ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, December 8, 2021

WAFUNGWA 38 WAFARIKI HUKU 69 WAKIJERUHIWA KATIKA MKASA WA MOTO WA GEREZA BURUNDI.

 


Takriban wafungwa 38 wamefariki dunia na wengine 69 kujeruhiwa katika moto ulioteketeza gereza kuu la mji mkuu wa Burundi City Gitega mapema Jumanne.

Haijabainika ni nini kilisababisha moto huo.





Kumi na wawili kati ya waliofariki walisakamwa na moshi huku 26 waliosalia wakipata majeraha ya moto, kulingana na makamu wa rais wa Burundi, Prosper Bazombanza, ambaye alitembelea kituo hicho na hospitali ambapo wengi wa majeruhi wanatibiwa.

Aliwaambia waandishi wa habari kuwa majeruhi 34 waliopata majeraha ya moto ya wastani na zaidi wamepelekwa hospitali huku wengine wakipatiwa matibabu katika eneo la gereza.

"Wafanyikazi wa afya wametupa hakikisho kwamba watapona", alisema.

Afisa huyo pia alitangaza bili yao ya matibabu italipwa kikamilifu na serikali.

Chanzo cha moto huo bado hakijabainika. Inasemekana kuwa moto huo ulizuka mwendo wa saa 10 asubuhi kwa saa za Burundi, na kuwashtukiza wafungwa wakiwa usingizini. Mashahidi wamethibitisha kwa shirika la habari la AFP kwamba waliona moto mkubwa ukitokea na kuteketeza kabisa sehemu za jengo la gereza.

Mmoja wa wafungwa ambaye ameweza kuongea kwenye simu amesema alipiga kelele "tutachomwa moto tukiwa hai, lakini, ameongeza, polisi walikataa kufungua milango ya sehemu tulikuepo, wakisema" haya ni maagizo ambayo tumepokea ". Wafungwa wenzake waliteketea kwa moto akisuhudia kwa macho yake.
Hali mbaya ya usalama ilifanya iwe rahisi kwa moto huo kuenea haraka katika gereza ambalo awali lilikusudiwa watu 400 lakini sasa lilikuwa na wafungwa zaidi ya 1500.

Kiwango kamili cha uharibifu kilikuwa bado hakijajulikana.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.