ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, August 3, 2021

BABU WA LOLIONDO KUZIKWA KESHO SAMUNGE.

 


Mwili wa Mchungaji Ambikile Mwasapile maarufu Babu wa Loliondo unatarajiwa kuzikwa kesho katika Kijiji cha Samunge, wilaya ya Ngorongoro mkoa wa Arusha sehemu ambayo alikuwa akitoa tiba ya mitidawa maarufu kama kikombe cha Babu.

Mkuu wa wilaya ya Ngorongoro, Raymond Mwangwala amethibitisha taarifa hiyo akiliambia Gazeti la Mwananchi, familia imekubaliana mazishi ya Mchungaji Ambikile kuwa Samunge.

Babu wa Loliondo alifariki Julai 30 akiwa na umri wa miaka 86, aliugua nimonia kali ambayo ilimsababisha kupata changamoto ya upumuaji na kupeleka kifo chake.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.