ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, July 22, 2025

MUDATHIR YAHYA AJITIA KITANZI YANGA SC HADI 2027


 KIUNGO wa Kimataifa wa Tanzania, Mudathir Yahya Abbas (29) amesaini mkataba mpya wa miaka miwili kuendelea kuichezea klabu ya Yanga ya Dar es Salaam.

Yanga wameposti video ya Mudathir akiwa anasaini na kuambatanisha a maelezo kwamba mchezaji huyo ni mali yao hadi mwaka 2027.
Mudathir Yahya Abbas aliyezaliwa Mei 6, 1996 huko Jang’ombe, visiwani Zanzibar alijiunga na Yanga Januari mwaka 2023 akitokea Azam FC na katika misimu miwili na nusu ya kuwa wana Jangwani hao amejijengea heshima kubwa kwa uhodari wake kwenye eneo la kiungo.

Kisoka Muda aliibukia katika akademi ya Azam FC mwaka 2012 kabla ya kupandishwa timu ya wakubwa chini ya Kocha Muingereza, Stewart John Hall na kufanikiwa kuwa mchezaji muhimu.

Hata hivyo, mara mbili Muda alikwenda kucheza Singida Black Stars baada ya kupoteza nafasi kwenye kikosi cha kwanza cha Azam FC na mar azote alirejeshwa baada ya kufanya vizuri, kabla ya kuhamia Yanga Januari 2023.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment