ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, October 27, 2018

SAUDI ARABIA YAPEWA RUNGU KUWACHUNGUZA WAHUSIKA WA MAUAJI YA MWANDISHI KHASHOGGI.

Waziri wa mambo ya nje wa Saudi Arabia amesema kuwa washukiwa wote wa mauaji ya mwandishi Jamal Khashoggi, mashtaka yao yatasikilizwa nchini Saudi Arabia.

Katika kikao mjini Bahrain, Adel al-Jubeir amevishutumu vyombo vya habari vya magharibi kwa kuongeza chumvi katika kuripoti taarifa ya kesi hiyo.

Kauli yake imekuja siku moja baada ya serikali ya Uturuki kutaka kuwaamisha washukiwa 18 waliohusika na mauaji hayo.

Mwandishi huo aliuwawa nchini Saudi Arabia mjini Istanbul wiki tatu zilizopita.

Mchumba wa Jamal,Riyadh amekanusha madai ya kuhusishwa kwa familia ya kifalme katika mauaji hayo na badala yake amelaumu watu waliowataja kuwa''maajenti wakatili''

Awali Saudi Arabia ilikana kuhusika kwa lolote dhidi ya mwandishi huo lakini mwendesha mashtaka wa serikali sasa ameweza kueleza jinsi mauaji hayo yalivyotokea.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.