ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, August 31, 2024

CCM KIBAHA MJI YATEMA CHECHE ZAKE KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA

 


NA VICTOR MASANGU, KIBAHA

 
Chama cha mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kibaha mjini kimewataka viongozi wa CCM  kuanzia katika ngazi za Kata, Wilaya na Mkoa kutoingilia kabisa  maamuzi ya wana ccm pamoja na wananchi katika suala zima la  kuwachagua viongozi wanaowapenda katika uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika Novemba 27 mwaka huu kwani wao ndio wanawafahamu  vizuri uwezo wao wa kuchapa  kazi.
 
Kauli hiyo imetolewa na  Mwenyekiti wa Chama cha mapinduzi (CCM) mwalimu Mwajuma Nyamka wakati wa kikao cha Halmashauri kuu  CCM Wilaya ya Kibaha mji ambacho kimefanyika kwa lengo la kuweza  kupitisha utekelezaji wa Ilani kwa kipindi cha kuanzia Januari  hadi mwezi Juni mwaka 2024 na kuhudhuriwa na viongozi mbali mbali wa serikali pamoja na chma.


Nyamka amebaainisha kwamba lengo  kubwa la chama cha mapinduzi ni kuhakikisha inaweza kushinda kwa kishindo katika mitaa yote hivyo ni wajibu wa viongozi wote wa CCM  kuanzia ngazi za mashina na matawi kushikama kwa pamoja na kwamba kutokana na kazi nzuri ambayo imefanywa na Rais Samia Suluhu Hassan katika miradi mbali mbali ya maendeleo watatembea kifua mbele katika kuomba kura kwa wananchi.


Kadhalika Mwenyekiti huyo aliwapongeza madiwani wa Halmashauri ya mji Kibaha pamoja na Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini Silvestry Koka kwa kuweza kushirikiana bega kwa bega katika suala zima la utekelezaji wa miradi mbali  mbali ikiwa sambamba na kutatua kero na changamoto  za wananchi.

"Pamoja na juhudi kubwa ambazo zinafanywa na CCM kusimamia utekelezaji wa Ilani lakini bado kuna baadhi ya watendaji wa mitaa,na kata wamekuwa ni kama tatizo kubwa kwa wananchi kiasi cha kupelekea kuwakwaza kwa kiasi kikubwa kutokana na kutoa lugha zisizokuwa na staha kabisa na kwamba hawataweza kuwawafumbia macho hata kidogo  watendaji wa namna hiyo kwani watatupunguzia kura katika uchaguzi wa serikali za mitaa,"alisema Nyamka.

Pia katika Katika kikao hicho Mwenyekiti Nyamka amesema kwamba  wameiagiza Halmashauri ya mji Kibaha kuhakikisha kwamba wanaitunza miradi mbali mbali ya maendeleo ambayo imemalizika hususan katika miundombinu ya barabara.

"Tumepitisha utekelezaji wa Ilani kwa kipindi cha kuanzia mwezi Januari hadi kufikia mwezi Juni mwaka huu wa 2024, lakini kitu kikubwa tumeagiza halmashauri yetu ya mji kuitunza miundombinu ya barabara hasa katika maeneo yenye lami kwani kumukuwa na changamoto ya kutozitunza maana utakuta maeneo  mengine nusu kifusi cha mchanga na nusu lami,"alibainisha Nyamka.

Aidha Mwenyekiti huyo amebainisha kwamba kuna baadhi ya halmashauri nyingine wameweka mikakati ya kuzitunza barabara zao kwa kuzifanyia usafi na kuzifagia lakini kwa upande wa Halmashauri ya kibaha mjini jambo hilo linakuwa ni vigumu hivyo linapaswa kufanyiwa utekelezaji.

Pia Mwalimu Nyamka amesema kwamba  kumekuwepo na uharibifu mkubwa wa miundombinu ya barabara ambao unafanywa na baadhi ya madereva kupitisha magari ya mchanga yenye uziti mkubwa ambayo ndio yamekuwa ni moja ya chanzo cha kufanya barabara ziweze kuharibika kwa haraka.
 
Kwa upande wake Katibu wa Chama cha mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kibaha mji  Issack Kalleiya ametumia kikao hicho kutoa pongezi kwa mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya mji Kibaha kwa kuweza kubuni vyanzo vipya amabvyo vimepelekea kuongeza zaidi ukusanyaji wa kasi ya kuongeza mapato.

Kadhalika Katibu kalleiya amemshukuru Mkuu wa Wilaya ya Kibaha, madiwani,pamoja na Mbunge kwa kuweza kushikamana kwa pamoja katika kutekeleza Ilani ya chama kwa vitendo ikiwa sambamba na kusimamia miradi mbali mbali ya maendeleo katika nyanja mbali mbali ikiwemo sekta ya afya, elimu, maji, miundombinu ya barabara pamoja na huduma nyingine za kijamii.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nickson Simon amemshukuru na kumpongeza Rais wa awamu ya sita Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuweza kutenga fedha nyingi katika Halmasshauri ya mji wa Kibaha ambazo zimeweza kuleta matokeo chanya katika suala zima la kuwasaidia wananchi katika miradi mbali mbali za maendeleo.

Aidha Mkuu huyo alisema kwamba kwa ushirikiano mkubwa ambao anaupata kutoka kwa viongiozi wa chama cha mapinduzi (CCM) Madiwani wote pamoja na Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini,mkurugenzi wameweza kutekeleza Ilani ya chama kwa kiwango kikubwa ikiwemo kumsaidia Rais katika utekelezaji wa majukumu yake.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.