ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, February 24, 2023

WANAUME WANAOPIGA WAKE ZAO VIBAO/MAKOFI CHANZO CHA UKIZIWI - KUELEKEA SIKU YA USIKIVU DUNIANI PT 1

NA ALBERT G. SENGO/MWANZA Tatizo la usikivu linazidi kuongezeka siku hadi siku. Inakadiriwa kuwa zaidi ya asilimia 5 ya watu duniani wana tatizo la usikivu. Kipigo na makofi karibu na maeneo ya sikio imesababisha watu wengi hususani akinamama kuwa viziwi. Kuelekea Maadhimisho ya 'SIKU YA USIKIVU DUNIANI' inayoadhimishwa kila mwaka na kilele chake Tarehe 3 mwezi March, tunazungumza na Dr. Olivia Michael Kimario ambaye ni daktari bingwa wa kichwa, koo, pua, masikio na shingo, kutoka Hospitali ya Rufaa ya Bugando ambaye sanjari na kutoa elimu pia ametoa wito kwa kila mmoja wetu kuchukua hatua kujikinga na vitendo vinavyosababisha changamoto hiyo ikiwemo jamii hususani akinababa kuepuka kuwapiga wapenzi wao vibao au ngumi masikioni. Kuelekea maadhimisho hayo Hospitali ya Rufaa ya Bugando iliyopo jijini Mwanza imeandaa kliniki kwa wananchi kuonana na wataalamu na fanyiwa uchunguzi bure.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.