ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, August 4, 2021

AHUKUMIWA KIFUNGO NA FAINI BAADA YA KUKUTWA NA SILAHA NZITO AINA YA KIFARU NYUMBANI KWAKE.

 

 Mstaafu mmoja nchini Ujerumani ametiwa hatiani kwa kosa la kumiliki silaha baada ya kubainika kuwa na silaha kubwa binafsi kikiwemo kifaru.

Mtuhumiwa huyo ,84, amehukumiwa kifungo cha miezi 14 na ameamriwa kulipa faini ya pauni 213,469.

Maafisa walibaini kifaru na vifaa vingine vya kijeshi vya enzi ya vita vya pili vya dunia kwenye makazi ya mzee huyo katika mji wa Heikendorf mwaka 2015

Jeshi lilisaidia kuondoa vifaa hivyo.

Jumatatu, mahakama iliamuru kuwa mtuhumiwa huyo ambaye jina lake halikutajwa kwasababu ya sheria ya faragha ya Ujerumani, lazima auze au akigawe kifaru hicho na silaha ya kupambana na mashambulizi ya anga iwekwe kwenye makumbusho

Kwa mujibu wa wakili wa mtuhumiwa, idara ya makumbusho ya Marekaniina nia ya kununua kifaru.

Wanahistoria wengi wa Marekani wanasema kilikuwa kifaa bora zaidi kilichotumiwa na Ujerumani wakati wa vita vya pili vya dunia.

Mwanasheria amesema kuwa maafisa wanaokusanya vifaa vya kijeshi wa Ujerumani walitaka silaha nyingine kama vile bunduki na bastola, vyombo vya habari vya nchini humo vimeripoti.

Mamlaka za mji huo zilivamia makazi yake mwaka 2015 baada yakupata taarifa kuhusu vitu vinavyomilikiwa na mstaafu huyo, taarifa hiyo ilitolewa na wafanyakazi wenzao wa Berlin, ambao awali walifanya upekuzinyumbani kwake wakitafuta mchoro ulioibiwa baada ya enzi za Nazi.

Wanajeshi kama 20 hivi walitumia saa tisa kukiondoa kifaru hicho kutoka kwenye makazi ya mstaafu huyo

Vyombo vya habari vya huko viliripoti kwamba mtu huyo alikuwa ameonekana wakati mmoja wa baridi akitumia kifaru kama jembe la kuondolea barafu.

CHANJO ELFU TISINI ZATOLEWA MKOA KWA LENGO LA KUWAKINGA WANANCHI.

 


Na  Maridhia Ngemela

Mganga mfawizi wa hospitali ya rufaa Mkoa sekou toure Bahati Peter Msaki amewataka wananchi kuendelea kujitokeza kwa wingi kupata chanjo na kuachana na maneno ambayo yanasemwa kwenye mtandao ya kijamii

Msaki ameeleza hayo wakati wa zoezi la uzinduzi wa chanjo ya kinga ya ugonjwa wa uviko 19 iliyozinduliwa leo mkoani hapa amesema zaidi ya watoa huduma 200wamejiandikisha kw lengo la kupata kinga huyo kwani ni kundi moja wapi ambalo limepewa kipaumbele kutokana na kazii inayowakutanisha na watu mbalimbali.
 
Bahati ameeleza kuwa kinga ni bora kuliko kusubiri kuungua ndio ukapate matibabu hivyo hakuna sababu ya kuendelea kudanganyana juu ya chanjo kuwa ina madhara mwilini.

Aidha amewataka wananchi kuendelea kujikinga kwa kuchukua hatadhali kwa kivaa barakoa,  kunawa mikono na kuepuka misongamano isiyokuwa ya lazima.

Kisali Simba ni mmoja kati ya waandishi wa habari aliyejitokeza kupata chanjo  ameeleza kuwa hakuna changamoto yeyote ambayo ameipata baada ya kupata kuchanjo  hiyo ya Uviko 19 .

"Nimefurahi kupata chanjo hii kwani kuanzia sasa niko imara kabsa sina hofu juu ya maambukizi ya ugonjwa huu" alisema kisali.


MABONDIA CLASS NA NASSIBU WAPIGWA PINI NA SUPER D BOXING PROMOTION

 


NA MWANDISHI WETU

PROMOTA wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' amewapiga pini mabondia Ibrahimu class na Nasibu Ramadhani kwa kuingia nao Mkataba wa kuzipiga Septemba 24 jijini Dar esa Salaam 

Akizungumza baada ya kuingia mkataba na mabondia hao uliotiwa saini mbele ya rais wa kamisheni ya ngumi za kulipwa TPBRC Agapeter Basili zilizopo keko Dar .

Super D amesema kuwa anapenda kufungua milango kwa wafadhili mbalimbali kujitokeza kudhamili mpambano uhu kwani mpambano ulikuwa unasubiliwa kwa hamu kubwa sana na mashabiki wa mchezo wa masumbwi kwa kuwa hii ni dabi ambayo ina kila kitu katika mchezo wa masumbwi mana mabondia wana uwelewa wa mchezo wa ngumi pamoja na kujulikana kimataifa zaidi.

aliongeza kwa kusema kuwa mchezo wa masumbwi sio uhadui kwani michezo ujenga urafiki pamoja na kujenga udugu, mabondia hawa ambao wamekuwa wakifanya kazi za uchambuzi wa mchezo wa ngumi katika TV. 

ata hivyo kwa sasa wanaingia katika vita ya kutafuta heshima katika mchezo wa ngumi ambao wanaupambania kila kukicha.

mbali na mabondia hao mabondia wengine waliokwisha saini mkataba kupitia kampuni tanzu ya kizalendo ya Super D Boxing Promotion ni Issa Nampepeche ambaye atavaana na Juma Choki katika mpambano wa kugombania ubingwa wa taifa.

MZUMBE WAJA NA MKAKATI KUWATAMBUA MASHUHURI WALIOHITIMU CHUONI KWAO.



 "Kwa muda mrefu tumekuwa na wahitimu wengi wenye sifa mbalimbali viongozi maarufu ndani na nje ya nchi, wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa waliofanya na wanaofanya makubwa kwa taifa hili, hii sasa itakuwa forum itakayo waunganisha kuweza kupata mrejesho toka kwenye soko "

Tuesday, August 3, 2021

OLIMPIKI TOKYO: MWANARIADHA MJERUMANI MWENYE ASILI YA TANZANIA ASHINDA DHAHABU



Raia wa Ujerumani mwenye asili ya Tanzania Malaika Mihambo, amelishindia taifa lake medali ya dhahabu katika mashindano ya michezo ya Olimpiki ya long Jump.

Mwanaridha huyo aliruka urefu wa mita saba ili kuchukua ushindi.

Awali Mihambo alikabiliwa na changamoto kadhaa kabla ya mashindano hayo lakini hatimaye alifanikiwa kuonesha umahiri wake.

Katika fainali ya mchezo huo iliofanyika hii leo Jumanne, bi Malaika hakuonesha ishara zozote za kuibuka mshindi.

Urefu wa mita saba alioruka katika jaribio la sita ulimwezesha kuipatia Ujerumani nishani yake ya kwanza ya dhahabu katika mchezo huo tangu Heike Drechsler aliposhinda mwaka 2000.

Nishani ya fedha ilimwendea mshindi mara nne wa mashindano ya dunia na Olimpiki yaliofanyika mjini London Brittney Reese wa Marekani baada ya kuruka mita 6.97 huku Ese Brume wa Nigeria akijinyakulia medali ya shaba na kuiongezea Afrika idadi ya medali katika michezo hiyo.

MTAKA: HALI SI NZURI DODOMA, CHUKUENI TAHADHARI DHIDI YA COVID -19

 

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Anthony Mtaka amewataka wakazi wa Dodoma kuchukua hatua za tahadhari dhidi ya ugonjwa wa corona kwa sababu hali si nzuri mkoani humo.

Ameyasema hayo leo Jumanne Agosti 3, 2021 wakati akizungumza na askari wa usalama wa barabarani na viongozi wa masoko wa mkoa wa Dodoma.

Amewataka askari hao, viongozi wa masoko na wafanyabiashara kuhakikisha wanachukua hatua za kujikinga katika maeneo yao kwa kuvaa barakoa na kunawa maji tiririka na sabuni au kutumia vitakasa mikono.

Pia amewataka askari wa usalama wa barabarani kuhakikisha watu wote wanakaa kwenye viti (level seat) kwenye daladala na bajaji na kwenye bodaboda kuhakikisha hawabebi abiria zaidi ya mmoja.

Mkuu wa Usalama Barabarani Mkoa wa Dodoma, Boniface Mbao amesema watakapotoka katika kikao hicho wataenda kutekeleza maagizo hayo kwa kutoa elimu na ikibidi kwa ukali, ili kuhakikisha abiria wanakaa katika viti kwenye mabasi ya abiria.

Amesema hakuna gari litakalopita kwenye mkoa huu likiwa limejaza zaidi ya abiria waliokaa kwenye viti.

BABU WA LOLIONDO KUZIKWA KESHO SAMUNGE.

 


Mwili wa Mchungaji Ambikile Mwasapile maarufu Babu wa Loliondo unatarajiwa kuzikwa kesho katika Kijiji cha Samunge, wilaya ya Ngorongoro mkoa wa Arusha sehemu ambayo alikuwa akitoa tiba ya mitidawa maarufu kama kikombe cha Babu.

Mkuu wa wilaya ya Ngorongoro, Raymond Mwangwala amethibitisha taarifa hiyo akiliambia Gazeti la Mwananchi, familia imekubaliana mazishi ya Mchungaji Ambikile kuwa Samunge.

Babu wa Loliondo alifariki Julai 30 akiwa na umri wa miaka 86, aliugua nimonia kali ambayo ilimsababisha kupata changamoto ya upumuaji na kupeleka kifo chake.

WATATU WASIMAMISHWA KAZI, KAMATI YAUNDWA KUCHUNGUZA MOTO MSAMVU

 

Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani amewasimamisha kazi wahandisi watatu wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kupisha uchunguzi baada ya Kituo cha Kupoza na Kusambaza Umeme Msamvu kuungua moto na kusababisha hasara ya takribani shilingi Bilioni 2.

Aidha amemuagiza Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Kheri Mahimbali kuunda kamati ya kuchunguza na kubaini chanzo halisi cha Moto huo na hasara iliyopatika ndani ya siku tano kuanzia leo (Agosti 3, 2021).


Katika ziara hiyo, Dkt. Kalemani aliambatana na Naibu  Katibu Mkuu wizara hiyo, Kheri Mahimbali, Kamishna wa Umeme na Nishati Jadidifu, Edward Ishengoma, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Dkt.Tito Mwinuka pamoja na viongozi wengine waandamizi wa Wizara na TANESCO.

Sambamba na hilo aliiagiza Kampuni ya inayotekeleza Mradi wa Reli ya Umeme (SGR) kumchungumza mhandisi wake anayedaiwa kusababisha hitilafu hiyo kwa kukata waya wa umeme na kari la kuchimbua barabara wakati akitekeleza majukumu yake na kuchukuliwa hatua pindi itakapobainika.

Dkt. Kalemani alisema hayo, Mkoani Morogoro, Agosti 03, 2021 alipofanya ziara ya kukagua kituo cha Kupoza na Kusambaza Umeme cha Msamvu kilichoungua moto Jana baada ya kutokea hitilafu na kusababisha wananchi kukosa Umeme.


Dkt. Kalemani alifafanua kuwa wahandisi hao wa TANESCO, wamesimamishwa kwa kushindwa kubaini hitilafu iliyotokea katika mifumo ya kuendeshea mitambo kituoni hapo, na kusababisha harasa kubwa kwa taifa baada ya kituo hicho kuungua moto.

“Wahandisi waliokuwa zamu siku hiyo wasimamishwe kazi kuanzia Sasa kwa kushindwa kubaini mapema hitilafu iliyotokea katika mifumo na kusababisha hasara kubwa kwa Taifa, wakati walikuwepo kazini,pia matukio ya moto yamekuwa mengi lazima tuchunguze kufahamu kama kuna yeyote anahujumu miundombinu ya umeme”, alisema Dkt. Kalemani

Hata hivyo aliitaka TANESCO kufanya kazi usiku na mchana kuhakikisha umeme unarejea katika maeneo yote ndani ya saa 24 kuanzia leo,vilevile waongeze wataalam kutoka vituo vingine ili kuongeza nguvu kazi na kukamilisha kazi hiyo haraka.

Aidha Dkt. Kalemani aliwataka TANESCO kuharakisha manunuzi ya vifaa na miundombinu yoyote iliyoungua kwa kutumia mfumo wa dharura usioathiri taratibu za manunuzi ili kurejesha kituo hicho katika hali yake ya kawaida ndani ya kipindi kifupi.   

Vilevile aliwataka TANESCO kuhakikisha kuwa vituo vyote vya vilivyojengwa zamani vya kupoza na kusambaza umeme vinakuwa na mifumo maalum ya kubaini hitalafu ikitokea na namna ya kuidhibiti kabla ya madhara makubwa kutokea.

Pamoja na mambo mengine aliwaagiza kuweka alama katika maeneo yote ambayo miundombinu mikubwa ya umeme imepita chini ya ardhi hasa nyaya ili kutoa tahadhari kwa watakaokuwa wakifanya kazi au kupita maeneo hayo.

Pamoja na mambo mengine aliwataka wananchi ambao bado huduma ya umeme haijarejea kuendelea kuvuta subira wakati wataalam wakiendelea kufanya kazi zao, na kwamba tayari baadhi ya vifaa kutoka mkoani Singida viko njiani kuwasili eneo hilo ili kuhakikisha huduma ya umeme inarejea maeneo yote ndani ya muda mfupi.

Monday, August 2, 2021

WATAALAMU WA AFYA WAELEZA SABABU ZA WATOTO KUTOSHAMBULIWA KWA KIASI KIKUBWA NA UVIKO19

 


Wataalamu wa tiba za binadamu wamesema kuwa kufa na kuzaliwa kwa cell mara kwa mara kwa watoto ndio sababu inayopelekea watoto kutoshambuliwa na Virusi vya UVIKO 19 vinavyosababisha ugonjwa wa homa ya Mapafu.

Hayo yamebainishwa jijini Arusha na Mganga wa Hospitali ya Maunti Meru Dkt Sunday Wanyika wakati akitoa mada Kuhusu mlipuko wa Virusi vya UVIKO 19 kwenye mkutano wa wadau Kuhusu masuala ya msaada wa kisheria na upatikanaji haki kwa wananchi katika kipindi cha matumizi ya lugha ya kiswahili.

Mganga huyo ameeleza kuwa hali hiyo ndio imekuwa ikisababisha watoto kutoshambuliwa na Virusi hivyo maana vinapotaka kushambulia vinakuta cell zimekufa na kuanza kuzalishwa nyingine hivyo wao wakijikuta wanakuwa sugu na kuwa na uwezo wa kupokea na kuambukiza na kuathiri watu wazima.

"Zaidi ya aslimia 50 ya wagonjwa hawaonyeshi dalili na wanaongoza kwa kusambaza Virusi vya ugonjw huo hivyo wakati wa kujikinga usiwahofia ambao wameshaugua na kuonyesha dalili tu, muwe makini pia na kundi hilo, mpaka sasa watubmilioni 199 wameshapimwa na kukutw na maambukizi huku watu milioni 4 wakifariki na ugonjwa huo ulimwenguni,"amesema.

Ametoa wito kwa wananchi kuhakikisha wanakuwa makini kwa kujikinga na maambukizi ya virusi hivyo kwa kuchukua tahadhari zote ikiwa ni pamoja na kuhakikisha wanachoma chanjo ambalo ni lazima kutokana na hali halisi ilivyo sasa, kutokwenda kwenye mikusanyiko isiyo ya lazima na kutulia majumbani, kuvaa barakoa ambazo zinakinga, kutumia vitakasa mikono na kunawa maji tiririka.

"Simu za mkononi zinaongoz kwa mambukizi kutokana n kushikwa mara kwa Mara nawasii wannachi muwe nazo makini kw kutumia vitakasa mikono mara kwa Mara,"amesisitiza.

Akizungumzia Virusi vya UVIKO 19 awamu ya sasa amesema viko tofauti sana na vile vya awamu ya kwanza  vinasambaa kwa haraka zaidi na ni rahisi kusababisha kifo huku akitaja dalili namba moja kuwa ni kifua kuuma na kuwa kizito wakati awali ilikuwa ni kupta mfua, kukohoa na kushindwa kunusa.

Akifungua mkutano huo Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Godfrey Mizengo Pinda amewataka mawakala wa sheria kwenye maeneo yao wapambanie afya za watu wao suala la chanjo ni muhimu Sana kwa maisha ya watanzania hivyo amewaasha washiriki wote wajitokeze kuchoma chanjo katika zoezi la uzinduzi wa chanjo litakalofanyika kesho jijini Arusha ili kujikinga.

SERIKALI YAIAGIZA TIPER KUTOA TAARIFA ZA UENDESHAJI KAMPUNI KWA WAKATI

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Kheri Mahimbali akizungumza na Waandishi wa Habari wakati alipotembelea Kampuni ya Uhifadhi Mafuta (TIPER) iliyopo jijini Dar-esalaam  tarehe 31 Julai, 2021 kujionea hali halisi ya uendeshaji wa kampuni hiyo.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Kheri Mahimbali akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Uhifadhi Mafuta (TIPER) Michael Mjinja wakati alipotembelea Kampuni hiyo iliyopo jijini Dar-esalaam tarehe 31 Julai, 2021 kujionea hali halisi ya uendeshaji wa kampuni hiyo.


 Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Uhifadhi Mafuta (TIPER) Michael Mjinja akitoa maelezo kuhusu utendaji wa Kampuni ya TIPER kufuatia ziara ya Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Kheri Mahimbali kwenye kampuni hiyo tarehe 31 Julai, 2021.

 

Na Dorina G. Makaya – Dar-es-salaam


Serikali imeiagiza Kampuni ya Uhifadhi Mafuta (TIPER) kuhakikisha inatoa taarifa za uendeshaji wa kampuni hiyo kwa wakati, ili kuepusha changamoto ambazo zinaweza kujitokeza baadaye kutokana na kutokutoa taarifa kwa wakati.

Agizo hilo limetolewa jijini Dar-esalaam tarehe 31 Julai, 2021 na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati Kheri Mahimbali wakati wa ziara yake kwenye kampuni hiyo iliyolenga kujionea hali halisi ya uendeshaji wa kampuni ya TIPER.

Katika ziara yake, Naibu Katibu Mkuu Mahimbali, ametembelea kwenye maeneo mbalimbali ya kampuni hiyo ikiwa ni pamoja na matenki ya kuhifadhia mafuta jambo ambalo ameonyesha kuridhishwa na utendaji kazi wa kampuni hiyo.

Awali, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Uhifadhi Mafuta (TIPER) Michael Mjinja, ameishukuru Serikali kwa kufika katika eneo hilo ambapo wameweza kukubaliana masuala mbalimbali ikiwa ni pamoja na kupeana taarifa kwa wakati.

Amesema, licha ya mafanikio waliyonayo, bado kuna changamoto zinazowakabili huku kubwa ikiwa kuharibika kwa vifaa vya kusukuma mafuta pindi wanapoyatoa kwenye meli, vifaa ambavyo havipatikani nchini hadi viagizwe nje ya nchi.

Kufuatia hali hiyo, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Kheri Mahimbali amesema, endapo taarifa hizo zitatolewa mapema, itakuwa mwarobaini wa changamoto hizo.

Ziara hiyo ni mwanzo wa ziara nyingine katika taasisi zote zenye ubia na Serikali katika Sekta ndogo ya Mafuta hapa nchini kwa lengo la kuboresha ufanisi na utendaji.

Katika ziara hiyo, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati Kheri Mahimbali, aliambatana na baadhi ya viongozi na wataalam kutoka Wizara ya Nishati, Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Wakala wa Uagizaji wa Mafuta kwa Pamoja (PBPA), Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji Nchini Tanzania (EWURA) na Kampuni ya Serikali ya Uagizaji na Usambazaji wa Mafuta nchini (TANOIL).