaka haitambui utaratibu huo na inauchukulia kama kero kwa watumiaji wa simu ambao hutegemea kutumia njia hiyo ya mawasiliano kurahisisha mambo.

“Tuna imani mtu anapopiga simu ana shida ya haraka na anahitaji afanye mawasiliano, unapomuwekea matangazo kwa dakika tatu au nne ni usumbufu,” amesema.

Katika siku za karibuni imekuwa ni kawaida kwa mtu anayepiga simu kusikiliza wimbo au matangazo ya biashara na baadaye kuambiwa namba anayopiga haipatikani.

MASAUNI ATANGAZA MAJINA YA WATUHUMIWA 16 WA MAUAJI YANAYOENDELEA KIBITI, MKURANGA NA IKWIRIRI



 Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani), baada ya kufanya kikao na viongozi wa ngazi za juu wa Jeshi la Polisi kuhusiana na uhalifu katika maeneo ya Kibiti,Mkuranga na Ikwiriri,mkoani Pwani, ambapo alitangaza kutafutwa kwa watu 16 wanaotuhumiwa kuhusika na uhalifu huo.Kulia ni Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini(IGP), Simon Sirro.Mkutano huo umefanyika katika Ukumbi wa polisi makao makuu,jijini Dar es Salaam.
 Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akionyesha baadhi ya picha za watuhumiwa wa uhalifu katika maeneo ya Kibiti,Mkuranga na Ikwiriri kwa  waandishi wa habari (hawapo pichani), baada ya kufanya kikao na viongozi wa ngazi za juu wa Jeshi la Polisi  ambapo alitangaza kutafutwa kwa watu 16 wanaotuhumiwa kuhusika na uhalifu huo.
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini(IGP), Simon Sirro, akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani), baada ya kufanya kikao kuhusiana na uhalifu katika maeneo ya Kibiti,Mkuranga na Ikwiriri,mkoani Pwani, ambapo Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni(kushoto),alitangaza kutafutwa kwa watu 16 wanaotuhumiwa kuhusika na uhalifu huo.Mkutano huo umefanyika katika Ukumbi wa polisi makao makuu,jijini Dar es Salaam.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
IMEANDALIWA NA KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

UJASIRIAMALI MPYA WA DIAMOND KATIKA PICHA.





NA:- Abog
Nyota wa Bongo Flava Diamond Platnumz ameendelea kuushika mtaa na mara hii sio kuachia ngoma kama ambavyo amefanya wiki chache zilizopita alipoachia nyimbo mbili kwa mpigo (I miss you na Fire) lakini sasa amerudi kwenye bidhaa zenye brand yake kama alivyoanza na Nguo kabla ya kutambulisha Manukato yanayotambulika kama Chibu Perfume.

Ili kuhakikisha anamfikia kila shabiki wake nchini kote bila kujali kipato chake ameingia kwenye biashara ya vyakula, ambapo Juni 29, mwaka huu, ametambulisha Karanga zake ambazo zitapatikana nchini kote. Karanga hizo zimefungwa kwenye mfuko mdogo ambapo kila moja itakuwa inauzwa kwa shilingi mia tatu 300/=

Diamond Platnumz pamoja na Label yake ya WCB Wasafi wamepata mafanikio mwishoni mwa wiki iliyopita Juni 25, baada ya msanii Rayvany kutwaa tuzo ya BET katika kipengele cha Best International Viewers Choice Award.

 PICHA KUTOKA KWENYE UTAMBULISHO WA KARANGA ZA DIAMOND.













Huku wasanii wengi wakitumia muda wao mwingi kuuza tisheti, Diamond alianzisha manukato ya Chibu ambayo ni bidhaa ya kipekee.

Msanii huyo baadaye alifanya kile ambacho wengi hawakutarajia kwa kuzindua njugu karanga siku ambayo alimkaribisha Rayvanny nchini Tanzania.

Hivi ndivyo alivyoandika katika chapisho lake la akaunti yake ya facebook siku ya Alhamisi:
USISEME KARANGA SEMA DIAMOND KARANGA!!!!...Habari njema kwa Vijana wenzangu wote, sasa unaweza kujipatia Mtonyo wa ChapChap kupitia @diamondkaranga ambapo utaweza kununua kwa bei ya jumla ya shilingi elfu ishirini (20,000) kwa boksi moja lenye pakiti Mia moja (100) ndani ambazo ukiuza unapata faida ya elfu kumi fanya mawasiliano sasa na mawakala walio karibu yako.