ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, October 10, 2024

WANANCHI WA BUKOMBE KWA MH.BITEKO WAFURIKA ZOEZI LA UGAWAJI WA MITUNGI YA GESI DARASA LATOLEWA.

 ZAIDI YA MITUNGI YA GESI 1,500 YATOLEWA KWA BEI YA RUZUKU BUKOMBE

Wananchi wametakiwa kuunga mkono jitihada za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan za kutumia Nishati Safi ya Kupikia ili kuimarisha afya zao sambamba na kutunza mazingira. Wito huo umetolewa Oktoba 10, 2024 Wilayani Bukombe na Mkurugenzi wa Teknolojia za Nishati Jadidifu na Mbadala kutoka Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Advera Mwijage wakati wa Semina maalum ya Nishati Safi ya Kupikia kwa wakazi wa Wilaya hiyo. "Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kinara wa ajenda ya nishati safi ya kupikia, anatupenda na anafanya kila njia kuhakikisha kila mwananchi anapata bidhaa za nishati safi za kupikia kwa gharama nafuu", alisema Mhandisi Advera.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.