ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, October 7, 2024

TPA TANGA BILIONI 18 NDANI YA MIEZI 3

 VICTOR MASANGU,PWANI TV

 
Kilio cha walimu wa shule ya  msingi Boko Timiza iliyopo  kata ya Tumbi Halmashauri ya Wilaya ya  Kibaha mji   kilichokuwa kikiwakabiliwa kwa kipindi cha miaka zaidi ya 40  cha kuwepo na  changamoto  sugu ya  ukosefu mkubwa  wa kutokuwa na viti na meza hatimaye kimepatiwa ufumbuzi baada ya baadhi ya wadau wa maendeleo ya elimu kuamua kulivalia njuga suala hilo na kwenda kutoa msaada kutokana na kubaini walimu hao hawana sehemu maalumu ya kukaa.

Hayo yamebainishwa na Kaimu  Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Boko Timiza Rozania Kimate  wakati wa halfa fupi  iliyofanyika shuleni hapo kwa ajili ya kukabidhiwa  msaada huo wa viti na meza kutoka kwa mdau wa maendeleo Selina Koka ambaye pia ni mke wa Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini na  Mlezi wa Jumuiya ya Umoja wa wanawake (UWT)  Wilaya ya Kibaha mjini na kubainisha  msaada huo utakuwa ni mkombozi mkubwa kwa walimu.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.