ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, January 20, 2022

WAFUNGWA 10 DRC WAHUKUMIWA KWA UBAKAJI GEREZANI.


 
Wafungwa kumiwamepatikana na hatia ya kuwabaka makumi ya wafungwa wa kikewakati wa ghasia katika jela moja iliojaa wafungwa kupitia kiasi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC.


Wanawake 37 na msichana mmoja walitoa ushahidi kwamba walibakwa mara kadhaa wakati wa ghasia za siku tatu katika jela ya Kasapa Central Prison karibu na mji wa Lubumbashi 2020.


Baadhi ya wafungwa wa kike walipata uja uzitona kuambukizwa maradhi ikiwemo HIV


Wanaume hao 10 walipigwa faini na kuagizwa kuhudumia miaka mingine 15 jela kila mmoja wao.


Ijapokuwa baadhi ya wafungwa waliogopa kutoa ushahidi , makumi walitoa ushahidi mbele ya kiongozi wa mashtaka wa jeshi kwamba walibakwa wakat iwa ghasia hizo.


Melania Mumbo ambaye ni wakili wa waathiriwa, aliambia AFP News ‘’Tumeridhika na uamuzi baada ya kupigania haki kwa muda mrefu.


Gereza hilo lilitekwa na wafungwa wa kiume kwa siku kadhaa mwezi Septemba 2020. Walichoma eneo la wafungwa wa kike- ikiwemo msichana wa miaka 16- na hivyobasi kuwalazimisha wanawake hao kulała katika eneo jingine la jela hiyo ambapo walibakwa.


Takriban wafungwa 20 na askari jela waliripotiwa kuuawa wakat wa ghasia hizokabla maafisa wa usalama kuchukua udhibiti.


Ubakaji huo uliangaziwa na shirika la haki za kibinadamu la Human Rights Watch , ambao waliarifu watawala kuchunguza unyanyasaji huona kuwahudumia walioathiriwa.


Shirika hilo linasema kwamba jela hiyo iliojengwa kumiliki wafungwa 800 , ilikuwa na karibia wafungwa 2000 wakati wa ghasia hizo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.