ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, October 27, 2023

MUUZA MAYAI SHINYANGA ASHINDA MILIONI 50 ZA AIRTEL

 NA ALBERT G. SENGO/SHINYANGA

Ukisikia kulala masikini na kuamka tajiri ndiyo huku baada ya kijana Renatus Mashauri muuza mayai tena, mwajiriwa wa kibarua toka mjini Shinyanga kujishindia fedha taslimu milioni 50 za kitanzania baada ya kuibuka mshindi kwenye Droo ya mwisho ya mchezo wa UPIGE MWINGI kupitia Airtel.

SERIKALI YABAINISHA MIKAKATI ENDELEVU KWA AJILI YA KUIMARISHA MFUKO WA UDHAMINI WA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI.

 

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Ummy Nderiananga akifafanua jambo wakati wa kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI kilichofanyika Bungeni Dodoma Tarehe 23 Oktoba 2023 ambapo aliwasilisha Taarifa kuhusu Utekelezaji wa Mkakati Endelevu kwa ajili ya kuimarisha mfuko wa udhamini wa Kudhibiti UKIMWI Tanzania (AIDS TRUST FUND – ATF).






Picha Ikionesha baadhi ya wajumbe katika kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI kilichofanyika Bungeni Dodoma Tarehe 26 Oktoba 2023.

NA; MWANDISHI WETU – DODOMA

Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushirikiana na Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania, inaendelea kushauriana na Serikali kuhusu kuwa na chanzo endelevu na cha uhakika cha Mfuko wa udhamini wa kudhibiti UKIMWI nchini.

Hayo yamesemwa mapema leo Tarehe 26 Oktoba 2023 Bungeni Dodoma na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Buange na Uratibu) Mhe. Ummy Nderiananga alipowasilisha Taarifa kuhusu Utekelezaji wa Mkakati Endelevu kwa ajili ya kuimarisha mfuko wa udhamini wa Kudhibiti UKIMWI Tanzania (AIDS TRUST FUND – ATF), kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI.

Naibu Waziri Nderiananga alisema, Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushirikiana na Tume ya Kudhibiti UKIMWI (TACAIDS) inafanya mapitio ya Mkakati wa Ukusanyaji wa Rasilimali kwa kuzingatia wakati, mwelekeo na mahitaji ya sasa na kupitia upya vigezo na malengo ili kufanya maboresho kwa kuzingatia Mkakati ulioboreshwa wa kukusanya rasilimali.

Akiongelea suala la kukuza mchango wa sekta binafsi katika mapambano dhidi ya UKIMWI, Naibu Waziri Nderiananga alisema, Tume imeanzisha mfumo wa majadiliano na wadau kupitia vikao ili kujadili uendelevu wa rasilimali za afua za UKIMWI nchini.

“Malengo makuu ya kuanzishwa kwa Mfuko wa ATF ni pamoja na kupunguza utegemenzi wa rasilimali za kufadhili afua za VVU/UKIMWI kutoka nje ya nchi, kuongeza uendelevu wa huduma muhimu za UKIMWI.” Alisisitiza Nderiananga.

Aliendelea kusema kuwa, Serikali imeendelea kutekeleza sheria kwa kutenga bajeti ya Serikali kila mwaka kwa ajili ya mfuko huo, pamoja na kuimarisha ushirikiano na wadau mbalimbali kwa mujibu wa mwongozo wa mfuko.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI Mhe. Stansalus Nyongo alisema ni vizuri Serikali ikatenga na kuongeza fedha za kutosha kwa ajili ya Mfuko huo wa UKIMWI na kuendelea kusema kuwa kamati yake ipo tayari kuhamasiha upimaji wa VVU kupitia mabonanza mbalimbali ya michezo yanayofanyika..

RC TANGA AWATAKA WANANCHI KUACHA KUTUMIA MIFUMO YA KIZAMANI KUHIFADHI FEDHA ZAO

  Mkuu wa Mkoa wa Tanga Waziri Kindamba akizungusha mfano wa kadi ya NMB leo wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Mastabata –Halipoi uzinduzi uliofanyika kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani Mjini Tanga kulia ni Mkuu wa Idara ya Kadi ya Benki ya NMB Philbert Casmir


 Mkuu wa Mkoa wa Tanga Waziri Kindamba akizungusha mfano wa kadi ya NMB leo wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Mastabata –Halipoi uzinduzi uliofanyika kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani Mjini Tanga kulia ni Mkuu wa Idara ya Kadi ya Benki ya NMB Philbert Casmir

 Mkuu wa Mkoa wa Tanga Waziri Kindamba akizungusha mfano wa kadi ya NMB leo wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Mastabata –Halipoi uzinduzi uliofanyika kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani Mjini Tanga kulia ni Mkuu wa Idara ya Kadi ya Benki ya NMB Philbert Casmir

 Mkuu wa Mkoa wa Tanga Waziri Kindamba akizungusha mfano wa kadi ya NMB leo wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Mastabata –Halipoi uzinduzi uliofanyika kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani Mjini Tanga kulia ni Mkuu wa Idara ya Kadi ya Benki ya NMB Philbert Casmir

 Mkuu wa Mkoa wa Tanga Waziri Kindamba akizungusha mfano wa kadi ya NMB leo wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Mastabata –Halipoi uzinduzi uliofanyika kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani Mjini Tanga kulia ni Mkuu wa Idara ya Kadi ya Benki ya NMB Philbert Casmir


Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Waziri Kindamba akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Mastabara –Halipoi iliyofanyika kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani Mjini Tanga kulia ni Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Kaskazini Baraka Ladislaus,


Mkuu wa Idara ya Kadi ya Benki ya NMB Philbert Casmir akizungumzia wakati akielezea kampeni ya Mastabata –Halipoi leo kwenye viwanja vya Mkwakwani Mjini Tanga wakati wa uzinduzi wake kulia Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Kaskazini Baraka Ladislaus

Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Kaskazini Baraka Ladislaus akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Mastabata –Halipoi leo kwenye viwanja vya Mkwakwani Mjini Tanga


Watumishi wa Benki ya NMB Mkoa wa Tanga wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Mastabata –Halipoi leo kwenye viwanja vya Mkwakwani Mjini Tanga.


Na Oscar Assenga,TANGA.

WANANCHI wa Mkoa wa Tanga wametakiwa kuacha kutumia mifumo ya kizamani ikiwemo ya kutembea na fedha mifukoni badala yake watumie mifumo ya kibenki ya Master Card Qr kwani ndio njia salama na ya uhakika wa kuhifadhi fedha zao

Hatua hiyo inaeleza kwambaa itakuwa ni salama kwani itawaepusha wananchi hao na changamoto mbalimbali ambazo wanaweza kukutana nazo ikiwemo wizi

Wito huo ulitolewa leo na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Waziri Kindamba wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Mastabata-Halipoi inayoendeshwa na Benki ya NMB kwenye Halfa iliyofanyika kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani mjini Tanga.

Ambapo alisema wakitumia mifumo ya kibenki ya Master Card QR itawawezesha kuwa na usalama wa fedha zao ikiwemo kutokuchakaa haraka.

Alisema kwamba wananchi wakiwa na mwamko wa kufanya hivyo itawaepusha na kuharibika kwa fedha lakini pia kama nchi itasaidia kuondokana na kuingia gharama na ndio maana wanasistiza umuhimu wa kadi.

“Ndugu zangu leo tupo hapa kwenye uzinduzi wa kampeni hii ya Mastabata –Haipoi niwaambie huu ni mfumo salama na makini hivyo niwaase wana Tanga na watanzania tuuchangamkie”Alisema

Aidha aliwaeleza wakazi wa mkoa huo kutumia njia mbadala kwa ajili ya kufanya malipo kuna kuwa na faida nyingi hivyo niwapongeze benki ya NMB kwa kuja na ubunifu huu.
Hata hivyo aliwataka wananchi wa mkoa huo kuacha kutumia mifumo ya kizamani kutembea na fedha mfukoni ili kuepukana na changamoto mbalimbali ambazo wanaweza kukumbana nazo ikiwemo wizi.

Alisema kwa sababu unapotumia kadi kwa kufanya malipo Benki ya NMB haikuachi hivihivi bali inakupa na zawadi mbalimbali hivyo wananchi changamkieni fursa hiyo muhimu.

Awali akizungumza katika uzinduzi huo,Mkuu wa Idara ya Kadi wa Benki ya NMB Philbert Casmir alisema kampeni hiyo ni kusisitiza matumizi ya kadi wanaoita mastabata haipoi.

Alisema ili kurudisha faida ya benki ya NMB kwa jamii kila mwaka mwishoni wanafanya kampeni hiyo kwa kushirikiana na wadau wao wa mastakadi kwa kufanya kampeni kubwa kutoa zawadi kemukemu.

Aidha alisema utoaji wa zawadi hizo unakwenda sambamba na kuhamasisha wateja wao kuachana na matumizi ya pesa taslimu badala yake watumie kadi kufanya miamala,manunuzi.

Alisema pia watumie simu zao kufanya manunuzi ambapo kampeni hiyo leo wameizinduliwa Tanga na ilianza mwaka 2018 na 2022 waliita mastabata kivyakovyako na leo wanaita mastabata haipo.

Philbert alisema kwamba kupitia kampeni hiyo benki ya NMB inaendelea kuhamasisha malipo ya njia kidigitali na kuachana na pesa taslimu kupitia hiyo watakuwa na droo ya kila wiki,mwezi na hatimaye fainali droo sasa hapa mnisikilize kwa umakin.

Hata hivyo alisema kwamba benki ya NMB wakishirikiana wenzao wa mastakadi wameandaa milioni 350 zawadi ambazo zitakuwa zikishindaniwa na wateja wao huku akieleza vigezo kwanza zawadi za kila wiki.

Ambapo alisema watakuwa na washindi 100,kila mmoja atashinda pesa taslimu 100,000 lakini watafanya zoezi akikuta mtu afanaya manujnuzi kwa kutuimia kadi palepele anapewa 50,000.

Thursday, October 26, 2023

HASHEEM IBWE''NIMEKUJA KUUNGANA NA ALLY KAMWE TUPIGWE WOTE/NILINUSURIKA KUPIGWA NA CHUMA KIKALI

 Waziri wa Viwanda na Biashara Dr.Ashatu Kijaji pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani( FCC),William Erio wamekagua Godauni la Jezi feki za Yanga,Simba,Azam na Taifa Stars lilipo maeneo ya Mbozi Road Temeke, Dar Es Salaam zinazokadiriwa kuwa na thamani ya zaidi ya Shilingi za Kitanzania Bilioni 10.

Wednesday, October 25, 2023

TUME YA MADINI YASHIRIKI MKUTANO WA KIMATAIFA WA UWEKEZAJI SEKTA YA MADINI










Tume ya Madini kwa kushirikiana na Taasisi zilizopo chini ya Wizara ya Madini leo Oktoba 25, 2023 inashiriki katika Mkutano wa Kimataifa wa Uwekezaji Sekta ya Madini unaoendelea katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.

Viongozi wa Tume wanaoshiriki ni pamoja na Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula, Makamishna wa Tume ya Madini, Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini Eng. Yahya Samamba, Wakurugenzi, Mameneja na Maafisa Madini Wakazi wa Mikoa.

Mkutano huo unafunguliwa na Naibu Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Tuesday, October 24, 2023

MWANZA: ZAIDI YA BILIONI 1.6 ZAKAMILISHA MIRADI YA ELIMU UKEREWE

 

Zaidi ya shilingi bilioni 1.6 zimekamilisha ujenzi wa miradi ya elimu katika shule za msingi kupitia mpango wa BOOST katika Wilaya ya Ukerewe mkoani Mwanza, hatua ambayo itawaondoa adha ya wanafunzi katika mwaka ujao wa masomo unaonza mwezi Januari 2024.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe, Emmanuel Shelembi amesema miradi hiyo inahusisha ujenzi wa vyumba 50 vya madarasa, matundu 68 ya vyoo, madawati 660, viti 140, majengo mawili ya utawala na nyumba moja yenye muundo wa kutumika na waalimu wawili (2 in 1).

Shelembi amezitaja shule zilizonufaika na miradi hiyo kuwa ni pamoja na Murutilima, Nakasahenge, Mandela, Nyerere, Kalendelo, Mulezi, Namagubo, Bugorola pamoja na shule mpya za Kivukoni na Kilimabuye.

"Katika sekta ya elimu tumepunguza adha kwa wanafunzi wetu, hasa kutembea umbali mrefu kutoka visiwani jambo ambalo ni hatari ziwani. Pia itaondoa msongamano changamoto ya msongamano wa wanafunzi darasani kutoka wanafunzi 120 hadi 45" amesema Shelembi.

Amebainisha kuwa kati ya shilingi bilioni 1,670,700 zilizopokelewa kupitia BOOST, miradi iliyokusudiwa imekamilika kwa ubora na kufakiwa kubakiza chenchi ya shilingi milioni 60 pamoja na vifaa vyenye thamani ya shilingi milioni 10 zitakazoelekezwa kuboresha miundombinu yenye changamoto.

Pia Shelembi ametumia fursa hiyo kumpongeza Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuhakikisha anatatua changamoto mbalimbali za wananchi na kuwaletea wananchi maendeleo katika sekta mbalimbali ikiwemo elimu na afya.

"Kwa miaka miwili 2021/22 na 2022/23 tumepokea jumla ya shilingi bilioni 20.258 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo. Ni kazi kubwa inafanywa na Dkt. Samia Suluhu Hassan hivyo kazi yetu ni kumsaidia kwa kazi nzuri anayoifanya kwa watanzania" amesema Shelembi.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Ukerewe, Joshua Manumbu katika kuunga mkono kazi kubwa inayofanywa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Halmashauri hiyo imesimamia kwa asilimia 100 bajeti yake na kufanikiwa kukamilisha miradi ya wananchi ikiwemo zahanati, vituo vya afya na madarasa.

"Kipekee kabisa nimpongeze sana DC aliyepita (Denis Mwilla), Mungu ambariki huko Mbarali. Tulifanya kazi pamoja tukishirikiana na Mkurugenzi Shelembi na Kamati ya Siasa ikiongozwa na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Ukerewe, Ally Mambile. Tumetekeleza miradi yote kwa ubora na hakuna mradi uliokwama baada ya kupitiwa na mwenge" amesema Manumbu na kuongeza;

"Lakini pia nimpongeze Mhe. DC Hassan Bomboko ambaye bado ana muda mfupi Ukerewe, tunaona ufuatiliaji wake wa miradi ni mzuri, tuendelee kushirikiana ili kusimamia fedha za miradi ya maendeleo na Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2020/25" amesema Manumbu.

Naye Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Ukerewe, Ally Mambile amesema Serikali iko kazini na Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2020/25 inatekelezwa. "Mnyonge mnyongeni, haki yake mpeni, Mkurugenzi Emmanuel Shelembi amekuwa ni mfano wa watendaji bora katika kusimamia miradi ya maendeleo" amesema Mambile.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe, Hassan Bomboko amesema miradi ya maendeleo ikiwemo ya elimu imetekelezwa kwa ubora katika Wilaya hiyo na kukamilika kwa asilimia 100 ikiendana na thamani ya fedha iliyotumika.
Na George Binagi- GB Pazzo, BMG
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe, Emmanuel Shelembi akielezea utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika Halmashauri hiyo.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Ukerewe, Joshua Manumbu akieleza namna Halmashauri hiyo imetekeleza kwa viwango miradi mbalimbali ya maendeleo.
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Ukerewe, Ally Mambile akiwapongeza viongozi wa Halmashauri ya Ukerewe kwa kusimamia vyema miradi ya maendeleo.
Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe, Hassan Bomboko akizungumzia utekelezaji wa miradi ya maendeleo wilayani humo.
Mwonekano wa jengo la utawala katika Shule mpya ya msingi Kilimabuye iliyopo Kata ya Namagondo wilayani Ukerewe.
Mwonekano wa baadhi ya vyumba vya madarasa yaliyojengwa kupitia mradi wa BOOST wilayani Ukerewe.
Mwonekano wa nyumba ya waalimu (2 in 1) katika shule ya msingi Kilimabuye.
Mwonekano wa madarasa ya wanafunzi wa awali katika shule mpya ya Kivukoni iliyopo Kata ya Kakukuru wilayani Ukerewe yaliyojengwa kupitia mradi wa BOOST.
Mwonekano wa baadhi ya vyumba vya madarasa vilivyojengwa kupitia mradi wa BOOST wilayani Ukerewe.
Mwonekano wa ndani wa vyumba vya madarasa  katika shule ya msingi Nyerere wilayani Ukerewe.
Mratibu miradi ya BOOST Wilaya ya Ukerewe, Rasul Amiri akieleza namna miradi hiyo itaondoa changamoto kwa wanafunzi.
Mwalimu Mkuu shule ya msingi Nakasahenge, Mwl. Jenifer Damian ambaye alikuwa akisimamia ujenzi wa shule mpya ya msingi Kilimabuye iliyogharimu shilingi milioni 448.5.
Mwalimu Mkuu wa shule ya msingi Mandela iliyopo Kata ya Mukituntu, Mwl. Jacob Maranya amesema ujenzi wa vyumba sita vya madarasa pamoja na matundu matatu ya vyoo katika shule hiyo utasaidia kuondoa mrundikano wa wanafunzi katika shule ya Kazilankanda.
Diwani wa Kata ya Namagondo wilayani Ukerewe, Thomas Ng'afu amesema utekelezaji wa miradi ya BOOST imepokelewa vyema na wananchi kwani imewaondolea adha ya kuchangishana fedha kujenga madarasa hivyo wajibu walio nao ni kuhakikisha watoto wanaandikishwa shule na kuzingatia masomo yao.
PIA SOMA>>> HABARI ZAIDI HAPA

Imbeju ya Benki ya CRDB yatoa mtaji wezeshi shilingi bilioni moja mpaka sasa

 

Newala. Tarehe 22 Oktoba 2023: Katika kuwafikia na kuwanufaisha zaidi wanawake wajasiriamali, CRDB Bank Foundation imeshiriki Mkutano Mkuu wa nne wa Mwaka wa BUT Vicoba uliowakutanisha zaidi wanachama 3,500 kutoka vikundi 318 vilivyoshiriki na kutoa mtaji wezeshi wa fedha taslimu na pikipiki. 

Akizungumza na wanachama hao, Mkurugenzi Mtandaji wa CRDB Bank Foundation, Tully Esther Mwambapa kwa hamasa aliyoiona ameamini kuwa kweli BUTA Vicoba ni taasisi kubwa yenye uwakilishi nchi nzima jambo linaloleta matumaini ya kulikomboa kiuchumi kundi hilo.

Tully amesema ni jambo la kujivunia kuona wanawake wanakusanyika kwa pamoja kupanga maendeleo ya uchumi wao binafsi na wa familia zao jambo litakalowaongezea ushiriki wao kwenye uchumi wa taifa letu.
“Leo tunakabidhi mfano wa hundi ya shilingi milioni 20 pamoja na pikipiki 5 zenye thamani ya shilingi milioni 15 kwa wana BUTA Vicoba. Huu ni mtaji wezeshi kwa baadhi yenu waliokidhi vigezo. Lengo la kuanzishwa kwa CDRB Bank Foundation ni kuwahudumia Watanzania hasa makundi yasiyopewa kipaumbele na taasisi nyingi za fedha nchini ambayo ni wanawake na vijana. Mliopata mtaji huu wezeshi leo mnaungana na wenzenu ambao tayari tumeshatoa shilingi bilioni 1 kwao,” amesema Tully.

CRDB Bank Foudation ni kampuni tanzu ya Benki ya CRDB iliyoanzishwa na kusajiliwa mwaka 2022 kwa lengo mahsusi la kuwawezesha vijana na wanawake. Kwa sasa taasisi hii inatekeleza Programu ya Imbeju iliyotengewa bajeti ya kuanzia kiasi cha shilingi bilioni 5 kwa ajili ya makundi hayo.

Ili kuyafikia makundi hayo kirahisi, inashirikiana na wadau muhimu wenye mtandao mpana. Kwa vijana wenye bunifu za kiteknolojia (startups), taasisi inashirikiana na Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) pamoja na Tume ya TEHAMA (ICTC) na kwa wanawake wajasiriamali kuna BUTA Vicoba, Shirika la Care International, Citizen Foundation na wengine.
Tangu Programu ya Imbeju ilipozinduliwa Machi 12 mwaka huu, vijana 709 walijitokeza kutuma maombi ambayo yalipochujwa, miradi 196 ilikubaliwa na kuingia hatua ya mafunzo ya kujengewa uwezo wa kuendesha biashara kwa viwango vinavyofaa ndani ya nchi na kimataifa. 

Bunifu 51 kati ya 196 zilikidhi vigezo vya kuendelea na tayari baadhi ya vijana wakundi hili wameanza kupewa mtaji wezeshi ili kukuza miradi yao.

Kuhusu mafunzo ya ujasiriamali na elimu ya fedha, Tully amesema makundi yote mawili yanapata na mpaka sasa tayari zaidi ya wajasiriamali 100,000 wamefunzwa; wanawake kwa wanaume.

“Tunapowawezesha wanawake na vijana, naomba nieleweke kuwa tunaangazia wanawake na vijana waliopo kwenye vikundi, vile vilivyosajiliwa na ambavyo vimefanya kazi walau kwa miaka mitatu mpaka sasa na lazima viingie mkataba wa makubaliano (Memorandum of Understanding) na  CRDB Bank Foundation na kikundi kiwe na akaunti Benki ya CRDB. 
 
Vikundi ambavyo havijakidhi vigezo hivi pia vinakaribishwa kujiunga kwani watapewa mafunzo ambayo yatawakuza na kuwawezesha kunufaika na Programu ya Imbeju huko mbeleni,” amesema Tully. 

Tully pia aliitumia nafasi hiyo kumpongeza Mkurugenzi wa BUTA Vicoba, Semeni Gama kwa jinsi anavyojiyoa kuhakikisha wananchi wanachakarika nchini ili kujikwamua kiuchumi.

“Katika safari hii ya mafanikio tunao watu vinara waliotushika mkono sisi CRDB Bank Foundation na Programu ya Imbeju. Vinara hawa wanaongozwa na Mama Semeni. Sisi tunamwita mwamba kwani amekuwa na mchango mkubwa kwenye idadi ya wanawake tuliowapa mafunzo na wale waliofungua Akaunti ya Imbeju. 
 
CRDB Bank Foundation tunampongeza Mama Semeni kwa jinsi anavyojitoa kwa ajili ya maendeleo na mafanikio ya wanawake wenzake. Tukiwa na watu wengi kama hawa wasiotulia mpaka waone wenzao nao wanachakarika, nina uhakika tutafanikiwa kukabiliana na umasikini unaozisumbua kaya zetu nyingi hapa nchini,” amesema Tully.

Kwa upande wake, Semeni ameishukuru Benki ya CRDB kupitia taasisi yake ya CRDB Bank Foundation kwa jinsi ilivyojitoa kuwawezesha wanawake ambao wengi hawapewi nafasi kwenye taasisi nyingi za fedha kutokana na kutokidhi vigezo vilivyowekwa.

“Ili kupata mkopo kwenye taasisi nyingi za fedha nchini, mteja anahitaji kuwa na dhamana lakini wanawake wengi hawamiliki ardhi kutokana na mila zilizopo maeneo mengi. Programu ya Imbeju ambayo imeondoa kigezo hicho inawafaa wanawake wengi watakaoweza kuanzisha biashara zao hivyo kujiingizia kipato cha uhakika,” amesema Semeni.




SHIRIKA LA EMEDO LATOA MAFUNZO KWA WASANII WA MICHORO JIJINI MWANZA

 

Shirika la Usimamizi wa Mazingira na Maendeleo (EMEDO) limetoa mafunzo kwa wasanii wa sanaa za uchoraji jijini Mwanza, ili kuwaongezea elimu na ujuzi zaidi wa kuelimisha jamii kupitia kazi zao za sanaa huku wakijipatia kipato.

Mafunzo hayo yalianza Oktoba 17, 2023 katika ofisi za shirika la EMEDO jijini Mwanza kwa kushirikiana na taasisi ya NAAM Festival ya nchini Kenya na Wasanii Visual Art Arts ya Dar es salaam kupitia mradi wa Sanaa Ziwani Nyanza unaofadhiliwa na balozi za Uswis na Noray nchini Tanzania.

Mkuu wa Idara ya Mazingira kutoka Shirika la EMEDO, Lawrence Kitogo amesema sanaa ina mahusiano makubwa na mazingira hivyo kupitia mafunzo hayo, washiriki watapata ujuzi zaidi wa kutoa elimu kwa jamii kupitia michoro yao.

"Wasanii wa sanaa za michoro wana mchango mkubwa wa kuelimisha jamii hivyo tunapaswa kuungana nao katika kuhamasisha utunzaji wa mazingira hasa Ziwa Victoria kupitia kazi zao za michoro ambazo zinafikisha elimu kwa urahisi" amesema Kitogo na kuongeza;

"Sanaa ni mazingira, ndiyo maana msanii anachofikiria kuchora ndani yake ni mazingira hivyo baada ya mafunzo haya tunatarajia watatumia sanaa kuchora michoro inayotatua changamoto za jamii hasa utunzaji wa mazingira, Ziwa Victoria".

Naye Mkurugenzi wa taasisi ya NAAM Festival, Dave Ojay amewahimiza wasanii wa sanaa za michoro kufanya kazi kwa kuzingatia mahitaji ya jamii, kuchora michoro inayotoa majawabu ya changamoto za maisha na kufikisha ujumbe uliokusudiwa hatua itakayokuza soko la kazi zao ndani na nje ya nchi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa wasanii wa sanaa za michoro kutoka kikundi cha Clour Mwanza, Edward Tibasima amesema sanaa ya michoro inafikisha ujumbe kwa urahisi na inadumu kwa muda mrefu hivyo ni vyema Serikali na wadau mbalimbali wakatambua hilo na kuwatumia kuelimisha jamii.

"Michoro yetu ni rahisi kufikisha ujumbe kwa watu wengi, pia inadumu kuliko jumbe zinazoonyeshwa kwenye luninga" amesema Tibasima akitolea mfano michoro inayoweza kuchora katika miamba na mawe makubwa jijini Mwanza kufikisha ujumbe kwa jamii.

Mshiriki wa mafunzo hayo, Edwardina Njura amesema kupitia sanaa za michoro, uchongaji na ufinyanzi ni rahisi kuelimisha jamii, kuenzi utamaduni na kuhamasisha masuala mbalimbali ikiwemo utalii na utunzaji mazingira huku akiongeza kuwa mafunzo hayo yatawasaidia kuboresha zaidi kazi zao.

Mafunzo hayo yanatolewa kwa washiriki saba waliofudhu hatua ya mchujo kati ya wasanii 18 waliotuma maombi ambapo yamelengwa kuwaongezea ujuzi, kukuza vipaji vyao na kuwasaidia kujiongezea kipato kupitia kazi zao za sanaa.

Mafunzo yalianza Oktoba 17, 2023 yakitarajia kuhitimishwa Oktoba 28, 2023 kupitia maonesho ya kazi za sanaa yatakayofanyika katika ufukwe wa Kamanga jijini Mwanza.
Na George Binagi- GB Pazzo, BMG
Mkuu wa Idara ya Mazingira kutoka Shirika la Usimamizi wa Mazingira na Maendeleo (EMEDO), Lawrence Kitogo akifungua mafunzo kwa wasanii wa sanaa za michoro jijini Mwanza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika hilo, Editrudith Lukanga (hayuko pichani).
Mkurugenzi wa taasisi ya NAAM Festival ya nchini Kenya, Dave Ojay (kushoto) akizungumza wakati wa mafunzo kwa wasanii wa sanaa za michoro jijini Mwanza yenye lengo la kuwajengea uwezo kutumia sanaa kuelimisha jamii na kuleta suluhisho na changamoto mbalimbali ikiwemo utunzaji wa mazingira pamoja na Ziwa Victoria.
Wasanii wa sanaa wa michoro jijini Mwanza wakifuatilia mafunzo hayo wakifuatilia mada mbalimbali.
Mwenyekiti wa wasanii wa sanaa za michoro wanaounda kikundi cha Colour Mwanza, Edward Tibasima akizungumza wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo yaliyoandaliwa na shirika la EMEDO kwa kushirikiana na NAAM Festival kwa ufadhili wa ubalozi za Norway na Uswis nchini Tanzania.
Wasanii wa sanaa za michoro jijini Mwanza wakiwa kwenye mafunzo ya kuwajengea uwezo ili kutumia sanaa zao kuchora michoro yenye kuelimisha jamii. 
Mshiriki wa mafunzo hayo, Edwardina Njura ambaye ni msanii wa sanaa za kiutamaduni akichangia mada kwenye mafunzo hayo.
Mwonekano wa Kituo cha Taarifa na Maarifa ya Mazingira kilichopo katika Ofisi za shirika la EMEDO jijini Mwanza ambapo mafunzo kwa wasanii wa sanaa yalianza Oktoba 17, 2023 hadi Oktoba 28, 2023 yatakapohitimishwa kupitia maonesho ya kazi za sanaa yatakayofanyika katika ufukwe wa Kamanga.
PIA SOMA>>> HABARI ZAIDI HAPA