ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, February 13, 2024

"KIFO CHA LOWASSA HAKIWEZI KUSITISHA KUDAI HAKI ZA WATANZANIA" KUELEKEA MAANDAMANO YA CHADEMA MWANZA

 NA ALBERT G. SENGO/MWANZA

KUELEKEA Alhamisi ya tarehe 15 mwezi Februari 2024 siku ambayo Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) imeiteuwa kuwa ya kufanyika maandamano ya amani jijini Mwanza, napata nafasi ya kufanya mahojiano na wadau wa chama hicho waliopo kwenye maandalizi katika viwanja vya Furahisha. 1. Jeh ni ajenda zipi CHADEMA wanakwenda nazo katika maandamano yao jijini Mwanza? 2. Mnafanya Maandamano haya wakati Taifa likiwa kwenye simanzi ya kuondokewa na aliyewahi kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania Edward Lowassa, ambaye pia mnamo mwaka 2015 alikuwa mgombea urais kwa tiketi ya CHADEMA, pengine hamuoni ingekuwa busara kupisha kwanza hilo liishe kisha mkaendeleza ajenda zenu? 3. Pengine inawezekana Maandamano yenu yakaingiza hoja Mpya ya kuenzi Demokrasia kama mnavyosema ama mtabaki na hoja zile zile ambazo mmekuwa mkizinadi?

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.