ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, October 27, 2023

RC TANGA AWATAKA WANANCHI KUACHA KUTUMIA MIFUMO YA KIZAMANI KUHIFADHI FEDHA ZAO

  Mkuu wa Mkoa wa Tanga Waziri Kindamba akizungusha mfano wa kadi ya NMB leo wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Mastabata –Halipoi uzinduzi uliofanyika kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani Mjini Tanga kulia ni Mkuu wa Idara ya Kadi ya Benki ya NMB Philbert Casmir


 Mkuu wa Mkoa wa Tanga Waziri Kindamba akizungusha mfano wa kadi ya NMB leo wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Mastabata –Halipoi uzinduzi uliofanyika kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani Mjini Tanga kulia ni Mkuu wa Idara ya Kadi ya Benki ya NMB Philbert Casmir

 Mkuu wa Mkoa wa Tanga Waziri Kindamba akizungusha mfano wa kadi ya NMB leo wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Mastabata –Halipoi uzinduzi uliofanyika kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani Mjini Tanga kulia ni Mkuu wa Idara ya Kadi ya Benki ya NMB Philbert Casmir

 Mkuu wa Mkoa wa Tanga Waziri Kindamba akizungusha mfano wa kadi ya NMB leo wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Mastabata –Halipoi uzinduzi uliofanyika kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani Mjini Tanga kulia ni Mkuu wa Idara ya Kadi ya Benki ya NMB Philbert Casmir

 Mkuu wa Mkoa wa Tanga Waziri Kindamba akizungusha mfano wa kadi ya NMB leo wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Mastabata –Halipoi uzinduzi uliofanyika kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani Mjini Tanga kulia ni Mkuu wa Idara ya Kadi ya Benki ya NMB Philbert Casmir


Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Waziri Kindamba akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Mastabara –Halipoi iliyofanyika kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani Mjini Tanga kulia ni Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Kaskazini Baraka Ladislaus,


Mkuu wa Idara ya Kadi ya Benki ya NMB Philbert Casmir akizungumzia wakati akielezea kampeni ya Mastabata –Halipoi leo kwenye viwanja vya Mkwakwani Mjini Tanga wakati wa uzinduzi wake kulia Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Kaskazini Baraka Ladislaus

Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Kaskazini Baraka Ladislaus akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Mastabata –Halipoi leo kwenye viwanja vya Mkwakwani Mjini Tanga


Watumishi wa Benki ya NMB Mkoa wa Tanga wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Mastabata –Halipoi leo kwenye viwanja vya Mkwakwani Mjini Tanga.


Na Oscar Assenga,TANGA.

WANANCHI wa Mkoa wa Tanga wametakiwa kuacha kutumia mifumo ya kizamani ikiwemo ya kutembea na fedha mifukoni badala yake watumie mifumo ya kibenki ya Master Card Qr kwani ndio njia salama na ya uhakika wa kuhifadhi fedha zao

Hatua hiyo inaeleza kwambaa itakuwa ni salama kwani itawaepusha wananchi hao na changamoto mbalimbali ambazo wanaweza kukutana nazo ikiwemo wizi

Wito huo ulitolewa leo na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Waziri Kindamba wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Mastabata-Halipoi inayoendeshwa na Benki ya NMB kwenye Halfa iliyofanyika kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani mjini Tanga.

Ambapo alisema wakitumia mifumo ya kibenki ya Master Card QR itawawezesha kuwa na usalama wa fedha zao ikiwemo kutokuchakaa haraka.

Alisema kwamba wananchi wakiwa na mwamko wa kufanya hivyo itawaepusha na kuharibika kwa fedha lakini pia kama nchi itasaidia kuondokana na kuingia gharama na ndio maana wanasistiza umuhimu wa kadi.

“Ndugu zangu leo tupo hapa kwenye uzinduzi wa kampeni hii ya Mastabata –Haipoi niwaambie huu ni mfumo salama na makini hivyo niwaase wana Tanga na watanzania tuuchangamkie”Alisema

Aidha aliwaeleza wakazi wa mkoa huo kutumia njia mbadala kwa ajili ya kufanya malipo kuna kuwa na faida nyingi hivyo niwapongeze benki ya NMB kwa kuja na ubunifu huu.
Hata hivyo aliwataka wananchi wa mkoa huo kuacha kutumia mifumo ya kizamani kutembea na fedha mfukoni ili kuepukana na changamoto mbalimbali ambazo wanaweza kukumbana nazo ikiwemo wizi.

Alisema kwa sababu unapotumia kadi kwa kufanya malipo Benki ya NMB haikuachi hivihivi bali inakupa na zawadi mbalimbali hivyo wananchi changamkieni fursa hiyo muhimu.

Awali akizungumza katika uzinduzi huo,Mkuu wa Idara ya Kadi wa Benki ya NMB Philbert Casmir alisema kampeni hiyo ni kusisitiza matumizi ya kadi wanaoita mastabata haipoi.

Alisema ili kurudisha faida ya benki ya NMB kwa jamii kila mwaka mwishoni wanafanya kampeni hiyo kwa kushirikiana na wadau wao wa mastakadi kwa kufanya kampeni kubwa kutoa zawadi kemukemu.

Aidha alisema utoaji wa zawadi hizo unakwenda sambamba na kuhamasisha wateja wao kuachana na matumizi ya pesa taslimu badala yake watumie kadi kufanya miamala,manunuzi.

Alisema pia watumie simu zao kufanya manunuzi ambapo kampeni hiyo leo wameizinduliwa Tanga na ilianza mwaka 2018 na 2022 waliita mastabata kivyakovyako na leo wanaita mastabata haipo.

Philbert alisema kwamba kupitia kampeni hiyo benki ya NMB inaendelea kuhamasisha malipo ya njia kidigitali na kuachana na pesa taslimu kupitia hiyo watakuwa na droo ya kila wiki,mwezi na hatimaye fainali droo sasa hapa mnisikilize kwa umakin.

Hata hivyo alisema kwamba benki ya NMB wakishirikiana wenzao wa mastakadi wameandaa milioni 350 zawadi ambazo zitakuwa zikishindaniwa na wateja wao huku akieleza vigezo kwanza zawadi za kila wiki.

Ambapo alisema watakuwa na washindi 100,kila mmoja atashinda pesa taslimu 100,000 lakini watafanya zoezi akikuta mtu afanaya manujnuzi kwa kutuimia kadi palepele anapewa 50,000.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.