ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, December 1, 2010

GADNA AJIENGUA CLOUDS FM!!

MTANGAZAJI MAHIRI WA KIPINDI CHA JAHAZI KINACHO RUSHWA KILA SIKU JIONI SAA YA 10 HADI 12 KAMILI KUPITIA REDIO YA WATU CLOUDS FM AMEAMUA KUJIENGUA KWA SABABU AMBAZO AMESEMA NI ZA KUTAKA KUJARIBU UJASIRIAMALI BINAFSI.Uongozi wa CLOUDS FM umethibitisha habari hizo na kwamba kesho tarehe 2DEC.2010 utatoa tamko rasmi siyo tu kwa kuondoka GADNA ambaye alijulikana kama KEPTEEEEEIN!!na kumechi vilivyo na mtangazaji mwenzie KIBONDE katika kipindi pendwa cha jioni ambacho huwapa kampani sana watanzania kote inapofika redio hiyo.

Awali kabla ya hatua hiyo ya Gadna mtangazaji wa kike SOPHIA KESSY nae alitangaza kuvunja ndoa baina yake na kipindi cha Afrika Bambataa na kusema kuwa ameamua kujitosa kwenye majukumu mengine bila kufafanua kama ilivyo kwa Gadna ambaye pia hajafafanua juu ya ujasiliamali anaokwenda kudil nao.

"Habari za Gadna ni za kweli, ameondoka, hayo mengine tutayaweka bayana kesho tutakapotoa tamko rasmi wa jinsi tunavyo jiandaa na mambo mapya ya mabadiliko". Alisema mmoja wa wakurugenzi wa CLOUDS MEDIA, bwana RUGE MUTAHABA.

DUH NOVEMBER NI NOMA!!!

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.