ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, May 15, 2019

SAFARI YA ANTOINE GRIEZMANN KWENDA BARCELONA IMEKWIVA.


Katika ujumbe wake wa kuthibitisha kuondoka mwisho wa msimu huu na kuwaaga mashabiki wa klabu hiyo amesema "Imekuwa miaka mitano bora, asanteni kwa kila kitu, nimewaweka moyoni mwangu."

Mchezaji huyo mwenye miaka 28 amekuwa akihusishwa na uhamisho wa kwenda Barcelona tangu msimu uliopita na tetesi hizo zimeshika hatamu baada ya timu hiyo kupokea kipigo cha goli 4-0 kutoka kwa Liverpool.

Inadaiwa kuwa Barcelona ambao ni mabingwa wapya wa Ligi Kuu msimu huu nchini Uhispania, imeandaa kitita cha Paundi Milioni 108(Tsh. 321,442,041,276) ili kumsajili

Mchezaji huyo aliyejiunga Atletico mwaka 2014 akitokea Real Sociedad ameichezea timu hiyo michezo 256 na kufunga magoli 133 lakini pia amepiga pasi 50 zilizozaa magoli.

Ameiwezesha timu hiyo kushinda makombe ya Spanish Super Cup (2014-15), Europa League (2017-18) na UEFA Super Cup (2018-19).

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.