
Hayo ni kwa mujibu wa kitabu kipya kilichozinduliwa hii leo na professa wa chuo kikuu cha Havard Calestous Juma. Kitabu hicho 'The New Harvest' kinatoa wito kwa viongozi wa Afrika kutilia mkazo upanuzi wa kilimo kupitia sera na mikakati yao ya kitaifa.
Ripoti hiyo itawasilishwa kwa viongozi wa Afrika siku ya Ijumaa mjini Arusha katika mkutano unaofanyika ndani ya hoteli ya Ngurdoto Mountain Lodge nchini Tanzania, ambapo Marais wa Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi wanafanya kikao kuzungumzia usalama wa chakula pamoja na suala la mabadiliko ya hali ya anga.
Kwa mujibu wa Professa Juma, uzalishaji wa chakula duniani unaendelea kuongezeka lakini katika maeneo mengi ya Afrika hali ni tete licha ya kuwepo na ardhi ya kutosha ya kilimo.
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.