ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, July 26, 2025

WAPANDA MLIMA KILIMANJARO KUTOA UJUMBE MZITO WA TAHADHARI DHIDI YA MAAMBUKIZI YA VVU.

 NA ALBERT G.SENGO

Katika kuhakikisha jitihada za kupunguza maambukizi mapya ya Virusi vya Ukimwi (HIV), kuondoa unyanyapaa, na kupunguza vifo kufikia mwaka 2030, jamii imetakiwa kuendelea kuchukua tahadhari kwa kuacha ngono zisizo salama na kutumia kinga ili kuepukana na ugonjwa huo. Akiongea wakati wa kukabidhi vyeti vya pongezi kwa mashujaa wa kampeni ya GGML Kili Challenge waliopanda Mlima Kilimanjaro kwa miguu na baiskeli kupitia njia ya Machame inayofadhiliwa kwa pamoja na mgodi wa Geita Gold Mining Limited (GGML) na Tume ya Kudhibiti Ukimwi (TACAIDS), Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Bw.Nurdin Babu ameikumbusha jamii kuwa ugonjwa huo bado upo. #mountkilimanjaro #samiasuluhuhassan #habari

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment