ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, December 10, 2021

RAILA ODINGA KUTANGAZA IWAPO ATAWANIA URAIS 2022

 Aliyekuwa waziri mkuu nchini Kenya Raila Odinga hii leo anatarajiwa kuzindua azma yake ya urais katika uchaguzi mkuu wa 2022.


Raila ambaye atakuwa anawania wadhfa huo kwa mara ya tano, anatarajiwa kutoa uamuzi wake iwapo atajibwaga katika kinyanganyiro hicho katika sherehe kubwa inayofanyika katika uwanja wa Kasarani.


Baadhi ya viongozi wa kimataifa wakiwemo wale walioteuliwa humu nchini wanatarajiwa kushiriki katika hafla hiyo itakayoshuhudiwa na maelfu ya Wakenya waliosafiri hapo jana kutoka maeneo mbalimbali nchini.



Azma ya Raila kutangaza kuhusu kuwania uchaguzi inajiri baada ya kupata uungwaji mkono kutoka kwa viongozi na wafanyabiashara wa eneo la mlima Kenya – eneo ambalo rais Uhuru Kenyatta anatoka.


Hatahivyo baadhi ya viongozi walioshirikiana naye katika muungano wa Nasa katika uchaguzi mkuu uliopita huenda wasihudhurie hafla hiyo licha ya kualikwa.


Huku baadhi yao wakitofautiana naye kisiasa , wengine wamejipata katika shughuli za kitaifa katika mataifa ya kigeni.


Hii leo kuanzia mwendo wa saa moja uwanja wa kitiafa wa kasarani jijini Nairobi umekuwa eneo la shughuli nyingi baada ya wafuasi wa chama cha ODM nchini Kenya kuwasili katika uwanja huo tayari kwa mkutano huo wa Azimio la Umoja.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.