ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, December 1, 2010

MAAFALI YA MADAKTARI WETU YAJA.......!!!!

KUTOKA KUSHOTO MR.R.TIBAIJUKA, MKUU WA CHUO PROF. J.P MTABAJI NA PROF. W.MAHALU.
Chuo kikuu kishiriki cha sayansi za afya Weill Bugando cha chuo kikuu cha mtakatifu Agustino Tanzania jumamosi ya tarehe 4Desemba2010 kinataraji kufanya maafali yake ya tatu kutunukisha stashahada na shahada.
UONGOZI WA CHUO NA VYOMBO MBALIMBALI VYA HABARI.
Maafali hayo yatatanguliwa na kongamano la wafanyakazi na wanafunzi wote linalofanyika leo trh 1 Nyumbani hotel ambapo mada mbalimbali zitatolewa. Na tarehe 3 pambano la soka baina ya Wafanyakazi na Wanafunzi.

WAANDISHI WA HABARI NA KIFUNGUA KINYWA.
Tatizo la uhaba wa madaktari NCHINI limekuwa sugu kwa muda mrefu kutokana na wazazi wengi kutokuwa na uwezo wa kumudu gharama kubwa kuwasomesha vijana wao masomo hayo amabyo yanakadiriwa kufikia kiasi cha SHILLINGI MILLIONI 25 HADI 50 ILI KUWA DAKTARI KAMILI.

Mgeni rasmi wa maafali hayo atakuwa Mhashamu askofu mteule JUDE THADEUS RUWA'AINCHI. Chuo cha Bugando kimejitenga toka SAUTI kutokana na kuwa na uwezo wa kujilea, na kimeingia katika mchakato huo ili kujikita zaidi ktk fani ya tiba. Mwaka 2010 utakuwa wa kipekee kwa chuo hicho kwani vimeongezeka vitivo toka kimoja na kuwa vitano.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.